HUU NDIO MUONEKANO WA MFANYABIASHARA YUSUPH MANJI LEO MAHAKAMANI

 
 August 4,2017 Upande wa serikali umewasilisha pingamizi la awali Mahakama Kuu ya Tanzania kupinga maombi ya dhamana ya mfanyabiashara Yusuf Manji. Pingamizi hilo limewasilishwa leo na wakili wa serikali, Paul Kadushi mbele ya Naibu Msajili, Sian Mustafa kutokana na Jaji Isaya Arufan anayesikiliza maombi hayo kutokuwepo.

Katika pingamizi hilo, wakili Kadushi amedai kuwa Mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza maombi ya dhamana ya Manji. Pia kiapo kilichowasilisha cha kuhusu dhamana kinadosari kisheria, pamoja na kuwepo kwa vifungu visivyo sahihi. Baada ya kuwasilisha pingamizi hilo, Msajili Mustafa ameahirisha kesi hiyo hadi August 7/2017 kwa ajili ya kusikilizwa.
millardayo.com imezinasa picha hizi ambazo zinamuonesha Mfanyabiashara Yusuph Manji akiwa amefuga ndevu ikiwa ni tofauti na ambavyo amekuwa akionekana.
         

Comments

Popular posts from this blog