Aliyedai ‘wakala’ wa Freemason ala kichapo!

FREE MASON (3)     Bahati Anthony akichezea kichapo.
Stori: DUSTAN SHEKIDELE, WIKIENDA, MOROGORO
Fundi nguo maarufu mjini hapa, Bahati Anthony aliyedai ni ‘wakala’ wa jamii ya siri inayohusishwa na utajiri wa ghafla na imani za kishetani ya Freemason, amenusa kifo baada ya kunaswa kwa utapeli kwa wakala wa mitandao yasimu inayotoa huduma ya kuweka na kutoa fedha.
FREE MASON (4)Akiokolewa na polisi
Tukio hilo lilijiri mwishoni mwa wiki iliyopita maeneo ya Masika katikati ya Mji wa Morogoro kwenye duka la wakala aitwaye Gelasi Assenga ambapo jamaa huyo alijikuta akiloa damu chapachapa.
Akisimulia tukio hilo, Assenga alikuwa na haya ya kusema: “Jana huyu jamaa alikuja hapa akatuma shilingi 15, leo amekuja ameniambia nitume laki tatu kwenye namba ileile aliyonipa jana.
FREE MASON (5)“Baada ya kutuma, nimemwambia anipe hiyo laki tatu anadai yeye ni wakala wa Freemason hivyo baada ya dakika 10, begi alilobeba litajaa fedha na atanilipa. Nimesubiri dakika 10 zimepita.
“Nimemwambia anipe fedha zangu, anasema haijaingia, nikaamua kumpekua kwenye begi nikakuta mshumaa.”
“Wakati napekuwa ndipo akaanza kukimbia. Nilipoona nitapoteza fedha zangu, nikaona nimwitie mwizi ndipo watu wakamkamata na kumshushia kichapo.
FREE MASON (6)“Nilipoona wanataka kumuua, nilikodi bodaboda na kumpeleka polisi ambako baada Inaendelea Uk.4 Kutoka Moro ya kuhojiwa alisema yeye siyo mwizi bali alielekezwa kufanya hivyo na kiongozi wa Freemason.
“Hata hivyo, polisi walimwamuru kurudisha fedha zangu ambapo aliwapigia simu ndugu zake kutoka Kigoma ambao walidai kuwa watanitumia fedha yangu ndipo aachiwe huru.”
FREE MASON (7)Kwa upande wake, jamaa huyo aliyepokea kichapo alikuwa na haya ya kusema: “Nilisoma mabango ya Freemason yaliyozagaa mitaani yakihamasisha watu kujiunga, nilichukua namba za simu na kuwapigia ambapo waliniambia ili niwe tajiri natakiwa niwatumie shilingi elfu 15, nikatuma.
FREE MASON (8)Akipelkwa kituoni.
“Baadaye waliniambia ninunue begi jipya ndani yake niweke mshumaa na udi kisha niende palepale kwa wakala wa jana yake niwatumie shilingi laki tatu. “Niliwaambia fedha hiyo sina, wakaniambia nimwambie wakala anitumie tu baada ya dakika 10 begi langu litajaa fedha lakini haikuwa hivyo ndiyo maana  ssenga akaniitia mwizi nikapigwa.”
Kumekuwa na utapeli wa aina hiyo mkoani hapa hivyo Wikienda linawataka wasomaji wake kuwa macho ili wasilizwe.

Comments

Popular posts from this blog