Posts

BREAKING NEWS: Rais Magufuli afanya mazungumzo na Lowassa Ikulu

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 09 Januari, 2018 amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Edward Ngoyai Lowassa, Ikulu Jijini Dar es Salaam. Baada ya mazungumzo hayo Mhe. Edward Ngoyai Lowassa amempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa kazi nzuri anayoifanya na ametaja baadhi ya maeneo ambayo kazi kubwa imefanyika kuwa ni kutoa elimu bila malipo, ujenzi wa mradi wa uzalishaji wa umeme katika maporomoko ya mto Rufiji (Stiegler’s Gorge), ujenzi wa viwanda na ujenzi wa reli kwa kiwango cha kisasa (Standard Gauge) ambavyo vinazalisha ajira nyingi kwa Watanzania. “Nimepata faraja sana kuja hapa Ikulu kuonana na Mhe. Rais, tumezungumza nae na nimempongeza kwa kazi nzuri anayoifanya, lazima tukiri anafanya kazi nzuri na anahitaji kutiwa moyo. “Moja kubwa ambalo ni la msingi sana ni la kujenga ajira, katika kuanza ujenzi wa reli ya kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro hapo anajenga ajira, na kwenye nchi yoyote ina

Chid Benz Adakwa na ‘Unga’

Image
NGULI WA wa Hip Hop nchini Rashid Makwiro ‘Chid Benz anashikiliwa tena  na jeshi la polisi mkoani Dodoma kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya na hii inakuwa mara ya tatu kwa msanii huyu kukumbwa na sakata hili. Akithibitisha taarifa hizo Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma, SACP, Giless Muroto amesema kwamba ni kweli msanii huyo alikamatwa na taarifa kamili zitatolewa hapo kesho. Kamanda Muroto amesema; “ Ni kweli Chidi Benz mnamo Desemba 30, 2017, tulimkamata akiwa yeye na mke wake na vijana wawili. Tumemkamata akiwa na dawa za kulevya zidhaniwayo kuwa ni Heroine. jalada lake lipo tayari kwa Mwanasheria wa wa serikali linafanyiwa uchunguzi na muda wowote watapelekwa mahakamani “ Aidha ameongza kuwa watuhumiwa wote bado wako mahabusu.

Hizi ndizo sababu nyimbo za Lady Jaydee kutochezwa Clouds

Image
Lady Jaydee ameeleza kuhusu nyimbo zake kushindwa kuchezwa Clouds Media wakati ilionekana tayari wameshamaliza bifu lao. Akiongea na Dizzim Online msanii huyo amesema, hajawahi kukataza nyimbo zake kuchezwa na kituo hicho hata hivyo walisharuhusiwa na Seven lakini hakuna kilichofanyika. “Ilisemekana kuwa mimi ndio nilikataza nyimbo zangu kupigwa, jambo ambalo sio kweli. Mimi sikukataza nyimbo zangu kupigwa na hakuna sehemu yoyote niliyoandika nyimbo zangu zisipigwe, wao ndio waliamua kwa sababu kuongea kwangu kule kwamba nyimbo zisipigwe. Baada ya hapo walisema akitoa ruhusa nyimbo zake zipigwe zitapigwa. Seven aliongea na akatoa Go ahead je walipiga? Kwa hiyo hapo sio tatizo langu mimi, hapo inadhihirika wazi kabisa kuwa tatizo liko wapi na mtu anaweza kuongea kitu sio kwa kumaanisha,” amesema Jide. Mwishoni mwa mwezi Novemba mwaka 2016 Mkurugenzi wa Vipindi wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba alipokuwa akiongea na kipindi cha XXL alisema

Kumbe aliyejiunganishia bomba la mafuta ni mstaafu wa Tazama

Image
Aliyejiunganishia bomba la mafuta nyumbani kwake Samwel Kilanglani(63) amejulikana kuwa ni mfanyakazi mstaafu wa bomba la kusafirisha mafuta Tanzania na Zambi (Tazama). Kilanglani anatuhumiwa kutoboa bomba la mafuta ya dizeli la Mamlaka ya Bandari Tanzania(TPA) na kujiunganishia kwenye mantaki mawili yakiwa ndani ya nyumba yake iliyopo Tungi Kigamboni. Akizungumza na Mwananchi leo Jumanne, Kaimu Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Benedict Kitalika amesema mtuhumiwa huyo alijiunganishia na bomba la TPA kwa njia ya kuchomelea na kuunganisha moja kwa moja kwenye mantaki yake mawili yaliyochimbiwa chini ndani ya nyumba yake. Kitalika amesema mtuhumiwa alijiunganishia katikati na bomba kuu hivyo mafuta yanapopelekwa sehemu husika mengine yanaingia kwake hivyo hayafiki kama yalivyokusudiwa. "Mafuta yanaweza yakapelekwa lita 4,000 sehemu husika lakini hayafiki yote mengine yanaenda kwa mtuhumiwa huyu matokeo yake wanajiuliza haya mengine yameenda wapi,&

Muslim Hassanali Ajiunga CCM Akitokea Chadema

Image
Muslim Hassanali, aliyekuwa mgombea ubunge wa Jimbo la Ilala 2015. ALIYEKUWA mgombea ubunge Jimbo la Ilala kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika uchaguzi mkuu wa 2015, Muslim Hassanali, amejiunga na Chama Cha Mapinduzi  (CCM)  na kupokelewa na Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Philip Mangula na viongozi wengine wa CCM katika ukumbi wa Checkpoint Pugu jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa CCM Bara, Philip Mangula (katikati)akiwa na viongozi wengine. Kujiunga kwa Hassanali ni mwendelezo wa mfululizo wa viongozi wa upinzani wakiwemo wabunge na madiwani kuondoka na kwenda CCM. Muslim Hassanali (kushoto) akirudisha fomu ya kugombea ubunge Jimbo la Ilala kwa tiketi ya Chadema katika uchaguzi mkuu wa  2015. Viongozi kadhaa wakiwemo wabunge na wapinzani wamejiunga na CCM wakitokea upinzani kwa sababu mbalimbali  ikiwemo ya kuunga mkono serikali ya Rais John Magufuli.

Siri 3 Dereva Wa Lissu Kutimkia…

Image
Simon Bakari akiongea na Freeman Aikaeli Mbowe. SIRI tatu za dereva wa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema), Simon Bakari (pichani) kwenda Ubelgiji na bosi wake zimevuja. Mbunge mmoja ndani ya chama hicho aliyeomba jina lake lisiandikwe gazetini kwa kuwa siyo msemaji wa chama wala familia, alisema kamati maalum inayoratibu matibabu ya Lissu iliyokutana jijini Nairobi, Kenya iliona ni vema Simon aongozane na bosi wake pamoja na mkewe mbunge huyo, Alicia kwa kuwa ndiye aliyefanya kazi kubwa ya kumuuguza akiwa Nairobi akisaidiana na Mkuu wa Idara ya Uenezi, Hemedi Ali. Tundu Lissu (Chadema). “Pamoja na ukweli kwamba dereva Simon alikuwa ana matatizo ya kisaikolojia baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana akiwa na Lissu mkoani Dodoma Septemba 7, mwaka jana, alijitahidi kutoa huduma zisizo za kitabibu pamoja na Hemedi (Mkuu wa Idara ya Habari na Uenezi, Chadema) Nairobi ndiyo maana kamati maalum ya kuratibu tiba ya mbunge huyo ikaona ni vema

Mfungwa afufuka akiwa mochwari

Image
Mfungwa mmoja amezinduka na kujikuta yupo kwenye chumba cha kuhifadhia maiti baada ya madaktari watatu kuthibitisha kuwa alikuwa amefariki, vyombo vya habari Uhispania vimetoa taarifa hiyo. Gonzalo Montoya Jiménez alikuwa ni mfungwa katika gereza Asturias na alizinduka saa chache  kabla ya kufanyiwa upasuaji kwa ajili ya kugundua chanzo cha kifo chake. Gonzalo yupoa chini ya uangalizi wa madaktari katika chumba cha wagonjwa mahututi katika hospitali ya Oviedo. Mmoja wa ndugu zake ameliambia gazeti la La Voz de Asturias kwamba Gonzalo  “alikuwa amewekewa alama ya kufanyiwa upasuaji, tayari kupasuliwa”. Wataalamu wamesema hali hiyo inaitwa ‘catalepsy’ ni hali ambayo ishara muhimu za uhai hufifia kwenye mwili wa binadamu kiasi cha kutoweza kutambulika kama yupo hai.

Kingunge Ataka Kujua Hali ya Tundu Lissu

Image
Aliyekuwa mgombea wa urais katika uchaguzi mkuu wa 2015 kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Edward Lowassa (wa pili kushoto), akiwa na Mwenyekiti wa Chadema,  Freeman Mbowe,   wakimjulia hali  Kingunge Ngombale Mwiru aliyelazwa katika Hospital ya Taifa ya Muhimbili. MWANASIASA mkongwe , Kingunge Ngombale Mwiru, ambaye amelazwa katika hospitali ya Muhimbili kufuatia kung’atwa na mbwa amemkumbuka na kutaka kujua haliya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, ambaye amesafirishwa kutoka hospitalini Nairobi, Kenya,  kwenda Ubelgiji kwa matibabu zaidi. Kigunge ameulizia hali ya Tundu Lissu baada ya Mwenyekiti wa Chadema Taifa aliyekuwa amefuatana na Waziri Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema,  Edward Lowassa,  walipomtembelea leo Januari 8, 2018 katika hospitali ya Muhimbili. “Vipi hali ya  Tundu Lissu? Nimeona mimi jinsi wanavyonifanyia hapa (madaktari),  nimewauliza mimi tu niliyeng’atwa na mbwa mnanifanyia hivi, je Lissu mmemfany

Lowassa, Mbowe wamtembelea Kingunge Hospitali

Image
Mwenyekiti CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe ameongozana na Waziri Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu, Edward Lowassa kumjulia hali Mzee Kingunge Ngumbare Mwiru aliyelazwa katika Hospital ya Taifa ya Muhimbili anapopatiwa matibabu. Mzee Kingunge anatibiwa majeraha baada ya kushambuliwa na mbwa nyumbani kwake . Hivi karibuni Rais John Magufuli alifika hospitalini hapo kumjulia hali Kingunge ambaye ni miongoni mwa wazee wakongwe kwenye siasa za Tanzania ambaye amewahi pia kushika nyadhifa mbalimbali Serikalini tangu awamu ya kwanza hadi ya nne.

RAIS MAGUFULI AANIKA MADUDU ZAIDI WIZARA YA MADINI

Image
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameanika madudu mengine ya Wizara ya Madini akisema kuwa baadhi ya wateule wake katika wizara hiyo wamekuwa wazembe katika kutekeleza maagizo na kutimiza majukumu yao kama watendaji wa serikali. Magufuli ameyasema hayo leo Jumatatu wakati akimwapisha Mhe. Dotto Mashaka Biteko kuwa Naibu Waziri wa Madini Ikulu jijini Dar es Salaam. Rais ametolea mfano wa sheria mpya ya madini iliyopitishwa bungeni mwezi Julai mwaka jana, ambapo amesema mpaka sasa wizara hiyo haijapitisha kanuni (regulations) ili sheria hiyo iweze kufanya kazi jambo ambalo amesema ni uzembe usiovumilika huku akimwagiza Waziri wa Sheria, Prof. Palamagamba Kabudi kukamilisha kanuni hizo na kuzisaini kufikia Ijumaa ya wiki hii. “Nakushukuru Mhe spika kwa kutoa ushauri kwa serikali na sisi tumekuwa tukiufuata sana. Wizara ya madini ina changamoto sana na hata sasa ina changamoto na haifanyi kazi vizuri. Spika utakumbuka mwezi wa saba mlifany

RAIS ABAINI MADUDU TENA BANDARINI, ATEUA KAMISHNA WA MADINI

Image
RAIS Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Prof. Shukrani Elisha Manya Mhadhiri wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM) kuwa Kamishna wa Madini. Rais ametangaza uteuzi huo leo Jumatatu Januari 8, 2018 alipokuwa akitoa hotuba fupi mara baada ya kumuapisha Mhe. Dotto Mashaka Biteko kuwa Naibu Waziri wa Madini. Nimesikia tatizo ni kamishna wa madini, sasa nimeamua kumteua kamishna mpya wa madini, jina lake linaanza na Prof. Shukrani Elisha, huyo atakuwa ndiye mtendaji na msimamizi mkuu wa madini. Mambo ya hovyo ni mengi mno, nilipotembelea bandarini niliunda katume kasirisiri hivi, kwa kulihusisha Jeshi la Wananchi, TISS na Polisi. Yanayogundulika huko ni ya ajabu, kuna hadi simenti za zamani sana, yapo makontena bandarini na pale Ubungo. Mimi sio mwanasiasa mzuri wa kubembelezabembeleza, nikitoka mimi mtapata wakubembeleza, ila mimi nataka kabla ya Ijumaa regulations (kanuni za sheria ya madini) ziwe zimesainiwa. Pro Kabudi nendeni mkazifanyie kazi, tafuta watu wa kukusaid

BREAKING NEWS: NECTA YATANGAZA MATOKEO YA KIDATO CHA PILI, DARALA LA NNE

Image
BARAZA la Mitihani Tanzania (NECTA) limetangaza matokeo ya mitihani ya upimaji wa darasa nne na kidato cha pili iliyofanyika Novemba mwaka jana, huku idadi kubwa ya wanafunzi wakifaulu vizuri katika mitihani hiyo. Akitangaza matokeo hayo leo Jumatatu, Januari 8, Katibu Mtendaji wa baraza hilo, Dk Charles Msonde amesema jumla ya wanafunzi 1,086,156 waliofanya mtihani wa darasa la nne wamefaulu kati ya 1,158,444 waliofanya upimaji huo. Amesema wanafunzi hao wamefaulu kwa kupata alama zenye madaraja ya A,B,C na D wakati wanafunzi 72,288 sawa na asilimilia 6.24 wamepata alama za daraja E, ambao ni ufaulu usioridhisha. Kuhusu matokea ya upimaji wa kidato cha pili, Dk Msonde amesema jumla ya wanafunzi 433,453 sawa na asilimia 82.32 kati ya 486,742 waliosajiliwa kufanya mtihani huo wamepata ujuzi wa maarifa ya kuwawezesha kuendelea na kidato cha tatu. Dk Msonde alisema wanafunzi wa kidato cha pili 51,807 sawa na asilimia 10.68 wameshindwa kupata alama za kuwaweze

Pretty Kind afungiwa miezi sita kwakutoa Wimbo usio na maadili

Image
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza amemfungia msanii Suzan Michael maarufu kama Pretty Kind kujihusisha na sanaa kwa muda wa miezi sita. Akizungumza leo Jumapili Januari 7 jijini Dar es Salaam, Shonza amesema amechukua hatua hiyo kutokana na msanii huyo kutoa wimbo uitwao ‘viduduwasha’ usio na maadili. Msanii huyo pia amekutwa na kosa la kufanya  kazi ya sanaa bila kusajiliwa na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), kuweka mtandaoni picha ya nusu utupu kinyume na maadili. ‘’Kumekuwa na wimbi kubwa la wasanii kutoa nyimbo zenye maneno ya matusi na zisizo na maadili, pamoja wanawake kupiga picha wakiwa wamevaa nusu utupu na kuweka picha hizo katika mitandao,” amesema Shonza na kuongeza, “Nataka kuwapa angalizo wasanii wenye tabia hizi kuwa Serikali inawafuatilia kwa karibu na mwaka huu tumeanza na huyu na wengine wanafuata kama msanii Gift Stanford maarufu kama Gigy Money na  Jane Rimoy maarufu kama Sanchi.” Shonza amemtaka msanii

Madereva boda boda wenye hasira wateketeza Basi kwa moto

Image
Madereva wa Boda boda wenye hasira wameliteketeza Basi la abiria la Kampuni ya Simba  Coach lililokuwa linatokea jijini Nairobi kwenda Malindi nchini Kenya jana mchana. Basi hilo ambalo kabla ya tukio hilo mashuhuda wamesema kuwa lilimgonga muendesha bodaboda mmoja na kufa hapo hapo lakini halikusimama kitu ambacho kilipelekea waendesha boda boda kuanza kulikimbiza. Wakielezea tukio abiria wamesema dereva wa Basi alitaka ku-overtake gari ndogo katika eneo la Kijiwetanga na ndipo alipomgonga dereva huyo wa Boda boda. Abiria wamesema baada ya Basi hilo kusimamishwa na madereva boda boda waliamuriwa kutoka kwenye Basi hilo kabla ya kulichoma moto. Tayari Kamanda wa Polisi mjini Malindi,  Matawa Muchangi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na dereva wa gari hilo bado anatafutwa huku Dereva wa boda boda aliyegongwa mwili wake umepelekwa katika Hospitali ya Malindi. Chanzo:The Star Kenya

Tundu Lissu Awasili Ubelgiji Kwa Ajili Ya Matibabu Ya Mazoezi Ya Viungo

Image
Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Antipas Lissu akiwa na madaktari baada ya kufika Ubelgiji. Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Antipas Lissu amewasili katika uwanja wa ndege jijini Brussels, nchini Ubelgiji ambapo amepelekwa kwa ajili ya awamu ya tatu ya matibabu yake yatakayohusisha mazoezi ya viungo. Tundu Lissu amewasili jijini hapo akitokea katika Hospitali ya Nairobi, nchini Kenya alikokuwa anapatiwa matibabu kwa muda wa takribani miezi minne sasa kutokana na kushambuliwa kwa risasi mnamo septemba mwaka jana mkoani Dodoma Mbunge Tundu Lissu, ambaye pia ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, alishambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana alipokuwa akitoka Bungeni, majira ya saa 7 mchana, karibu na nyumbani kwake Area D, mjini Dodoma. Kwa mujibu wa taarifa ya madaktari waliokuwa wanamtibu, walieleza kuwa jumla ya risasi 16 zilimpata Tundu Lissu mwilini mwake na wamefanikiwa kuzitoa 15, isipokuwa moja ambayo ipo nyuma ya uti wa mgongo. Tundu Li

MENEJA WA WAKALA WA MAJENGO (TBA) KIGOMA AKAMATWA

Image
  Jeshi la polisi linamshikilia Meneja wa Wakala wa Majengo (TBA), Mhandisi Mgalla Mashaka kwa tuhuma za kushindwa kukarabati Shule ya Sekondari Kigoma. Meneja huyo alikamatwa akituhumiwa kushindwa kukarabati shule ya sekondari Kigoma kwa wakati licha ya kupewa zaidi ya shilingi milioni mia nne kati ya mia tisa tangu mwezi wa nane mwaka jana. Mhandisi Mgalla amekamatwa baada ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako, kufanya ukaguzi katika shule hiyo ambayo imeanza kupokea takribani wanafunzi elfu moja huku katika miezi mitano ya ukarabati hadi sasa ukarabati wa vyoo, mabweni, maabara na vyumba vya madarasa haujakamilika Prof. Ndalichako amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa TBA kufika Kigoma kutatua tatizo hilo ili kuepusha maafa yanayoweza kutokea. Kutokana na hali hiyo serikali imeamua kujenga vyoo vya muda ili wanafunzi waweze kuanza masomo wiki ijayo. 

Breaking News: BOT yazifutia leseni Benki Tano

Image
 Benki Kuu ya Tanzania(BoT) imezifutia  leseni ya kufanya biashara benki tano na kuziweka chini ya ufilisi. Taarifa iliyotolewa leo Alhamisi na BoT imezitaja benki hizo kuwa ni Covenant Bank For Women (Tanzania) Limited, Efatha Bank Limited, Njombe Community Bank Limited, Kagera Farmers' Cooperative Bank Limited, na Meru Community Bank Limited. BoT imeeleza kuwa imefanya hivyo kwa mamlaka iliyopewa chini ya kifungu cha 56(1)(g), 56(2) (a), (b) na (d), 58(2)(i), 11(3)(c) na (j), 61(1) na 41(a) cha Sheria ya Mabenki na Taasisi za Fedha ya mwaka 2006, Benki Kuu ya Tanzania imeamua kuzifunga; kusitisha shughuli zake zote za kibenki; kufuta leseni zake za biashara ya kibenki; na kuziweka chini ya ufilisi. “Kwa mamlaka iliyopewa chini ya kifungu Na. 41(a) cha Sheria ya Mabenki na Taasisi za Fedha ya mwaka 2006; Benki Kuu ya Tanzania imeiteua Bodi ya Bima ya Amana (The DEPOSIT INSURANCE BOARD) kuwa mfiiisi kuanzia tarehe 04 Januari 2018,” imeeleza taarifa hiyo.” “Ua

RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AKUTANA NA MJUMBE MAALUM WA RAIS WA UGANDA YOWERI MUSEVENI, WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA UGANDA SAM KUTESA IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mjumbe maalum wa Rais wa Uganda Yoweri Museveni ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Uganda Sam Kutesa mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam. < Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Mjumbe maalum wa Rais wa Uganda Yoweri Museveni ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Uganda Sam Kutesa mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Ujumbe Maalum uliotoka kwa Rais wa Uganda Yoweri Museveni na kuwasilishwa kwake na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uganda Sam Kutesa mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiufungua na kuusoma Ujumbe huo maalum uliotoka kwa Rais wa Uganda Yoweri Museveni na kuwasilishwa kwake na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uganda Sam Kutesa

NUNUA JIKO TUKUPELKEE HADI KWAKO BUREEE (DAR) NA ZAWADI YA MAFUTA BUREEEE

Image
Kwa Mara nyingine tena Bngo Deco Electronics, tunakuletea majiko makubwa ya kupikia kwa bei poa kabisa. Majiko haya yanadumu sana na yanakuja na warranty  ya mwaka mmoja, likisumbua tu tutakurekebishia. Nakwa kuthamini mchanngo wa Muungwana Blog kila mteja atakatoka katika Muungwana atapew dumu la mafuta ya alizeti BUREE na kama yupo Dar tutampelekea BUREE hadi kwake.   Kwa wateja wa mkoani gharama za kutuma jiko kwenda mkoani ni jukumu la mteja mwenyewe ila kama ni kumpelekea kwenye basi au lori la kuja mkoani basi tutatoa usairi BUREE hadi sehemu ya kutumia. Tupo Magomeni Mapipa mtaa wa Idrissa karibu kabisa na Butiama Restaurant.