Posts

Wolper Atokwa na Povu Baada ya Kubanwa Kuhusiana na Madai ya Kunuka Mwili

Image
Staa wa filamu ‘grade one,’ ‘Jacqueline Wolper’. STORI: ALLY KATALAMBULA NA BONIPHACE NGUMIJE, IJUMAA , HABARI Staa wa filamu ‘grade one,’ ‘Jacqueline Wolper’ ametokwa povu si la nchi hii baada ya kubanwa kuhusiana na madai ya kunuka mwili na kusema hajawahi kunuka maishani mwake na kwamba ingekuwa hivyo asingepapatikiwa na wanaume. Hivi karibuni Ijumaa lilimfungia kazi msanii huyo nyumbani kwake na katika moja ya maswali aliyobanwa lilikuwa juu ya ishu iliyosambaa kuwa eti anatoa harufu mbaya sehemu za mwili wake. Katika kuonesha kumaindi ile mbaya kuhusu madaia hayo, mrembo huyo ambaye kiukweli yuko bomba kwa muonekano alifunguka: “Aliyekuambia nanuka nani? Mimi sinuki wala sijawahi kunuka maishani mwangu, kuthibitisha hilo kwanza nisingekuwa napapatikiwa na wanaume kila kukicha sambamba na kuhongwa vitu kibao huku wengine nikiwaacha wakinililia. Hao wanaosema na kusambaza hayo ni njia tu ya kujipatia followers kwenye mitandao yao kupitia mimi.” Wolp

Polepole: Watu wanaishi kwa hofu

Image
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole amefunguka na kusema watu wamekuwa na hofu huku wengine wakihama makazi yao mkoani Pwani kutokana na vitendo vya mauaji vinavyoendelea mkoani humo. Polepole amesema wao kama CCM wanaitaka serikali ichukue hatua za haraka katika jambo hilo kwa kuwa ina vyombo vyote vya ulinzi na usalama, hivyo wanataka kuona jambo hilo linapewa umaalum katika kulishugulikia. "Sisi kama chama tumelifuatilia hili suala kwa umakini sana na tumeona ni vyema kusimama na Watanzania wakiwepo na wanachama wa CCM wa maeneo haya, tunatambua wanapitia wakati mgumu sana kwani wapo viongozi wetu, wapo wanachama wa CCM, na watendaji mbalimbali wamepoteza maisha. Wamepoteza maisha si kwa sababu ya mapenzi ya Mwenyezi Mungu bali maisha yao yamekatizwa kikatili" alisisitiza Polepole Kufuatia mambo haya kuendelea kutokea mkoani Pwani Chama Cha Mapinduzi kimetoa salamu za pole kwa wananchi wote ambao wameguswa na misiba ya watu am

Faida (6) za tangawizi

Image
Siku kadhaa zilizopita tuliona kwa uchache faida za tangawizi, naomba siku ya leo tuendelee faida nyingine za tangawizi ambazo ni; 1. Husaidia wenye kifafa au Msongo wa mawazo Wataalamu wanasema kifafa kinasababishwa na mishipa kuvimba na kukandamiza ubongo na tangawizi inatumika husaidia kuondoa mafuta katika mishipa, kutia joto mwili na kusaidia damu yenye oxygen kusambaa mwilini na kwenye ubongo bila shida. 2. Huondoa gesi tumboni Tangawizi husaidi mmeng'enyo wa chakula tumboni, kwa hiyo husaidia matatizo mengi yanayosababishwa na ulaji. 3. Husaidia kutibu mafua, kikohozi Unachitakiwa kufanya. Changanya mdalasini, pilipili manga kidogo, chemsha kama chai pamoja na tangawizi. Husaidia sana mafua na kikohozi. 4. Huongeza nguvu za kiume Tangawizi inauwezo wa kuongeza joto mwilini, hivyo huamsha mishipa ya fahamu katika mwili wa mwanaume mwenye tatizo hilo. 5.Huongeza maziwa kwa kina mama wanyonyeshao. Kwa kina mama wanaonyenyesha tangawizi inachoche

NAIBU WAZIRI DKT.KINGWANGALLA AMTEMBELEA MZEE MAIGE’NGOSHA ‘ MUHIMBILI

Image
Naibu Waziri Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Hamisi Kingwangalla akiongea na Mzee Maige ambaye amelazwa kwenye chumba cha kitengo cha dharura cha Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambapo asubuhi ya leo mzee huyo alihamishiwa hapo kwa uchunguzi wa afya na matibabu zaidi kutoka hospitali ya Rufaa ya Amana. Daktari Bingwa wa magonjwa ya dharura Renatus Tarimo(kushoto) akimueleza Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto jinsi walivyompokea na kumuhudumia kwenye kitengo chao na hali ilivyo hadi sasa,Dkt. Tarimo amesema hali ya Mzee maige inaendelea vizuri na wameshamfanyia uchunguzi wa awali na wanaendelea na uchunguzi zaidi Mkuu wa Kitengo cha Dharura Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Dkt. Juma Mfinanga (katikati) akimueleza jambo Naibu Waziri Dkt. Kingwangalla mara baada ya kutoka kwenye chumba alicholazwa Mzee Maige.Mzee Maige au kwa jina maarufu anajulikana kama Ngosha ndiye aliyebuni Nembo ya Taifa ambayo ina

COUPLE YAJIUWA, YAACHA UJUMBE MZITO KISHA KUJITUPA MTONI

Image
Mume na mke walioamua kujitupa ndani ya mto kwa kile walichokiita 'mkataba wa kujiua'  wameacha ujumbe na kusema kwamba hiyo imewalazimu baada ya kuona kuwa hakuna msaada kwa ajili ya afya ya akili ya mwanamke. Jennifer Slack, 63, na mume Graham, 62, walikufa maji katika Mto Yare Couple iliacha ujumbe kwa madai Bibi Slack hakupata 'msaada' kwa matatizo ya akili.  Uchunguzi umesema kulikuwa na ucheleweshaji wa kesi yake zinashughulikiwa na shirika la NHS trust. Mstaafu muuguzi Jennifer Slack, 63, na mume wake Graham, 62, wamejifunga wenyewe pamoja na kujitupa kwenye Mto Yare katika eneo maarufu kama Gorleston karibu na Great Yarmouth.  Miili yao ambayo ilikutwa ikiwa imeliwa na ndege wa asubuhi na kufunikwa kwa matope  ilikutwa imetupwa pembeni ya gorofa jirani Breydon.

Jenga Heshima kwa Jamii Kwa kufanya Mambo Haya Matatu

Image
Hakuna ubishi wowote, heshima ni moja ya kitu ambacho karibu kila mtu anakitafuta katika maisha yake. Hakuna mtu ambaye hataki asiwe wa kuheshimika, heshima inatafutwa na watu wengi sana. Ndio maana utakuta kuna watu wanatumia pesa au mbinu nyingi sana kuweza kujenga heshima. Hali hiyo yote inaonyesha kwamba heshima ni mojawapo ya kitu cha thamani na kinachokubalika sana katika jamii yoyote ile. Pamoja na umuhimu wa heshima kwa wengi, sasa kitu ambacho tunatakiwa tujiulize mimi na wewe ni kwamba, je, kati yetu ni wangapi hasa wanajua namna ya kujenga heshima zao katika jamii? Je, pesa peke yake ndio ina uwezo wa kujenga heshima? Au ni kitu gani ambacho unatakiwa uwe nacho ili kikusaifdie kuweza kujenga heshima kubwa katika jamii na kujikuta ukikumbukwa pengine vizazi na vizazi? Kama nia yako ni kutaka kujenga heshima na ukawa mtu wa kuheshimika, fahamu mambo haya;- 1. Toa thamani. Ili uweze kujenga heshima kubwa kwa jamii inayokuzunguka, toa thamani, fanya vi

Dodoma waanza kutenga maeneo ya biashara

Image
MWENYEKITI wa Kamati ya Mipango Miji na Mazingira ambaye pia ni Diwani wa Kikuyu Kusini, Anselm Kutika amesema kata zote za Manispaa za Dodoma zitatenga maeneo kwa ajili ya wafanyabiashara, jambo litakaloondoa tatizo la wafanyabiashara kufanya kazi zao katika maeneo yasiyoruhusiwa. Kutika alisema kata zote za Manispaa ya Dodoma ni lazima zitenge maeneo kwa ajili ya wafanyabiashara ili kuuweka mji katika hali ya usafi. Alitaja sehemu ambazo tayari zimetenga maeneo kwa ajili ya biashara kuwa ni Kisasa, Tambukareli, Kikuyu Kusini, Kizota, Chang’ombe, Nkuhungu, Makole na Kiwanja cha Ndege. “Kamati ya Mipango Miji imepitipisha maeneo kwa ajili ya wafanyabiashara na maeneo hayo yatakuwa kikata na wananchi watakuwa walinzi namba moja,” alisema. Akaongeza, “Kikuyu Kusini tulitoa matangazo kama kuna mtu aliyefikiwa na tangazo na walengwa walikuwa ni wakazi wa kata, hapo awali changamoto ilikuwa baadhi ya D centre zilivamiwa na wakazi wan je ya kata.” Alisema baadh

MANENO YA MWIGULU NCHEMBA, POLISI,VIONGOZI NA 'VILIO VYA WANANCHI' SAKATA LA MAUAJI KIBITI

Image
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba, amefanya ziara ya kushtukiza wilayani Kibiti mkoani Pwani na kuteta kwa faragha na askari wa operesheni maalumu ya kuwasaka wauaji. Alisema  mauaji sasa yametosha na Serikali haitikuwa tayari kuona vitendo hivyo vinaendelea   kama ilivyo nchini Somalia. Ziara ya ghafla  imetokana na matukio ya mauaji ya mara kwa mara ya raia katika eneo hilo ambayo yamekuwa yakifanywa na watu wasiojulikana. Akizungumza  wilayani hapa  baada ya kuwatembelea  polisi   katika kambi maalumu ya operesheni ya kusaka wahalifu katika Kata ya Bungu, Mwigulu alisema  Serikali haiwezi kuvumilia mauaji ya mara kwa mara kama yanayotokea Somalia. Waziri alisema serikali  imejipanga kudhibiti hali hiyo kwa sababu kufuga wauaji na wahalifu kuna gharama. “Tunaendelea kufuatilia kazi ambazo mnaendelea kufanya, mapambano ambavyo yameendelea, tuendelee kusonga mbele. “Nikiziangalia takwimu na mwenendo, nazidi kupata maswali n

TABIA 4 ZINAZOHARIBU KINGA ZA MWILI BILA KUJIJUA

Image
Kinga ya mwili ni ile hali ya mwili kuwa na uwezo wa kujikinga wenyewe dhidi ya maradhi mbalimbali.  Mtu anapokuwa na kinga imara za mwili, huepuka kuugua mara kwa mara na kwa kifupi unaweza kusema kwamba kinga ya mwili ndiyo kila kitu katika afya ya binadamu.  Kuumwa mara kwa mara ni dalili tosha kuwa kinga yako ya mwili imeshuka na hivyo unahitaji kuchukua hatua za kuziimarisha. Kwa kawaida Mungu alituumba miili yetu ikiwa na uwezo wa kujikinga na magonjwa yote, laikini mwili utaweza kufanya hivyo endapo tu utapatiwa vyakula vinavyohitaji ili kuimarisha kinga zake. Leo tuangalia aina ya vyakula vya kuepuka ili kuzifanya kinga za mwili kufanya kazi zake vizuri. 1. Mhusika anapaswa kuepuka vyakula vyenye sukari nyingi Sukari siyo nzuri kwa afya yetu hasa inapotumiwa kupita kiwango. Kiwango cha kawaida cha sukari kinachoruhusiwa kutumiwa ni kijiko kimoja kidogo (teaspoon), kinapozidi hapo huwa kinachangia kudhoofisha mfumo wa kinga ya mwili. Inaelezwa kuw

KIGOGO WA SERIKALI ANAYEBANJUKA NA MSANII BATULI HUYU HAPA,MENGI MAZITO YAFICHUKA

Image
UBUYU ulionyooka kabisa umetua kwenye meza ya gazeti hili ukidai kuwa, waziri kijana katika serikali ya Rais Dk.John Magufuli ‘JPM’, amedata kinomanoma na penzi la msanii wa filamu Bongo mwenye shepu bomba, Yobnesh Yusuf ‘Batuli’, Ijumaa lina full stori. Awali zilivuja taarifa kuwa, waziri huyo wa wizara nyeti ambaye ni mume wa mtu (jina lake linahifadhiwa kwa sasa) kafa, kaoza kwa mrembo huyo ambaye ni kada wa CCM na hivyo ameamua kumng’arishia maisha yake ili aweze kumfaidi vizuri. KISIKIE CHANZO “Kama ni kuyapatia maisha, Batuli sasa hivi kayapitia maana mheshimiwa….(anamtaja jina) ndiyo kajiweka kwake sasa hivi, anamhudumia kwa kila kitu, ndiyo maana unamuona mambo yake sasa hivi supa kuliko hata mastaa wengine,” alimwaga ubuyu mtoa habari huyo kisha akaongeza: “Kampangishia mjengo kule Kunduchi na ndinga pia kamnunulia, nyie fuatilieni mtajua ukweli wa ubuyu huu ninaowapa.” IJUMAA KAZINI Baada siri hiyo kuvuja, mmoja wa waandishi wetu alimpigia

KULIKONI !? Sumaye Kujiuzulu ujumbe wa bodi CRDB, KISA?!

Image
Waziri Mkuu mstaafu na Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Mashariki, Frederick Sumaye, amejiuzulu ujumbe wa bodi ya Benki ya CRDB ili atekeleze zaidi majukumu yake ya kisiasa. "Nina shughuli nyingi za kisiasa ambazo zitaninyima nafasi ya kuhudhuria vikao vya bodi.  Sipendi pia kuona CRDB ikihusishwa na msimamo wangu kisiasa. Hii ni taasisi huru ambayo ina wanahisa wengi ambao sitapenda kuona maslahi yao yakiingiliwa kutokana na siasa,"  amesema Sumaye.

Uthibitisho wa Simba kufika FIFA

Image
Ushahidi kuwa klabu ya Simba imewasilisha malalamiko yake kwa Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa), umepatikana. Kitendo cha Simba kuwasilisha rufaa hiyo na picha ikionyesha ushahidi huo, inaonekana kuwakwaza zaidi ya mashabiki wa Yanga ambao walikuwa wameanza sherehe za ubingwa. Baadhi ya mashabiki wa Yanga, wameonekana kukerwa na jambo hilo huku wakiwaita Simba “Wazee wa pointi za mezani”. Lakini mashabiki wa Simba wamekuwa wakijibu mapigo na kusema, “Haki ni haki” na sheria itafuata mkondo wake. Yanga na Simba zimemaliza ligi zikiwa na pointi 68 kila moja, lakini Yanga ina wastani mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa GD. Silaha ya Simba, inabaki kuwa suala la pointi za Kagera na kama kweli Fifa itaamuru irejeshewe, basi itafikisha pointi 71 na kutangazwa kuwa bingwa. Simba ilishinda rufaa yake kupitia kamati ya Saa 72 ambayo ilibaini kuwa kweli beki Mohammed Fakhi alikuwa na kadi tatu za njano wakati Simba ilipolala kwa mabao 2-1 katika mechi ya ligi

WATANZANIA 11 WAMEFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUMBAKA KWA ZAMU MAMA MJAMZITO AFRIKA KUSINI

Image
Wanaume 11 ambao ni raia wa Tanzania wamekamatwa na Polisi na kufikishwa Mahakamani wiki hii Johannesburg Afrika Kusini .Radioni na Mtandaoni Johannesburg wiki hii kumeripotiwa kuwa kosa lililofanya Wanaume hao 11 kukamatwa na Polisi ni kumbaka Mwanamke mjamzito mwenye umri wa miaka 22 aliyekuwa akitoka kazini saa kumi na moja alfajiri.Mwanamke huyo alikuwa akitoka kazini na Mfanyakazi mwenzake ambaye ni Mwanaume ambapo ghafla walivamiwa na kundi la Wanaume wenye silaha za moto na wakamvuta Mwanamke huyo kabla ya kumpiga Mfanyakazi mwenzake ambae baadae alifanikiwa kutoroka.Baada ya Mfanyakazi huyo kutoroka aliwapigia simu Polisi na wakafanikiwa kuwahi eneo la tukio na kukuta Wanaume hao wakimbaka kwa zamu Mwanamke huyo mwenye ujauzito wa miezi mitatu.Polisi wapatao kumi waliingia kwenye jengo tukio lilikofanyika na kumuokoa Mwanamke huyo aliyekua kwenye hali mbaya ambapo walimpeka Hospitali huku Watuhumiwa wakichukuliwa na kupandishwa Mahakamani siku ya Jumatano.

Dalili za Ugonjwa wa Vidonda vya Tumbo

Image
Hapo kabla tulisoma kwa kirefu kuhusu vidonda vya tumbo, kisha tukasoma kuhusu dawa mbadala ya vidonda vya tumbo, tukasoma tena kuhusu chakula cha mgonjwa wa vidonda vya tumbo, na leo tunaendelea kuangalia dalili za ugonjwa wa vidonda vya tumbo. Dalili zitakazokufanya ujihisi una vidonda vya tumbo ni pamoja na; Kuchoka choka sana bila sababu maalum Kuuma mgongo au kiuno Kupungukiwa au kupoteza kabisa nguvu za kijinsia Kizunguzungu Kukosa usingizi Usingizi wa mara kwa mara Maumivu makali sehemu ya mwili Kifua kwa ndani kana kwamba unachomwa na kitu cha moto au chenye ncha kali. Maumivu hayo wakati mwingine hutokeza mgongoni na huchoma kama sindano yenye sumu na kuacha maumivu makali Kichefuchefu Kiungulia Tumbo kujaa gesi Tumbo kuwaka moto Maumivu makali sehemu kilipo kidonda Kukosa choo au kupata choo kwa shida tena kikiwa kigumu na chenye kukatika kama cha mbuzi Kutapika nyongo Kutapika damu au kuharisha Sehemu za mwili kupata ganzi Kukosa hamu ya k

WACHIMBAJI WA MADINI WAFARIKI KWA KUKOSA HEWA MGODINI TANZANIA

Image
Wachimbaji wawili wadogo wa madini ya dhahabu katika kijiji cha Masuluti kata ya Magulilwa tarafa ya Mlowa wilaya ya Iringa mkoani Iringa wamefariki dunia baada ya kukosa hewa. Wananchi wa Msuluti kata ya Magulilwa wilaya ya Iringa wakiwa wamebeba mmoja kati ya miili ya wachimbaji wadogo wawili waliokufa mgodini kwa kukosa hewa leo Miili ya wachimbaji wadogo wawili katika mgodi ya Mamweli Msigwa ukiingizwa kwenye gari la polisi Kamanda wa polisi mkoa wa Iringa Julius Mjengi katikati mwenye kofia nyeusi akionyeshwa shimo la mdogi wa dhahabu ambalo limesababisha vifo vya watu wawili Wananchi wakiwa eneo la tukio Askari polisi na wananchi wakitazama mgodi huo uliouwa Milili ya wachimbaji wadogo wawili walipoteza maisha mgodini leo Kamanda wa polisi mkoa wa Iringa Julius Mjengi kushoto akitazama shimo la mgodi katika kijiji cha Msuluti kata ya Magulilwa wilaya ya Iringa ambalo wachimbaji wawili wadogo wawili walipoteza maisha kwa kukos