Posts

Baada ya Sintofahamu… Zitto Kabwe ajitokeza

Image
                   Kiongozi Mkuu wa ACT Zitto Kabwe amejitokeza leo kwenye ofisi za makao makuu ya chama hicho, Kijitonyama jijini Dar es Salaam baada ya taarifa kutolewa jana na chama chake kuwa hawajui alipo tangu juzi Jumamosi juni 11. Akizungumza na wanahabari leo baada ya kujitokeza, Mh. Zitto Kabwe amesema kuwa hatishiki na vitisho vinavyotolewa na Jeshi la Polisi nakwamba amekusudia kufanya kongamano la kujadili bajeti kesho Makao Makuu ya Chama hicho huku akiitaka jeshi la Polisi kuacha kumvizia na badala yake limkamate kwa kufuata Sheria. Hii hapa ni taarifa iliyolewa jana Jumapili na uongozi wa Chama Cha ACT wazalendo kuhusu kupotea kwa Kiongozi wao Zitto Kabwe. TAARIFA KWA UMMA Tunaujulisha UMMA kwamba Kiongozi wa Chama chetu cha ACT Wazalendo ndg. Zitto Kabwe amekuwa anatafutwa na Polisi tangu jana usiku. Mpaka sasa hatujui Kiongozi wetu yupo wapi na yupo kwenye Hali gani. Askari kanzu wanalinda nyumbani kwake na kwa watu wake wa karibu.  Sisi kama cha

JPM Awaapisha Mwigulu Nchemba na Tizeba

Image
Rais Magufuli akimuapisha Mh. Mwigulu Nchemba kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Leo Ikulu Jijini Dar es Salaam. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli akimkabidhi hati ya kiapo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mh. Mwigulu Nchemba mara baada ya kumuapisha Leo Ikulu Jijini Dar es Salaam. Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Dkt. Charles Tizeba akila kiapo mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli Leo Ikulu Jijini Dar es Salaam. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli akisaini hati ya kiapo mara baada ya kumuapisha Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Dkt. Charles Tizeba Leo Ikulu Jijini Dar es Salaam. Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Dkt. Charles Tizeba na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mh. Mwigulu Nchemba wakipongezana mara baada ya kuapishwa Leo Ikulu Jijini Dar es Salaam. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli akimpongeza Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mh. Mwigulu Nchemba mara

Trich; hushambulia sehemu nyeti za mwanamke

Image
Ugonjwa wa Trich ni ugonjwa unaosababishwa na vimelea vya jamii ya Protozoan na huathiri mrija wa kupitisha mkojo unaojulikana kama Urethra na tupu ya mwanamke Vagina . Ugonjwa huu huweza kuwapata wanaume lakini huwapata na kuonekana zaidi kwa wanawake na daktari anaweza kumuambia mgonjwa anayeugua maradhi haya kuwa ana Trichomonas Vaginalis. UNAAMBUKIZWAJE? Mwanamke au hata mwanaume anaweza kukumbwa na ugonjwa huu akifanya tendo la ndoa na mtu mwenye maambukizi bila kutumia kinga. Kwa kawaida vimelea vya Trichomonas Vaginalis ni vidogo mno ni sawa na chembechembe moja ya damu nyeupe kwa upana (10 μm) ingawa wakati mwingine ukubwa waweza kutofautiana kulingana na mazingira.Wengine huuita ugonjwa huu Trichomoniasis. Watu walio na ugonjwa wa Trich wana hatari ya kupata ugonjwa wa Ukimwi (HIV) au magonjwa mengine ya zinaa kwa sababu bakteria hawa huharibu seli aina ya Epithelium na kusababisha vidonda Microulcerations katika tishu zilizo ndani ya utupu wa mwakamke. DALILI K

Staa wako ni Wema, Shilole, Kajala, Rose Ndauka au Wolper?

Image
<a href='http://kwanza.co.tz/login/www/delivery/ck.php?n=a397efbc&cb=INSERT_RANDOM_NUMBER_HERE' target='_blank'><img src='http://kwanza.co.tz/login/www/delivery/avw.php?zoneid=31&cb=INSERT_RANDOM_NUMBER_HERE&n=a397efbc' border='0' alt='' /&g 58

Aliyedai ‘wakala’ wa Freemason ala kichapo!

Image
     Bahati Anthony akichezea kichapo. Stori: DUSTAN SHEKIDELE, WIKIENDA, MOROGORO Fundi nguo maarufu mjini hapa, Bahati Anthony aliyedai ni ‘wakala’ wa jamii ya siri inayohusishwa na utajiri wa ghafla na imani za kishetani ya Freemason, amenusa kifo baada ya kunaswa kwa utapeli kwa wakala wa mitandao yasimu inayotoa huduma ya kuweka na kutoa fedha. Akiokolewa na polisi Tukio hilo lilijiri mwishoni mwa wiki iliyopita maeneo ya Masika katikati ya Mji wa Morogoro kwenye duka la wakala aitwaye Gelasi Assenga ambapo jamaa huyo alijikuta akiloa damu chapachapa. Akisimulia tukio hilo, Assenga alikuwa na haya ya kusema: “Jana huyu jamaa alikuja hapa akatuma shilingi 15, leo amekuja ameniambia nitume laki tatu kwenye namba ileile aliyonipa jana. “Baada ya kutuma, nimemwambia anipe hiyo laki tatu anadai yeye ni wakala wa Freemason hivyo baada ya dakika 10, begi alilobeba litajaa fedha na atanilipa. Nimesubiri dakika 10 zimepita. “Nimemwambia anipe fedha zangu, anasema haijaingia,

Mbunge: Simu za watu mil.6 kwenda na maji!

Image
Stori: GABRIEL NG’OSHA, WIKIENDA DAR ES SALAAM: Zikiwa zimebaki siku tatu sawa na saa 72 kabla ya kufungiwa kwa simu feki nchini Tanzania, Alhamisi wiki hii na Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA -Tanzania Communication Regulation Authority), inakadiriwa simu za watu zaidi ya milioni 6 zitakwenda na maji. Imeelezwa kuwa unapozungumzia watu zaidi ya milioni sita maana yake yake ni zaidi ya simu feki milioni sita kwani kuna wengine wana simu zaidi ya moja. Kufuatia hali hiyo, Wikienda lilizungumza na watu mbalimbali akiwemo Mbuge wa Mtera (CCM) mkoani Dodoma, Livingstone Lusinde ambaye alisema serikali imefanya makosa kama ilitaka udhibiti wa vitu feki basi ingedhibiti kwenye uingiaji na siyo kujitwisha mzigo kwa dhambi ya kuwasababishia Watanzania kutumia vitu feki. “Kiukweli serikali ilichofanya ilifikiri ni kama kuhamisha mfumo wa mawasiliano wa analojia kwenda digitali lakini imekosea sana, imejitwisha mzigo mkubwa wa dhambi, kwanza serikali itapoteza mapato lakini hata hi

Nafasi za kazi United States African Development Foundation

Image
Job Vacancy >  Program Driver Location >  Dar Es Salaam  Position Type >  Full Time Organization Type >  NGO Website > http://www.usadf.gov Application Deadline: 23 Jun 2016 PROGRAM DRIVER POSITION DESCRIPTION: Position Description Document (download) APPLICATION INSTRUCTIONS: Applications should be e-mailed thru  APPLY NOW  with the subject line "TFSAADF16CI0008 Tanzania Program Driver, attention JMCCLEAD/TAYERS" and received before 11.59pm EST on June 23 rd 2016 AVOID SCAMS: NEVER PAY TO HAVE YOUR CV / APPLICATION PUSHED FORWARD. ANY JOB VACANCY REQUESTING PAYMENT FOR ANY REASON IS A SCAM. IF YOU ARE REQUESTED TO MAKE A PAYMENT FOR ANY REASON, PLEASE USE THE  REPORT ABUSE , OR CALL +255 768 982 800 TO REPORT THE SCAM. IF YOU ARE QUALIFIED FOR THIS POSITION  Apply Now  report abuse or errors AddThis Sharing Buttons

Mbowe na Wenzake wa Chadema Wakamatwa, Alipo Zitto Bado ni Utata

Image
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe Wakati Polisi ikimshikilia kwa saa mbili Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe mkoani Mwanza, jeshi hilo limefuta kongamano la kujadili Bajeti ya Serikali lililoandaliwa na ACT Wazalendo jijini Dar es Salaam huku kiongozi wake, Zitto Kabwe akisakwa. Jeshi hilo lilizuia mkutano wa hadhara wa Chadema uliokuwa ufanyike wiki iliyopita mjini Kahama ambako lilitumia mabomu ya machozi kuwatawanya wanachama na wafuasi wa chama hicho, katika kile kilichoelezwa kulikuwa na dalili za uvunjifu wa amani. Jeshi hilo pia lilizuia msafara wa viongozi wa chama hicho kuingia katika ofisi zake za Shinyanga walipokuwa wakielekea Mwanza. Taarifa iliyotolewa jana na msemaji wa chama hicho, Tumaini Makene ilieleza kuwa mbali na Mbowe, jeshi hilo pia lilikuwa linawashikilia Mwenyekiti wa Baraza la Vijana wa Chadema (Bavicha), Patrobas Katambi na Katibu Mkuu wa Bavicha, Julius Mwita. Wengine ni Mbunge wa Tunduma, Frank Mwakajoka na viongozi wengine na w

BREAKING NEWS : GOODLUCK OLE MEDEYE AIKIMBIA CHADEMA,AHAMIA UDP

Image
​ Kada wa CHADEMA na mbunge wa zamani wa Arumeru Magharibi, Goodluck Ole Medeye leo ametangaza kuhamia UDP. Asema inasimamia haki na demokrasia. Anasema anataka demokrasia ya kweli na jukwaa la haki ktk kuleta haki na maendeleo kwa Watanzania. Ameyasema haya akiongea na waandishi wa habari muda mfupi uliopita.

Utafiti umeonesha wanaume wenye vipara ni wanaume wenye mvuto zaidi kimapenzi!

Image
Kuna vitu vingi humvutia mtu inapokuja swala la kumchagua mpenzi, siwezi taja sifa zote, kila mtu anasifa zake na vigezo vyake, ila ngoja tuongelee mvuto wa kipekee unaopatikana kwa wanaume wenye vipara. Nikiongelea vipara naongelea wale walio na vipara asili, achilia mbali wale wanaopenda kunyoa vipara japokuwa kuna baadhi ya sifa hapa wanaweza wakawa nazo pia. Muonekano wa kiume: wanaume wenye vipara wengi huwa na muonekana wa kiume zaidi,muonekano nadhifu  sina maana kama wanaume wengine walio na nywele ndefu ama wastani hawana mvuto lah, nauongelea mvuto zaidi ama mvuto wa kipekee. Ujasiri: wanaume wa aina hii wengi huonekana ni wajasiri kwa muonekano wao tu, hii huwafanya kuwa kivutio kwa wanawake. Wana hisia kali za kimapenzi: daktari kutoka Chuo cha Yale Marekani , James B. Hamilton alisema katika utafiti wake wanaume wengi walio na vipara miili yao huwa inazalisha mbegu nyingi za kiume kuliko wanaume wenye nywele, japokuwa si kwa asilimia 100 alisema pi

SERIKALI YATANGAZA UTARATIBU MPYA MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA, PIA YAFAFANUA FEDHA ZILIZOOKOLEWA KUTOKANA NA WATUMISHI HEWA

Image
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Mhe. Angellah Kairuki akiongea na waandishi wa Habari kuhusu Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2016.   Na. Aron Msigwa – Dar es salaam. SERIKALI imetangaza utaratibu mpya utakaofuatwa wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kuanzia Juni 16 hadi 23, 2016 ambapo imewaagiza Watendaji Wakuu katika Wizara, Idara zinazojitegemea, Wakala na Taasisi za Serikali kutenga siku moja ya kukutana na watumishi katika sehemu zao za kazi kwa lengo la kusikiliza kero mbalimbali zinazowakabili na kuzitafutia ufumbuzi. Aidha, imewaagiza watendaji hao kutenga siku nyingine moja kwa ajili ya kukutana na wananchi, kusikiliza na kuzitafutia ufumbuzi kero zao zinazohusiana na huduma zinazotolewa na Taasisi zao. Akitangaza utaratibu huo leo jijini Dar es salaam Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Mhe. Angellah Kairuki amesema kuwa Serikali imeamua kubadili mfumo wa maadhimisho h

WAZIRI MKUU, MAJALIWA AONGOZA MATEMBEZI YA WAFANYAKAZI WA BENKI KUU.

Image
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisalimiana na wasanii wa Benki Kuu baada ya kuongoza matembezi  kuchangia madawati ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 ya Benki kuu ya Tanzania. Matembezi hayo yalianzia Benki Kuu hadi viwanaj vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam Juni 11, 2016.  Zaidi ya shilingi milioni263 zilichangwa. Bendi ya Poli ikiongoza matembezi  ya kuchangia madawati ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 ya Benki kuu ya Tanzania. Matembezi hayo yalianzia Benki Kuu hadi viwanaj vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam Juni 11, 2016.Zaidi ya shilingi263 milioni zilichangwa.    Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiongoza matembezi ya kuchangia madawati ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 ya Benki kuu ya Tanzania. Matembezi hayo yalianzia Benki Kuu ha viwanaj vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam Juni 11, 2016.Kushoto kwake ni Gavana wa Benki Kuu, Benno Ndulu na kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda. Zaidi ya shilingi milio

RAIS MAGUFULI AFANYA MABADILIKO MADOGO KATIKA BARAZA LA MAWAZIRI

Image
Aliyekuwa Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba ameteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi.   Mbunge wa Buchosha Dkt. Charles John Tizeba ameteuliwa kuwa Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi.  

Wawili wawachinja wake zao, mwingine amuua mama yake!

Image
Matukio ya Dodoma Samson Joramu(44), mkazi wa Chololo, Kata ya Kikombo, alimchinja mke wake, Rehema Joram (43) kabla ya kujiua kwa kunyonga katika shamba lake. Watu walioshuhudia walisema, Joramu baada ya kumuua mkewe alijinyonga na aliandika ujumbe uliokutwa mfukoni kwake, ukisomeka: “Mama tunza wanangu, mimi nimekufa.” Kadhalika aliandika orodha ya watu anaowadai. Katika tukio jingine, Amos Kalenda, mkazi wa Kikombo, Dodoma anadaiwa kumuua mama yake mzazi, Joyce Kalenda kwa kumchinja. Chanzo cha mauaji hayo kinadaiwa ni mama huyo kumnyima chakula. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa akizungumzia tukio hilo alisema kuwa: “Ni kweli taarifa za vifo kutoka Kikombo ninazo, yule mmoja alimuua mama yake kwa kumkatakata sehemu mbalimbali za mwili jana (juzi), na huyu mwingine alimuua mke wake asubuhi ya leo (jana) kisha naye akajinyonga,” alisema. Tukio la Tarime Mkoani Mara katika Wilaya ya Tarime, Wambura Mariba (50) mkazi wa Matongo, Nyamongo, T

ANGALIA PICHA ZA SHEREHE UFUNGUZI WA MICHUANO YA EURO 2016

Image
Michuano ya UEFA Euro 2016 ilianza rasmi kufanyika Ufaransa usiku wa June 10 2016 kwa kupigwa mchezo kati ya Ufaransa dhidi ya Romania, kabla ya kuanza kwa mchezo huo kulifanyika sherehe mbalimbali za kuashiria usiznduzi wa michuano hiyo. Wakati wa uzinduzi wa michuano hiyo kulikuwa na burudani mbalimbali ikiwemo perfomance za muimbani Zara Larsson na David Guetta walikuwepo pia kuburudisha watu katika michuano hiyo kwa mwaka 2016.