Posts

Linah: Mastaa Afrika wananitaka kimapenzi

Image
  Staa wa Muziki wa Bongo Fleva, Estalina Sanga ‘Linah’. Ikiwa imepita miezi kadhaa tangu staa wa Muziki wa Bongo Fleva, Estalina Sanga ‘Linah’ aachane na mchumba wake, amekiri kutakwa kimapenzi na mastaa wa muziki nje ya nchi (Afrika). Akichonga na Amani Linah amesema, mara nyingi amekuwa akisumbuliwa kimapenzi na mastaa wengi wa muziki Afrika lakini hakuwa tayari kuwaweka wazi na wala kutaja kama alishawahi kubanjuka na mmoja wapo kati ya hao. “Ni kweli wapo wengi walionitaka kimapenzi, lakini itabaki kuwa siri yangu kujua ni wangapi na nilimkubalia nani kati ya hao,” alisema Linah.

DKT. KIGWANGALLA AUNDA KIKOSI KAZI KUBORESHA HUDUMA ZA MFUKO WA AFYA YA JAMII (CHF)

Image
Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Dkt. Hamisi Kigwangalla. Na Rabi Hume, Modewjiblog Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Dkt. Hamisi Kigwangalla ameanzisha kikosi kazi cha watu 24 ambacho kitakuwa na kazi ya kutengeneza mpango mkakati wa kuwezesha kuboresha Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF). Katika taarifa ambayo imetolewa na Dkt. Kigwangala imeeleza kuwa kazi ya kuanzisha kikosi kazi hicho ni agizo kutoka kwa Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu ambaye alimtaka aanzishe kikosi hicho ili washirikiane kuanzisha mpango mkakati wa kuwezesha kuboresha Mfuko wa Afya ya Jamii. “Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Ally Mwalimu alinipa kazi ya kuunda kikosi kazi maalum na kushirikiana nacho kutengeneza mpango mkakati wa kuboresha Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF),” alisema Dkt. Kigwangalla. Dkt. Kigwangalla amewa

DIAMOND PLATINUMS ATANGAZA NAFASI YA KAZI

Image
  

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AWASILI DODOMA

Image
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,Chiku Galawa baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Dodoma January 20, 2016 ambako pamoja na mambo mengine anatarajiwa  kuhudhuria vikao vya Bunge. Kulia ni mkewe Mary. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

WATU WAWILI WANASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA BAADA YA KUKUTWA WAKIWA NA DAWA ZA KULEVYA

Image
Madawa ya kulevya yaliyokamatwa mkoani Mbeya. JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANI WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI JESHI LA POLISI TANZANIA.   TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI “PRESS RELEASE” TAREHE 19.01.2016. KATIKA TUKIO LA KWANZA, MWANAMKE MMOJA ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA NURU ISMAIL [31] MFANYABIASHARA NA MKAZI WA JIJINI DAR ES SALAAM ANASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA AKIWA NA MADAWA YA KULEVYA AINA YA BHANGI UZITO KILO 7 NA GRAMU 100 ZIKIWA ZIMEHIFADHIWA KWENYE MABEGI YA NGUO. MTUHUMIWA ALIKAMATWA MNAMO TAREHE 18.01.2016 MAJIRA YA SAA 05:30 ASUBUHI HUKO CUSTOM MPAKANI MWA TANZANIA NA ZAMBIA KATIKA MJI MDOGO WA TUNDUMA, WILAYA YA MOMBA, MKOA WA MBEYA. AIDHA MTUHUMIWA ALIKAMATWA AKIWA SAFARINI AKITOKEA SOUTH AFRIKA KUELEKEA JIJINI DSM AKIWA NA PASSPORT NO. AB.767234 ILIYOTOLEWA DSM TAREHE 21/10/2015 NA KUSAFIRI KWENYE BASI LENYE NAMBA ZA USAJILI T.595 BPR MALI YA KAMPUNI YA FALCON IKITOKEA LUSAKA KU

Breaking News: Ghorofa Latitita Kariakoo, Dar

Image
WANANCHI waishio maeneo ya Mtaa wa Mchikichini na Livingstone, Kariakoo jijini Dar es Salaam, wamekumbwa na taharuki baada ya ghorofa linalojengwa eneo hilo kutitia leo. Chanzo: ITV

MISA YA KUMBUKUMBU YA MAREHEMU LETICIA NYERERE NCHINI MAREKANI.

Image
Misa ya kumbukumbu ya marehemu Leticia Nyerere iliyofanyika siku ya Jumamosi January 16, 2016 katika kanisa la Mt. Edward Baltimore, Maryland na kuhudhuriwa na ndugu, jamaa na marafiki kutok kila kona ya Marekani. Mwili wa marehemu Leticia Nyerere unatarajia kufika Tanzania kesho Jumanne January 19, 2016 na utaagwa Dar es Salaam na mazishi yake yanatarajiwa kufanyika Butiana. Picha na Iska Jojo. Wana familia wakifuatilia misa ya kumbukumbu ya marehemu Leticia Nyerere iliyofanyika siku ya Jumamosi January 16, 2016 katika kanisa la Mt. Edward Baltimore, Maryland nchini Marekani. Kutoka kushoto ni Bi. Kijogoo kutoka Arizona,,Margareth Mageni na ,Flora Mageni Wanafamilia wakiwemo watoto wa marehemu kutoka kushoto ni Julius Nyerere, Helena Nyerere na Julia Nyerere kulia ni Edlaila  Nyerere ambaye ni wifi wa marehemu kutoka Atlanta jimbo la Georgia nchini Marekani  wakifuatilia misa ya kumbukumbu ya mpendwa mama yao Leticia Nyerere aliyeaga Dunia siku ya Jumapili Jan

DIAMOND PLATINUMZ ANA MTOTO MWINGINE MWANZA ....AELEZA STORY NZIMA SOMA HAPA

Image
Tiffah Dangote ana ndugu yake, aliyezaliwa na msichana aliyekutana kimapenzi na baba yake (one night stand), Diamond Platnumz enzi anaanza kuupata ustaa. Taarifa hizo zilitolewa hivi karibuni na Diamond mwenyewe wakati akihojiwa kwenye kipindi cha Papaso cha TBC FM. Anasema tukio hilo lilitokea mwaka 2010, Mwanza alikoenda kufanya show. “Huyo mwanamke story ilivyokuwa alikuwa ametoka kwenye chumba cha brother Dully akaja kwangu mimi nikafanya yangu, mimi nikarudi huku mtoto akawa ananimbia ‘ebwana mimi nina mimba,” alisimulia Diamond. “Basi ilivyokuwa mtoto ‘bana eeh mimi nina mimba’ na mimi nikawa nachezesha nini nikawa namhudumia, huku na huku bahati mbaya nikaanza na demu fulani hivi kwahiyo demu mwenyewe akanimind, nikawa nampigia simu hapokei nikaenda Mwanza kumsakanya huku na huhu nasikia kwao wakanimind nikaonekana kama mimi nazingua,”alisema. “Siku moja nikaenda nikambanabana ‘nikamwambia wewe una mtoto’ akanikatalia kwasababu aliniambia ile mimba n

Mkurugenzi Mamlaka ya Viwanja vya Ndege afariki dunia

Image
  Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Mhandisi Suleiman Said enzi za uhai wake. Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Mhandisi Suleiman Said amefariki dunia mapema leo asubuhi akiwa katika mazoezi ya kuogelea,taarifa zinaeleza kuwa baada ya tukio hilo Bwa.Suleiman alikimbizwa hospitali ya Agakhan kwa matibabu, na baadae ikaelezwa kuwa amekwisha fariki na kuwa mazishi yanatarajiwa kufanyika leo.

Waziri Mkuu amwakilisha Rais Magufuli mkutano wa SADC Gaborone

Image
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi wa Botswana, Bw. Tshenolo Mabeo baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Sir Seretse Khama uliopo Gaborone Januari 17, 2016. Majaliwa amemwakilisha Rais John Magufuli katika Mkutano wa SADC. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Katibu Mtendaji wa SADC,Dkt, Srergomena Tax mjini Gaborone ambako Mheshimiwa Majaliwa anamwakilisha Rais John Magufuli kwenye mkutano wa SADC Januari 17, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

BREAKING NEWS : WANANCHI WA BONDE LA MKWAJUNI WAFUNGA BARABARA NA KUFANYA FUJO

Image
Hali si shwari hivi sasa katika eneo la Bonde la Mkwajuni Kinondoni jijini Dar es salaam, na inaelezwa kuwa baadhi ya Wananchi wamechoma mataili pande zote za barabara na hakuna gari kupita. Jeshi la Polisi lipo eneo la tukio hivi sasa kukabiliana na tukio hilo ambalo chanzo chake unadaiwa ni baadhi ya vijana wanaodaiwa kuwa walikuwa wakazi wa eneo lililobomolewa ambao wameingia barabarani na kufanya fujo. Pia gari la zimamoto limefika eneo la tukio ili kuzima moto huo. (Picha zote na Henry Mdimu) Endelea kutufuatilia kwa habari zaidi.  

Wakurugenzi watendaji Manispaa za Kigoma, Mpanda wasimamishwa

Image
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mhe. George B. Simbachawene. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mhe. George B. Simbachawene amewasimamisha kazi wakurugenzi watendaji wa manispaa za Kigoma, mkoa wa Kigoma na manispaa ya Mpanda, mkoa wa Katavi kwa tuhuma za kuridhia na kutekeleza maamuzi ambayo yamesababishia serikali hasara na upotevu wa fedha. Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma, Mhandisi Boniface Nyambele anakabiliwa na tuhuma ya uuzaji wa nyumba za halmashauri bila kufuata sheria, kanuni na taratibu zilizopo na bila kibali cha waziri mwenye dhamana kama sheria inavyoelekeza. Mkurugenzi wa Manispaa ya Mpanda, Ndugu Suleiman Lukanga anakabiliwa na tuhuma za ununuzi hewa wa gari la kusomba taka kwa kiasi cha shilingi milioni tisini na mbili, laki saba na elfu hamsini (92,750,000/=) na ubadhirifu wa fedha za ujenzi wa skimu ya umwagiliaji ya Kakese kiasi cha shilingi milioni mia m

UKAWA WASHINDA KITI CHA UMEYA MANISPAA YA ILALA.

Image
Meya wa Manispaa ya Ilala, Charles Kwiyeko akizungumza na madiwa wa Manispaa ya Ilala leo mara bada ya kushinda  kwa Kura 31 katika uchaguzi wa meya wa manispaa hiyo katika ukumbi wa Karimjee leo jijini Dar es Salaam. Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala Omary Salum Kumbilamoto  akiwashukuru madiwani waliompigia kura leo mara ya kuibuka kidedea katika uchaguzi uliofanyika katika ukumbi wa Karimjee leo jijini Dar es Salaam. Baadhi ya  wapiga kura wakipiga kura za Meya na Naibu leo katika uchaguzi  wa kuwapata viongozi hao wa Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam. Matokeo ya Meya na Naibu Meya yakujumlishwa na baadhi ya wajumbe wa Meya,naibu Maya  wakiwa na Mwanasheria wao leo mara baada ya kumaliza kugika kura katika uchaguzi uliofanyika katika ukumbi wa Karimjee leo jijini Dar es Salaam.  Baadhi ya viongozi wakiwa kwenye ukumbi wa Karimjee leo jijini Dar es Salaam.  Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala, Isaya Mgurumi akitangaza matokeo ya Ume

HATUA AMBAZO ZIMECHUKULIWA DHIDI YA STANBIC BANK TANZANIA LIMITED KUHUSU USHIRIKI WAKE KUWEZESHA MKOPO WA SERIKALI WA DOLA ZA KIMAREKANI MILIONI 600

Image
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt Philip Mpango (kushoto) akiongea na waandishi wa habari (hawamo pichani)jijini Dar es Salaam, kuhusu hatua zilizochukuliwa na Serikali dhidi ya Benki ya Stanbic Tanzania kutokana na ushiriki wake katika kuwezesha mkopo wa Serikali wa Dola za Kimarekani Milioni 600 na Kulia kwake ni Naibu Gavana  wa Benki Kuu ya Tanzania(BOT) Bw. Lila Mkila. Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt Philip Mpango (katikati)  akitoa tamko kwa waandishi wa habari (hawamo pichani) jijini Dar es Salaam, kuhusiana na kusudio la kuitoza Benki ya Stanbic faini ya shilingi bilioni 3.  Kulia kwake ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dkt. Servicius Likwelile na Kushoto kwake ni Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Bw. Lila Mkila. ……………………………………………………………………………………… Utangulizi Mwezi Julai 2013, Benki Kuu ya Tanzania kupitia ufuatiliaji wa kawaida wa shughuli za mabenki iligundua matatizo yaliyohusiana na hasara i