Posts

UJUMBE WA VANESSA MDEE KWA JUX WA WAKUNA WENGI

Image
Staa wa Bongo Fleva, Vanessa Mdee ‘Vee Money’ ametumia fursa ya siku ya kuzaliwa ya mpenzi wake, ambaye pia ni Staa wa muziki wa R&B hapa Bongo, Juma Jux kumwandikia ujumbe muhimu kudhihirisha ni kwa kiasi gani anampenda huku akiutaja wimbo wao wa pamoja, #Wivu kuwa ndiyo nguzo ya kukutana na kuanzisha uhusiano wao: Kuoitia ukurasa wake Instagram, Vee Money ameandika; When we first met I was an upcoming songstress with a fast tongue and one hit song on the radio. You … well you were pretty much the same. Your boy asked me if I would spit some bars on your song. I said no. Then walked into the studio and met you and instantly had a change of heart. Fast forward to 2yrs later, tumekuwa. You’ve got the biggest song in the country #Wivu and a multi million dollar brand #AfricanBoy and as for me well … kitu kimoja hakijabadilika though. Kwako sisikii. Lol! Lakini hayo yoteee ni mifano tu ya jinsi gani ukiwa na mahusiano na mtu anayekujenga kifikra na vinginevyo

JPM Kubadili Noti Kuwakomoa Walioficha Mabilioni Majumbani

Image
Rais John Magufuli amewataka watu walioficha fedha majumbani kuziachia ziingie kwenye mzunguko vinginevyo anaweza kuamua kuzibadili ili wakose mahali pa kuzipeleka.  Amesema watu hao wamekuwa na utaratibu wa kutoa fedha zao katika benki na kuzificha kwa kuogopa kuwa atabaini kiasi walichonacho, hivyo akawataka kuachana na tabia hiyo kwa sababu fedha hizo ni mali yao. Akizungumza katika mkutano wa 14 wa mwaka wa wahandisi uliofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City jana, Rais Magufuli aliyetumia dakika 73 kuzungumza na wahandisi hao na kueleza mikakati na changamoto zinazoikabili Serikali ukiwamo wizi na ufisadi, alisisitiza;   “Huu ujumbe ni kwa wale wanaoficha fedha, waziachie na wajiandae, naweza kuamua baada ya siku mbili tatu nabadilisha fedha na hizo zilizofichwa katika magodoro ziozee huko. Ni nafuu mzitoe mziweke katika mzunguko zikafanye kazi,” alisema. Katika mkutano huo uliohudhuriwa na mawaziri, naibu mawaziri, makatibu wakuu na wahandisi kutoka ndani

Mwanzilishi wa Facebook Alivyokutana na Akina Yemi Alade Nigeria

Image
Lagos, Nigeria MWANZILISHI na mmiliki wa mtandao maarufu duniani wa Facebook, Mark Zuckerberg juzi Jumanne alianza ziara yake ya siku mbili nchini Nigeria, ikiwa ni ziara yake ya kwanza kwa nchi za Afrika, na kukutana watu mbalimbali wakiwemo wasanii maarufu wa uigizaji filamu na muziki nchini humo. Katika ziara hiyo, Zuckerberg aliwasili Lagos Jumanne na kufika kwenye kituo maarufu cha ubunifu wa masuala ya mitandao ya kijamii cha Yaba, kilichopo eneo lijulikanalo kam Silicon Valley. Zuckerberg alifanikiwa kutoa elimu ya biashara na masoko kwa watu waliohudhuria kwenye mkutano wake huku akitanua wigo wa watumiaji wa mitandao anayoimiliki ikiwemo Facebook, Instagram na WhatsApp. Baada ya somo hilo la juzi Jumanne, Zuckerberg jana aliamkia mitaani asubuhi akitembelea vijana kwenye Jiji la Lagos bila ulinzi. Alionekana akikifanya jogging kwenye daraja la Lekki Bridge na vijana. Baadhi ya wasanii wa filoamu na muziki nchini Nigeria jana ni pamoja na Richard M

Acer Yazindua Laptop Yenye Kikoo Kilichopinda

Image
Kampuni ya Vifaa vya kielektroniki ya Acer imezindua laptop ya kwanza yenye kioo kilichojipinda. Acer inasema kuwa uvumbuzi huo utaiwezesha kucheza michezo ya video. Televisheni kadhaa pia zimetumia uvumbuzi huo,lakini umezua mgawanyiko kwa kuwa una umuhimu na ubaya wake. Kampuni hiyo ya Taiwan pia ilitangaza kwamba imefanikiwa kupata teknolojia ya pet katika mkutano na wanahabari mjini Berlin. Kampuni kadhaa za kielektroniki ikiwemo Samsung, Lenovo, DJI, Sony na Huawei zinatarajiwa kuzindua sura mpya ya laptop zake katika maonyesho ya kiteknolojia ya Ifa katika Mji Mkuu wa Ujerumani wiki hii. Laptop hiyo ina kioo kikubwa ikilinganishwa na laptop ya kawaida ya Acer,lakini ni umbo lake ambalo liliifanya kampuni hiyo kudai kuwa ya kwanza kuzinduliwa duniani.

RAIS DKT MAGUFULI AFUNGUA MKUTANO MKUU WA WAHANDISI, ATEMBELEA KIKOSI CHA ANGA MAJUMBA SITA UKONGA

Image
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akifungua Mkutano Mkuu wa 14 wa Wahandisi katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam leo Septemba 1, 2016  Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipata picha ya  pamoja na Wanajeshi wa JWTZ Kikosi cha Anga 603 KJ Majumba Sita Ukonga jijini Dar es salaam  alikotembelea kuwapongeza kwa kusherehekea miaka 52 ya Jeshi la Wananchi leo Septemba 1, 2016 Rais Magufuli awataka wahandisi nchini kufanya kazi kwa weledi na uadilifu Na Sheila Simba-MAELEZO  Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Magufuli amewataka  wahandisi nchini kufanya kazi kwa weledi na uadilifu ili kuiwezesha nchi kufikia uchumi wa kati kupitia ujezi na uendelezaji viwanda. Amesema hayo leo jijini Dar es salaam katika mkutano wa 14 wa Bodi ya Wahandisi Nchini,na kuwaasa kutumia taaluma yao kusaidia nchi kufikia uchumi wa kati ili kuleta maendeleo kwa haraka kw

MKUTANO WA 36 WA SADC UMEMALIZIKA NA TANZANIA YATEULIWA KUWA MWENYEKITI WA TROIKA

Image
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiweka saini katika moja ya makubaliano yaliofanywa na nchi za SADC kwenye mkutano wa 36 wa Wakuu wa Nchi na Serikali uliofanyika Lozitha, Mbabane nchini Swaziland.  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (kushoto)akizungumza na Makamu wa Rais wa Angola Mhe. Manuel Domingos Vicente wakati wa kuhitimisha mkutano wa 36 wa nchi za SADC mjini Mbabane Swaziland. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (katikati) akiwa kwenye mkutano wa 36 wa nchi 15 za SADC uliofanyika mjini Mbabane Swaziland, kulia ni Makamu wa Rais wa nchi ya Angola Mhe. Manuel Domingos Vicente na kushoto ni Waziri Mkuu wa Madagascar Mhe.Mahafaly Solonandrasana Olivier. Mwenyekiti wa SADC Mfalme Mswati wa III(kulia) akizungumza na Katibu Mkuu Mtendaji wa SADC Dr. Stergomena L. Tax wakati wa kuhitimisha mkutano wa 36 wa SADC mjini Mbabane,Swaziland. Mw

MSICHANA APEWA MIMBA NA NYOKA AKIWA USINGIZINI, CHA KUSHANGAZA ZAIDI AJIFUNGUA MTOTO HUYU!

Image
  Kehinde Adegoke, a teenager who is an indigene of Ogbomoso in Oyo State Nigeria, has revealed how she had s*x with a snake in her dream for four years and eventually got pregnant without any physical relationship with any man. Nigerian Tribune reports that the 19-year-old girl was delivered of a baby boy in the early hours of March 28, 2015 but the baby later died on Sunday, March 29 without any sickness attached to it. Narrating her story, she said: “My parents live in Niger but I am from Ogbomoso, Oyo State. I was troubled by an unseen spirit. I would see the snake beside me. The snake would then turn to a Fulani man who would have intercourse with me. It started about four years ago. “After the intercourse, the Fulani man would turn to a snake again and leave. Whenever I woke up, I would not see any semen indicating that I had s*xual intercourse. But in the dream, he would climax and release in me. “I have never had any man who wooed me in real life and l

JPM Amthibitisha Msigwa Kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu

Image

Chadema Wasitisha Maandamano ya UKUTA

Image
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetangaza kisitisha maandamano yaliyokuwa yafanyike nchi nzima kesho Septemba Mosi yaliyopewa jina la UKUTA. Akitangaza uamuzi huo, Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe amesema kuwa, wamefanya mazungumzo na viongozi mbalimbalia wakiwemo viongozi wa dini, BAKWATA, Baraza la Maaskofu, Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, Taasisi ya Mwalimu Nyerere na Jukwaa la Katiba na Jukwaa la wahariri na kuona wana kila sababu ya kusikiliza ushauri huo. Aidha, maandamano hayo yameahirishwa kwa mwezi mmoja ili kwa viongozi wa dini kutafuta muafaka wa hali ya kisiasa nchini.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE TAREHE 30.08.2016

Image

MAGAZETI YA MICHEZO NA BURUDANI LEO TAREHE 30/8/2016

Image

Lema Apandishwa Kizimbani kwa Kesi Mbili Tofauti, Aachiwa kwa Dhamana

Image
  Dar es Salaam. Mbunge wa Arusha Mjini kwa tiketi ya Chadema, Godbless Lema amepandishwa mahakamani leo katika kesi mbili tofauti. Kesi ya kwanza namba 351/2016 anatuhumiwa kumtumia ujumbe wa simu wa uchochezi Mkuu wa Mkoa Arusha, Mrisho Gambo wenye maneno kuwa “Karibu tutakudhibiti kama mashoga walivyodhibitiwa Uarabuni” Kesi ya pili namba 352/16 Lema anatuhumiwa kuhamasisha maandamano Septemba Mosi kinyume cha sheria. Hakimu amepinga hoja za wakili wa Serikali,  Vincent Njau kuzuia dhamana kwa sababu za kiinterejensia kwa usalama wake. Baadaye vurugu ziliibuka mahakamani wakati polisi wanataka kumpeleka Lema magereza kwa madai kuwa wanadhani wamechelewa, lakini mbunge huyo alipinga hatua hiyo kwa maelezo muda wa mahakama saa 9.30 ulikuwa bado. Baada ya kusomewa kesi hiyo, Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha imemuachia Mbunge wa Arusha, Godbless Lema kwa dhamana baada ya kulala mahabusu kwa siku tatu bila kula

Mbowe, Lowassa, Mnyika na Dkt. Mashinji Wakamatwa na Polisi, Dar

Image
Kikao cha Kamati Kuu ya CHADEMA kilichokuwa kinafanyika katika Hoteli ya Giraffe iliyopo Mbezi jijini Dar, kimezingirwa na jeshi la polisi huku viongozi wake wakikamatwa na kupelekwa Kituo Kikuu cha Polisi cha Dar es Salaam kwa ajili ya mahojiano. Akizungumzia kukamatwa kwa viongozi hao Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu alisema waliokamatwa na polisi kwa ajili ya mahojiano ni Edward Lowassa, Freeman Mbowe, John Mnyika, Dk Vincent Mashinji na  Said Issah “Tulikuwa kwenye kikao cha Kamati Kuu kilichojumuisha wajumbe na wabunge kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali ya chama. Jumla ya wajumbe walikuwa 170. Tukiwa kwenye kiako walikuja watu wanasema tunatakiwa polisi kwa sababu tumekiuka agizo la lilitokataza mikutano.”

UVCCM WAAHIRISHA MAANDAMANO YAO,WATII AGIZO LA JESHI LA POLISI

Image
Agosti 22, 2016 Umoja wa Vijana wa CCM tuliutangazia umma na dunia kwamba ifikapo Agosti 31 mwaka huu tutaitisha maandamano ya amani nchi nzima yenye lengo la kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dk John Pombe Magufuli kwa utendaji wenye tija, ufanisi na uliorudisha imani na matumaini kwa wananchi. Msimamo na dhamira ya kufanya maandamano hayo ya amani yenye maudhui na kusudio hilo, bado uko pale pale ingawaje si kwa tarehe tuliopanga na kutangaza awali yaani Agosti 31 mwaka huu. Jumuiya yetu kama mjuavyo ni ya Vijana wa CCM, (UVCCM) inapata malezi kwa karibu mno na Jumuiya ya Wazazi ya CCM. Wiki ya jana Mwenyekiti wa Wazazi Taifa Nd. Abdallah Bulembo alikutana na waandishi wa habari akitutaka UVCCM tuahirishe maandamano ya Agosti 31 mwaka huu hadi wakati mwingine. Kwa mujibu wa Katiba ya Chama Cha Mapinduzi, Jumuiya ya Wazazi ndiyo Msimamizi wa Malezi, Maadili na Adabu kwa Vijana wote nchini, sisi UVCCM tunaamini kuwa siki