Posts

AMPIGA RISASI BABA MKWE WAKE KANISANI

Image
Chanzo cha mwandishi wa habari wa kujitegemea, Elias Mhegera kumpiga risasi baba mkwe wake kanisasni juzi ni hisia kuwa mzazi wa mwanamke huyo ndiye chanzo cha kuvunjika kwa ndoa yao miaka 10 iliyopita. Mhegera ambaye kwa sasa anashikiliwa na Jeshi la Polisi tangu juzi amekuwa katika mvutano na mke wake ambaye waliachana miaka 10 iliyopita. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni amethibitisha kutokea kwa tukio hilo juzi majira ya saa1:30 asubuhi katika Parokia ya Bikira Maria, Kibangu na kueleza kuwa chanzo ni ugomvi wa kifamilia. “Adrian Mpande alijeruhiwa bega la kushoto na mtu anayedaiwa kuwa ni mkwe wake. Uchunguzi wa awali umebainisha kuwa sababu ni mambo ya kifamilia,” alisema Kamanda Kaganda na kuongeza: “Tunaendelea na uchunguzi na kukiwa na umuhimu tutawaeleza kwa uwazi. Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo ambaye hakutaka jina lake litajwe alisema kuwa Mzee Mpande alipigwa risasi mbili wakati akijiandaa kuingia kanisani kwa ibada juzi Jumapili. N

Mabasi 11 yafungiwa kufanya safari za mikoani

Image
Jeshi la polisi mkoa wa Arusha limefanya ukaguzi wa kushitukiza kwa mabasi ya kusafirisha abiria kwenda mikoani wilayani na maeneo ya vijijini na kugundua makosa mengi kwenye magari hayo  ambapo zaidi ya mabasi arobaini yametozwa faini huku  mabasi kumi na moja  yakifungiwa kusafirisha abiria baada ya kukutwa na makosa makubwa yanayohatarisha uhai wa wasafiri. Katika ukaguzi huo maafisa wa jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabarani wamegundua makosa mengi yakiwemo kukosa mikanda ya abiria uchakavu wa maumbo ya magari na kati ya zaidi ya mabasi hamsini yaliyokaguliwa madereva watano wenye makosa sugu wamefikishwa mahakamani. Wakizungumzia operesheni hiyo wafanyakazi wa mabasi na mawakala wamekuwa na maoni tofauti wakati wengine wakidai kutopatiwa muda wa kutosha kufanya marekebisho wengine wameunga mkono  zoezi hlo  huku abiria wakieleza walivyoathirika.

SPIKA JOB NDUGAI ATAMBULISHWA KWA MASPIKA WA MABUNGE YA JUMUIYA YA MADOLA BARANI AFRIKA

Image
Mhe Spika Job Ndugai akitambulishwa katika mkutano wa Maspika wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola Barani Afrika unaofanyika Abuja Nigeria.Mkutano huo unafanyika kujadili masuala mbali mbali yanayohusu mabunge hayo unashirikisha Maspika toka nchi 18 za Jumuiya ya Madola Barani Afrika

Baba Adaiwa Kutaka Kumtoa Kafara Mwanaye!

Image
Msichana anayedaiwa kupewa mimba na Babu mmoja.   STORI: IMELDA MTEMA, DAR DUNIA imekwisha! Ndivyo unavyoweza kusema kufuatia kuwepo kwa matukio mawili ya kusikitisha, moja la baba aliyefahamika kwa jina la Ombani Emmanuel mkazi wa Pansiansi jijini Mwanza, kukamatwa na polisi kwa kumfanyia vitendo vya kikatili mwanaye ikiwa ni pamoja na kudaiwa kutaka kumtoa kafara na tukio lingine ni la babu mmoja kudaiwa kumpa mimba mjukuu wake. Katika tukio la kwanza imedaiwa kuwa Emmanuel, hivi karibuni alikamatwa na polisi kwa kile kinachodaiwa kumfanyia mambo ya ajabu mwanaye mwenye umri wa miaka 10, huku majirani wakidai kuwa, kulikuwa na kila dalili za baba huyo kutaka kumtoa kafara. …Akiwa katika pozi. Akizungumza na gazeti hili, Mkurugenzi wa Taasisi ya Nitetee, Flora Lauo alidai mambo aliyokuwa akifanya baba huyo yalikuwa yakiwakera majirani wengi kwa sababu mbali na kuwepo kwa dalili za kutaka kumfanyia tukio baya, pia alikuwa hamruhusu kujichanganya na mtu yeyot

SHILOLE: UMAMA N’TILIE UMENITEKA KULIKO MUZIKI

Image
Zuwema Mohammed ‘Shilole. MWANAM-UZIKI wa miondoko ya mduara, Zuwema Mohammed ‘Shilole’ ameweka wazi kuwa huenda akaukacha muziki siku za usoni kutokana na kunogewa na biashara yake ya kuuza chakula katika mgahawa wake.Akizungumza na Risasi Vibes, Shilole alisema anaona biashara yake hiyo inampa faida nyingi kuliko uigizaji na hata muziki anaofanya, hivyo kutokana na maisha magumu ni bora kufanya kitu kinachomu-ingizia kipato. “Huku kwa mama ntilie naona kunanilipa zaidi ya sehemu nyingine ambazo nipo, sasa ni bora kufanya kitu ambacho kina kuingizia kipato kuliko kung’ang’ania sehemu ambayo haikulipi au inakulipa kidogo tena kwa kusubiri,” alisema Shilole.

“Wanaume wa WCB wote Waaminifu” – Babutale

Image
 Kutoka Makao Makuu ya WCB kwa Meneja wa mwimbaji staa wa Bongofleva Diamond Platnumz na Tip Top Connection, Babutale leo July 25, 2017 amepost picha yenye maneno yalioandikwa ‘Wanaume wa WCB wote waaminifu’ kupitia ukurasa wake wa Instagram @babutale

Lile sakata la mama kuibiwa mtoto kutua kwa JPM

Image
DAR ES SALAAM: Lile sakata la mwan­amama Asma Juma (29) aliyedai kujifungua watoto wawili mapacha katika Hospitali ya Temeke Machi mwaka huu, limechukua sura mpya baada ya familia yao kusema italifikisha suala hilo kwa Rais Dk. John Pombe Magufuli ili kupatiwa suluhisho. Hatua ya familia hiyo inatoka­na na kutoridhishwa na ripoti iliyotolewa na timu iliyoundwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu ambayo ilidai baada ya uchunguzi wa kina, ilibainika kuwa mama huyo al­ijifungua mtoto mmoja, tofauti na madai yake kuwa alikuwa na ujauzito wa mapacha waw­ili. Akizungumza na Risa­si Mchanganyiko jana, mama huyo alisema yeye na mumewe, hawajakubaliana hata kidogo na ripoti hiyo ili­yotolewa siku chache zilizopi­ta na kwamba msimamo wao upo palepale. “Ile ripoti iliniumiza mno, ni ngumu kwangu kukubaliana nayo, tumeona bora kwenda kwenye haki za binadamu ili watusaidie swala letu, kwa mujibu wa ripoti hiyo inasema sikuzaa mapach

TRA yaanika deni la Acacia, ni sawa na 'bajeti ya miaka 13'

Image
Mamlaka ya Mapato (TRA) imeitaka Kampuni ya Acacia kulipa zaidi ya Sh424 trilioni kutokana na ukwepaji kodi ilioufanya kuanzia mwaka 2000. Kwa kutumia bajeti ya sasa, fedha hizo ni sawa na bajeti ya Tanzania ya miaka 13. Deni hilo, ambalo ni sawa na dola 190 bilioni za Kimarekani limetokana na hesabu zilizopigwa kwa kutumia taarifa iliyotolewa na kamati mbili zilizoundwa na Rais John Magufuli kuchunguza usafirishaji wa mchanga wa madini unaofanywa na kampuni hiyo kutoka migodi ya Bulyanhulu na Buzwagi. Taarifa iliyotolewa jana na kampuni hiyo imekataa kulipa deni hilo kwa maelezo kwamba haijapewa ripoti ya kamati zote mbili. “Hatuyakubali makadirio haya. Kampuni itaangaalia haki na namna zote zilizopo kuhusu suala hili,” inasema taarifa hiyo. Kwa mujibu wa Acacia, deni hilo limeelekezwa kwa kampuni zake tanzu ambazo ni Bulyanhulu Gold Mine (BGML) inayoendesha mgodi wa Bulyanhulu, na Pangea Minerals (PML) inayosimamia mgodi wa Buzwagi. Taarifa hiyo iliyo

Masanja Alivyokutana na Majeruhi wa Lucky Vicent nchini Marekani

Image
Emmanuel Mgaya, Maarufu kama Masanja Mkandamizaji akiwa nchini Marekani amekutana na kuzungumza na watoto Sadia na Wilson ambao ni majeruhi ya ajali ya shule ya Lucky Vicent ya jijini Arusha wanaopatiwa matibabu nchini humo.  Masanja pia kupitia ukurasa wake wa instagram amethibisha kukutana na watoto hao: MUNGU AMENIPA NEEMA YA KWENDA KUWAONA WADOGO ZETU WALIOPATA AJALI SADIA NA WILSON NA KUWEPO MAREKANI KWA MATIBABU….. IMEKUWA SIKU NJEMA KWETU SOTE TUMEFURAHI PAMOJA NAO KULA NAO NA KUMTAFAKARI MUNGU KWA PAMOJA. LAKINI PIA NIMEZUNGUMZA NA WENYEJI WAO WALIOFANIKISHA SAFARI YA WAO KUJA MAREKANI!! HAKIKA MUNGU NI MWEMA WAMEENDELEA KUIMARIKA NA WANAENDELEA VIZURI!! SHUKRANI KWA MADAKTARI NA KILA ALIYETENGA MDA WAKE KUWAOMBEA!! WAZAZI WAO WANAWASALIMU NA WANAWASHUKURU KWA USHIRIKIANO NA MAOMBI YENU..🙏🏾🙏🏾🙏🏾 Tazama picha:

TCU Yataja Vyuo Vilivyozuiliwa Kudahili Wanafunzi 2017/18

Image
Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU) imetoa orodha ya vyuo vilivyozuiliwa kufanya udahili wa wanafunzi wa mwaka wa kwanza wa masomo 2017/18. Orodha hii imetolewa wakati wahitimu wa kidato cha sita wakiwa wanaendelea na mchakato wa kutuma maombi vyoni.  

Rihanna ‘The Bad Gal’ Uhuni, Usela Vinampa Mkwanja Mnono

Image
Rihanna. UKIMTAZAMA mwonekano wake jinsi alivyo mrembo, mwenye haiba nzuri ya kike, mvuto wa asili na sauti yenye utamu wa aina yake, huwezi kumdhania kwamba nyuma ya pazia ni mhuni na ‘msela’ aliyepitiliza! Jina lake halisi anaitwa Robyn ‘Rihanna’ Fenty, anapenda zaidi ukimuita Riri au The Bad Gal, mwanadada asiyechuja kutoka Visiwa vya Barbados, anayefanya poa kinoma kwenye anga la muziki wa kimataifa, maskani yake yakiwa nchini Marekani. Jina lake ni miongoni mwa wasanii wachache wa kike wanaoitingisha dunia kwa sasa, akichuana vikali na Beyonce Knowles, ingawa wapo baadhi ya watu wanaosema si sahihi kuwapambanisha wawili hao kwani Beyonce ni mkongwe na ana mafanikio zaidi ya Rihanna. Miongoni mwa matukio ya hivi karibuni yanayodhihirisha jinsi Rihanna ‘alivyopinda’, ni kwenye video ya Wimbo wa Wild Thoughts wa DJ Khaled , akiwa amemshirikisha mwanadada huyo na chalii mwingine, Bryson Tiller. Ukiisikiliza ngoma hii iliyoachiwa mwishoni mwa mwezi uliopita,

ZARI THE BOSS LADY AIBUA MAZITO TENA BAADA YA KIFO CHA MAMA YAKE,WASEMA ANA ROHO NGUMU

Image
Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ akiwa na mama yake, Halima Matovu Hassan ‘Mama Zari’ enzi za uhai wake. Kifo cha mama mzazi wa staa ambaye ni mjasiriamali Afrika Mashariki, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, Halima Matovu Hassan ‘Mama Zari’ (58) kilichojiri Alhamisi iliyopita nchini Uganda, kimeibua gumzo ambalo si la nchi hii.Gumzo hilo kutoka nyumbani kwa mama Zari huko Busunju, Munyonyo jijini Kampala, Uganda lilihitimishwa wikiendi iliyopita na vyombo vya habari za mastaa nchini humo baada ya mazishi ya mama Zari yaliyofanyika mchana wa Ijumaa iliyopita, kuwa, Zari ana roho ngumu aisee!Kwa mujibu wa vyombo hivyo, wakati wa kifo cha aliyekuwa mume wa Zari, Tycoon Ivan Ssemwanga ‘Don Ivan’ aliyefariki dunia Mei 25, mwaka huu, mwanamama huyo, kabla, wakati na baada ya mazishi ya baba watoto wake huyo alikosolewa juu ya tabia alizozionesha wakati wa msiba huo.Ilielezwa kuwa, baadhi ya mambo aliyoyafanya wakati ule ikiwemo kuposti vitu mitandaoni, mara akik

Ruby Ajazwa Kibendi

Image
Msanii Hellen George ‘Ruby’ JAZA ujazwe! Habari ya mjini kwa sasa inamhusu sexy lady wa Bongo Fleva, Hellen George ‘Ruby’ kujazwa kibendi na staa mkubwa wa muziki huo, licha ya kwamba mwanadada huyo amekuwa akifanya siri. Chanzo makini kililieleza Ijumaa Wikienda kuwa, Ruby ana ujauzito ambao umekuwa ukimfanya ajifichefiche huku akimficha aliyemjaza kibendi hicho kwa madai kuwa, jamaa aliyempachika kibendi amezaa na wanawake tofauti. Kama ilivyo desturi yake, Ijumaa Wikienda lilimnyatia Ruby ambaye alikiri kuwa mjamzito, lakini akatia ngumu kumtaja baba kijacho na umri wa mimba yake kwani wakati muafaka haujafika. “Mimba bado ni changa, siwezi kusema ina miezi mingapi. Kuhusu nimepewa na mwanamuziki mkubwa, siyo kweli ila ipo siku wakati ukifika nitasema ni ya nani,” alisema Ruby

MUIGIZAJI WA HOME ALONE AFARIKI DUNIA

Image
Aliyekuwa muigizaji wa Home Alone1,Home Alone 2 na Lost in New York, John Heard ameripotiwa kufariki dunia akiwa katika chumba cha hoteli moja jijini Callifonia. Muigizaji huyo ambaye amepata umaarufu kupitia filamu hizo zilizotamba miaka ya 90, amefariki akiwa na miaka 72, Mpaka sasa chanzo cha kifo cha muigizaji huyo hakijawekwa bayana. Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, marehemeu alikuwa amejipumzisha katika hoteli hiyo baada ya kufanyiwa upasuaji siku ya Jumatano katika kituo cha afya cha Stanford. Marehemu ameacha mke Margot Kidder na mtoto wake mmoja aitwaye John Matthew “Jack”

Uwoya, Kelvina Hapatoshi!

Image
Irene Uwoya. SIFA ya ubuyu wenye rangi nyekundu ni kuacha rangi midomoni vivyo hivyo penzi ni kikohozi kulificha huwezi! Wamama wawili wa Bongo Muvi, Irene Uwoya na Kelvina John, wanadaiwa kuingia kwenye vita nzito ya penzi la msanii wa Bongo Fleva, Patrick Chrisopher ‘PCK’ na sasa hapatoshi, ni Ijumaa Wikienda pekee lenye ubavu wa kukupa ubuyu ulionyooka. MAPENZI SHATASHATA Chanzo makini cha ubuyu huo kililieleza Ijumaa Wikienda kuwa, kwa sasa PCK na Kelvina ni mahaba niue au mapenzi shatashata, jambo ambalo linamchukiza Uwoya ambaye anasemekana kwamba, aliwahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanaume huyo anayesifika kwa kuwachanganya na kuwapanga kama mafungu ya nyanya mastaa wa kike Bongo. “Hivi watu wa ubuyu mnajua kuwa kuna vita nzito kati ya Uwoya na Kelvina? Unaambiwa sasa hivi vita yao siyo ya nchi hii na wanaviziana kama Korea Kaskazini na Marekani, eti, kisa nasikia wanagombea penzi la PCK. WAKUTANA BAA YA UWOYA “Tukio bichi la Uwoya na Kelvin

Lipumba Atangaza Kuwavua Uanachama Wabunge 8 wa CUF

Image
Profesa Ibrahim Lipumba. Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la Chama cha Wananchi (CUF) limewavua uanachama wabunge wanane wa chama hicho kwa madai ya utovu wa nidhamu, yakiwemo kukisaliti chama hicho. Mwenyekiti wa CUF, anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Profesa Ibrahim Lipumba amesema, baraza pia limewavua uanachama madiwani wawili wa viti maalumu mkoani Dar es Salaam, kwa makosa kama hayo. Profesa Lipumba ametangaza uamuzi huo leo Jumatatu, Julai 24 wakati wa mkutano na wanahabari uliofanyika makao makuu ya CUF, Buguruni, Dar es Salaam. “Leo asubuhi tumewasilisha nyaraka  za hatua hizi kwa Spika na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kwa hatua zaidi,” amesema Profesa Lipumba. Amesema wabunge hao wanane ni kati ya 10 walioitwa hivi karibuni na Kamati ya Maadili na Nidhamu kwa mahojiano wakitakiwa kujibu tuhuma zinazowakabili za kukihujumu chama hicho kwa maelezo kuwa walitaka kushirikiana na Chadema kumwondoa yeye madarakani.

WAZIRI PROF. MAGHEMBE AMEWAPOKEA MABILIONEA 28 KUTOKA MABARA YOTE DUNIANI KATIKA HIFADHI YA TAIFA YA SERENGETI

Image
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe akizungumza na Mabilionea 26 kutoka taasisi ya Young Presidents Organisation (YPO) wakiwa na wenza wao katika moja ya hoteli ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti wakati wa mapokezi yao jana kwa ajili ya ziara yao ya siku tatu nchini Tanzania. Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Alan Kijazi (katikati waliosimama) akizungumza na Mabilionea hao. Kulia kwake ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe . Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe akizungumza na Mabilionea hao jana katika moja ya hoteli ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti. Kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Alan Kijazi. Kiongozi wa msafara wa Mabilionea hao, Perry Amber akizungumza wakati wa mapokezi hayo jana katika moja ya hoteli ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.  Mabilionea hao kutoka taasisi ya Young Presidents Organ

Mboto: Mzee Majuto Hajafa Jamani!

Image
MSANII wa filamu nchini, Haji Salum maarufu kama Mboto , amekanusha taarifa zinazosambaa mitandaoni zinazodai kuwa nguli wa vichekesho katika tasnia ya uigizaji , Amri Athuman maarufu kama King Majuto amefariki dunia. Mboto baada ya kupata taarifa hizi alifunga safari kuelekea mkoani Tanga ambapo ni nyumbani kwa Mzee Majuto na kumkuta hai, na amekanusha uvumi huo kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kuposti picha inayowaonyesha yeye na Majuto wakiwa nyumbani kwake, na picha hiyo iliambatana na maneno yafuatayo: “ Baada ya kupata taarifa mbaya kuhusu Mzee Majuto nimelazimika kuja kwake Tanga . Ni kweli anaumwa ila anaendelea vizuri na si kama watu walivyozusha kuwa mzee hatunaye. Kwa sasa mzee ni mzima nipo naye Tanga ,” ameandika Mboto . Siku chache zilizopita, gazeti la Ijumaa Wikienda liliripoti taarifa za kuumwa kwa Mzee Majuto , anayesumbuliwa na tatizo la ngiri, lakini jana kwenye mitandao ya kijamii zikaenea taarifa zisizo za kweli kwamba King Majuto amefariki

FAHAMU MADHARA YA KUTOBOA PUA, MDOMO NA ULIMI!

Image
Katika zama hizi za utandawazi na muingiliano baina ya tamaduni zetu za asili na tamaduni za kimagharibi, imekuwa ni kawaida kwa vijana wa rika tofauti na jinsia zote kutoga ulimi, mdomo, kitovu ama kivimbe cha nyusi kwa sababu tofauti tofauti sana. Hivyo basi, ni muhimu sana kufahama ukweli kuhusu faida ama hasara za kutoga ulimi ama mdomo kabla hujatekeleza azma yako ya kutoga viungo hivi vya mwili. Kutoga Ulimi ama Mdomo kunaweza kukusababishia madhara yasiyotarajiwa.  Matokeo mazuri zaidi ya kutoga ulimi ama mdomo ni kutokutokea kwa kidonda ama kivimbe, wakati matokeo mabaya kutokea kwa baadhi ya watu ni pamoja na kuvunjika kwa meno/jino, kuvuja kiasi kikubwa cha damu, ama maambukuzi ya bakteria kwenye kidonda. Kutoga ulimi hujumuisha kutumika kwa sindano inayopenyezwa katikati ulimi ili kupitisha na kuhifadhi kipini, ama ndoana ama hereni ya urembo. Kazi hii ya kutoga ulimi mara nyingi ganzi huwa haitumiki. Baada ya kutoga, kuvimba kwa ulimi na maumivu ya m

RAIS DKT MAGUFULI AMFAGILIA KAFULILA NYUMBANI KWAO

Image
Mh.David Kafulila Na Editha Karlo- Globu ya Jamii Kigoma RAIS Wa Jamuhuri wa Muungano Wa Tanzania Dkt John Magufuli amempongeza aliekuwa Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kusini ,David Kafulila kwa kujitoa Muhanga kutetea Watanzania kupitia sakata la Escrow(IPTL) na kuonesha uzalendo Mkubwa ambao hawezi kusahaulika katika historia ya Tanzania.Akizungumza na Wananchi wa Kata ya Nguruka,leo Katika uzinduzi wa Mradi mkubwa wa Maji uliopo Tarafa ya Nguruka katika Wilayani Uvinza, alisema atakuwa mnafiki akishindwa kumpongeza Kafulila kwa kazi kubwa aliyoifanya ya kuibua Ubadhilifu uliofanywa na Kampuni ya IPTL ambapo kwasasa suala hilo ameanza kulifanyia kazi na mafanikio yameanza kuonekana. Amesema Kafulila alitukanwa sana alipo ibua sakata la Escrow na kuitwa majina mengi ya kudhalilishwa kama tumbili na mengine mengi ya ajabu kwasababu ya uzalendo wake wa kutetea Taifa. "Mimi ninafahamu unapoibua kitu cha kizalendo lazima usemwe, hivyo ninampongeza Kafulil