Posts

VIDEO: Halima Mdee alivyotumia neno "fala" "mpumbavu" Bungeni

Image
 T azama Video:

Chadema, CUF vyatinga Mahakamani kupinga matokeo ya uchaguzi EALA

Image
Twaha Taslim aliyekuwa Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki pia Mwanasheria wa CUF  VUGUVUGU la Uchaguzi wa wabunge wa Afrika Mashariki wazidi kulitikisa bunge. tayati Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema na Chama Cha Wananchi CUF vimepanga kutinga mahakamani kupinga matokeo hayo. Jana Mweyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Freeman Mbowe alitoa kauli ya kupinga matokea hayo mahakamani kutokana na kudai kuwa uchaguzi huo ulikwenda kinyume na taratibu za uchaguzi. Leo akizungumza na Muungwana Blog kaimu Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF), Ahmed Katani, amesema kuwa uchaguzi huo umeendeshwa kinyume cha taratibu na kanuni za uchaguzi huo. Amesema kuwa jana majira ya saa 8 na dakika 37 kabla ya uchaguzi huo alipokea  barua kutoka kwa msimamizi wa uchaguzi Dk, Thomas Kashililah. Kwa mujibu wa barua hiyo ya Msimamiza wa uchaguzi ambayo alikiri kuwa kwa wagombea wa CUF kuna matatizo na kwamba hatuweza kushiriki kuchaguzi. Katani amesema aliandik

Mbowe amtuhumu Rais Magufuli, kwa jambo hili.

Image
MWENYEKITI wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Freeman Mbowe amtuhumu Rais John Magufuli pamoja na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuhusika kwa alichodai kuwa ni kukeukwa kwa taratibu za uchaguzi. Mbowe ameongea hayo jana usiku mara baada ya kutoka kwenye ukumbi wa bunge  ambapo amedai kuwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na Rais Magufuli kuhusika kwenye mchakato wa kuyakataa majin ya wagombea wa Chadema. Mbowe amesema  kuwa, wao hawatakubaliana na hilo kwa sababu Spika wa Bunge amekiuka kanuni za bunge, na uchaguzi wote ulikuwa wa kasoro. Wagombea waliopendekezwa na Chadema  Wenje Na Masha kupigiwa kura za hapana katika  kuwania kuiwakilisha Tanzania katika bunge la Afrika Mashariki Majina ya wagombea na matokeo KUNDI A: WANAWAKE 1. Ndg. Happiness Elias LUGIKO - KE - CCM - KURA 196 2. Ndg. Fancy Haji NKUHI - KE - CCM - KURA 197 3. Ndg. Happiness Ngoti MGALULA - KE - CCM - KURA 125 4. Ndg. Zainabu Ras

Jinsi Facebook ilivyohusika mkasa wa binti aliyejitosa baharini

Image
KISA cha binti mwenye umri wa miaka 16 (jina linahifadhiwa kutokana na miaka yake) kujitupa baharini akiwa katika boti ya Kilimanjaro V akitoka Dar es Salaam kwenda Zanzibar juzi, kinaanzia kwenye mawasiliano yake na mvulana mmoja, kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook, imefahamika. Msichana huyo alikuwa akiwasiliana na mvulana huyo ambaye walifahamiana kupitia Facebook, kwa kutumia simu ya mkononi. Nipashe ilifika Kikwajuni, nyumbani kwa msichana huyo ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha tatu (shule inahifadhiwa) na kuikuta familia yake ikiwa na majonzi, huku wakiwa hawaamini kilichotokea na binti huyo akiwa bado hai. Akizungumza kwa huzuni, mama mdogo wa msichana huyo, Asha Saleh Mandhi, alisema palitokea mzozo baina yake na binti huyo baada ya kumkuta na simu ya mkononi wakati wazazi wake hawajamnunulia. Alisema Jumatano iliyopita majira ya jioni akiwa nyumbani hapo na baada ya kupata taarifa kuwa mtoto wake wa kumlea anamiliki simu, alimwita na

Washindi wa Bunge la Afrika Mashariki

Image
Wabunge watakaoiwakilisha Tanzania kwenye bunge la Afrika Mashariki wamepatikana.

Kauli ya ACT Wazalendo kuhusu Rais Magufuli kumteua Mwanachama wao , Prof. Kitila Mkumbo Kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Image
Leo asubuhi Rais John Pombe Magufuli amemteua Mshauri wa Chama chetu Prof. Kitila Mkumbo kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji. Chama cha ACT Wazalendo kimepokea kwa mikono miwili taarifa juu ya uteuzi wa mshauri wa chama chetu Kwa sababu imeonyesha kuwa Rais ameona kuwa hata Watanzania walio kwenye Vyama vya Upinzani wana uwezo, weledi na uzalendo wa kutumikia nchi yetu. Kwa nafasi hii ya Ukatibu Mkuu wa Wizara, ndugu Kitila hawezi kuendelea kuwa Mshauri wa Chama nafasi ambayo inamfanya kuhudhuria vikao vyote vya Chama ikiwemo Kamati Kuu. Ndugu Mkumbo ameandika barua ya kujiuzulu nafasi yake ya mshauri wa Chama na kubaki kuwa mwanachama wa kawaida tu. Nimeipokea barua yake na kumkubalia Kwa maslahi mapana ya nchi yetu. ACT Wazalendo tunamshukuru ndugu Kitila Mkumbo kwa mchango wake katika uongozi wa Chama chetu kwa wakati wote ambao alikitumikia Chama chetu kama mshauri wa chama. Msimamo wa chama chetu ni utumishi wa kizalendo kwa Ta

KITILA AMEFUNGUKA HAYA BAADA YA KUTEULIWA NA JPM

Image
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Prof. Kitila Mkumbo amemshukuru Rais Magufuli kwa kumteua kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo akichukua nafasi ya Mhandisi Mbogo Futakamba ambaye amestaafu. Prof. Mkumbo ambaye pia ni kada na mshauri wa Chama cha ACT Wazalendo kinachoongozwa na Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe, amesema Rais amempa heshima kubwa kwa nafasi hiyo, na yeye kama mtumishi wa umma hawezi kuikataa kwa kuwa ni kazi aliyotumwa na mkuu wa nchi. “Ukishapewa kazi na mkuu wa nchi, unaipokea na unaifanya kwa bidii kama yalivyo matarajio, kwahiyo nimepokea uteuzi, nimekubali, mkuu wa nchi akikupa kazi utaikataa vipi, mkuu wa nchi akikupa kazi unaifanya, kumbuka mimi ni mtumishi wa umma” Amesema Prof Kitila

Eritrea yapinga vikwazo vya Marekani

Image
Eritrea imepinga vikwazo ilivyowekewa na Marekani kwa kufanya biashara ya vifaa vya kijeshi na Korea kaskazini. Mpango huo ulibainika katika ripoti ya kamati ya baraza la usalama la Umoja wa Mataifa ya 2016 iliotolewa mnamo mwezi Februari, ambapo masanduku 45 ya vifaa vya kijeshi vya mawasiliano vilipatikana vikielekea Eritrea kutoka North Korea. Eritrea imepinga matokeo ya ripoti hiyo Mamlaka za Asmara zimeonekana kujibu hatua za Marekani na kuzilaani vikali. Taarifa kutoka wizara ya habari zimesema kwamba hatua ya Marekani siyo ya haki na kwamba haifai kabisa. Asmara imeongeza kwamba sera ya Marekani kwa nchi hiyo ni ya kupotosha na kwamba hatua hii inaambatana na vikwazo vya Umoja wa Mataifa vilivyotarajiwa kujadiliwa upya mwezi huu. Marekani huwekea vikwazo kwa taifa lolote ambalo huweka mikataba ya kijeshi na Iran, Korea Kaskazini na Syria. Vikwazo vya sasa vimelenga jeshi la wanamaji la Eriterea pamoja na jeshi la Sudan. Hii inamaana kwamba serikali ya M

Jacqueline Wolper: Harmonize hawezi nipiga chini

Image
Malkia wa filamu Jacqueline Wolper amefunguka kwa kudai kuwa mpenzi wake wa sasa Harmonaze hana uwezo wa kumuacha kimapenzi pamoja na tetesi ambazo zimekuwa zikisikika kwamba mwanamuziki huyo kuwa ana warembo wengine anaotoka nao kimapenzi. Wawili hao kwa sasa wako karibu zaidi baada ya wiki chache zilizopita kudaiwa wameachana. Akiongea na mtandao wa Central Filamu wiki hii, Wolper amedai yeye na Harmonize wako vizuri na hawadhani kama wenaweza kutengena hivi karibuni. “Wengi wanaongea sana kuhusu mpenzi wangu kama anatoka na wanawake wengi pengine inaweza kuwa ndio sababu ya kuniacha mimi hicho hakiwezekana wanaongea kama kuna wasichana wanajipendekeza watachezewa tu,” alisema Wolper. Muigizaji huyo amedai Harmonaze hana uwezo wa kumwacha kwani yeye ni muhimu kwake.

Yaliyojiri Mahakamani kwenye kesi ya Mume wa Shamsa Ford

Image
Leo April 4, 2017 ambapo mume wa mwigizaji wa filamu Shamsa Ford aiitwae Chid Mapenzi alifikishwa Mahakama ya Kinondoni kufuatia kuitwa Polisi kwa sakata la dawa za kulevya. Kwa mujibu wa wakili wake aitwae Reuben Simwanza  ameiambia millardayo.com kuwa kesi imeahirishwa mpaka tarehe 13  mwezi April kwa kosa la matumizi ya dawa hizo. ‘Kwa kifupi ni kweli kesi imekuja leo Mahakama ya Kinondoni amesomewa shtaka kwa mara ya kwanza kuhusu sheria ya madawa ya kulevya na usafirishaji wa madawa haramu, kimsingi madawa  yalitajwa kwa lugha inayoeleka ni marujuana huku mshtaki amekana mashtakiwa hayo hiyo yuko nje kwa dhamana na kesi itatajwa tena tarehe 13/4/2017 ndio atarudi Mahakamani’- Wakili

MAMA SALMA KIKWETE AAPISHWA KUWA MBUNGE

Image
Spika wa bunge, Job Ndugai akimwapisha Mama Salma Kikwete kuwa mbunge, bungeni mjini Dodoma Aprili 4, 2017. Mama Salma Kikwete akiapa kuwa mbunge, bungeni mjini Dodoma Aprili 4, 2017. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimpongeza Mama Salma Kikwete baada ya kuapishwa kuwa mbunge, bungeni mjini Dodoma Aprili 4, 2017. Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Jakakaya Mrisho Kikwete akishiriki kuimba wimbo wa taifa kabla ya kuanza kwa kikao cha bunge mjini Dodoma Aprili 4, 2017. Mheshimiwa Kikwete alikwenda bungeni kushuhudia kuapishwa kwa mkewe mama Salma. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

ANGALIA NAFASI 92 ZA AJIRA TANZANIA NATIONAL PARKS (TANAPA)

Image
Tanzania National parks (TANAPA) is a Parastatal Organization whose mandate is to manage and regulate the use of areas designated as National Parks. The organization currently manages sixteen National Parks which form part of larger protected ecosystems set aside to preserve Tanzania’s rich natural heritage. In her endeavor to promote professionalism, the organization seeks to recruit high caliber, results oriented and self-driven professionals with integrity to fill Ninety-Two (92) posts of *Park Rangers* to work in various National Parks. Park Rangers Grade IV (92 POSTS) Reporting Relationship:Report to Park Wardens / Heads of Protection Department in the Respective Parks Duty Station: National Parks /(i) Qualifications: Form IV Certificate with Basic Certificate in Wildlife Conservation from Pasiansi Wildlife Conservation Training Institute. Candidates with Certificate in basic military training from the National Service will be

YALIYOJIRI LEO BUNGENI MJINI DODOMA BAADA YA VIKAO VYAKE KUANZA LEO

Image
Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Mhe. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili katika Viwanja vya Bunge kwa ajili ya kushuhudia kiapo cha Mke wake Mama Salma Kiwete aliyeteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Mbunge. Mbunge wa kuteuliwa Mhe. Salma Kikwete akiwasili katika viwanja vya Bunge Mjini Dodoma kwa ajili ya kula kiapo na kuanza majukumu yake.  Mbunge wa kuteuliwa Mhe. Salma Kikwete akisindikizwa na wabunge wanawake kwenda kula kiapo cha kutumikia kazi yake leo Bungeni Mjini Dodoma. Mhe. Salma Kikwete akila kiapo cha kuwa mbunge mbele ya Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai leo bungeni Mjini Dodoma.  Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai akiongoza kikao cha kwanza cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 Mjini Dodoma. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angella Kairuki akijibu hoja mbalimbali za wabunge katika kikao cha kwanza cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 Mjini Dodoma. Wa

TAARIFA YA UTEUZI WA WAGOMBEA WA UJUMBE WA BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI

Image
1.     Tarehe 17 Machi, 2017 nilitoa Tangazo kwenye Gazeti la Serikali Namba 376 kuhusu Siku ya uteuzi na Siku ya Uchaguzi. Katika Tangazo hilo, nilipanga Siku ya tarehe 30 Machi, 2017, saa Kumi (10.00) Jioni kuwa Siku ya Uteuzi wa Wagombea na pia siku ya tarehe 04 Aprili, 2017 saa Tano (5.00) Asubuhi kuwa Siku ya Uchaguzi wa Wajumbe wa Bunge la Afrika Mashariki. 2.     Aidha, natoa shukrani zangu za dhati kwa wadau wote hususan Vyama vyote vya siasa nchini kwa ushirikiano mzuri nilioupata kutoka kwao katika zoezi zima la mchakato wa uteuzi wa wagombea. 3.     Vile vile, navipongeza na kuvishukuru vyama vyote vya siasa vyenye haki ya kushiriki uchaguzi kwa kuendesha mchakato wa uteuzi wa wagombea kwa uwazi na demokrasia kubwa. 4.     Pia navishukuru vyombo vya habari na wanahabari wote kwa ujumla kwa kuhabarisha umma kuhusu mchakato huu muhimu kwa Bunge na Taifa kwa ujumla. 5.     Kipekee nawashukuru na kuwapongeza wananchi wote waliojitokeza kupi

BREAKING NEWS : RAIS MAGUFULI AMTEUA PROF KITILA MKUMBO KUWA KATIBU MKUU WA WIZARA YA MAJI NA UMWAGILIAJI

Image

Ridhiwani amwangukia Majaliwa

Image
MBUNGE wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete (CCM), amemwangukia Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, kwa kumuomba amsaidie kutatua changamoto ya maji inayowakabili kwa muda mrefu wananchi wa jimboni kwake. Ridhiwani alitoa ombi hilo juzi katika ziara ya Waziri Mkuu Majaliwa aliyoifanya jimboni humo kwa lengo la kutembelea chanzo cha maji kilichopo Mto Wami, kama sehemu ya kukagua utekelezaji wa mradi wa maji wa awamu ya tatu wa Wami-Chalinze. “Changamoto ya upatikanaji wa maji jimboni Chalinze, bado ni kubwa na inahitaji nguvu ya ziada ili kufikia malengo ya kuhakikisha wananchi wanapata maji kama ilivyokusudiwa na Serikali. “Suala la maji kwa Jimbo la Chalinze, imekuwa kama sehemu ya siasa na si huduma kwa kuwa tangu mradi wa awamu ya kwanza wa Wami –Chalinze uanze kutekelezwa, ni vijiji 20 tu vya mwanzo ndivyo vilivyopata maji. “Ieleweke kwamba, Mkoa wa Pwani ni mkoa ambao unakua kwa kasi na una viwanda vingi. Hivyo basi, mahitaji ya maji ni makubwa zaidi ukilinganisha na

Mjane mwingine aibukia wanahabari na Zigo la nyaraka

Image
Mjane Farida Saleh Amrani amejitokeza mbele ya vyombo vya habari na kulalamika kudhulumiwa nyumba yake aliyoachiwa na marehemu mme wake aliyefariki mwaka 2011. Akizungumza na kuonesha hati halali za nyumba hiyo yenye kitalu namba 2111 iliyopo Mbezi Beach Kata ya Maliasili, Farida alisema kuwa katika nyumba hiyo walihamia mwaka 2002 na hati ya nyumba hiyo ilikuwa kwa mwanasheria kipindi chote hata pale marehemu mumewe alipofariki. Amesema kuwa, baada ya mume wake kufariki mtoto wa marehemu mkubwa aliambiwa afungue mirathi lakini akawa anasema taratibu za kabila la kihaya ni baada ya mwaka mmoja kumalizika. Farida ameeleza kuwa, mumewe Alfred Kyoma alifariki akiwa safarini Bukoba na amemuacha na watoto wawili ambao baada ya kumalizika kwa msiba familia nzima walikubaliana nyumba ipangishwe ili fedha zitakazopatikana ziwasomeshe watoto,ambao mmoja yupo kidato cha tano sasa hivi na mwingine cha kwanza. Nyumba hiyo kwa Yusuph Shaban Omari ambaye ni mmiliki

Mh! kwa Nape Hapana!- UWOYA

Image
IRENE Uwoya amekataa katakata kuzungumzia chochote kuhusiana na kutumbuliwa kwa aliyekuwa Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye na kusema chochote ambacho kipo, kiendelee kubaki hivyo hivyo lakini kwa upande wake ameziba mdomo. Gazeti hili lilikuwa likimtaka Uwoya kuzungumzia kuachwa kwa waziri huyo katika mabadiliko madogo ya baraza la mawaziri yaliyofanywa hivi karibuni na Rais Dk. John Pombe Magufuli na nini mtazamo wake kwa waziri mteule, Harrison Mwakyembe, lakini muigizaji huyo alikataa katakata. “Jamani mimi kwenye hilo sitaki kuzungumzia chochote jamani mambo ya siasa mimi hapana kwa sasa kilichopo ndicho kiendelee hivyohivyo,” alisema Uwoya.

Dkt Mwele Aliyetumbuliwa na JPM, achukuliwa umoja wa mataifa

Image
Dkt. Mwele Malecela aliyekuwa Mwanamke wa kwanza kuwa Mkurugenzi Mkuu wa NIMR na kisha 'kutumbuliwa' baada ya kutangaza uwepo wa homa ya Zika nchini, sasa anakuwa Mkurugenzi wa Vituo vya kuzuia na kudhibiti magonjwa Afrika wa Umoja wa Mataifa (WHO-AfRO) Mwele alipata kuwa mwanamke wa kwanza kuongoza Taasisi ya Utafiti ya Magonjwa ya Binadamu(NIMR), baadae uteuzi wake ulitenguliwa.

KAIRUKI: SERIKALI HAITAMVUMILIA MTUMISHI MWENYE VYETI FEKI

Image
Inakadiriwa kuwa watumishi 4,300 wapya wanataajiriwa kuajiriwa katika kada ya elimu na wasanifu wa maabara ambapo ajira hizo mpya zinakuja baada ya kukamilika kwa zoezi zima la kuhakiki watumishi hewa.Hayo yamebainishwa mkoani Tabora na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma Mh. Angela Kairuki, wakati akizungumza na watumishi na wanachuo, ambapo amesema kwa muda mwingi taifa limekuwa likikabiliwa na changamoto ya watumishi hewa huku likipoteza fedha nyingi.Aidha Mhe. Kairuki amesema kuwa kamwe serikali haitamvumilia mtumishi ambaye atabainika kuwa na vyeti feki, huku akiwataka watanzania kutambua madhara ya vyeti hivyo kuwa ni kutopatikana kwa huduma stahiki.Amewataka wahitimu katika kada mbali mbali kutowaonea haya watu ambao wanataka kupora ajira za wenzao.