BREAKING: “Hans Pope amefuta uamuzi wa kujiuzulu uongozi Simba” – Haji Manara


Baada ya kuripotiwa taarifa za kujiuzulu kwa Hans Pope Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili wa Simba, leo Jumatatu May 15, 2017 ripoti mpya kutoka kwa Afisa Habari wa club hiyo Haji Manara kutoka kwenye Instagram yake ameandika kuwa kiongozi huyo amefuta uamuzi wake.
Kupitia Instagram Haji Manara ameandika >>> Rasmi Hanspope arejea kundini, afuta uamuzi wake wa kujiuzulu, na ndio maana fans wetu nawaomba mtulie, hakuna kitakachoharibika, ni upepo mbaya ulipita na sasa umetulia, Karibu tena kamanda Pope<<< –Manara

Comments

Popular posts from this blog