Posts

Mahakama Yaamuru mmiliki wa IPTL Akatibiwe Muhimbili

Image
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeamuru mmiliki wa IPTL, Harbinder  Sethi akatibiwe katika Hospital ya Taifa Muhimbili baada ya mshtakiwa huyo kulalamika afya yake imearibika sana. Mbali ya Sethi, mshtakiwa mwingine ni mfanyabiashara James Rugemarila ambapo kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka 12 ya uhujumu uchumi, utakatisha fedha na kuisababisha Serikali hasara ya USD 22, 198,544.60 na Bilioni 309. Mwendesha Mashtaka wa TAKUKURU, Leornad Swai amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi leo March 28, 2018 kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na pia wanafatilia vielelezo vya upelelezi nje ya nchi. Baada ya kueleza hayo, Seth alisimama na kumueleza Hakimu Shaidi kuwa; 'Afya yangu imearibika sana, nahitaji kupelekwa hospitali.' Kutokana na maelezo hayo, Hakimu Shaidi amesema ni dhahiri afya ya mshtakiwa ikiangaliwa hata kwa macho inaonekana ni dhahifu. “Naamuru mshtakiwa akatibiwe katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ili afya yake iwe njema,” amesema

BASATA Yakanusha Kuzifungulia Nyimbo Mbili za Diamond

Image
Staa wa muziki wa Bongo fleva Diamond Platnumz. Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), limesema nyimbo mbili za Diamond, hazijafunguliwa kama inavyodhaniwa. Katibu Mtendaji wa Baraza hilo Godfrey Mngereza amesema nyimbo za Wakawaka na Hallelujah hazijafunguliwa na jambo hilo halina ukweli wowote na kuwataka wananchi kulipuuza. Kadhalika, Mngereza ametoa ufafanuzi kwa nini msanii Diamond amekutana na Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe na Naibu wake, Juliana Shonza na sio wasanii wengine. Mngereza ametoa ufafanuzi huo baada ya kusambaa kwa taarifa iliyoeleza msanii huyo kakutana na mawaziri hao. Baada ya taarifa hizo, kulizuka gumzo mitandaoni ambapo watu walihoji kwa nini wakutane na msanii huyo wakati kuna waliofungiwa nyimbo zao kama yeye na wengine kufungiwa kufanya muziki kwa miezi sita. Mngereza amesema hatua hiyo imetokana na majibizano yaliyokuwa yanaendelea kati ya Diamond na naibu waziri Shonza na ndio sababu iliyowafan

Vyakula vya Kukufanya Usizeeke

Image
KIINI CHA YAI L EO kwenye safu hii nitakuletea vyakula ambavyo ukila vitakufanya usizeeke kwani siku hizi watu wanazeeka haraka licha ya kuwa na umri mdogo.  Kama unataka kusafisha ubongo wako ambao huchoka mara kwa mara tumia kiini cha yai, kina wingi wa Klorine ambayo ni virutubisho muhimu vinavyowezesha ubongo kufanya kazi. COCOA Kama unafanya urembo wa ngozi hasa chini ya macho kwenye ngozi inayoweka weusi paka cocoa ina wingi wa vitamin itakayosaidia kulinda ngozi yako isizeeke. KAHAWA NA MAFUTA YA NAZI Kama unataka kuwa na nguvu kwa siku chukua kahawa yako iweke na vijiko viwili vya chai vya mafuta ya nazi kisha kunywa. Mafuta ya maboga kwa kuondoa msongo wa mawazo, Kama wewe ni mtu mwenye msongo wa mawazo mara kwa mara tumia mafuta ya maboga yana wingi wa asidi ya amino na glutamate ambayo yanasaidia ubongo kukaa sawa na wewe kujisikia vizuri. Mafuta haya ni mazuri kuyatumia hata kwa mtu mwenye mba kichwani ili kuzitibu yapake kwenye ngoz

JK' kuwa mgeni rasmi katika harambee

Image
RAIS mstaafu, Jakaya Kikwete anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika harambee ya kukusanya fedha kiasi cha Sh. bilioni moja, kwa ajili ya ukarabati wa Shule ya Sekondari Lindi iliyoungua Julai 2016. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi alisema harambee hiyo itafanyika kesho jijini Dar es Salaam. Zambi alisema maandalizi yote kwa ajili ya harambee hiyo yamekamilika na inatarajia kuhudhuriwa na wadau wa sekta ya elimu nchini. Alisema harambee hiyo imepanga kukusanya Sh. bilioni moja ikiwa ni karibu nusu ya mahitaji ya Sh. bilioni mbili zinazotakiwa kwa ajili ya ukarabati wa shule hiyo kongwe. “Kutokana na fedha tutakazokusanya, tumepanga ujenzi uanze wakati wowote. Zoezi hili litakwenda sambamba na mpango wa mkoa kuboresha mfumo mzima wa masuala ya elimu toka ngazi ya awali,” alisema Zambi. Mkuu wa mkoa huyo alikiri kuwa mkoa wake ni mmoja kati ya inayofanya vibaya kwenye matokeo ya mitihani ya kitaifa,

Rungwe aliomba Jeshi la Polisi kusaidia upatikanaji wa ndugu zake

Image
Mwanyekiti wa Chama Cha Ukombozi wa Umma (CHAUMA) Hashim Rungwe ameliomba jeshi la polisi kusaidia upatikanaji wa Mpwa wake Saida Hilal (40) na mumewe Abdallah Kutiku ambao hawajaonekana tangu Machi 26, 2018 majira ya asubuhi. Hashim Rungwe amesema hayo leo Machi 27, 2018 na kudai Saida Hilal aliaga wenzake ofisini na kwenda kituo cha polisi kufuatilia suala la mume wake Abdallah Kutiku ambaye alichukuliwa na polisi "Huyu binti alikuwa anafuatilia habari za mumewe polisi kwa kuwa mumewe alikuwa amekamatwa na polisi hivyo naye hapatikani kwa hiyo wote wawili hawaonekani kwani tulipofika kituo cha polisi walisema hawa watu hatuwafahamu na wala hawajafika pale, tangu hapo Bi. Saida Hilal hapatikani kwenye simu zake na tumefanya jitihada kumtafuta kwenye vituo vya polisi na mahospitali kama Muhimbili, Mwananyamala na sehemu zingine za usalama bila mafanikio" Rungwe aliendelea kuelezea kuwa "sehemu zote ambazo alikuwa anapenda kutembelea zote tumepita na

Linex azungumzia ishu ya kupotezwa na Ulevi

Image
Sunday Mangu ‘Linex’ MSANII wa Bongo Fleva, Sunday Mangu ‘Linex’, ameibuka na kufungukia tetesi zinazozagaa dhidi yake kuwa ulevi ndiyo umempoteza kimuziki na kusema siyo kweli bali wanaozungumza hivyo ni wabaya wake ambao hawana nia nzuri kwake. Akipiga stori na Risasi Vibes, Linex alisema kuwa muziki ni kama biashara nyingine na mtu anaweza kushuka na kupanda hivyo kilichompoteza ni changamoto za maisha kuwa nyingi na kushindwa kuzimudu ila anaamini atarejea tena na kuwa kama alivyokuwa zamani. “Wanaosema kwamba nimepotea kimuziki kisa ulevi hawana nia njema na mimi, mwanamuziki yeyote anaweza kupotea bila kujali umaarufu alionao, ndiyo maana hata Bill Gates leo anaweza kuwa namba moja kwenye listi ya matajiri duniani na baada ya muda hata kwenye kumi bora akawa hayumo tena,” alisema Linex. Linex azungumzia ishu ya kupotezwa na Ulevi Muungwana Blog 5 Wednesday, March 28, 2018 Sunday Mangu ‘Linex’ MSANII wa Bongo Fleva, Sunday Mangu ‘Linex’, ameibuka na kufu

MAKONDA: UKIMPA UJAUZITO MWANAMKE DAR UJIPANGE

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, akizungumza na wataalamu hao. . …Makonda akiendelea kuzungumza katika tukio hilo. Baadhi ya wataalamu wa masuala ya kisheria waliohudhuria kwenye hafla hiyo. Mkutano huo na wataalamu wa kisheria ukiendelea. JOPO la Wataalamu kutoka Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Maofisa Ustawi wa Jamii, Wanasheria pamoja na askari Polisi kutoka Dawati la Jinsia  wamemuhakikishia Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda, kuwa wamejidhatiti vyema kuwasikiliza akinamama waliotelekezwa na hawapatiwi pesa ya matunzo ya mtoto kwenye zoezi la siku tano za kuwapatia msaada wa kisheria linalotaraji kuanza Aprili 9 mwaka huu. Akizungumza na wataalamu hao leo, Makonda amesema tatizo la wamama waliotelekezwa ni kubwa na limekuwa likisababisha kinamama na watoto kuishi maisha ya tabu na kusababisha ongezeko la watoto wa mitaani na vizazi vya watoto wenye chuki na baba zao. Makonda amesema lengo la zoezi hilo sio ugomvi bali ni kumw

Mbowe, Mashinji, Mnyika na Wengine Wawekwa Mahabusu Sentro

Image
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa, Freeman Mbowe na baadhi ya viongozi wengine waandamizi wa chama hicho akiwepo Katibu Mkuu Dkt Vincent Mashinji, John Mnyika, Salum Mwalimu na Ester Matiko wamewekwa mahabusu katika Kituo Kikuu cha polisi Dar es Salaam. Mkuu wa Idara ya Mawasiliano na Habari CHADEMA Tumaini Makene amethibitisha hilo na kusema kuwa viongozi hao wamewekwa mahabusu leo Machi 27, 2018 baada ya kuripoti Kituo Kikuu Cha Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam wakitimiza masharti ya dhamana yao. “Viongozi Wakuu wa Chama pamoja na wabunge waliokuwa wameripoti Kituo Kikuu cha Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam wakitimiza masharti ya dhamana yao, wamewekwa mahabusu. Polisi hawajaeleza sababu ya kufanya hivyo. Mawakili wetu wanashughulikia. Tutaendelea kuwapatia taarifa zaidi,” alisema Makene.

Maua Sama afunguka mwaka wa kuolewa

Image
Maua Sama.   MKALI mwenye sauti ya kumtoa nyoka pangoni, Maua Sama kwa mara ya kwanza ametaja mwaka wa kuolewa kuwa mambo yakienda sawa mwaka huu unaweza kuwa wake. Awali zilienea tetesi kuwa, staa huyo anayebamba na Ngoma ya Nakuelewa amechumbiwa na mpenzi wake ambaye ni Mzungu lakini mwenyewe ameibuka na kukanusha. “Nilishangaa kwa kweli hilo suala la kuchumbiwa na Mzungu kwani halikuwa la kweli, kuhusu kuolewa nimekuwa nikisikia kwa mashabiki sana, ndoa ni mipango, maombi yao yanaweza kunifanya nikatimiza hilo na inawezekana hata mwaka usiishe,” alisema Maua.

Wapiga picha za utupu wadakwa na Jeshi la Polisi

Image
Jeshi la Polisi Mkoani Morogoro linawashikilia watu 6 akiwemo Mabula Mabula mkazi wa mji mpya kwa tuhuma za kujifanya askari na kuwakamata wanawake nyakati za usiku, kuwapora mali, kuwafanyia vitendo vya kikatili kuwalawiti na kuwapiga picha za utupu. Hayo yamethibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Ulrich Matei na kusema kukamatwa kwa mtuhumiwa Mabula ni kufuatia matukio kadhaa ya aina hiyo yaliyo ripotiwa kutokea katika maeneo tofauti ya mji huo. Kamanda Mtei amesema baada ya kupata taarifa, jeshi hilo kwa kushirikiana na timu ya wataalam wa makosa ya mitandao pamoja na Kikosi cha kupambana na ujambazi wakafanikisha kupatikana kwake ambaye baada ya mtuhumiwa kuhojiwa alikiri kuhusika matukio hayo na kudai anafanya hivyo kwa lengo la kujipatia fedha. Kwa upande mwingine, Jeshi hilo linawashikilia watu watatu ambao ni vinara wa matukio ya utapeli pamoja na wizi kwa njia ya mtandao wakiwa na simu 9 pamoja na line 57 za mitandao mbalimbali zinazotumika kufa

BREAKING NEWS:JPM Awasimaisha Kazi Wakurugenzi Halmashauri Kigoma Ujiji, Handeni

Image
IKULU: Rais Magufuli amewasimamisha kazi Wakurugenzi wa Halmashauri za Kigoma Ujiji na Pangani baada ya kuandikiwa hati chafu kwenye Vitabu vya Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) iliyowasilishwa leo. “Kuna Wilaya mbili, Halmashauri Mbili zina hati chafu, Mimi nafikiri Kigoma Ujiji na Pangani, Mimi nafikiri saa nyingine tuchukue hatua kwa vile Waziri wa TAMISEMI upo hapa WAKURUGENZI wa Wilaya hizo WASIMAMISHWE kazi leo” -Rais Magufuli

MAJIBU YA DAKTARI SIMBA BAADA YA MKUDE KUUMIA JANA

Image
Kiungo mchezaji wa Simba, Jonas Mkude , aliumia jana wakati kikosi hicho kikijiandaa na mazoezi kuelekea mchezo ujao wa ligi dhidi ya Njombe. Mkude aliumia wakati akiwania mpira na kiungo mshambuliaji, Mzamiru Yassin na kuepelekea kuanguka chini kisha kutolewa nje ya Uwanja wa Boko Vetarani. Kufuatia kuumia huko, kwa mujibu wa Afisa Habari wa Simba, Haji Manara, Daktari wa timu hiyo, Yassin Gembe , alisema Mkude hajapata maumivu makali, na anaweza akarejea baada ya siku mbili mpaka tatu. Wakati Simba inajiandaa kuivaa Njombe Mji, Aprili 3 2018 , kumekuwa na hofu kubwa kwa mashabiki kama ataweza kurejea mapema, japo majibu ya Daktrari yameeleza hatachukua muda mrefu. Na George Mganga.

Breaking: Abdul Nondo Asimamishwa Masomo Chuo Kikuu

Image
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) , Profesa William Anangisye, amemsimamisha masomo Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi (TSNP), Abdul Nondo hadi kesi yake ya kutoa taarifa za uongo mitandaoni na kudanganya kutekwa itakapomalizika. Nondo alipewa dhamana na mahakama ya Iringa, jana Jumatatu,Machi 2018 baada ya kusota rumande kwa wiki kadhaa. TAARIFA YA CHUO KIKUU DAR ES SALAAM

Marekani: FBI Aliyetambua Shamulio la Osama Afariki kwa Sumu

Image
SHIRIKA la Uchunguzi la Marekani (FBI) limesema limempoteza mwanamama mmoja ambaye ni miongoni mwa waliotambua shambilizi la kigaidi la Septemba 11, 2001 lililofanywa na Osama BinLaden, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 48. Melissa S. Morrow alifariki juzi Alhamisi akiwa na miaka 48 kwa kansa ya ubongo huku ikielezwa kuwa, huenda kifo chake kilisababishwa na kuwekewa vitu vyenye sumu (kemikali). Mtaalam huyo wa uchunguzi, amefanya kazi ndani ya FBI kwa miaka 22, na wakati umauti unamfika alikuwa ana siku chache tangu ahamishiwe katika kituo kipya cha kazi, Kansas City. Taarifa ya FBI imeeleza kuwa, Morrow alikuwa amejitoa kwa kiasi kikubwa kulitumikia taifa lake kwa kuchunguza na kubaini ukweli wa shambulio la Spetemba 11, katika Makao Makuu ya Jeshi la Marekani, Pentagon,. Inadaiwa mama huyo baadaye alikutwa kwenye  ghala lenye sumu mwaka 2013 jambo lilliloplekea kuzorota wa kwa fya yake  licha ya kutibiwa kwa zaidi ya wiki 10 huku akikusanya taarif

Waziri Mkuu Majaliwa aridhishwa na ujenzi wa Terminal III

Image
 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametembelea mradi wa ujenzi wa jengo la tatu la abiria katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) na kwamba ameridhishwa na maendeleo yake. Mradi wa ujenzi wa jengo hilo umefikia asilimia 70 na unatarajiwa kukamilika Juni 2019 na utakuwa na uwezo wa kuegesha ndege kubwa 24 kwa wakati mmoja, pamoja na kuhudumia abiria milioni sita kwa mwaka na kuwa na. Waziri Mkuu ambaye ametembelea mradi huo leo (Ijumaa, Machi 23, 2018) amesema amefarijika na maendeleo ya ujenzi wa mradi huo pamoja na kukuta Watanzania wengi wakishiriki katika kazi za ujenzi. “Serikali imejiimarisha katika kuboresha usafiri wa anga, ambapo kukamilika kwa jengo hili kutachangia ongezeko la ndege kubwa nyingi kutua nchini. Pia sekta ya utalii nayo itaimarika kwa kuwa watalii wanaoingia nchini wataongezeka.” Amesema mbali na ujenzi wa jengo hilo, pia Serikali inaendelea kuvikarabati viwanja mbalimbali vya ndege nchini kikiwemo cha Musoma, Iring

Saba Wafariki Ajalini Mkoani Kigoma

Image
Lori likiwa limepinduka. Hali ilivyokuwa mahali ilipotokea ajali. Mashuhuda wakitazama mabaki ya lori hilo. Watu saba wamefariki katika ajali iliyohusisha lori aina ya Scania lililokuwa likitokea kijiji cha Mkongoro mkoani Kigoma ambapo dereva wake alishindwa kulimudu wakati akishuka kwenye mteremko uliokuwa na kona kali na kumgonga mtembea kwa miguu na kisha likapinduka. Mkuu wa Polisi mkoani Kigoma, Martin Otieno, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.

ALIYETEKA NDEGE YA TANZANIA MWAKA 1982 KUMTAKA NYERERE AJIUZULU AFARIKI

Image
  Wakili nguli Yasin Memba anayedaiwa kuteka ndege ya Tanzania mwaka 1982 amefariki dunia jana Jumanne Machi 20, 2018 jijini Dar es Salaam baada ya kuugua kwa muda mrefu. Kwa mujibu wa wakili wa kujitegemea na mwanachama wa Chama cha Wanasheria Tanganyika, (TLS) Mathew Kakamba, amesema Memba amefariki dunia katika Hospitali ya Aga Khan na kuzikwa katika makaburi ya Kinondoni jijini humo. Memba ni miongoni mwa watanzania wawili wanaodaiwa kuteka ndege ya Tanzania iliyokuwa na abiria 90, Februari 1982 wakishinikiza Rais wa wakati huo, Julius Nyerere kujiuzulu. Chanzo - Mwananchi

BARAZA LA MITIHANI -NECTA LAFANYA MABADILIKO MTIHANI DARASA LA SABA

Image
Wanafunzi wa darasa la saba ambao watafanya mtihani mwaka huu watakutana na mabadiliko ya mfumo wa utungaji wa mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi . Mabadiliko hayo yamefanywa na Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) jana na kutangazwa na Katibu Mtendaji wa baraza hilo, Dk Charles Msonde. Ofisa Habari wa Necta, John Nchimbi amesema mabadiliko hayo aliyatangaza Dk Msonde katika mkutano mkuu wa tano wa maofisa elimu mkoa na wilaya unaofanyika Dodoma. Nchimbi amesema katika muundo huo mpya kila somo litakuwa na maswali 45, kati ya hayo, maswali 40 yatakuwa ya kuchagua jibu sahihi na matano yasiyo ya kuchagua (yatakuwa ya kujieleza/kuonyesha njia na jibu nk). Amesema maswali 40 kila swali litakuwa na alama moja na maswali matano kila swali litakuwa na alama mbili huku majibu ya maswali 40 yatajibiwa kwenye OMR FORM na maswali matano yatajibiwa kwenye karatasi maalum itakayoandaliwa. Kutokana na muundo huo mpya, Necta imetoa wito kwa walimu

Faida 10 za kutumia Mafuta ya Nazi

Image
1. Mafuta ya nazi kwa afya ya Moyo: Mafuta ya nazi yana asidi mhimu sana kwa afya ya moyo iitwayo ‘lauric acid’ ambayo ina uwezo mkubwa kuuweka moyo wako katika hali ya afya na furaha kwa kuidhibiti kolesteroli/lehemu mbaya katika moyo na mwili kwa ujumla. Lauric acid huongeza uwepo wa kolesteroli nzuri mwilini ijulikanayo kwa kitaalamu kama High Density Lipoprotein (HDL) huku ikiishusha ile kolesteroli mbaya ijulikanayo pia kwa kitaalamu kama Low Density Lipoprotein (LDL) jambo ambalo ni mhimu kwa afya ya moyo kama anavyosema Lovisa Nilsson, mtaalamu wa lishe wa Lifesum. 2. Mafuta ya nazi huuongezea nguvu mfumo wa mmeng’enyo wa chakula: Hii ndiyo moja ya faida ya mafuta ya nazi niipendayo zaidi. Ndiyo mafuta ya nazi yanayo uwezo kusaidia kudhibiti uzito uliozidi kwa sababu mafuta haya ni mepesi kumeng’enywa na hayagandi kama yalivyo mafuta mengine mazito (fatty acids) jambo linalosaidia kuuondoa uzito uliozidi mwilini. Kutokana na kitendo hiki cha kuongeza uwezo wa

Breaking News: Abdul Nondo Arudishwa Iringa, Apandishwa Kizimbani

Image
Mwenyekiti wa mtandao wa wanafunzi, Abdul Nondo amerudishwa mkoani Iringa na kufikishwa Mahakama ya Wilaya. Awali Nondo alitolewa Iringa baada ya mahojihano na Polisi na kupelekwa Dar kwa Mkurugenzi wa Upelelezi makosa ya Jinai kwa mahojiano. Kwa mujibu wa Wakili wake, Jebra Kambole, amesema dhamana ya Nondo itatazamwa Jumatatu ijayo Machi 26, baada ya hakimu kuomba kusoma sheria inasemaje juu ya kuzuiwa dhamana kwake. Imeelezwa kuwa, Nondo amesomewa mashtaka kwa makosa ya kutoa taarifa za uongo Mitandaoni na kosa la pili ni kudanganya kuwa alitekwa. Shauri limeahirishwa na mtuhumiwa amepelekwa rumande.