Posts

Breaking News: Winnie Mandela afariki dunia

Image
Winnie Mandela, mke wa zamani wa Nelson Mandela, ambaye pia alipigana dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi Afrika Kusini amefariki dunia akiwa na miaka 81. Habari za kifo chake zimethibitishwa na msaidizi wake. Winnie alizaliwa mnamo 26 Oktoba mwaka 1936, na ingawa yeye na mumewe - Nelson Mandela - walitalikiana mapema miaka ya 1990, Winnie Madikizela Mandela kama alivyofahamika rasmi alisalia kutoa mchango katika maisha ya Bw Mandela. Alikuwepo na walishikana mikono alipokuwa akiondoka gerezani baada ya kufungwa kwa miaka 27. Lakini maisha yake pia yalikumbwa na utata. Winnie alikuwa na miaka 20 hivi pale alipojipata katika siasa. Alisomea kazi ya utoaji huduma za kijamii na haraka aliyazoea maisha ya kuwa mama na mwanasiasa. Kujitolea kwakena ukakamavu wake vilionekana mumewe alipofungwa jela maisha mwaka 1964 na akaachwa kuendeleza harakati za kisiasa. "Kamwe sitakata tamaa na watu wangu hawatapoteza matumaini kamwe, bila shaka tunatarajia kwamba kazi

WAZIRI MKUU AZINDUA MBIO ZA MWENGE MKOANI GEITA

Image
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi Mwenge wa Uhuru kiongozi wa vijana sita watakaokimbiza Mwenge huo, Charles Kabeho wakati alipozindua mbio za Mwenge wa Uhuru kwenye uwanja wa Magogo mjini Geita, Aprili 2, 2018. Wapili kulia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Jenista Mhagama. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwansha Mwenge wa Uhuru kuzindua mbio zake kwenye uwanja wa Magogo mjini Geita, Aprili 2, 2018

Sababu Za Kuwashwa Baada Ya Kuoga

Image
      “Wataalamu wa afya ya ngozi pia wanabainisha kuwa kuoga muda mrefu na mara kwa mara, matumizi ya sabuni zenye harufu kali na povu jingi ni mambo mengine yanayochangia kutokea kwa mzio pamoja na ukavu wa ngozi kutokana na uwezo wake wa kuondosha kiasi kikubwa cha mafuta yanayolinda ngozi. Ili kupunguza hali ya muwasho, “Tumia sabuni zenye mafuta, lakini zisiwe na marashi makali.” Katika hali ya kawaida kitendo cha kuoga kinapaswa kuchukuliwa kama jambo la kufurahisha kutokana na ukweli kwamba huufanya mwili uburudike na kuwa safi. Lakini kwa baadhi ya watu mambo ni tofauti. Kuoga huwa sawa na karaha. Moja ya matatizo ya kiafya ambayo yanayosumbua watu wengi duniani na kuwanyima raha ya maisha, ni tatizo la mwili kuwasha mara baada ya kuoga. Muwasho baada ya kuoga unaweza kujitokeza mwili mzima au unaweza kuhusisha baadhi ya sehemu. Hali hii inaweza kuwa inajitokeza kwa muda wa dakika chache au inaweza kuchukua muda mrefu na kwa baadhi ya watu, hili linaweza kuwa t

Sakata la Wambura lafikia Patamu

Image
RUFAA ya aliyekuwa Makamu wa Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Michael Richard Wambura, sasa imefikia patamu baada ya juzi Jumamosi kusikilizwa katika makao makuu ya shirikisho hilo, Karume jijini Dar es Salaam na hivi sasa watu wengi wanataka kujua nini kinachofuatia. Hivi karibuni, Wambura alikata rufaa Kamati ya Rufaa ya Maadili ya TFF kupinga maamuzi ya Kamati ya Maadili ya shirikisho hilo ya kumfungia maisha kujihusisha na soka kwa madai ya kufanya ubadhirifu wa fedha za shirikisho hilo pamoja na makosa mengine. Wakili wa Wambura, Emmanuel Muga, ameliambia C hampioni Jumatatu kuwa, kamati hiyo iliziita pande mbili zote zinazochuana katika sakata hilo na kuzisikiliza kwa umakini mkubwa. Alisema katika kikao hicho, mambo yalienda vizuri, kwa hiyo kinachosubiriwa tu hivi sasa ni maamuzi ya hiyo kamati. “Kamati imesikiliza kwa umakini utetezi wa Wambura, vilevile TFF nao wakizungumza ya kwao kuhusiana na mustakabali mzima wa kesi hiyo. Kwa hiyo tun

Mamba akutwa katika bwawa la kuogelea Florida, Marekani

Image
Polisi katika jimbo la Florida, Marekani wamesema mamba wa urefu wa futi 11 alipatikana kwenye bwawa la kuogelea la familia moja katika jumba hilo. Polisi wamepakia picha za mamba huyo mtandaoni, Wakazi wa Nokomis waliwapigia simu polisi na kuomba usaidizi baada ya kumgundua mnyama huyo. Afisa wa polisi wa eneo la Sarasota alipakia mtandaoni picha ya afisa wa wanyama aliyeitwa kumnasa akiwa anamburuta mnyama huyo kutoka kwenye maji Jumamosi. Polisi wanasema mamba huyo alifanikiwa kupita kwenye uzio uliokuwepo na kuingia kwenye bwawa hilo, Mamba nchini Marekani kwa kawaida hukua hadi kuwa na futi kati ya 11 na 15 na wanaweza kuwa na uzani wa kilo 454. Mamba wa Marekani hupatikana mashariki mwa Marekani katika majimbo ya Florida na Louisiana, kila jimbo likiwa na zaidi ya mamba milioni moja. Eneo la kusini mwa Florida ndilo pekee ambalo mamba wa Marekani na mamba wa kawaida huishi kwa pamoja. Ingawa awali walikuwa wameorodheshwa kama wanyama walio hatari

Nafasi za Kazi zilizotangazwa Leo

Image
Bonyeza links zifuatazo Kusoma zaidi na Kuapply: 200+ Vacancies in Public and Private institutions in Tanzania, March 2018 Job Opportunity at the US Embassy Tanzania: Chauffeur Job Vacancy at Save the Children Tanzania - FINANCE ASSISTANCE Job Opportunity at UN Organization - Consultancy Process Expert Volunteer Job Opportunity at UN Organization - Marketing & Promotional Materials Expert Volunteer Job Opportunity at UNHCR - Registration Officer Job Opportunity at a Reputable NGO - Consultant to Conduct Assessment of BEST-Dialogue Support to Print Media Job Opportunity at Plan International Tanzania Nafasi zingine ingia  www.ajirayako.co.tz

Gabo, Wema na Kitale walivyoshinda tuzo za SZIFF April 1

Image
Usiku wa April 1 2018 Mlimani City Dar es Salaam zilifanyika tuzo za Sinema Zetu International Film Festival SZIFF na kuhudhuriwa na mastaa na watu mbalimbali kutoka tasnia tofauti tofauti. Rais mstaafu wa awamu ya nne Dr Jakaya Mrisho Kikwete ndio alikuwa mgeni rasmi na alishuhudia tuzo 19 zikitolewa kwa wasanii wa filamu, watayarishaji, wahariri na wabunifu wa sound track za movie hiyo. Miongoni mwa mastaa wa filamu waliyofanikiwa kushinda tuzo hizo ni pamoja na muigizaji Wema Sepetu aliyeshinda tuzo mbili za Best Actress na People’s Choice Award na Gabo ambaye ameshinda tuzo ya Best Actor huku Kitale akishinda tuzo ya Best Comedian. Alichozungumza Wema Sepetu baada ya ushindi wa tuzo ya Best Actres s

Aamka na kukuta Jeneza Nje ya Nyumba!

Image
MBEYA:  NELSON Edson, mkazi wa Mtaa wa Nsalaga Kata ya Nsalaga jijini hapa amejikuta kwenye taharuki kubwa baada ya kuamka na kukuta jeneza tupu dogo nje ya mlango wa nyumba yake. Tukio hilo lililoibua hekaheka mtaani hapo lilijiri asubuhi ya Machi 27, mwaka huu. Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Mtaa wa Nsalaga, Paul Ngonde, alipokea taarifa kutoka kwa Edson na kuamua kwenda eneo la tukio ili kushuhudia. Alisema kuwa, baada ya kuwashirikisha wazee wa mila juu ya jambo hilo, walilifungua jeneza hilo na kukuta likiwa tupu, lakini likiwa na sanda nyeupe iliyoviringishwa ndani yake. “Nimeshangaa asubuhi kuamka na kukuta jeneza nje ya mlango wa nyumba yangu, sijaelewa ni nini madhumuni ya kuwekewa jeneza hilo,” alisema Edson huku akionesha kustaajabishwa na tukio hilo. Kwa mujibu wa mwenyekiti huyo, mtaa huo umekuwa na matukio ya ajabuajabu yakiwemo ya kutupa watoto, lakini tukio hilo la jeneza limekuwa ni tukio la kwanza kutokea mtaani kwake.   Kwa upande wake, Kamanda wa P

“Kuna kitu MUNGU anataka kutuambia kupitia Waraka wa Maaskofu” Askofu Shoo

Image
Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheli, Askofu  Frederck Shoo amewata baadhi ya watu kuacha  kupotosha ukweli wa waraka wa maaskofu kwa kuupaka matope na kusema anae fanya hivyo  ni mjinga. Askofu Shoo ametoa kauli hiyo leo April 1, 2018 katika Usharika wa Moshi Mjini Dayosisi ya kaskazini, mkoani Kilimanjaro wakati akitoa salamu za Pasaka. Askofu Shoo amenukuliwa akisema   “Wapo wanaotumia nguvu nyingi kutaka kupotosha ujumbe wa waraka wa Maaskofu na wamekuwa wakilipaka Kanisa matope ili waweze kurejea katika waraka ule, watu hawa naweza kuwaita ni wajinga lakini pamoja na hilo nataka wakayatafakari na kama wanaona kuna hatua za kuchukua wachukue.”   “Kanisa limekuwa linapata kejeli za aina mbalimbali kutoka kwa watu hao na kuwatuhumu kuwa maskofu walifikia maamuzi ya kuandika waraka huo kutokana na sababu za kimaslahi kwa maana ya sadaka makanisani kupungua jambo ambalo si la kweli.” -As

Mpenzi wa Cristiano Ronaldo ametumia Kiswahili leo

Image
Lugha ya Kiswahili inaonekana kuzidi kukuwa na kuwavutia watu mbalimbali dunia kuitumia, leo April 1 2018 moja kati ya post za mitandao ya kijamii zilizochukua headlines ni post ya mwanamitindo  Georgina Rodríguez ambaye ni mpenzi wa staa wa soka wa Real Madrid Cristiano Ronaldo. Georgina Rodríguez ni mwanamitindo na ndio mpenzi wa sasa wa Ronaldo na wamefanikiwa kupata mtoto mmoja anayejulikana kwa jina la Alana Martina , hivyo katika insta story yake amepost picha yake na Ronaldo na kuandika ‘Hakuna Matata’ Msemo wa hakuna matata ni msemo wa Kiswahil i ambao umeonekana kupendwa na umekuwa msemo maarufu sana kwa wageni wanaopenda kujua lugha ya Kiswahili, huo huwa ni msemo wao wa kwanza kujifunza lakini haijajulkana bado  Georgina Rodríguez ameujulia wapi msemo huo.

PRETTY KIND AWAIBUA WABONGO TENA,KISA MABADILIKOYA AJABU

Image
Mrembo Suzan Michael ‘Pretty Kind’ aliyekuwa Bingwa wa picha za utupu mtandaoni ameonesha kubadilika kitabia hasa katika mitandao ya kijamii na hilo limeonekana baada ya kuanza kuutumia mtandao wake wa kiijamii wa Instagram. _ Ikiwa ni siku chache za msanii huyo kuwa huru baada ya kusamehewa kwa adhabu yake ya kifungo cha kutojihusisha na masuala ya muziki kwa muda wa miezi sita kutokana na hatua za Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo dhidi ya kukiuka maadili kupitia Naibu wa wizara hiyo Mhe. Juliana Shonza mwezi Januari mwaka huu.   Hizi ni picha baadhi za Msanii huyo ambazo anaonekana kubeba kitabu kitakatifu ‘Biblia’ na kuandika kuwa Mwenyezi Mungu kwa sasa anaweka sawa mambo ya kila kilichotoka katika mstari wake.

Rais Magufuli Aungana na Wakristo Kuadhimisha Misa ya Pasaka Kanisa la Mt. Joseph Dar

Image
Rais Magufuli leo ameungana na Wakristo wote Tanzania katika maadhimisho ya Misa Takatifu ya sikukuu ya Pasaka iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Joseph, Jimbo Kuu la Dar es Salaam. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakilakiwa kwa furaha na Paroko Msaidizi Venance Tegete walipojumuika na waumini wengine katika Maadhimisho ya Misa ya Sikukuu ya Pasaka katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam leo Jumapili Aprili 1, 2018 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli na waumini wengine wakisikiliza kwa makini mahubiri ya Paroko Msaidizi Venance Tegete katika Maadhimisho ya Misa ya Ibada ya sikukuu ya Pasaka katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam leo Jumapili Aprili 1, 2018 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakitoa sadaka katika Maadhimis

Meli ya abiria ya Uingereza iliyozamishwa mwaka 1942 yaondolewa baharini

Image
Meli ya abiria ya Uingereza iliyozamishwa wakati ilishambuliwa kwa bomu na ndege za Japan wakati wa vita vya pili vya dunia, imeinuliwa kutoka baharini pwani mwa Sri Lanka baada ya miaka 75. SS Sagain, ambayo abiria wake wengi na mizigo iliokolewa mwaka 1942, imeinuliwa na kundi la wapiga mbizi kutoka kwa jeshi la wanaji wa Sri Lanka, Ilikuwa karibu umbali wa futi 35 chini ya bahari katika bandari ya Trincomalee. Shughuli ya kuiinua meli hiyo ilichukua miezi kadhaa na ilifanywa na kikosi cha wanamaji cha Mashariki mwa Sri Lanka.

RAY C ATIBUKA VIBAYA,ATOA MANENO TATA KISA LADY JAY DEE,ASEMA BORA ATIWE MIMBA AZAE

Image
Muimbaji Ray C amefunguka mazito kwa kile anachoona kinaenda ndivyo sivyo katika muziki wa Bongo Flava kwa sasa. Ray C amefikia hata hatua ya kutumia maneno makali kueleza hisia zake kwa yale ambavyo hakubaliani nayo kwenye tasnia hiyo. Kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika; Kuna muda huwa nafikiria mambo mengi sana! kuna muda najiskia kuamua kutiwa mimba, nizae niwe tu mama wa nyumbani! maana kuna muda nikiangalia wasanii wenye maendeleo kwenye Bongo Flava ni wachache saaaaana! na sijiongelei mimi maana mimi mwenyewe kuna wakati nilivurunda mwenyewe! Nakubali nilibugi na nikagundua nimebugi haswa na ndio maana nimepambana mpaka hapa niliko baada ya kugundua baraka tele nilizozawadiwa na Mungu ni kubwa mno kuliko starehe za muda za ndogo na za kibwege!!! Ila huwa nakaa najiuliza miaka kama sita ambayo nilipotea kwenye industry! kuna wasanii nilianza nao na wana vipaji vya ajabu maskini lakini wengi wao wamezimwa kama taa!!! Namkumbuka Nature, Joseline, B

Halima Mdee Akamatwa na Polisi Akitokea Afrika Kusini

Image
Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee. Jeshi la Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemkamata Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee. Mdee amekamatwa leo alfajiri uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere akitokea nchini Afrika Kusini inakoelezwa alilazwa kwa matibabu. Meya wa Ubungo, Boniface Jacob amethibitisha kukamatwa kwa Halima Mdee ambapo amesema; “Ni kweli amekamatwa leo Saa 9 alfajiri Airport, akitokea Afrika Kusini alipokuwa amelazwa kwa matibabu na sasa yupo Central.” Mdee ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha) huenda akaunganishwa na vigogo wengine sita akiwamo Mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman Mbowe katika kesi inayowakabili. Vigogo hao wengine tayari wamekwisha kupandishwa kizimbani katika mahakama ya hakimu mkazi Kisutu, Dar es Salaam na kusomewa mashtaka nane. Kukamatwa kwa Mdee kunafikisha watuhumiwa saba kati ya nane ambao wamekwisha kuhojiwa mwingine ambaye bado na huenda anatafutwa na jeshi hilo ni mbun

ZARI THE BOSS LADY AKINUKISHA KUTUA BONGO NA KUTOENDA MADALE.MAMA YAKE DIAMOND ATIBUKA

Image
DAR ES SALAA: Zarinah Hassan ‘Zari The Boss lady’, aliyekuwa baby mama wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu abdul ‘Diamond Platnumz’, amekinukisha ile mbaya baada ya kutua Bongo na kutokwenda nyumbani kwa jamaa huyo, Madale-Tegeta jijini Dar, risasi Jumamosi limenyetishiwa. ATUA USIKU WA MANANE, AFIKIA HOTELINI Zari alitua Dar usiku wa manane wa Jumanne iliyopita na kufikia katika Hoteli ya Hyatt Regency The Kilimanjaro, zamani Kempinski iliyopo Posta, Dar na mapema kesho yake (Jumatano iliyopita), alisaini dili nono na Kampuni ya Softcare. Zari alisaini dili hilo la mamilioni, tukio lililofanyika mbele ya vyombo vya habari kwenye ukumbi wa hoteli hiyohiyo na sasa akawa ndiye balozi mkuu wa pampers za watoto zinazosambazwa na kampuni hiyo. Zari The Boss lady akiwa na Diamond. AULIZWA KUHUSU DIAMOND Katika zoezi hilo la kusaini dili hilo, ulipofika muda wa maswali, Zari aliulizwa juu ya uhusiano wake na Diamond ambapo ‘aliwaka’ na kusema kwamba, kilichomleta Bongo ni dili

Nafasi za Kazi 30 Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma

Image
Mkurugenzi  wa Halmashauri  ya Manispaa ya Dodoma , kupitia kibali cha Ajira anapenda kuwatangazia wananchi wote wa Tanzania wenye sifa za kuajiliwa katika Utumishi wa Umma kuleta maombi ya kazi kwa nafasi ya Mtendaji wa Kijiji kama ifuatavyo

Madhara ya kujichubua

Image
Katika baadhi ya sehemu duniani watu wanaamini kuwa ngozi angavu huashiria uzuri, utajiri na uwezo(kifedha) alionao mtu.Katika baadhi ya sehemu watu wenye ngozi nyeusi huchukuliwa kuwa wapo chini ya kiwango, hii hupelekea watu hawa kutumia ving´arisha ngozi kama krimu, vidonge au nyenzo zingine kubadilisha ngozi zao.  Tafiti zinaonyesha kwamba wavulana na wasichana hupendelea kutumia bidhaa zinazong´arisha ngozi ili waweze kupata hadhi nzuri katika kundi la familia zao, na jamii. Kwa kweli,hata matangazo yanayoonyeshwa kwenye televisheni mbalimbali huonyesha kitu hiki. Mambo hayo yote huwa na athari kubwa juu ya mawazo ya vijana wa kiume na wakike ambayo hupelekea kuwafanya wachague chochote wanachomudu kati ya krimu au vidonge. Madhara ya kujichubua ni yapi? Mtu anaeyejichubua anaweza kupata kansa ya ngozi, chunusi, uvimbe katika ngozi, ngozi kuwa nyembamba,Kuongezeka kwa hamu ya kula na uzito,kutokwa na mabaka, pumu, kupata watoto wenye kasoro, kupata ma

MAGAZETI YA LEO 29/3/2018

Image