Posts

MBUNGE ZITTO KABWE AMPONGEZA KAMANDA TUNDU LISSU BAADA YA USHINDI WAKE

Image
CHAMA cha ACT-Wazalendo kinachoongozwa na Zitto Kabwe, kimempongeza Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu, kwa kushinda kiti cha urais wa Chama cha Wanasheria (TLS) katika uchaguzi uliofanyika juzi jijini Arusha. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Naibu Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo, Msafiri Mtemelwa, alisema Lissu anastahili pongezi kwa kufanikiwa kushinda nafasi hiyo kutokana na changamoto zilizomkumba katika kuisaka. Alisema kuwa licha ya kupitia misukosuko mingi iliyokuwa inaonyesha njia ya kumkwamisha kufikia malengo yake, Lissu hakukata tamaa na alionyesha ujasiri. Mtemelwa alisema kupata nafasi hiyo kwa kiongozi kutoka upinzani ni dalili njema na kipimo kwa wapinzani na kwamba anapaswa kuitendea haki nafasi hiyo kwa ustawi wa vyama hivyo vya upinzani. “Mimi niseme tu kwamba, Lissu anastahili pongezi," Mtemelwa alisema. "Tunahitaji watu kama hawa, watu majasiri. Pamoja na kwamba ali

Nape aunda tume kuchunguza uvamizi wa Makonda Clouds

Image
Dar es Salaam. Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye ameunda kamati ya kuchunguza kuhusu tukio lililofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na kutaka apewe matokeo ndani ya saa 24. Nape ameyasema hayo leo wakati akizungumza na wanahabari  mara baada ya Mkurugenzi wa Vipindi na Uaandaji wa Clouds Media Groups, Ruge Mutahaba kuthibitisha kuwa Makonda alivamia kituo hicho, Ujumaa usiku akiwa na polisi wenye silaha.  “Matukio kama haya hutokea pindi nchi inapotaka kupinduliwa, lakini kama Rais yupo na nchi haijapinduliwa  basi kuingia ndani ya chombo cha habari na silaha, huku ni sawa na kunajisi uhuru wa habari,” alisema Nape

RUGE MUTAHABA AFUNGUKA YOTE JUU YA RC MAKONDA KUVAMIA KITUO CHAO

Image
Stori iliyotrend jana siku nzima kuhusu Mkuu wa Mkoa Paul Makonda Kuvamia kituo cha Polisi na Bunduki usiku wa Ijumaa imedhibitishwa leo na Mkurugenzi wa Kituo hicho Ruge Mutahaba akiongea katika kipindi cha 360 Ruge Mutahaba amefunguka A to Z na Kuelelezea tukio lilivyotokea mpaka Mkuu huyo wa mkoa kuchukua recordings za dada ambaye alirekodiwa na Shilawadu lakini hawakuweza kurusha kwa vile stori haukubalance.... Ruge Amedai Makonda ni Rafiki yake lakini kwa hilo inabidi aombe radhi Watanzania Kwa vile Radio ya Clouds inasikilizwa na watu wengi Tanzania...

NEWS ALERT: Mkuu Wa Mkoa Anusurika Kufa Kwa Kugongwa Gari Akifanya Mazoezi Asubuhi Hii

Image
Watu wawili wamenusurika kifo baada ya kuwagonga wananchi waliokuwa katika mazoezi asubuhi ya leo Jumamosi Machi 18,2017 mjini Iringa huku mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza na katibu tawala Wamoja Ayubu wakinusurika katika ajali hiyo. Ajali hiyo imetokea nje ya lango la kamanda wa polisi mkoa wa Iringa dakika tatu tu baada ya kuanza mazoezi kuelekea uwanja wa Samora. Ajali hiyo imesababishwa na dereva taxi kuwaparamia wafanya mazoezi hao. Taarifa kamili inakuja hivi punde...

Mahabusi ajinyonga rumande

Image
Mtuhumiwa anayedaiwa kupatikana na meno ya tembo yenye thamani ya Sh500 milioni, Daudi Matola (41) mkazi wa Wilaya ya Namtumbo amekutwa amekufa akiwa mahabusu mjini hapa. Anadaiwa kujinyonga hadi kufa kwa kutumia suruali aliyoifunga kwenye dirisha la choo cha mahabusu ya Kituo Kikuu cha Polisi cha Songea. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Zuberi Mwombeji amesema tukio hilo lilitokea Machi 9 saa 9:55 usiku. Mwombeji amesema inadaiwa siku ya tukio Matola akiwa mahabusu alienda chooni ambako alijinyonga kwa kutumia suruali yake.

RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA RAIS WA ZANZIBAR DKT. SHEIN, MJINI DODOMA LEO

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein walipokutana kwa mazungumzo Ikulu ya Chamwino mjini Dodoma leo Jumatatu Machi 13, 2017. Picha na IKULU Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahi jambo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein walipokutana kwa mazungumzo Ikulu ya Chamwino mjini Dodoma leo Jumatatu Machi 13, 2017. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongozana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein walipokutana kwa mazungumzo Ikulu ya Chamwino mjini Dodoma leo Jumatatu Machi 13, 2017.

Waziri Ndalichako awaambia maofisa elimu kuhakikisha somo la Skauti linawekwa kwenye masomo ya ziada

Image
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako, amewataka maofisa elimu wa shule za msingi na sekondari nchini, kuhakikisha vyama vya skauti vinakuwa na masomo ya ziada katika shule hizo. Profesa Ndalichako aliyasema hayo hivi karibuni akiwa jijini Arusha kwa niaba ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, katika maadhimisho ya siku ya skauti Afrika ambayo kwa mwaka huu yalifanyika nchini. “Kama rais wa skauti na waziri mwenye dhamana ya elimu, naomba nitoe wito kwa maofisa elimu wote wa mikoa kuhakikisha suala la skauti shuleni linakuwa ni sehemu ya masomo ya ziada. Nasema hivyo kwa sababu mikoa mingine hapa washiriki ni wachache na nauliza kwanini tunawanyima vijana kushiriki kwenye mambo ambayo yana manufaa kwa Taifa,” alisema. “Tunataka wafanye nini, wakienda vijiweni hatuwaruhusu, hivyo tuwatengenezee mazingira na tutumie nguvu walizonazo katika mambo yatakayowajenga kuwa raia w

Zitto Kabwe ampongeza Kikwete kwa kuzindua taasisi yake ya maendeleo

Image
Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete leo amezindua Taasisi ya Maendeleo ya Jakaya Mrisho Kikwete (JMKF).Taasisi hiyo imeundwa ili kusaidia Tanzania na Afrika katika kuimarisha amani, afya, utawala bora na maendeleo endelevu. Taasisi hiyo inajikita katika maendeleo endelevu kwa kusaidiana na wadau wengine kukabiliana na umaskini, kusaidia mkulima mdogo, kulinda mazingira na kukabiliana na athari za tabia nchi. Baada ya uzinduzi huo Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe amempongeza Rais huyo mstaafu kupitia akaunti yake ya Facebook: “Hongera Sana Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete kwa kuzindua Mfuko Wa Wakf Wa Jakaya Kikwete Foundation. Natumai utaitumikia vema nchi yetu na bara la Afrika katika ustaafu wako. Jambo moja kubwa uwekeze kwalo ni kuandaa Viongozi Vijana. Naona timu imesheheni watu wenye uwezo mkubwa. Kila la kheri.

HUYU NDIYE ALIYEMFUNDISHA OSAMA BIN LADEN UGAIDI

Image
Anaandika.Emanuel john. Ni Ali Mohamed alikuwa double agent wa CIA na EIJ( Egyptian islamic jihad) ambayo ndio ilipelekea kuundwa kwa ALQAEDA huku yeye akiwa mwendesha mafunzo wa mbinu za kivita na kijasusi wa kwanza kwenye kambi zao kwa ajili ya kuwaandaa na mapambano dhidi ya utawala wa kisovieti nchini Afghanistan miaka ya 90. yeye ndiye mwalimu wa kwanza wa Osama bin Laden na Ayman Zawahiry( kiongozi wa sasa wa Alqaeda) Ali anaelezwa kuwa mtu mwenye uzito wa kilo 90, urefu futi 6 huku akielezwa mtu aliye fiti kimwili, aliyebobea kwenye sanaa za mapigano( martial art),mwenye ufahasa mzuri wa lugha za kiingereza,kifaransa,kiyunani na kiarabu. alikuwa mwenye nidhamu ya juu, mwenye uwezo mkubwa wa kufikiri, mwenye kujichanganya na watu na uwezo wa kupata marafiki kwa urahisi. Uhusiano wake na CIA kwa mara ya kwanza aliingia marekani kama mkalimani wa Ayman Zawahiry( kiongozi wa sasa wa alqaeda) wakati alipoenda kuchangisha michango kusaidia wana mgambo katika harakat

Hatimaye RC Paul Makonda aanza kazi tena leo hii baada ya kurejea toka Afrika ya Kusini

Image
Picha ikimuonyesha RC Makonda akizindua ujenzi wa barabara ya zege leo jijini Dar. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amezindua Barabara ya Shimo la Udongo, Kilwa EPZ iliyopo Kurasini ya Umbali wa Kilomita 1. – Barabara hiyo iliyojengwa kwa kiwango cha zege na kampuni ya wazalendo ya Grant Tech imegharimu takribani milioni 350.

Msukuma afunguka mazito, Ni kuhusu alivyokamtwa na Polisi

Image
JOSEPH Kasheku “Msukuma” Mbunge waa Jimbo Geita Vijijini na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Geita ametoa siku tano za kuombwa na radhi na wanaodaiwa kuwa ni maofisa usalama wa Taifa waliotoa taarifa za uongo dhidi yake na kusababisha akamatwe Mjini Dodoma, anaandika Charles William. Juzi Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma, liliwatia nguvuni Msukuma, Hussein Bashe, Mbunge wa Jimbo la Nzega Mjini na Adam Malima, aliyewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Mkuranga kwa madai ya kupanga kufanya vurugu katika Mkutano Mkuu wa CCM uliofanyika jana. Wanasiasa hao walikamatwa na kuhojiwa, kabla ya kuachiwa kwa dhamana. Hata hivyo Msukuma amesema hawezi kukaa kimya juu ya suala hilo na kwamba wapo maofisa usalama waliosambaza taarifa juu yake na kusababisha hofu lazima wamuombe radhi. “Hawa ni wapiga dili, Rais lazima aiangalie upya Idara ya Usalama wa Taifa. Wameniundia mimi zengwe, mpaka nikakamatwa, na nchi ikawa kwenye presha, kama chama kisipozungum

KINANA AFUNGUA SEMINA ELEKEZI YA MABADILIKO NDANI YA CHAMA KWA WENYEKITI NA MAKATIBU WA CCM MJINI DODOMA LEO

Image
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akifungua semina elekezi kuhusu mabadiliko ndani ya Chama, kwa Wenyeviti na Makatibu wa mikoa na wa wilaya na watendaji, leo katika Ukumbi wa Sekretarieti katika Jengo la Ofisi ya Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma. Washiriki wakiwa kwenye semina elekezi kuhusu mageuzi ndani ya Chama Cha Mapinduzi, leo katikaUkumbi wa Sekretarieti Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma. Washiriki wakiwa kwenye semina elekezi kuhusu mageuzi ndani ya Chama Cha Mapinduzi, leo katikaUkumbi wa Sekretarieti Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma. Washiriki wakiwa kwenye semina elekezi kuhusu mageuzi ndani ya Chama Cha Mapinduzi, leo katikaUkumbi wa Sekretarieti Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma. Katibu wa Sekretarieti ya CCM, Anamringi Macha (kulia) akiratibu semina elekezi kuhusu mageuzi ndani ya Chama Cha Mapinduzi, leo katikaUkumbi wa Sekretarieti Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma. Washiriki wakiwa kwenye semina elekezi kuhusu mageuzi ndani y

HIVI NDIVYO HALI ILIVYO JIJINI DAR LEO BAADA YA MVUA KUNYESHA

Image
 Kutokana na Mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali hapa jijini Dar es salaam leo, soko la Sinza limelazimika kufungwa kwa muda kutoka na kujaa maji eneo lote la soko hilo.  Barabara nyingi za Dar leo zimejaa maji, hali inayopelekea magari mengi 'kubuma' kama ionekanavyo pichani hapa. Afande akitafakari jambo kufuatia uwingi wa maji katika barabara ya Bagamoyo eneo la Goigi jijiji Dar es salaam leo. Wadau wakifanya mambo katika moja ya chemba iliyoziba kutoka na wingi wa uchafu uliokuwa umesombwa na maji hayo.  Magari yote yamelazimika kupita upande mmoja wa barabara kutoka na wingi wa maji upande mwingine.

BREAKING NEWZZ….Sir. George Kahama afariki dunia!

Image
Mmoja wa waasisi wa Taifa la Tanzania, Sir. George Kahama amefariki dunia jioni ya leo ktk Hospitali ya Taifa, Muhimbili.

JK kuzindua taasisi yake ya maendeleo

Image
RAIS wa Serikali ya Awamu ya Nne, Dk Jakaya Kikwete kesho anatarajiwa kuzindua Taasisi ya Maendeleo ya Jakaya Mrisho Kikwete (JMKF) . Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na taasisi hiyo, uzinduzi huo utafanyika katika Hoteli ya Hyatt Kempinsk The Kilimanjaro jijini Dar es Salaam na baada ya uzinduzi huo, Dk. Kikwete ataendesha kikao cha kwanza cha bodi ya taasisi hiyo. Taasisi hiyo imeundwa ili kusaidia Tanzania na Afrika katika kuimarisha amani, afya, utawala bora na maendeleo endelevu.Aidha taasisi hiyo itajikita katika maendeleo endelevu kwa kusaidiana na wadau wengine kukabiliana na umasikini, kusaidia mkulima mdogo, kulinda mazingira na kukabiliana na athari za tabianchi. Taasisi hiyo itasaidia pia katika afya ya mama na mtoto, kukabiliana na ugonjwa wa malaria na kuboresha lishe ya wananchi.Katika elimu, itaboresha elimu katika kuwasaidia wajasiriamali kwa mafunzo na pia itasaidia katika utawala bora na utafutaji amani. Taasisi hiyo imesajiliwa na itakuwa ch

MWENYEKITI WA CCM,RAIS DKT JOHN POMBE MAGUFULI AONGOZA MKUTANO MKUU MAALUM MJINI DODOMA

Image
Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri wa Tanzania, Dk. Joseph Magufuli akiwahutubia wajumbe wapatao 2356,ambapo walipaswa kuwa wajumbe 2380 katika mkutano huo Mkuu Maalum wa CCM uliokuwa na lengo kuu la kufanya baadhi ya mabadiliko ndani ya Katiba ya chama hicho,ambapo mabadiliko hayo yamepitishwa kwa asilimia 100 na wajumbe hao waliohuhudria mkutano huo. Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza mambo mbalimbali mbele ya wajumbe waliohudhuria katika Mkutano Mkuu Maalum mjini Dodoma. Baadhi ya Wajumbe wa mkutano mkuu Maalum wa CCM wakishangilia kwa shangwe huku wakiwa na mabango yao yakionesha mikoa wanayoiwakilisha.  Sehemu ya baadhi ya wajumbe wa mkutano huo pamoja na wageni waalikwa wakiwa tayari ukumbini.  Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri wa Tanzania, Dk. Joseph Magufuli akisalimiana na aliyekuwa Mwenyekiti wa chama hicho na Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Dkt. Jakaya Kikwete wakati

Ukumbi mpya wa CCM wapewa jina la Kikwete

Image
Dodoma. Wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalum wa CCM wamekubaliana kuita ukumbi mpya uliopo eneo la Dodoma Makulu ‘Kikwete Hall’. Makubaliano hayo yametokana na Mwenyekiti wa Taifa wa CCM Rais Dk John Magufuli kupendekeza kwa wajumbe hao ukumbi huo uitwe Kikwete. “Leo tumekaa katika ukumbi huu mzuri kuna watu wamefanya kazi na miongoni mwao atakuwa ni Mzee wetu Jakaya Kikwete (Rais Mstaafu wa awamu ya nne). Mtakumbuka kabla ya hapa tulikuwa tukikaa kule yanatolewa magunia tunakaa,”amesema. Wajumbe hao walikubaliana na wazo hilo na baadaye Rais Magufuli walishikana mkono na Rais Kikwete.

Magufuli: Hatuna Muda wa Kumbembeleza Mtu Kukichangia Chama Chetu

Image
Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk John Magufuli amesema chama hicho hakitambembeleza mtu kukichangia katika shughuli mbalimbali. Akihutubia mkutano Mkuu wa CCM unaofanyika leo Dodoma, Dk Magufuli amewaambia wajumbe wa mkutano huo kuwa kwa miaka yote CCM kimekuwa kikiomba hata kwa watu ambao hawastahili. “Matokeo yake wamekuwa wakitumia nafasi hiyo kudhalilisha. Hakuna tena omba omba hatutaki kumbembeleza mtu akitaka kutuchangia atuchangie,” amesema. Amesema kuwa chama hicho kina utajiri unaokiwezesha kujitegemea na kwamba mwanachama atakayetumia mali za chama kwa maslahi binafsi atachukuliwa hatua kali.

Umoja wa Mataifa waingilia kati sakata la kupotea kwa Ben Saanane

Image
Sakata la kupotea kwa mkuu wa Idara ya Sera na Utafiti wa Chadema, Ben Saanane limechukua sura nyingine baada ya Umoja wa Mataifa (UN) kusema upo tayari kutuma watu nchini kwa ajili ya uchunguzi. Saanane, ambaye pia ni msaidizi wa mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alipotea katika mazingira ya kutatanisha Novemba 18 mwaka jana na hadi sasa haijaeleweka kuwa alitekwa au kuuawa, ingawa Chadema imehusisha kutoweka kwake na taarifa ambayo Saanane aliitoa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu utata wa elimu ya baadhi ya viongozi. Siku chache baada ya kupotea kwa Saanane, Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu aliitaka Serikali kueleza kama inamshikilia kada huyo au ifanye uchunguzi wa kina kuhusu kupotea kwake. Sanjari na hilo, Lissu aliitaka Serikali kufuatilia ujumbe wa vitisho ambao Saanane aliwahi kutumiwa kwenye simu yake ya mkononi na mtu ambaye bado hajafahamika. Akisisitiza msimamo wa chama chake, Lissu alizitaka mamlaka zote husika na usalama wa raia ziseme h

MBUNGE BASHE:SINA HOFU NA TIMU TIMU NDANI YA CCM

Image
Mbunge wa Nzega Mjini Hussein Bashe amefunga mazito leo asubuhi kuhusiana na sakata la timua timua linaloendelea dhidi ya wanachama wasaliti ndani ya CCM huko Jijini Dodoma katika Mkutano Mkuu Maalum wa CCM. Mbunge huyo amesema hawezi kuwa na hofu ya aina yeyote kwa kuwa hana jambo baya alilolifanya ndani ya chama hicho hivyo hawezi kuteteleka na wanaotimuliwa wanachama. “Sina hofu na timua timua ya wanachama wasaliti kwasababau naamini wamefanya maamuzi kwa kupitia mchakato ndani ya chama, kwa hiyo sina hofu kwasababu chama chetu kinaongozwa na katiba pamoja  na kanuni zilizopo unakuwa na hofu pale unahisi kuna jambo umelifanya kinyume na taratibu”-Alisema Bashe  Kwa upande mwingine Mbunge huyo amegoma kuzungumzia sakata la yeye kushikiliwa na Jeshi la Polisi hapo jana na kusema suala hilo kamuachia Katibu Mkuu wa chama hicho ndugu Abdurahaman Kinana.