Ukumbi mpya wa CCM wapewa jina la Kikwete


Dodoma. Wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalum wa CCM wamekubaliana kuita ukumbi mpya uliopo eneo la Dodoma Makulu ‘Kikwete Hall’.

Makubaliano hayo yametokana na Mwenyekiti wa Taifa wa CCM Rais Dk John Magufuli kupendekeza kwa wajumbe hao ukumbi huo uitwe Kikwete.

“Leo tumekaa katika ukumbi huu mzuri kuna watu wamefanya kazi na miongoni mwao atakuwa ni Mzee wetu Jakaya Kikwete (Rais Mstaafu wa awamu ya nne). Mtakumbuka kabla ya hapa tulikuwa tukikaa kule yanatolewa magunia tunakaa,”amesema.

Wajumbe hao walikubaliana na wazo hilo na baadaye Rais Magufuli walishikana mkono na Rais Kikwete.

Comments

Popular posts from this blog