Posts

Watumishi wa zahanati mbili wote feki"

Image
Mbunge wa Mchinga (CUF), Hamidu Bobali amefunguka na kusema zahanati mbili katika halimashauri yao zimefungwa kutokana na watumishi wake wote kukutwa na vyeti feki, jambo ambalo linapelekea wananchi katika kata hizo kukosa huduma.  Mbunge wa Mchinga (CUF), Hamidu Bobali. Hamidu Bobali alisema hayo jana bungeni na kusema sakata la vyeti feki limeleta athari katika halimashauri yao "Hili suala la vyeti feki Mh. Mwenyekiti limeleta athari kubwa sana katika halimashauri yetu, hivi hapa napoongea kuna zahanati mbili zote zimefungwa kutokana na ukweli kwamba watumishi wake wote wameonekana na vyeti feki" alisema Hamidu Bobali  Mpaka sasa sakata la vyeti feki limeanza kuleta athari katika baadhi ya maeneo baada ya watumishi wengine kuamua kujiondoa wenyewe makazini kama amri ya Rais Magufuli ilivyoagiza kuwa wajiondoe wenyewe na kuachia nafasi hizo. 

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AFUNGUA KUTANO WA ROTARY CLUB ARUSHA

Image
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akivishwa beji ya uanachama wa Rotary Club na Dk. Manoj Desai kwenye mkutano wa 92 wa mwaka unaojumuisha nchi za Uganda na Tanzania (District 9211) katika ukumbi wa AICC jijini Arusha Mei 4, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Rotary Club kwenye mkutano wa 92 wa mwaka unaojumuisha nchi za Uganda na Tanzania (District 9211) katika ukumbi wa AICC jijini Arusha Mei 4, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akifungua mkutano wa 92 wa mwaka wa Rotary unaojumuisha nchi za Uganda na Tanzania (District 9211) katika ukumbi wa AICC jijini Arusha Mei 4, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) Washiriki wa Mkutano mkutano wa 92 wa mwaka wa Rotary unaojumuisha nchi za Uganda na Tanzania (District 9211) wakishangilia mara baada ya Waziri Mkuu kutangaza kuwa yeye na mke wake, Mary Majaliwa wanajiunga na Rotary Club katika ukumbi wa AIC

Faida za kutumia juisi ya miwa katika kuimarisha afya zetu

Image
Bila shaka unaifahamu juisi ya miwa, watu wengi tumekuwa tunakunywa na wengine tukiwa tunaibeza pia, hii ni kwasababu tumekuwa hatujui faida zitokanazo na unywaji wa huisi hiyo. Leo nataka nikupashe japo kwa uchacje faida za kunywa juisi ya miwa katika afya zetu. Kunafaida nyingi za juisi ya miwa. Baadhi ya faida hizo ni kama zifuatazo; 1. Juisi ya miwa inauwezo mkubwa wa kuipatia miili nguvu kwa haraka na kukata kiu ya maji.  Hii ni kwa sababu juisi ya miwa ina sukari "sucrose" ambayo kazi yake kuu ni kutengeneza nguvu mwilini. Kwahiyo wakati mwingine ukiwa na nguvu au uchovu, badala ya kunywa vinywaji vya viwandani tafuta juisi ya miwa. 2.  Husaidia figo kufanya kazi vizuri. Juisi ya miwa inasaidia kuongeza kiwango cha protein mwilini na ku-imarisha ufanyaji kazi wa figo. Juisi a miwa iliyochanganywa na maji ya Nazi husaidia kupunguza maumivu hasa yanayosababishwa  na mawe yaliyopo kwenye figo. 3. Hupunguza uwezrkano wa kupata ugonjwa wa kansa. Ju

MFAHAMU JOHN STEPHEN ,MTANZANIA MAARUFU ULIMWENGUNI KULIKO HAPA TANZANIA

Image
John Steven Akhwari ni mwanariadha mstaafu. Alizaliwa mwaka 1938 kule Mbulu- Mkoani Manyara. Aliiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Olimpic mwaka 1968 nchini Mexico, katika mashindano ya riadha ya kilomita 42. Washiriki walikuwa 75, lakini waliomaliza shindano ni 57 pekee, huku John Steven Akhwari akimaliza wa mwisho kabisa. Kwa nini alimaliza wa mwisho?   Baada ya mbio kuanza, walipofika kilomita ya 19, mshiriki mojawapo alimparamia, kumsukuma na kuanguka vibaya mno. Aliumia begani, na goti la mguu wa kulia lilitenguka. Gari la huduma ya kwanza lilimfikia na kumpa matibabu, akaweza kusimama tena na kuendelea na riadha. Umaarufu wake duniani. Watu waliomhudumia walimlazimisha kuaihirisha shindano na apande kwenye gari lakini alikataa katakata. Aliendelea na riadha huku akichechemea. Alifanikiwa kumaliza kilomita zote 42, jioni ya saa 1 kwa saa za Mexico. Watu wachache waliokuwa wamebakia uwanjani walimshangilia sana. Mwishoni kabisa, waandishi wa habari

Kiama kingine cha Majina wenye vyeti feki J’tano

Image
WAKATI watumishi wa umma 9,932 wakiwa wamebainika kuwa na vyeti feki mpaka sasa, idadi hiyo inatarajiwa kuongezeka Jumatano ijayo, siku ambayo Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi itatangaza majina zaidi. Ijumaa iliyopita, serikali ilitangaza kukamilika kwa zoezi la uhakiki wa vyeti vya kuhitimu kidato cha nne, sita na ualimu kwa watumishi wa Sekretarieti za Mikoa, Tawala za Mikoa, Wakala wa Serikali, Taasisi za umma na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dk. Laurean Ndumbaro, alisema uhakiki wa vyeti unaendelea kwa watumishi wa wizara zilizosalia na taasisi mbalimbali. Alisema uhakiki huo wa awamu ya pili na ambao utafuatiwa na awamu ya tatu, unatarajiwa kukamilika Jumatano. Alisema baada ya matokeo ya uhakiki huo kuwekwa hadharani, uamuzi wa serikali utatolewa. “Maamuzi ya watumishi 9,932 waliobainika kuwa na vyeti vya kugushi ili

WAZIRI LUKUVI AMTUMBUA AFISA MIPANGO MIJI LINDI

Image
  Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akimsimamisha kazi  Ndugu Castory Manase Nkuli Afisa Mipango Miji wa Lindi kuhusu tuhuma za kumilikisha ardhi kinyume cha sheria. Na. Hassan Mabuye & Muhammad Salim Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi ameamuru kusimamishwa kazi Afisa Mipango Miji wa Lindi Ndugu Castory Manase Nkuli baada ya kunyang`anya ardhi ya vijiji vya Ruvu na Mchinga hekari 4000 na kumilikisha kampuni ya Azimio Housing Estate kinyume cha sheria ya Ardhi. Mhe. Lukuvi aligundua hayo baada ya kuona utaratibu wa umilikishaji wa ardhi haukufuatwa  na badala yake kuonekana kuwa na mianya ya rushwa kwa kuwa ardhi hiyo imehamishwa kutoka ardhi ya kijiji hadi kumilikishwa kwa kampuni ya Azimio ambapo kisheria ilitakiwa hati ya eneo hilo itoke kwa idhini ya Rais. Aidha, Afisa Mipango Miji huyo aligundulika kuwa na kosa la kughushi kwa kujifanya ni Afisa ardhi baada ya kuandika barua na kuisai

JB RAY NA RICH WAFUNGUKA MAZITO KUHUSU TUHUMA ZA KUHONGWA VIWANJA NA PESA

Image
Baada ya kuwepo kwa madai kuwa mastaa wa filamu Bongo, Jacob Steven (JB), Single Mtambalike (Rich) na Vincent Kigosi (Ray) walihongwa fedha na viwanja ili ‘kuinjinia’ maandamano ya hivi karibuni kupinga sinema za nje, mastaa hao wamebanwa na hatimaye kufungukia ishu hiyo inayowatafuna, Risasi Mchanganyiko lina mkanda kamili. Chanzo kilicho karibu na tasnia hiyo kililiambia Risasi Mchanganyiko kuwa kampuni moja ya usambazaji filamu (jina kapuni kwa sasa), iliwapa fedha baadhi ya waigizaji ili wafanye maandamano ya kuziondoa sokoni filamu hizo za nje, zinazodaiwa kukingiwa kifua na Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania, Simon Mwakifwamba. Inadaiwa kuwa baada ya kampuni hiyo ya usambazaji ‘kupenyeza sumu hiyo’ waigizaji hao walikwenda kwa kigogo mmoja wa kisiasa na kumshawishi kuwaunga mkono, ambaye naye alikubali na kuwaomba waigizaji hao kufanya kila wawezalo, kumtoa kwenye kiti chake, Simon Mwakifwamba, kwani ana ukaribu na hasimu wake wa siasa. “Kuna watu w

Hali ya Mbunge wa Chadema Tarime si Shwari

Image
Hali ya Mbunge wa Tarime Vijijini Mh. John Heche imebadilika usiku wa kuiamkia leo na amekimbizwa hospitalini Dodoma.  Huenda akahamishiwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Tumuombee comrade Heche na pole sana kwa familia na wabunge wenzake.

SPIKA JOB NDUGAI ATOA MAANA YA "FALA"BUNGENI

Image
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Job Ndugai jana ameonyesha aliumizwa na kitendo cha Mbunge wa Kawe kwa tiketi ya CHADEMA Mh. Halima Mdee kumwambia 'fala' bungeni na kusema hata kama mtu humpendi lakini si vyema kumtusi matusi. Job Ndugai alisema hayo alipokuwa akitoa maana ya neno fala bungeni ambapo ilibidi arejee maana hiyo kwa kusoma kupitia kamusi ya Kiswahili ambayo ilitoa maana kuwa fala ni mtu ambaye akili zake hazifanyi kazi vizuri. "Kwa neno ambalo alilisema Halima Mdee humu ndani, kamati imeenda kwenye tafsiri ikachukua Kamusi kwa neno lile alilosema ambalo maana yake kwa yule unayemwambia 'Fala' ni mtu ambaye akili zake hazifanyi kazi vizuri, ni mtu mpumbavu, ni mtu bwege, ni mtu mjinga, ni mtu bozi, ni gulagula. Ndiyo maana nikasema sisi Waafrika hata kama humpendi namna gani mwenzako huwezi kumfanyia hivyo"  alisisitiza Job Ndugai

Dk Mwakyembe: Televisheni, Redio kusoma vichwa vya habari tu kwenye magazeti kuanzia kesho

Image
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe   Mwanza.Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe amezitaka Televisheni na Redio kuanzia kesho kusoma vichwa vya habari vya magazeti tu ili kuwavutia wasomaji kununua magazeti kwa habari kamili. Dk Mwakyembe amesema hayo leo jijini Mwanza katika maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari nchini ambapo pia amesema ataendelea kutetea na kulinda haki za waandishi wa habari huku akiwahakikishia ulinzi waandishi wa habari za uchunguzi. Pamoja na mambo mengine Dk Mwakyembe amehakikisha kuwepo kwa ushirikiano wa kutosha kwa wamiliki wa vyombo vya habari  na kwamba ameagiza idara ya mawasiliano kutengeneza mawasiliano ya kudumu na wawe wanakutana angalau mara moja kwa mwezi kujadili udhaifu unaoweza kujitokeza na kuchukua hatua lengo ni kuwekana  sawa.

SAMATTA AMEANZA KUIKAMATA KRC GENK, SHABIKI AINGIA NA BANGO AKIOMBA JEZI

Image
Ukisema mambo yanaanza kunyooka, baada ya mashabiki wengi wa KRC Genk kuonyesha imani kubwa kwa mshambulizi, Mbwana Samatta.Samatta anaonekana kuwa bora zaidi kutokana na kuwa tegemeo katika kikosi cha Genk cha Ubelgiji.Imeonekana mmoja wa shabiki akiwa na bango uwanjani, akiomba jezi ya Samatta.Imekuwa kawaida kwa mashabiki wa Ulaya kuomba jezi kwa wachezaji wanaowapenda wakitumia mabango kama shabiki huyo wa Genk. Samatta amekuwa akifunga mfululizo na wakati mwingine kushindwa kufanya hivyo kwa kipindi fulani lakini imani kwa benchi la ufundi na mashabiki inaonekana kupanda kwa kiwango cha juu kabisa.

CHADEMA wateua majina mapya ya Wagombea wa Bunge la Afrika Mashariki

Image
Chadema wafanya uteuzi wa wagombea Ubunge EALA.   Tazama majina yao: 

Faida za Mchaichai kiafya

Image
Faida za mchachai zipo nyingi sana wengi wetu hudhani mchaichai ni kuongo cha kuweka kwenye chai pekee, au ni dawa kwa ajili ya kuua mbu pekee, ila mchaichai huwa na faida lukuki zaidi ya hizo tu. Naomba uweze kusoma makala haya ili uone faida nyinginezo za mchaichai. Zifuatazo ni faida za kutumia mchaichai kiafya. 1. Mchaichai ni kinga dhidi ya saratani. Tafiti mbalimbali zimeonyesha kuwa kwenye kila gram 100 ya mchaichai, kuna viondosha sumu ambavyo vina uwezo wa kuukinda mwili dhidi ya ugonjwa wa saratani. Mwaka 2006, timu ya watafiti kutoka Chuo kikuu cha Gurion, Israel waligundua mchaichai un uwezo wa kuua seli zinaweza kusababisha saratani. 2. Hutibu magonjwa ya kuhara. Husaidia umeng’enyaji wa chakula Chai ya mchaichai hurahisisha utaratibu wa mmeng’enyo wa chakula na pia hutibu magonjwa ya kuhara na maumivu ya tumbo ikiwamo kujaa gesi. Hurahisisha utaratibu wa kuondoa uchafu mwilini Katika matibabu, unatibu magonjwa mengi ikiwemo kushusha joto, hasa

BAJETI YA WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO YAPITISHWA

Image
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (katikati), akimsikiliza Katibu Mkuu (Sekta ya Ujenzi), Eng. Joseph Nyamhanga (Kulia), mara baada ya kumaliza kuwasilisha Bajeti ya Wizara hiyo kwa mwaka wa Fedha 2017/2018. Kushoto ni Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Eng. Deusdedit Kakoko. Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akipongezana na Watendaji wa Wizara hiyo mara baada ya kumaliza kuwasilisha Bajeti ya Wizara hiyo kwa mwaka wa Fedha 2017/2018. Watendaji wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano wakipongezana mara baada ya Bunge la Bajeti kupitisha Bajeti ya Wizara hiyo kwa mwaka wa Fedha 2017/2018. Mtendaji Mkuu Wa Shirika la Reli Nchini (TRL), akizungumza na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bw. George Masaju mara baada ya Bunge la Bajeti kupitisha Bajeti ya Wizara hiyo kwa mwaka wa Fedha 2017/2018. Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasilia

KAULI YA EMMANUEL MBASHA BAADA YA FLORA KUOLEWA TENA

Image
Mwimbaji wa nyimbo za Injili nchini Tanzania, Emmanuel Mbasha, ambaye alikuwa mume wa Flora ameweka wazi kuwa hana shida na Mume mpya wa madam Flora Daudi Kusekwa.  Kupitia eNewz ya EATV, Emmanuel Mbasha amesema kuwa hana shida na mume mpya wa Flora kwani yeye hamfahamu na kama akikutana naye hawezi kumfanya lolote maana huyo mtu hakuwahi kumuingilia katika ndoa yake, ila Mbasha akasema mtu ambaye yeye anamchukia ni yule aliyeingilia ndoa yake ambaye Watanzania wanamjua. "Sijaona kama nimepungukiwa, jamaa ambaye amemuoa Flora sina shida naye, anaweza kuwa mtu ambaye ananihofia kuwa nikikutana naye naweza kumdunda. Ila huyo jamaa mimi simchukii na wala simjui.Hajawahi kuniingilia kwenye issue yangu yoyote ya mapenzi ila mimi namchukia jamaa ambaye aliniingilia kwenye ndoa yangu ndiye mbaya wangu, na Watanzania wote wanamjua." Alisema Emmanuel Mbasha.  Mbali na hilo Emmanuel Mbasha alisema kuwa Flora amemkimbia kutokana na maisha aliyoyachagua lakini si

Spika aziweka rehani ajira watumishi Bunge

Image
SPIKA WA BUNGE, JOB NDUGAI. SPIKA wa Bunge, Job Ndugai, ametishia kuwafukuza kazi watumishi wanne wa Bunge wanaofanya kazi kwenye ofisi za Kambi Rasmi ya Upinzani ikiwa wataendelea kuandika hotuba alizoziita zenye maneno machafu dhidi ya uongozi wa Bunge. Aliyasema hayo bungeni jana wabunge walipoazimia kuwasamehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Alexander Mnyeti, Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema) na Mbunge wa Bunda Mjini, Ester Bulaya (Chadema) waliokutwa na hatia ya kukidharau chombo hicho cha kutunga sheria. Ndugai mbali na kuipongeza Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kwa kazi nzuri ya kuwahoji viongozi hao waliolalakiwa, alisema amebaini kuna ‘mchezo mchafu’ dhidi ya uongozi wa Bunge unaofanywa na wanaoandika hotuba za upinzani. Alisema hotuba kadhaa za upinzani zimekuwa na maneno yanayoashiria kudharau Bunge, hasa Kiti cha Spika. “Nimefanya utafiti wangu. Kw

KAJALA MASANJA AIBUKA TENA,SASA AMWANIKA MWANAUME WA KUMUOA

Image
MUIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Kajala Masanja, amefunguka kuwa, endapo ataolewa tena, basi kigezo cha kwanza cha huyo mtarajiwa wake kitakuwa ni kudekezwa. Kajala ambaye aliolewa kisha ndoa yake kupata matatizo na mumewe kufungwa gerezani na hivi karibuni kuachiwa, alisema endapo itatokea ameolewa kwa mara nyingine basi kigezo cha huyo mwanaume ni lazima awe anayejua kudekeza. “Nampenda mwanaume mwenye mapenzi ya kweli lakini zaidi ya yote mimi napenda kudekezwa hivyo mwanaume atakayenioa lazima awe na sifa hizo vinginevyo atanisikia kwenye bomba,” alisema Kajala huku akiomba asimzungumzie mumewe ambaye ametoka gerezani hivi karibuni.

Lissu akomalia vyeti vya Bashite kortini

Image
WAWKILI Tundu Lissu na wenzake wa Chama Cha Wanasheria Tanganyika (TLS) wamelikomalia vilivyo sakata maarufu la Bashite linalohusiana na tuhuma za kughushi vyeti vya kielimu linalomkabili mmoja wa wakuu wa mikoa kwa kulifikisha kortini ili lipatiwe ufumbuzi. Aidha, Lissu na wenzake hao wamedhamiria kuona kuwa kigogo huyo anayetuhumiwa kuliacha jina lake halisi la Daudi Albert Bashite kutokana na matokeo mabovu ya sekondari na kutumia jina la mtu mwingine, achukuliwe hatua za kisheria ikiwamo kufungwa jela kwa kosa la kughushi ikiwa itathibitika kuwa ana hatia. Akizungumza jana na waandishi wa habari mjini Dodoma jana, Lissu ambaye ni Rais wa TLS, alisema uamuzi huo wa kulifikisha mahakamani suala la Bashite umetokana na maazimio ya baraza la uongozi la chama hicho, lengo likiwa ni kulinda utawala wa sheria na uwajibikaji nchini. Tofauti na matarajio ya baadhi ya watu, sakata hilo la Bashite halikupatiwa jibu kutokana na ripoti ya uhakiki wa vyeti vy

Tujikumbushe :Hotuba ya Mwalimu Julius K. Nyerere Aliyitoa kwwenye Mei Mosi 1995

Image
Mwalimu Nyerere alialikwa kuwa Mgeni Rasmi kwenye kilele cha Sikukuu ya Wafanyakazi Duniani iliyofanyika kitaifaUwanja wa Sokoine Mjini Mbeya Mei 1, 1995. Katika hotuba yake, Mwalimu alielezea historia ya Vyama vya Wafanyakazi duniani. Aidha alitumia fursa hiyo kutoa maoni yake kuhusu hali ya kisiasa na kiuchumi nchini pamoja na ushauri kuhusu mambo ambayo wananchi wanapaswa kuzingatia wakati wa Uchaguzi Mkuu mwezi wa Oktoba mwaka ule. Hasa sifa za wagombea nafasi za uongozi kuwa ni pamoja na kila mmoja kujiuliza ataifanyia nini nchi yake baada ya kuchaguliwa na anakwenda kufanya nini Ikulu? Ifuatayo ni hotuba ya Mwalimu. Ni muhimu kukumbuka kuwa hotuba hii imefuata mlolongo wa mazungumzo ambayo Baba wa Taifa alikuwa nayo kwa wananchi katika maeneo mbalimbali ambapo alikuwa anajaribu kuamsha dhamira ya viongozi wetu wa wakati ule. Hotuba hii ni miongoni mwa hotuba ambazo ukweli wa hoja zake ni hazina kubwa kwa vizazi vijavyo vya Watanzania. Mwenyekiti wa OTTU, Vi