Mwalimu Afungwa Jela Miaka 90 kwa kuwanajisi wanafunzi

kenya 
Mwalimu John Gichia Mugi.
Nairobi, Kenya
Mwalimu mmoja wa shule ya msingi aliyetambulika kwa jina la John Gichia Mugi mwenye umri wa miaka 23 nchini Kenya amehukumiwa kifungo cha miaka 90 jela kwa kuwanajisi wanafunzi wake wenye umri kati ya miaka 13 hadi 16.
Hii ni moja kati ya vifungo vya muda mrefu zaidi kuwahi kutolewa kwa watu wanaowaingilia watoto kijinsia nchini Kenya.
kenya primary
Mwalimu John Gichia alishtakiwa kwa kuwabaka wavulana 9 wa shule ya msingi ya Muthiria iliyopo Muran’ga takriban kilomita 120 Magharibi mwa Nairobi nchini humo mnamo Januari na Mei mwaka 2015.
Mwalimu huyo atatumikia kifungo cha miaka 10 kwa kila kosa alilotenda yaani kubaka watoto 9, hivyo kufanya jumla ya miaka atakayotumikia jela kufikia 90.
Jaji alisema mwalimu walikuwa amesaliti dhamana na imani aliyopewa na wazazi wa wanafunzi hao wachanga ambao alipaswa kuwatunza, inasemekana alikuwa akiwafanyia vitendo hivyo viovu watoto hao baada ya muda wa masomo wa usiku (preps).
Wavulana hao walikuwa na ushahidi kuwa Mugi aliwaguswa sehemu zao za siri na wakati mwingi anawabusu. Wakati huo alikuwa akihudumu kama mwalimu anayesimamia maswala ya bweni katika shule hiyo.
Kifungo hicho cha miaka 90 ni ishara tu kuwa sera za serikali ya Kenya imeanza kuchukua hatua kali dhidi ya wale wanaowadhulumu watoto nchini kenya. Ikiwa atajaaliwa na maiasha marefu, Mugi ataachiliwa akiwa na umri wa miaka 113.

Comments

Popular posts from this blog