HAMISA MOBETO KUZAA NA BWANAKE… ZARI THE BOSS LADY ATINGA BONGO KUPATA UKWELI


                      Zarina Hassan Tiale ‘Zari The Boss Lady’ . BAADA ya maneno mengi kusemwa Bongo kufuatia madai ya bwana’ke kuzaa na mwanamitindo mwenye jina kubwa, Hamisa Hassan Mobetto, mwanamama mjasiriamali mwenye jina kubwa Afrika Mashariki, Zarina Hassan Tiale ‘Zari The Boss Lady’ anadaiwa kuendelea kuliamsha dude baada ya kutinga Bongo na kuanza kudodosa ili kupata ukweli wa ishu hiyo.

Kwa mujibu wa chanzo chetu ambacho ni makini, awali Zari alitinga Bongo mapema wiki iliyopita na kupigwa chabo na ‘wadakuz’ AKIWA KATakiwa nyumbani kwa jamaa huyo ambaye ni msanii wa Bongo Fleva huko Madale jijini Dar. Akiwa katika pozi. Ilidaiwa kwamba, hata hivyo, hakukaa sana kwani aliondoka kwenda kwenye kumbukumbu ya siku 40 za kifo cha mama yake, Halima Hassan nchini Uganda kabla ya kurejea Bongo wikiendi iliyopita.

            Kwa taarifa yenu Zari amejaa tele Bongo na lengo lake ni kuchimba na kupata ukweli juu ya madai ya Hamisa kuzaa na bwana’ke.Unajua akiwa Sauz hapati mtiririko mzuri wa kinachoendelea Bongo ndiyo maana ameona aje kuchimba mwenyewe ili ajue mbivu na mbichi na ajue nini cha kufanya,” kilidai chanzo hicho.Kilizidi kutiririsha madai kwamba, endapo Zari atabaini ukweli kuhusu mzazi mwenzie huyo kuzaa na Hamisa, basi kuna uamuzi mzito atachukua. Hamisa Hassan Mobetto.

                Hata hivyo, gazeti hili lilizungumza na mmoja wa memba wa familia ya msanii huyo ambaye amezaa na Zari watoto wawili ambaye alithibitisha uwepo wa mwanamama huyo, lakini akaomba hifadhi ya jina.Wewe jua tu kwamba, yupo, amejaa tele. Kuhusu hayo mambo yake na Hamisa mimi sijui maana sijamsikia akilizungumzia. So labda anafanya kimyakimya,” alisema memba huyo wa familia.

Kwa upande wake Hamisa, habari zilizolifikia Ijumaa Wikienda katika dakika za lala salama kuelekea kiwandani zilidokeza kuwa, mrembo huyo kwa sasa ameamua kumuhudumia mwanaye mwenyewe na kwamba, maandalizi ya shughuli ya 40 ya kumtoa mtoto wake huyo yamepamba moto. Stori: Imelda Mtema | Ijumaa Wikienda

Comments

Popular posts from this blog