Rais Kenyatta, Odinga Waahidi Kuwaunganisha Wakenya

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta (kushoto) akiwa na kiongozi wa muungano wa upinzani nchini humo Raila Odinga.
RAIS wa Kenya Uhuru Kenyatta amekutana na kiongozi wa muungano wa upinzani nchini humo, Raila Odinga, katika ofisi yake ya Jumba la Harambee, Nairobi,a mbapo viongozi hao kwa pamoja wamekubaliana kuunda taifa lenye umoja.

“Tumekubaliana tutawaleta pamoja wananchi na kujadiliana kuhusu matatizo yanayoathiri taifa letu na wananchi, na kuunda taifa lenye umoja na lililo imara ambapo hakuna raia anayehisi ametengwa,” alisema Rais Kenyatta baada ya mkutano huo.

“Tumekutana na ndugu yangu Kenyatta, tumeongea kwa kirefu na kukubaliana kwamba tunataka kuiunganisha Kenya iwe taifa moja. Mgawanyiko ambao umekuwepo tangu uhuru utakwisha  na sisi tutembee pamoja,” alisema Raila Odinga katika hafla hiyo.

Comments

Popular posts from this blog