Breaking News: Abdul Nondo Arudishwa Iringa, Apandishwa Kizimbani

Mwenyekiti wa mtandao wa wanafunzi, Abdul Nondo amerudishwa mkoani Iringa na kufikishwa Mahakama ya Wilaya. Awali Nondo alitolewa Iringa baada ya mahojihano na Polisi na kupelekwa Dar kwa Mkurugenzi wa Upelelezi makosa ya Jinai kwa mahojiano.

Kwa mujibu wa Wakili wake, Jebra Kambole, amesema dhamana ya Nondo itatazamwa Jumatatu ijayo Machi 26, baada ya hakimu kuomba kusoma sheria inasemaje juu ya kuzuiwa dhamana kwake.

Imeelezwa kuwa, Nondo amesomewa mashtaka kwa makosa ya kutoa taarifa za uongo Mitandaoni na kosa la pili ni kudanganya kuwa alitekwa. Shauri limeahirishwa na mtuhumiwa amepelekwa rumande.

Comments

Popular posts from this blog

PICHA ZA UTUPU ZILIZOPIGWA NA MWANAFUNZI WA UDOM ILI KUTANGAZA SOKO LA MWILI WAKE. TAZAMA HAPA

ZITTO KABWE AWAPONDA LOWASSA NA MAGUFULI