Posts

Simba Hawaukosi Ubingwa

Image
KWA staili hii Simba inakosaje ubingwa wa Ligi Kuu Bara? Vigogo wa Simba wameibuka na kutangaza ofa mpya kwa wachezaji wa timu hiyo kwamba kila mechi watakayoshinda kila mchezaji atapata fedha ya maana. Simba hadi hivi sasa tayari imefanikiwa kushinda michezo 12 ya ligi kuu kati 17, ikitoka sare michezo mitano huku ikiwa haijapoteza mchezo wowote. Kwa mujibu wa taarifa ambazo imezipata Championi Jumatatu, wachezaji hao wameongezewa morali ya kupata ushindi na kuwawekea motisha ya fedha kwa kila mechi watakayoshinda ya ligi kuu na michuano ya kimataifa Afrika. Simba hivi sasa inawategemea zaidi Emmanuel Okwi na John Bocco katika kupata ushindi. Mtoa taarifa huyo alisema, motisha hiyo ya fedha imegawanywa kwa mafungu, ipo inayowahusisha wachezaji wa kikosi cha kwanza, akiba na wanaokaa ambao wao wanapata sawa. “Kiukweli hivi sasa mabosi na viongozi wa Simba, wamedhamiria kuuchukua ubingwa wa ligi kuu msimu, kwani wameandaa motisha kwa wachezaji kwa kila me

KISA MNYETI, HECHE ASUBURI KAULI YA JPM

Image
MBUNGE wa Tarime Vijijini, John Heche amedai litakuwa jambo la ajabu kwa Watanzania kunyamazia ubaguzi unaofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti ikiwa walikuwa mstari wa mbele kupinga ubaguzi wa rangi. Heche ametoa kauli hiyo mchana wa leo ikiwa ni muda mfupi baada ya taarifa za Mkuu huyo wa Mkoa kusambaa akiweka wazi wilayani Mbulu  kwamba hayuko tayari kutoa msaada kwa diwani wa chama cha upinzani kwa kuwa yeye anatekeleza ilani ya chama kilichopo madarakani. “ Kama Watanzania walikua mstari wa mbele kupinga ubaguzi wa rangi itakua jambo la ajabu kunyamazia ubaguzi na chuki ya Mnyeti dhidi ya Watanzania wengine, nasubiri kusikia kauli ya Chama chake na rais aliemteua Mnyeti.” alisema Heche.

Haya ndio mambo matatu waliozungumza Zitto Kabwe na Mh.Lissu Ubelgiji

Image
Jana Jumapili Februari 11, 2018 Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo Mhe. Zitto Kabwe alimtembelea Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki, Mhe Tundu Lissu ambaye yupo kwenye matibabu nchini Ubelgiji. Zitto Kabwe amesema kuwa walipokutana waligusia mambo makubwa matatu ambayo ni juu ya Gharama za matibabu yake, Suala la uchunguzi wa shambulio lake na maendeleo ya afya yake na mbinu za kuleta mabadiliko nchini. Kuhusu suala la matibabu Mhe. Zitto Kabwe amesema Lissu anasikitika kuwa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mpaka leo sio tu halimhudumii Lakini pia hata stahili zake za msingi kama Mbunge hapewi. Licha ya kutibiwa kwa misaada ya wasamaria wema, lakini ana mahitaji mengine kama mwanadam na wajibu kama mzazi. Sheria ya Bunge imeweka wazi kuwa Mbunge anapokuwa ametibiwa nje ya nchi Bunge humgharamia maisha yake. “Suala la Gharama za matibabu yake.,Lissu anasikitika kuwa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mpaka leo sio tu halimhudumii Lakini pia

Ajali Mbaya Yaua Sita Papo Hapo- Tanga

Image
WATU watano wamefariki dunia papo hapo na wengine sita kujeruhiwa vibaya, baada ya basi kubwa kugongana na Hiace katika eneo la Kabuku wilayani Handeni. Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoani Tanga, Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP) Leonce Rwegasira alisema ajali hiyo ilitoke saa 5:30 asubuhi katika eneo hilo la Kabuku. Alitaja magari yaliyohusika katika ajali hiyo ni basi la Kampuni ya AJ Safari lililokuwa likitoka Lushoto kwenda Dar es Salaam likiendeshwa na Khalifa Mussa Omary mkazi wa Chamanzi Dar es Salaam lenye namba za usajili T 497 BJB mbalo limegongana na Hiace iliyokuwa ikitoka Mkata kwenda Segera yenye namba T591 AKE. Aliwataja waliokufa kuwa ni pamoja na dereva wa Hiace aliyefahamika kwa jina moja la Shabaan, wengine majina yao hayajatambulika na maiti zao zimehifadhiwa Kwenye Hospitali ya Magunga wilayani Korogwe. ACP Rwegasira alisema majeruhi ambao hawakuchukuliwa majina yao kutokana na uharaka wa kuwasaidia kuwafikisha katika Kituo cha Afya Kabuku kwa

'Maafisa Habari, TEHAMA ni Mawakala wa Mabadiliko’

Image
February 12, 2018 Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mara,Raphael Joseph Nyanda akifungua Semina kwa Maafisa hao wa Mkoa wa Mara na Arusha. Ndugu Wakili Mtebe, Meneja Mradi wa PS3, akiwakaribisha wageni wakati wa Ufunguzi. Mkuu wa Mawasiliano kutoka OR TAMISEMI, Bibi Rebecca Kwandu, akiteta jambo na Kaimu Katibu Tawala Mkoa muda mfupi kabla ya Ufunguzi wa Mafunzo hayo. Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mara, Raphael Joseph Nyanda, amewakumbusha Maafisa Habari na Maafisa wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) nchini kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia weledi, maarifa na ubunifu, kwakuwa wao ni mawakala wa mabadiliko. Dkt. Peter Kilima, Mkurugenzi wa Utawala Bora na Ushirikishwaji wa Wananchi kutoka PS3, akizungumza wakati wa Mafunzo hayo Akifungua kikao cha siku nne mkoani humo kilichoandaliwa na Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwa kushirikiana na Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3), Ndugu Nyanda amewatahadharish

Rais Magufuli afanya uteuzi huu

Image
Rais Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Dkt. Omari Rashid Nundu kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL Corporation) na Bw. Waziri Waziri Kindamba kuwa Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo. Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Gerson Msigwa amesema kuwa Uteuzi wa Dkt. Omari Rashid Nundu na Bw. Waziri Waziri Kindamba umeanza tarehe 01 Februari, 2018. Kabla ya Uteuzi huu Dkt. Omari Rashid Nundu alikuwa Mwenyekiti wa Bodi ya iliyokuwa Kampuni ya Simu Tanzania (Tanzania Telecommunication Company Limited – TTCL) na Bw. Waziri Waziri Kindamba alikuwa Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo. Pamoja na kufanya uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi na Mkurugenzi Mkuu wa TTCL Corporation, Mhe. Rais Magufuli ameiagiza Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kuwahamisha wafanyakazi wote na maafisa wa umma (Employees and Public Officers) wa iliyokuwa TTCL kwenda TTCL Corporation. Pia Mhe. Rais Magufuli amemuagiza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Ma

BREAKING : ANGALIA MTOTO WA KIUME AFUMANIWA NA BABA YAKE MZAZI CHUMBANI

Image
Kijana mmoja aliyetajwa kwa jina la Dullah, mkazi wa Chamwino, Kibao cha Shule mkoani Morogoro amedaiwa kufumaniwa akijaribu kumlawiti Baba ake mzazi. tukio hilo lakusikitisha lilitokea jumatatu iliyopota usiku nyumbani kwa mzee mmoja maarufu (jina linahifadhiwa kwasababu za kimaadili) anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 70. Habari zinasema kijana huyo inadaiwa baada ya kutaka kufanya unyama huo, baba yake alipiga yowe kuomba msaada ambapo baadhi ya wananchi walimwita mwandishi wetu ambaye alipofika eneo la tukio alikuta kundi la wananchi wakijadili, huku mtuhumiwa akiwa amekimbia.

UTAPELI MPYA FEDHA KWENYE SIMU YAKO WATIKISA NCHINI!

Image
IGP Sirro. BADO wizi wa fedha za kwenye mitandao ya simu unaendelea kutikisa nchini ambapo kwa sasa njia mpya imeibuka ambayo unaibiwa fedha kwenye simu yako ukiwa nayo mkononi. Wakizungumza na Risasi Mchanganyiko baadhi ya wananchi walilalamikia utapeli huo na kusema wameibiwa fedha zao ambazo zilikuwa kwenye simu zao. Mmoja wa wananchi hao, Agatha John wa Mwenge jijini Dar alisema aliibiwa fedha zake shilingi 60,000 baada ya kupigiwa simu na mtu ambaye hamfahamu aliyemtaja jina lake kiufasaha na kumdanganya kwamba yeye ni ofisa wa mtandao wa simu anaoweka fedha zake. “Mtu huyo aliniambia kuna zawadi kemkem zitatolewa na mtandao huo kwa wateja ambao wana fedha zaidi ya shilingi 50,000 hivyo alinishauri nimtajie namba yangu ya siri ili fedha na zawadi ziweze kutumwa ndani ya siku tatu,” alisema Agatha. Aliongeza kwamba baada ya kumtajia namba zake za siri aliamini kwamba fedha zake zitakuwa salama kwa sababu simu na kadi yake anayo yeye, hivyo alidhani

Nape Nnauye awakomalia usalama wa Taifa

Image
Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye ameibuka na kuituhumu Idara ya Usalama wa Taifa nchini haifanyi kazi zake ipasavyo inavyohitajika na badala yake wamekalia kusikiliza simu za watu wanavyoongea pamoja na kufanya mambo ambayo hayalindi uchumi wa Tanzania. Nnape ametoa kauli hiyo wakati alipokuwa akichangia bungeni taarifa ya Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama katika mkutano wa 10 kikao cha nane cha Bunge mjini Dodoma na kuishauri kamati hiyo ipeleke mapendekezo ili waweze kupitia upya sheria ya Usalama wa Taifa na kuiwezesha mikono yao iende mbali, kukumbuka jukumu lao la la kuhakikisha wanalinda uchumi nchi katika kipindi hichi, ambacho demokrasia ya siasa inahama na kuelekea kwenye demokrasia ya uchumi ambapo muda mwingi wanapaswa kuutumia huko na sio pengine. Kutoka na hayo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora), Kapteni George Mkuchika amemjibu Nape na wabunge wengine kwamba kazi ya Idara ya Usal

Hoja ya biashara ya ngono, madanguro yajibiwa na Serikali

Image
Serikali imesema ina andaa mikakati itakayowezesha kudhibiti biashara ya ngono na uwepo madanguro nchini, hasa kwenye maeneo ya mijini. Hayo yamesemwa jana Bungeni Mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile wakati akijibu swali la Mbunge wa Mtambwe, Khalifa Mohammed Issa aliyehoji juu mpango serikali katika kudhibiti biashara ya ngono na madanguro ili kupunguza maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi (VVU) nchini. Akijibu swali la Issa, Dkt. Ndugulile alisema Serikali inaandaa mikakati mbalimbali ikiwemo utoaji wa elimu kuhusu madhara ya biashara ya ngono kwa jamii pamoja na kuchukua hatua za kisheria kwa wanaojihusisha na baishara hiyo, pamoja na kudhibiti uwepo wa madanguro. Katika hatua nyingine, Dkt. Ndugulile alisema serikali inaendelea kuchukua hatua katika kudhibiti mila na desturi potofu zinazochangia maambukizi mapya ya VVU, ikiwemo ukeketaji na urithishaji wa wajane kwa ndugu w

Akiwa Safarini, Mbasha Akombwa Kila Kitu Mchana Kweupe

Image
 ALIYEKUWA mume wa Flora Mbasha, Emmanuel Mbasha akiwa safarini Arusha amekombwa kila kitu na majambazi nyumbani kwake Tabata Kimanga mchana kweupe. Mtu wa karibu na Mbasha aliiambia Mikito Nusunusu kuwa, Mbasha alichanganyikiwa baada ya kurudi na kukuta amekombwa kila kitu cha ndani na majambazi. Baada ya habari hizi kutua kwenye dawati la Mikito Nusunusu, lilimtafuta Mbasha ambaye alikiri kuibiwa kila kitu na kusema kuwa mpaka sasa amesharipoti polisi na uchunguzi bado unaendelea. “Yaani sina la kusema walioniliza wamefanya kazi kwani wamechukua kila kitu cha ndani na kwa kweli wamenirudisha nyuma sana hata sielewi naanzia wapi,” alisema Mbasha. Wakielezea tukio hilo majirani wa eneo hilo walisema kuwa mitaa hiyo mida ya mchana huwa ni tulivu sana kwani watu wengi huwa wanakwenda makazini ndio maana hata majambazi hao wakafanikiwa kuiba kila kitu bila kushtukiwa. “Si unajua nyumba zetu ni za mageti makubwa mtu kujua moja kwa moja kuwa kwa f’lan kaingia mt

Akiwa Safarini, Mbasha Akombwa Kila Kitu Mchana Kweupe

Image
 ALIYEKUWA mume wa Flora Mbasha, Emmanuel Mbasha akiwa safarini Arusha amekombwa kila kitu na majambazi nyumbani kwake Tabata Kimanga mchana kweupe. Mtu wa karibu na Mbasha aliiambia Mikito Nusunusu kuwa, Mbasha alichanganyikiwa baada ya kurudi na kukuta amekombwa kila kitu cha ndani na majambazi. Baada ya habari hizi kutua kwenye dawati la Mikito Nusunusu, lilimtafuta Mbasha ambaye alikiri kuibiwa kila kitu na kusema kuwa mpaka sasa amesharipoti polisi na uchunguzi bado unaendelea. “Yaani sina la kusema walioniliza wamefanya kazi kwani wamechukua kila kitu cha ndani na kwa kweli wamenirudisha nyuma sana hata sielewi naanzia wapi,” alisema Mbasha. Wakielezea tukio hilo majirani wa eneo hilo walisema kuwa mitaa hiyo mida ya mchana huwa ni tulivu sana kwani watu wengi huwa wanakwenda makazini ndio maana hata majambazi hao wakafanikiwa kuiba kila kitu bila kushtukiwa. “Si unajua nyumba zetu ni za mageti makubwa mtu kujua moja kwa moja kuwa kwa f’lan kaingia mt

Hatma ya Zitto mikononi mwa Spika

Image
KUADHIBIWA ama kutoadhibiwa na Bunge kwa Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT-Wazalendo) kuko chini ya Spika Job Ndugai baada ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kukamilisha uchunguzi wa shauri lake. Kiongozi huyo wa ACT-Wazalendo anakabiliwa na tuhuma za kudharau mamlaka ya Spika kutokana na kauli yake kwamba, "Bunge limewekwa mfukoni na serikali." Akiwasilisha bungeni mjini hapa jana taarifa ya shughuli za Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kwa kipindi cha kuanzia Januari 2017 hadi Januari 2018, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Almas Maige, alisema tayari wameshakamilisha uchunguzi wa shauri hilo. Pia alisema kamati yake imeshamshauri Spika hatua za kuchukua kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge toleo la Januari 2016. Maige ambaye pia ni Mbunge wa Tabora Kaskazini (CCM), alisema kuwa katika mkutano wa nane wa Bunge, baada ya Spika kupokea na kuikabidhi serikali taarifa za kamati mbili alizoziunda Julai tano kwa ajili ya kufan

Chanzo Cha Maumivu Ya Tumbo Mara Kwa Mara!

Image
Maumivu ya tumbo. MAUMIVU ya tumbo ni tatizo linaloweza kumpata mtu yeyote, mwanamke au mwanaume, mkubwa au mdogo. Maumivu haya husumbua kwani huwa hayaishi, yaani yanatulia kwa muda flani na kurudi tena, aina hii ya maumivu pia inaweza kuwa ya moja kwa moja, yaani hayatulii na wakati mwingine mgonjwa hupata nafuu kwa kujikunja au kushikilia tumbo. Maumivu yanaweza kuwa upande wa juu wa tumbo au upande wa chini na yanatulia kwa vipindi na kurudi yakiwa makali au madogo lakini hayaishi. JINSI TATIZO LINAVYOTOKEA Kama tulivyoona, humtokea yeyote mwanamke au mwanaume, utokeaji wake hutofautiana kwa jinsi. Kwa mwanaume vyanzo vya maumivu haya vinaweza kuwa hernia au ngiri au matatizo kwenye korodani, lakini kwa wote vyanzo vinaweza kuwa vidonda vya tumbo, matatizo ya mkojo, kidole tumbo, matatizo ya utumbo mkubwa, kukosa au kufunga kupata haja kubwa, gesi kujaa tumboni. Yapo mengine kama kuwa na mawe kwenye mfumo wa mkojo au kifuko cha nyongo, matatizo ya ini na mengi

Professor Jay;Sugu kaniambia niwaambie msiogope endeleeni kupaza sauti

Image
Baada ya Mbunge wa Mikumi, Joseph Haule (Professor Jay) kwenda Mahakamani kusikiliza kesi inayomkabili Mbunge wa Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (Sugu), Mbunge huyo amesema kuwa Sugu amesema kuwa wasiogope waendelee kupaza sauti. Professor Jay amesema kuwa kesi hiyo itaendelea kusikilizwa leo ambapo RCO na RPC wa Mbeya watasimama kutoa ushahidi wao. “SUGU kaniambia niwaambie ‘MSIOGOPE’ bali endeleeni kupaza Sauti!!Kesi yao inaendelea leo saa Tatu asubuhi hii katika mahakama kuu ya Mbeya, ambapo RCO na RPC wa Mbeya watasimama kutoa ushahidi wao LEO,” ameandika Proffesor Jay kwenye ukurasa wake wa Insta. Sugu anakabiliwa na kesi ya kutoa lugha ya uchochezi dhidi ya Rais Magufuli. Ambayo wanadaiwa kuitoa Disemba 30 kwenye mkutano wa hadahara uliofanyika katika uwanja wa shule ya msingi Mwenge.

PUTIN ASEMA: SIJAWAHI KUWA NA ‘SMARTPHONE’

Image
Rais wa Russia, Vladimir Putin (kulia) aliyekiri hana simu ya kisasa (smartphone). Kiongozi huyo aliyewahi kuongoza pia shirika la ujasusi la Urusi ya Kisoviet (KGB) amesema huwatumia wasaidizi wake kumtafutia habari anazotaka. “SINA simu ya smartphone,” ndivyo ambavyo husema Rais wa Russia, Vladimir Putin, kila anapoulizwa iwapo ana simu hizo za kisasa. Licha ya kuambiwa kwamba “kila mtu ana smartphone mfukoni”  huko Siberia, nchini Russia, wakati akiwa ziarani, kiongozi huyo pia aliwahi kusema kwamba hataki kutumia tovuti (website) na aliwahi kukiri kwamba mtandao wa Internet ni kimradi cha shirika la ujasusi la Marekani – CIA – na kwamba nusu ya kazi yake ni kuonyesha ngono. Pamoja na kwamba watu wengi nchini mwake, wakiwemo wanafunzi,  huchakarika ili kupata aina hizo za simu, Putin amefichua kwamba analitawala taifa hilo la watu milioni 144 bila kutumia smartphone. Akiwa amekiri pia kwamba hapendi mambo ya technolojia mpya, amesema kamwe huwa hatumi

Wema apigwa mamilioni ya pesa

Image
Miss Tanzania 2006/07, Wema Isaac Sepetu. Wiki moja baada ya akaunti ya Mtandao wa Kijamii wa Instagram ya Miss Tanzania 2006/07, Wema Isaac Sepetu kudukuliwa na wajanja wa mjini, mrembo huyo anadaiwa kupigwa mamilioni. Habari zilizolifikia dawati la gazeti hili zilieleza kuwa, tangu mrembo huyo adukuliwe akaunti yake hiyo yenye wafuasi zaidi ya milioni tatu, wajanja hao wamekuwa wakiitumia ndivyo sivyo kwa kuposti matangazo mbalimbali ya kibiashara ambapo wanachukua pesa bila ya Wema kujua. Inaelezwa kuwa, Wema alikuwa akitumia akaunti hiyo kupitia namba ya simu ya mtandao maarufu wa mawasiliano nchini ambapo wadukuzi walifanikiwa kumiliki namba hiyo ambayo hutumia moja kwa moja kuwasiliana na wafanyabiashara mbalimbali wa mtandao kwa mgongo wa Wema na kuvuna pesa. Wajanja hao, kwa siku moja tu hutumia akaunti hiyo kuvuna zaidi ya laki saba ambapo kwa wastani wa tangazo moja huchukua kiasi cha shilingi elfu hamsini hadi laki moja. WATAALAMU WANASEMAJE?

Chanzo Cha Maumivu Ya Tumbo Mara Kwa Mara!

Image
Maumivu ya tumbo. MAUMIVU ya tumbo ni tatizo linaloweza kumpata mtu yeyote, mwanamke au mwanaume, mkubwa au mdogo. Maumivu haya husumbua kwani huwa hayaishi, yaani yanatulia kwa muda flani na kurudi tena, aina hii ya maumivu pia inaweza kuwa ya moja kwa moja, yaani hayatulii na wakati mwingine mgonjwa hupata nafuu kwa kujikunja au kushikilia tumbo. Maumivu yanaweza kuwa upande wa juu wa tumbo au upande wa chini na yanatulia kwa vipindi na kurudi yakiwa makali au madogo lakini hayaishi. JINSI TATIZO LINAVYOTOKEA Kama tulivyoona, humtokea yeyote mwanamke au mwanaume, utokeaji wake hutofautiana kwa jinsi. Kwa mwanaume vyanzo vya maumivu haya vinaweza kuwa hernia au ngiri au matatizo kwenye korodani, lakini kwa wote vyanzo vinaweza kuwa vidonda vya tumbo, matatizo ya mkojo, kidole tumbo, matatizo ya utumbo mkubwa, kukosa au kufunga kupata haja kubwa, gesi kujaa tumboni. Yapo mengine kama kuwa na mawe kwenye mfumo wa mkojo au kifuko cha nyongo, matatizo ya ini na m

MWANAUME AOA WANAWAKE SITA KWA KULIPWA,SABABU Z A TUKIO HILO HIZI HAPA

Image
mmoja wa Marekani katika Jimbo la Massachusetts ameshtakiwa Mahakamani kwa hati ya makosa ya jinai baada ya kuoa wanawake wengi katika kipindi cha mwaka 2003 hadi 2013.   Mtuhumiwa huyu Peter Hicks, 57, alifanya vitendo hivi huku akilipwa kwa lengo la kuwasaidia wanawake hao kukwepa hatua za kupata nyaraka zote za kuwatambua kama wahamiaji wa nchi hiyo. Inaelezwa kuwa Hicks alioa wanawake 6 katika kipindi hicho chote. Wanawake hao wanaripotiwa kutoka katika nchi za Kusini mwa Afrika na alikuwa tayari ameshaomba haki zote wanazotakiwa kupewa wahamiaji wanne kati yao

MZEE MAJUTO: Niombeeni Jamani, Tezi Dume Si Mchezo!

Image
Amri Athuman ‘Mzee Majuto’ MKONGWE wa filamu za Kibongo aliye kipenzi cha wengi, Amri Athuman ‘Mzee Majuto’ ambaye kwa sasa ni mgonjwa ametoa ya moyoni kuwa bado anaumwa hivyo kuwaomba wasanii wenzake na Watanzania kumuombea. Akizungumza na Star Mix, Mzee Majuto alisema Februari 11, mwaka huu anatarajia kurudi tena katika Hospitali ya Tumaini, Dar alikokuwa amelazwa awali na kuruhusiwa baada ya daktari wake kufiwa ambapo ndiyo ataenda kufanyiwa upasuaji wa ugonjwa wa tezi dume unaomsumbua.   “Niliruhusiwa Jumamosi iliyopita lakini bado naumwa, tezi dume si mchezo, ninachoweza kuwaambia wasanii wenzangu na Watanzania kwa jumla, waniombee tu,” alisema Mzee Majuto