Balaa Jipya Makalio ya Kichina

mchina1
Stori: Hamida Hassan na Boniface Ngumije
Dar es Salaam: Tabia ya baadhi ya wasichana hasa wa mjini kuwa na tamaa ya kuwa na makalio makubwa na hivyo kulazimika kutumia dawa mbalimbali, imekuwa ikishamiri kila siku licha ya serikali kupiga marufuku uingizwaji wa dawa hizo.
jayjay 
Jayjay
Gazeti hili matoleo yaliyopita liliwahi kuandika jinsi mastaa wengi Bongo wanavyotumia dawa hizo lakini uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa, kasi ya matumizi ya dawa hizo yamekuwa yakishamiri huku waathirika wengi wakijiuguza kwa siri baada ya kupata madhara.
gillaGilla.
Katika tukio jipya la hivi karibuni, mwanamke mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Hamisa ambaye alidai ni mke wa mtu alisema kuwa, alishawishiwa na rafiki yake kutumia dawa hizo ili naye awe na ‘zigo’ lakini ameanza kuona zinamletea matatizo.
“Nimekuwa nikisikia kuwa dawa hizi zina madhara lakini kuna rafiki yangu mmoja ambaye aliwahi kutumia na yuko poa ndiye aliyenipeleka kwenye duka moja lililopo Kijitonyama na kununua. Awali sikuona tatizo lakini kadiri siku zinavyokwenda nahisi maumivu f’lani, najuta kuzitumia dawa hizi kwa kweli,” alisema mwanamke huyo. 
kidoaKidoa.
OFM mtaani
Baada ya kupata malalamiko hayo, waandishi wetu walifanya uchunguzi na kubaini kuwa dawa hizo zinauzwa kwa siri sana tangu serikali icharuke na kutoa tamko la kuwashughulikia wale wanaoziuza.
Katika uchunguzi huo, yamegundulika maduka kibao mitaa ya Kariakoo, Kinondoni na Mwenge jijini Dar ambapo wauzaji huziuza dawa hizo ‘kimagutu’ kana kwamba wanauza madawa ya kulevya au bangi.
Mwandishi wetu alifika kwenye duka moja lililopo Msimbazi baada ya kulengeshwa kuwa dawa hizo zinauzwa hapo, muuzaji alipoulizwa uwepo wa dawa hizo, kwanza alikataa lakini baadaye alikubali huku akionekana ni mwenye wasiwasi.
DSC00858Afisa Habari wa Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania, Gaudensia Simwanza.
Dukani kwa Maimartha
Ilidaiwa kuwa, asilimia kubwa ya mastaa wanaotumia dawa hizo wanazinunua kwenye duka la Mtangazaji wa Azam TV, Maimartha Jesse na ili kujiridhisha OFM walitinga kwake na kumkuta dada ambaye jina lake halikufahamika ambaye alisema dawa hizo hawana dukani hapo ila mwandishi akitaka anaweza kutafutiwa.
Baada ya mwandishi kujifanya anazihitaji kwa udi na uvumba, mdada huyo alimpigia simu mtu ambaye haikujulikana ni nani na ndani ya muda mfupi akawa amezileta dawa hizo ambazo zipo kwenye mfumo wa losheni.
Alipopigiwa simu Maimartha na kabanwa juu ya kudaiwa kuwaharibu wanawake wenzake kwa kuwauzia dawa hizo, aliruka kimanga na kusema:
“Mimi  sitaki kuzungumzia kuwa nauza au siuzi kwa sababu naiheshimu sana serikali na nafuata maelekezo wanayotoa, lakini ninavyojua dawa hizo zinauzwa kwa siri sana na wanaotaka kuuziwa ni wengi.”
Aidha, wasanii wengi hawa wa kike wamekuwa wakidaiwa kutumia dawa hizo huku mastaa wa kizazi cha sasa kama vile Gift Stanford Gigy, Glasnost Kalinga ‘Gilla’, Asha Salumu ‘Kidoa’, Janet Jackson ‘Jayjay’ na wengine wakidaiwa kuwa maumbile waliyonayo siyo ‘orijino’.
Ijumaa lilipata fursa ya kuzungumza na wadada hao ambao sasa ni habari ya mjini kutokana na maumbo yao ambapo kila mmoja alifunguka kivyake:
Gigy: Kusema ukweli sijawahi kutumia dawa hizo, nazisikia tu. Umbo langu ni orijino na wala hayo masponji zivai, hata nikivua sasa.
Kidoa: Shepu yangu ni ya kuzaliwa nayo, najua dawa za Kichina ni shida hivyo siwezi kuthubutu kuzitumia.
Gilla: Mh! Wapo wanaoniambia natumia dawa hizo, kiukweli nimezaliwa hivyo na hivi sasa nimepungua hapo mwanzo si ndo mgenishangaa.
 TFDA wanasemaje?
Baada ya OFM kufanya uchunguzi wake, waandishi wetu walizungumza na Afisa Habari wa Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania, Gaudensia Simwanza ambaye alisema wanapambana kuhakikisha dawa hizo haziingii nchini na atakayekamatwa cha moto atakiona.
“Lakini kwa kuongeza tu ni kwamba kuhusu watumiaji wanaopata madhara kwa matumizi ya dawa hizo wengi unakuta hatuna taarifa nao kwa sababu huwa hawaji kwetu moja kwa moja, wanakwenda mahospitali na sehemu nyingine kupata tiba, ila tunapopata taarifa kama hizi tunafuatilia na kuzitendea kazi,” alisema Simwanza.
Aidha, dokta mmoja anayefanya kazi katika wizara ya afya ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini alisema kuwa, sasa hivi wako makini kuhakikisha uuzwaji holela wa dawa zenye madhara kwa watumiaji unakoma.
“Unajua hiki siyo kipindi cha mchezo, TFDA wanafanya kazi yao lakini wizara ya afya nayo inapambana, kikubwa ni tahadhari kwa watumiaji wa dawa hizo, wajue kwamba kuna madhara makubwa ambayo yanaweza kuhatarisha maisha yao hivyo waache,” alisema dokta huyo.

Comments

Popular posts from this blog