Posts

Hatimaye Mtatiro ‘Amchana’ Prof. Lipumba, Amuita ni Jemedari Aliyekimbia Vita

Image
Dar es Salaam: Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya CUF, Julius Mtatiro amesema aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba amekiacha chama kwenye wakati mgumu baada ya kujiuzulu wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 2015. Agosti, mwaka jana, Profesa Lipumba alitangaza kujiuzulu nafasi hiyo na kukabidhi barua kwa uongozi baada ya kushauriana kwa kipindi kirefu na viongozi na wazee wa chama hicho, akisema nafsi yake inamsuta kwa kuwa walikiuka malengo ya Ukawa. Hata hivyo, hivi karibuni Profesa Lipumba aliandika barua ya kutengua uamuzi wa kujiuzulu na uchaguzi ulipoitishwa ili kujaza nafasi hiyo hakuchukua fomu ya kugombea. Akizungumza katika mahojiano maalumu, Mtatiro amesema Profesa Lipumba amekitelekeza chama kikiwa katikati ya uwanja wa mapambano. Mtatiro aliyeteuliwa hivi karibuni na Baraza Kuu la CUF kuongoza kamati ya uongozi wa chama hicho baada ya kuvunjika kwa mkutano mkuu ulioitishwa kuziba nafasi ya mwenyekiti, amesema walijaribu kila mbin

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI TAREHE 08.09.2016

Image
Posted by  PHARS MSIRIKALE at Thursday, September 08, 2016

MAGAZETI YA MICHEZO NA BURUDANI TAREHE 08/09/2016

Image

Wazee Wahofia Chadema Kuhujumiwa

Image
BARAZA la Wazee la Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) limesema lina hofu ya kuhujumiwa chama chao kupitia kwa ofisi ya msajili wa vyama vya siasa nchini kwa kuundiwa njama za kukifuta chama hicho kwenye orodha ya vyama vya siasa. Akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu Baraza la Wazee Taifa wa Chadema, Roderick Lutembeka, amesema pamoja na juhudi kubwa wanazozifanya kutatua mgogoro wa kisiasa, wamepata taarifa za kuwepo kwa njama hizo zinazopikwa dhidi ya Chadema kupitia baraza la vyama vya siasa. “Ni vyema msajili wa vyama vya siasa akawa wazi kwa Watanzania kwani Baraza la Vyama vya Siasa lililo chini yake limekuwa likiaandaa na kuahirisha vikao vya kukutana na vyama vyote vya siasa pasipo kututaarifu. “Mfano Agosti 29-30, ilikuwa baraza likae lakini likaahirisha hadi Septemba 3-4 napo pia wakaahirisha tena bila sisi kupewa taarifa yoyote,” alisema Lutembeka. Katibu Mkuu Baraza la Wazee la Chadema, Roderick Lutembeka akizu

Salum Mwalimu na Wafuasi 18 wa Chadema Waachiliwa kwa Dhamana

Image
Mahakama ya Hakimu Mkazi Simiyu imewaachia kwa dhamana Naibu Katibu Mkuu wa Chadema (Zanzibar), Salum Mwalimu na wafuasi wengine 18 wa chama hicho baada ya kukaa mahabusu kwa zaidi ya siku 12. Kiongozi huyo wa Chadema na wafuasi hao 18 walikuwa wakishikiliwa katika mahabusu za jeshi la polisi kwa tuhuma za kuandaa na kuhamasisha maandamano na mikutano ya Oparesheni ya chama hicho iliyopewa jina la UKUTA, ambayo ilipigwa marufuku na jeshi hilo. Walifanikiwa kupata dhamana baada ya Hakimu wa Mahakama hiyo kueleza kuwa ameridhia hoja za upande wa utetezi baada ya kusikiliza pande zote mbili na kubaini mapungufu kwenye maombi ya upande wa mashtaka. Awali, Mwendesha mashtaka aliitaka Mahakama hiyo kuwanyima dhamana washtakiwa hao kwa madai kuwa endapo wataachiwa wataendelea kufanya kosa hilo. Hata hivyo, Hakimu alitupilia mbali maombi hayo akieleza kuwa wameshindwa kuthibitisha pasipo shaka kuwa endapo washtakiwa hao wataachiwa watafanya tena kosa hilo. Pia

UHURU KENYATTA AKANUSHA KUWEPO MVUTANO WA KIUCHUMI KATI YA TANZANIA NA KENYA

Image
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya Jumamosi alikanusha ripoti za vyombo vya habari kwamba kuna mvutano baina ya Kenya na Tanzania. Akizungumza mjini Mombasa wakati wa ufunguzi gati la makontena katika bandari ya Mombasa, Kenyatta alipuuzia maneno kwamba kuna mvutano wowote na badala yake akasema kuwa nchi hizo zinasaidiana. Alisema anaona kwenye vyombo vya habari kwamba kuna “mgogoro baina yetu, lakini nataka kusema wazi wazi kwamba Kenya na Tanzania hazina mgogoro wowote baina yao,” alisema.Kenyatta alisema uchumi wa nchi hizo mbili umefungana kwa miaka mingi na ni kwa ajili ya faida ya watu wa nchi hizo mbili. Alitaja kufunguliwa kwa njia inayojulikana kama “northern frontier” ambayo itaunganisha bandari ya Mombasa kupitia mkoa wa Kilimanjaro, Tanzania, hadi Bujumbura, Burundi – njia ambayo itafupisha urefu wa kutoka Bujumbura hadi Mombasa kwa kilomita 300 nzima. “Afrika Mashariki haiko katika mashindano ya wenyewe kwa wenyewe,” alisema Kenyatta. “Afrika M

MAGAZETI YA LEO JUMATATU TAREHE 05.09.2016

Image

Polisi Wafyatua Risasi & Mabomu ya Machozi Kuwatawanya Wafuasi wa Lipumba

Image
  Jeshi la Polisi limelazimika kufyatua risasi angani na kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wanachama wa Chama cha Wananchi (CUF) wanaodhaniwa kuwa ni wafuasi wa aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho Prof. Lipumba waliokuwa wakimzuia mwenyekiti wa muda wa CUF, Julius Mtatiro, kuingia ofisini eneo la Buguruni. Wafuasi hao wameeleza kuwa wameamua kumzuia kwani Msajili wa Vyama vya Siasa ametaka shughuli zozote ndani ya CUF zisiendelee hadi hapo mgogoro wa uongozi utakapotatuliwa. Itakumbukwa hivi karibuni CUF kilimteua Julius Sunday Mtatiro kuwa mwenyekiti wa muda baada ya mwenyekiti aliyekuwepo, Prof. Lipumba kijiuzulu Agosti 2015. Julius Mtatiro leo amefanya mkutano na waandishi wa habari  katika ofisi za Makao Makuu ya CUF, Buguruni, Dar es Salaam ili kuzungumzia kauli zilizotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli akiwa visiwani Zanzibar.

WAZIRI MAHIGA AONGOZA TIMU YA WAANGALIZI WA UCHAGUZI YA SADC UCHAGUZI WA JAMHURI YA SHELISHELI

Image
 Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustino Mahiga akifungua Misheni ya timu ya Uangalizi wa Uchaguzi wa Wabunge tarehe 2 Septemba, 2016, Mahe Seychelles. Mhe Waziri anamuawakilisha Mhe. Rais John pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye ni Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC. Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika picha ya pamoja na  Misheni ya timu ya Uangalizi wa Uchaguzi wa Wabunge tarehe 2 Septemba, 2016 huko Mahe, Seychelles. Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Augustine P. Mahiga (Mb.), jana tarehe 2 Septemba, amezindua Misheni ya Waangalizi wa Uchaguzi wa SADC kwenye uchaguzi wa Jamhuri ya Shelisheli kwa niaba ya Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika -SADC Organ.  Misheni hiyo ya wa

UJUMBE WA VANESSA MDEE KWA JUX WA WAKUNA WENGI

Image
Staa wa Bongo Fleva, Vanessa Mdee ‘Vee Money’ ametumia fursa ya siku ya kuzaliwa ya mpenzi wake, ambaye pia ni Staa wa muziki wa R&B hapa Bongo, Juma Jux kumwandikia ujumbe muhimu kudhihirisha ni kwa kiasi gani anampenda huku akiutaja wimbo wao wa pamoja, #Wivu kuwa ndiyo nguzo ya kukutana na kuanzisha uhusiano wao: Kuoitia ukurasa wake Instagram, Vee Money ameandika; When we first met I was an upcoming songstress with a fast tongue and one hit song on the radio. You … well you were pretty much the same. Your boy asked me if I would spit some bars on your song. I said no. Then walked into the studio and met you and instantly had a change of heart. Fast forward to 2yrs later, tumekuwa. You’ve got the biggest song in the country #Wivu and a multi million dollar brand #AfricanBoy and as for me well … kitu kimoja hakijabadilika though. Kwako sisikii. Lol! Lakini hayo yoteee ni mifano tu ya jinsi gani ukiwa na mahusiano na mtu anayekujenga kifikra na vinginevyo