Posts

Kesi ya Madawa: Shahidi Afunguka Alichokikuta Chumbani kwa Wema

Image
Msanii wa filamu, Wema Sepetu (katikati) akiwa na mama yake mzazi Miriam Sepetu (kulia)  wakitoka kusikiliza kesi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. Mama mzazi wa Wema Sepetu akishuka ngazi za mahakama baada ya kusikiliza kesi inayomkabili mwanaye. Wema Sepetu na mama yake, Miriam Sepetu  wakijadili jambo baada ya kusikiliza kesi nje ya mahakama. MJUMBE wa Shina Namba 39, nyumbani anakoishi msanii wa filamu, Wema Sepetu, Steven Alphonce ambaye ni shahidi katika kesi inayomkabili staa huyo, amedai wakati wa upekuzi walikuta kipande cha sigara wala si bangi. Alphonce amesema hayo leo Jumatatu, Machi 12, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba akiongozwa na Wakili wa Serikali, Constantine Kakula, wakati akitoa ushahidi wake katika kesi ya matumizi ya dawa za kulevya inayomkabili Wema na wenzake wawili na kusema alishiriki katika upekuzi nyumbani kwa Wema na kukuta kipande hicho cha sigara jikoni na chumbani kwa

ASLAY HATIMAYE AANIKA UKWELI KUHUSU KUTOKA NA NANDY,AFICHUA YOTE

Image
Msanii wa muziki Bongo, Aslay amefunguka kuhusu ukaribu wake na Nandy kwa sasa. Muimbaji huyo wa ngoma ‘Natamba’ ameiambia FNL ya EATV kuwa kinachowaunganisha ni kazi tu hakuna mahusiano ya kimapenzi kama inavyokuwa ikiripotiwa. Nafikiri mashabiki zangu ambao wananifuatilia wanajua ni mtu ambaye nina mtoto, kuna mwanamke ambaye nimezaa naye. Nandy tupo kwenye kazi tu, tunafanya lakini hamna chochote kinachoendelea kati yangu na Nandy,” amesema. Aslay na Nandy kwa sasa wanafanya vizuri na ngoma ‘Subalkheri’ ikiwa ni ngoma yao ya pili kutoa pamoja baada ya Mahabuba.

MAUWAJI YA KUTISHA TENA ,MTOTO ATEKWA NA KUUAWA KINYAMA

Image
MASKINI MTOTO HUYU! Atekwa na Kuuawa, Mama Mzazi Hoi! Maskini mtoto wa watu! Ndivyo walivyosikika mashuhuda wa tukio la mwanafunzi, Doricka Majeshi, anayesemekana kutekwa kisha kukutwa akiwa ameuawa na watu wasiojulikana ndani ya nyumba inayoendelewa kujengwa na kuibua simanzi nzito. Kwa mujibu wa mashuhuda hao, mtoto Doricka mwenye umri wa miaka nane aliyekuwa anasoma darasa la kwanza katika shule ya msingi ya Lukobe mjini hapo alidaiwa kukutwa na mkasa huo tangu Jumanne ya wiki iliyopita kisha kusakwa kwa siku tatu bila mafanikio, kabla ya mwili wake kukutwa ukiwa na majeraha Alhamisi iliyopita nyuma ya nyumba hiyo

Naibu Katibu Mkuu wa BAVICHA Ajiuzuru

Image
Naibu Katibu Mkuu Baraza la Vijana Chama cha Demokrasia na Maendeleo – Chadema (BAVICHA), Getrude Ndibalema amesema amejiuzuru nafasi hiyo na kubaki mwanachama wa kawaida ili kutimiza majukumu binafsi.

WAZIRI MWAKYEMBE AFUNGUA MKUTANO WA 14 WA MAAFISA HABARI, MAWASILIANO NA UHUSIANO SERIKALINI

Image
    Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe akizungumza na Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano Serikalini wakati wa ufunguzi mkutano wa 14 wa kikao kazi cha Maafisa hao kilichoanza leo Jumatatu tarehe 12-16 Machi, 2018 Jijini Arusha. Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Susan Mlawi akizungumza na Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano Serikalini wakati wa ufunguzi mkutano wa 14 wa kikao kazi cha Maafisa hao kilichaonza leo Jumatatu tarehe 12-16 Machi,2018 Jijini Arusha.  Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) nchini, Alvaro Rodriguez akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kikao Kazi cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini kilichaonza leo Jumatatu tarehe 12-16 Machi,2018 Jijini Arusha.  Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Gabriel Daqqaro akuzungmza na Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano Serikalini wakati wa ufunguzi mkutano wa 14 wa kikao kazi cha Maafisa hao kilich

Man United Vs Liverpool, Salah Aundiwa Tume Manchester Utd

Image
Kiungo mshambuliaji wa Liverpool, Mo­hamed Salah (kulia) Paul Labile Pogba. MANCHESTER United inatarajiwa kuwa mwe­nyeji wa Liverpool, ke­sho Jumamosi kwenye Uwanja wa Old Trafford, mchezo huo ni mkubwa na unasubiri­wa kwa hamu. Kuelekea mtanange huo, gumzo kubwa ni juu ya uwezo wa kiungo mshambuliaji wa Liverpool, Mo­hamed Salah ambapo mashabiki wa Unit­ed wameanza kupata hofu kuhusu mchezaji ambaye atamzuia. Kawaida Salah amekuwa akipangwa kushambulia akitokea kulia, kwa aina ya ulinzi wa United beki wa kushoto am­baye atatakiwa kukutana naye ni Ashley Young au Luke Shaw, sasa hapo ndipo patamu, imeibuka hoja juu ya nani mwe­nye uwezo kati yao anayeweza kumficha Salah. Mchezo uliopita timu hizo zilipoku­tanaa ulimalizika kwa suluhu, huku Mar­teo Darmian akipangwa kucheza beki wa kushoto, kwa sasa beki huyo siyo chaguo la kwanza la Kocha Jose Mour­inho. Kutokana na ubora wa Salah kufun­ga, mashabiki wa United kutoka mataifa mbalimbali wamepaza sauti wa

Rais Kenyatta, Odinga Waahidi Kuwaunganisha Wakenya

Image
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta (kushoto) akiwa na kiongozi wa muungano wa upinzani nchini humo Raila Odinga. RAIS wa Kenya Uhuru Kenyatta amekutana na kiongozi wa muungano wa upinzani nchini humo, Raila Odinga, katika ofisi yake ya Jumba la Harambee, Nairobi,a mba po viongozi hao kwa pamoja wamekubaliana kuunda taifa lenye umoja. “Tumekubaliana tutawaleta pamoja wananchi na kujadiliana kuhusu matatizo yanayoathiri taifa letu na wananchi, na kuunda taifa lenye umoja na lililo imara ambapo hakuna raia anayehisi ametengwa,” alisema Rais Kenyatta baada ya mkutano huo. “Tumekutana na ndugu yangu Kenyatta, tumeongea kwa kirefu na kukubaliana kwamba tunataka kuiunganisha Kenya iwe taifa moja. Mgawanyiko ambao umekuwepo tangu uhuru utakwisha  na sisi tutembee pamoja,” alisema Raila Odinga katika hafla hiyo.

AJALI MBEYA: Wanne Wafariki Dunia, 20 Wajeruhiwa Vibaya

Image
MBEYA: Watu wanne wamefariki dunia na wengine zaidi ya 20 kujeruhiwa baada ya basi la Kampuni ya Super Rojas kugongana na lori jana Machi 8, 2018 katika eneo la Igawa wilayani ya Mbarali mkoani Mbeya. Ajali hiyo imetokea katika barabara inayounganisha mikoa ya Mbeya na Iringa, baada ya basi hilo lenye namba za usajili T 170 DKS lililokuwa likitoka Mbeya kwenda Njombe kugongana na lori lenye namba za usajili T 838 DRE aina ya Scania lililokuwa limebeba kontena. Kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo,  chanzo cha ajali ni dereva wa basi aliyekuwa akijaribu kulikwepa tawi la mti lililokuwa limeegeshwa barabarani kama ishara ya kuonyesha kuwepo kwa gari bovu mbele yake.

Rais Magufuli awaonya wanaotaka kufanya maandamano

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John  Magufuli amevionya vyama vya siasa na wananchi ambao wamepanga kufanya maandamo siku za hivi karibuni kwa mujibu wa taarifa ambazo zimekuwa zikisambaa mitandaoni. Amesema hayo leo, Machi 9, 2018 wakati akizindua Tawi la CRDB-Bank, Chato mkoani Geita na kuwataka waliojiandaa kutekeleza mpango waache mara mora vinginevyo watashughulikiwa. “Nchi hii ni ya amani, ndiyo maana uvunjifu wa amani ulipoanza kutokea kule Kibiti tuliamua kuufuta mara moja. Kuna watu wanadhani tunafanya siasa kila wakati, kama wametumwa na baba zao kuandamana, watawasimulia vizuri.  “Wapo Watanzania wachache ambao hawapendi kuambiwa ukweli, wanapenda kuambiwa maneno matamu. Mimi niliomba kura kwa wananchi wangu kwa kusema ukweli, nitaendelea kusisitiza ukweli daima,” alisema Magufuli. Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB, Dkt. Charles Kimei ameeleza kwamba uanzishwaji wa Tawi la Benki hiyo Chato ni kutokana na utafiti uliofan

Wakali Wanne wa Kimataifa Waitwa Taifa Stars

Image
KOCHA wa Timu ya Taifa ya Soka Tanzania (Taifa Stars), Salum Mayanga, leo Machi 8, ametaja majina ya wachezaji 23 watakaoingia kambini kwa ajili ya michezo miwili ya kirafiki mwezi huu. Katika orodha hiyo aliyoitaja asubuhi hii kwenye makao makuu ya shirikisho la soka nchini TFF Karume Ilala, Mayanga amewajumuisha kikosini nyota wanne wa kimataifa akiwemo nahodha Mbwana Samatta, Thomas Ulimwengu anayechezea klabu ya AFC Eskilstuna ya Sweden, Mlinzi wa Baroka FC ya Afrika Kusini, Abdi Banda na Faridi Mussa anayechezea Club Deportivo Tenerife ya Hispania. Katika majina hayo 23, Simba imechangia wachezaji 6, Yanga ikitoa wachezaji 5 huku nahodha wa Singida United, Mudathir Yahya naye akijumuishwa kikosini. Taifa Stars inatarajia kucheza michezo miwili ya kirafiki ikianzia ugenini nchini Algeria, Machi 22 dhidi ya wenyeji, The Greens kabla ya kurejea nyumbani, Dar es Salaam kuwakaribisha DR Congo, Machi 27, katika Uwanja wa Taifa.

Naibu Wazri Ikupa atekeleza ahadi yake

Image
Naibu Waziri wa sera, Bunge, Kazi, vijana, ajira na walemavu, Mh. Stella Ikupa leo amefanya ziara ya ya kutembelea shule ya Sekondari Jangwani, Uhuru Mchanganyiko na Pugu jiji Dar es salaam na kukabidhi  vifaa mbalimbali kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu  . Katika ziara hiyo Mh, Ikupa ametoa Magongo ya kutembelea, viti mwendo, fimbo nyeupe kwa wasiona, miwani ya jua, kofia, lenzi za kusomea kwa watu wenye uono hafifu, na ualubino ili kutatua changamoto kwa kundi hilo maalumu. Naibu Waziri wa sera, Bunge, Kazi, vijana, ajira na walemavu Mh Stella Ikupa akimkabidhi baiskeli mwendo mwanafunzi wa Pugu Sekondari Naibu Waziri  Ikupa amesema kama Serikali tunatambua changamoto hizi hivyo tunajitahidi kukabiliana nazo na kidogo kinachopatikana tunakigawa kwa kila mmoja ili kupunguza matatizo haya kidogokidogo na mwisho wa siku yataisha. Pia serikali hii inayoongozwa na Rais Magufuli itaendelea kutennga fedha kwa ajili ya kuendeleza kuwahudumia watoto weny

Manyara: Mbunge CCM Ahojiwa Sentro kwa Amri ya DC

Image
MBUNGE wa Jimbo la Hangang kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Mary Nagu amehojiwa katika Kituo Kikuu cha Polisi kwa amri ya Mkuu wa Wilaya hiyo, Sara Ali,  kwa kile kinachodaiwa kukaidi amri halali ya DC ya kuzuia mikutano ya mbunge huyo. Inadaiwa Nagu na Mwenyekiti wa CCM Wilaya, Mathew Darema, waliwekwa ndani kwa saa kadhaa juzi kabla ya kuhojiwa. Ikumbukwe kuwa, hii ni mara ya pili sasa kwa tukio kama hili kujitokeza kwa  Nagu wilayani humo ambapo Mara ya kwanza DC Sara aliwafikisha polisi Katibu wa CCM Wilaya na Mbunge wake kwa madai kuwa walifanya fujo katiika Kikao cha Kamati ya Siasa cha Wilaya. CREDIT: JF

AJIRA SERIKALINI: MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA (NHIF)- INTERNAL AUDITOR II

Image
INTERNAL AUDITOR II – 2 POST Employer:  Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Date Published:  2018-03-05 Application Deadline:  2018-03-19 JOB SUMMARY: N/A DUTIES AND RESPONSIBILITIES: i. Participates in audit assignments of the Fund, including pre auditing of providers’ claims and Board claims/payments; ii. Assists to inspect validity of vouchers, receipts, payments, cheque registers and their respective source documents; iii. Assists to check bank reconciliation statements; iv. Assists in auditing journals and other accounting entries; v. Participates in inspection of goods/stocks received and verifies stock records in the store; vi. Assists in performing all his day to day duties as stipulated and specified in the job description of that position; vii. Assists to review imprests retired, checking adherence to imprests regulations, validity of receipts (if any) and performing any other related clerical works; and viii. Performs any other related duties a

AJIRA SERIKALINI: Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF)- ACCOUNTANT II

Image
ACCOUNTANT II – 1 POST Employer:  Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Date Published:  2018-03-05 Application Deadline:  2018-03-19 JOB SUMMARY: N/A DUTIES AND RESPONSIBILITIES: Accountant II– Expenditure i. Ensures that all payments are made in accordance with financial regulations and approved budget; ii. Maintains Zonal administrative imprest accounts and ensures timely refunds and replenishments; iii. Oversees the management of the petty cash account; iv. Oversees maintenance of the non-current assets register; v.  Prepares financial statements; vi. Prepares periodic reports on the status of expenditure; vii. Administers and maintains non-current assets register; viii. Maintains subsidiary legers for staff loans; ix. Monitors imprest returns from Zonal offices and takes corrective actions whenever necessary; x. Maintains ledgers for imprest; xi. Monitor and control of salary advances; xii. Deals with all issues pertaining to replenishing funds at

Breaking News:Abdul Nondo apatikana Mafinga mkoani Iringa

Image
Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo, ambaye pia ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) aliyekuwa hajulikani alipo tangu usiku wa kuamkia jana na kuacha ujumbe usemao “I AM AT HIGH RISK”, amepatikana Mafinga mkoani Iringa. Mkurugenzi wa Idara ya Sheria ya Mtandao wa Wanafunzi Tanzania, Paul Kisabo amesema  kwamba Abdul Nondo amepatikana mkoani Iringa katika wilaya ya Mafinga jana jioni baada ya kuzinduka na kujikuta ametupwa barabarani. “Nondo amepatikana Mafinga katika Kituo cha Polisi hivi punde, amezinduka na kujikuta akiwa ametupwa, akauliza watu eneo alipo ndipo wakamwambia yupo Mafinga, amejikokota na kuelekea kituo cha polisi kuripoti. “Kilichomsaidia alikuwa anakumbuka namba mojaya dada yake ambayo alikuwa ameikariri kichwani, ikabidi aombe simu polisi, kumpigia dada yake ambaye naye alijulisha baba yake mdogo aliyepo Dar es Salaam kuwa ndugu yao amepatikana. “Nondo ameongea na baba yake mdogo kupitia simu ya polis

Kikosi cha Simba dhidi ya Waarabu Leo

Image
KOCHA Mkuu wa Simba, Mfaransa, Pierre Lechantre, tayari ameshakipanga kikosi chake ambacho kitaanza leo Jumatano kwenye mchezo wao dhidi ya Al Masry ya Misri, huku akiwapa jukumu zito la kufunga mabao washambuliaji wake, Emmanuel Okwi na John Bocco. Mchezo huo utakaopigwa kwenye Uwanja wa Taifa ni wa raundi ya kwanza ya Kombe la Shirikisho Afrika na utaanza majira ya saa 12 jioni, ingawa Lechantre hakufura­hishwa na muda huo uliopangwa na viongozi. Katika mazoezi ya juzi Jumatatu yaliyoanza majira ya saa 12 jioni kwenye Uwanja wa Boko uliopo jijini Dar, Championi lilimshuhudia Lechantre akipanga kikosi chake kilichoonekana ndicho cha maan­gamizi ambacho kitatumika kum­maliza Mwarabu leo. Katika kikosi hicho ambacho golini yupo Aishi Manula, walinzi wake ni Shomary Kapombe, Asante Kwasi, Erasto Nyoni, Yusuf Mlipili na James Kotei. Kwenye kiungo wapo; Jonas Mkude, Nicholaus Gyan, Shiza Kichuya, Bocco na Okwi. Katika ma­zoezi hayo yaliyomalizika saa 1:30 usiku, kocha huyo

Mwenyekiti Mtandao wa Wanafunzi Hajulikani Alipo

Image
TAARIFA zilizoenea mchana huu zinadai kuwa Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo, ambaye pia ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) anadaiwa kupotea katika mazingira ya kutatanisha na hajulikani alipo tangu jana saa sita usiku. Marafiki za Nondo wamedai alituma ujumbe kwa viongozi wenzake wa TSNP kuwa yuko katika hatari na baada ya kutuma ujumbe huo simu yake ilikuwa ikipokelewa lakini hakuwa akiongea chochote, na baada ya muda alianza kujiondoa kwenye magroup ya WhatsApp. Taarifa kutoka kwa mmoja wa viongozi wa TSNP kuhusu Nondo inasema hajulikani alipo wakiwemo wazazi wake.   Viongozi wa TSNP wamefika Kituo cha Polisi kilichopo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM) na  kutoa taarifa za kupotea kwake. Feb 18, 2018, Nondo alijitokeza na kuikosoa mienendo ya Jeshi la Polisi na Waziri wa Mambo ya Ndani, na mara ya mwisho kuongea na wanahabari, alishinikiza Waziri  Mwigulu Nchemba ajiuzulu. Hivi karibuni pia akizungumza na

TFDA kuzuia soseji kutoka Afrika Kusini zenye bakteria

Image
Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) imesema itazuia uingizaji wa soseji kutoka Afrika Kusini zilizobainika kuwa na bakteria aina ya listeria. Uamuzi wa TFDA unatokana na soseji hizo aina ya Polony kubainika kuwa na aina hiyo ya bakteria wanaosababisha ugonjwa wa listeriosis uliosababisha vifo vya watu 180 nchini Afrika Kusini. Msemaji wa TFDA, Gaudensia Simwanza akizungumza na Mwananchi jana alisema mamlaka hiyo inalifanyia kazi suala hilo ikiwa ni pamoja na kuzuia uingizwaji wa soseji hizo nchini, “Tunalifanyia kazi kwa kufanya ukaguzi na kujiridhisha kama soseji husika zipo katika soko,” alisema. Soseji hizo kwa mujibu wa habari zilizochapishwa na vyombo kadhaa vya kimataifa zinatengenezwa na kiwanda cha tiger brands unit enterprises na cha RCL foods vyote vya Afrika Kusini. Waziri wa Afya wa Afrika Kusini, Aaron Motsoaledi alikaririwa na mitandao ya kijamii akisema ameagiza kuondolewa sokoni soseji hizo, huku akiwashauri wananchi kuacha kula. Mot

Tanzia:Aliyewahi kuwa Mbunge wa Kigoma mjini afariki dunia Muhimbili

Image
ALIYEWAHI kuwa Mbunge wa Kigoma Mjini, Dkt. Amani Walid Kabourou amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alikokuwa akipatiwa matibabu. Dkt. Kabourou ambaye alizaliwa Mei 23, 1949, amewahi kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini (CHADEMA) kabla ya kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kigoma. Aidha, Dkt. Kabourou amewahi kuwa Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki akiiwakilisha Tanzania kuanzia Juni 05, 2007 hadi Juni 04, 2012. Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Zitto Kabwe ambaye ni mbunge wa sasa wa Kigoma Mjini amesema kwao huo ni msiba mkubwa, na umewaacha na majonzi tele. “Tumeamka asubuhi na habari za kusikitisha kuwa Dkt. Amani Walid Kabourou, Mbunge Mstaafu wa Kigoma Mjini ametangulia mbele ya haki. Hakika ni msiba mkubwa kwetu. Mola ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi,” ameandika Zitto.

MAGAZETI YA LEO 5/3/2018

Image