Uhuru Kenyatta Ampa Onyo Raila Odinga



Aliyekuwa Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta.

Aliyekuwa Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta amefunguka na kutoa onyo kwa mpinzani wake Raila Odinga kuwa asahu kuhusu tume mpya ya uchaguzi lakini pia amemtaka Jaji Mkuu wa Kenya David Maraga kutoingilia kwani wao wameheshimu maamuzi ya mahakama.

Uhuru Kenyatta mpinzani wake Raila Odinga (kushoto).
Uhuru Kenyatta amesema chama chake cha Jubilee kipo tayari kwa uchaguzi huo wa marudio na sasa wanasubiri Tume ya Uchaguzi nchini Kenya IEBC iweze kutangaza siku ya uchaguzi na wanaiomba itangaze siku hiyo haraka.
Aidha Uhuru Kenyatta amesema kuwa wapinzani hao hawana haja ya uchaguzi bali ni watu ambao wanataka serikali ya mseto kitu ambacho yeye hawezi kukiruhusu hata kidogo
Mahakama ya juu nchini Kenya Septemba 1, 2017 ilifuta matokeo ya Urais nchini Kenya na kuamuru kuwa uchaguzi mpya ufanyike katika nafasi ya Urais kutokana na mahakama hiyo kubaini baadhi ya mapungufu wakati wa utoaji wa matokeo hayo ya uchaguzi uliofanyika Agosti 8, 2017.
Mtazame hapa Uhuru Kenyatta akifunguka mengi zaidi

Comments

Popular posts from this blog