Posts

DR.SLAA: SIKUWAHI KUSEMA NIMEACHA SIASA.

Image
Katibu mkuu wa zamani chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) na balozi mteuli awamu ya tano, Dr. Wilbroad Slaa amesema kuwa hakuwahi kusema ameacha siasa bali alisema ameacha siasa za vyama vingi. Kupitia kipindi cha Clouds 360 kinachorushwa na runinga ya Clouds Media Group (CMG), leo jumanne Februari 2018, Dr. Slaa amesikika akiyasema hayo na kuongezea kuwa kutokuwa na chama haimanishi ameacha siasa. “Skuwahi kusema nimecha siasa na kama kuna mtu alikuwepo kwenye mkutano wangu pale Serena Hotel nilisema naachana na siasa za vyama vingi, na sina chama lakini haimanishi nimeacha siasa” Dr. Slaa. Akizungumzia kuhusu uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, amesema kila mtu ana mapungufu yake kwa wagombea waliokuwepo ila Magufuli ana afadhali. Pia amesema Bunge ni maazimio na huleta maana pale mijadala inapopigiwa kura na kuongeza kuwa bungeni sio kuongea kwa ukali. Akijibu swali aliloulizwa kuhusu kukimbilia Canada amesema kuwa ni nchi ambayo ina rekodi nzuri ya haki za b

CUF yamtaka Diwani wao kuacha kuandamana na mgombea wa Chadema

Image
Dar es Salaam. Katibu wa CUF  Ally Mkandu amemtaka Diwani wa kata ya mzimuni Ally Kondo kuacha kuongozana na mgombea wa Chadema Salum Mwalimu. Amesema kwamba diwani huo asipoacha kuongozana na mgombea huyo chama kitamchukulia hatua kali za kisheria ikiwa ni pamoja na kutumia katiba kumvua uanachama. Amesema hayo leo Februari 5 wakati akimnadi mgombea Ubunge  wa Kinondoni Rajabu Salum. Mkurugenzi wa Habari na uenezi Abduli Kambaya amewaambia wakazi wa mzimuni  kwamba mwaka 2015  CUF ilipata  ushindi kwa kufanya kazi kubwa kwenye kata ya mzimuni. ‘’Leo anajitokeza mtu anawashawishi mumchague mgombea mwingine  inauma sana’’amesema  Kambaya Naye mgombea  Rajabu Salum amesema kwamba ‘’Mimi nilikuwa meneja kampeni wa mgombea wa huyu aliyehamia  CCM( Maulid Mtulia)  hivyo mimi nilikuwa mwalimu wake’’ Amesema mgombea huyo sasa ameanza kutumia sera za Cuf  kwenye majukwaa. ‘’CCM na Chadema wameahidi kunipa kura kwa kuwa wagombea wao hawakushiriki kwenye kura za mao

Makamu wa Rais aguswa na Cover ya wimbo wa Nandy na Aslay

Image
Makamu wa Rais, Bi Samia Suluhu Hassan (katikati) akiwa na wasanii Nandy na Aslay. MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan jana jioni aliwakaribisha nyumbani kwake wasanii wa Bongo Fleva, Aslay Isihaka ‘Dogo Aslay’ na Faustina Charles maarufu kama Nandy kwa ajili ya mazungumzo mafupi na chakula cha jioni. Katika mazungumzo yake na wasanii hao, Bi Samia alieleza kuvutiwa sana na marudio ya kibao cha SUBALKHERI kilichorudiwa na wakali hao wa Bongo Fleva hivi karibuni na kuwapa wosia wa kuendelea kufanya kazi nzuri zaidi na kujiepusha na makundi mabaya.

Esma aweka wazi mahaba yake kwa Wema Sepetu

Image
Esma Abdul ‘Esma Platnumz’ MWANADADA Esma Abdul ‘Esma Platnumz’ ameonesha mahaba yake kwa staa mkubwa wa filamu Bongo, Wema Sepetu akidai kuwa, amekuwa shosti wake kwa muda mrefu na hivyo hawezi kujitenga naye. Akipiga stori na gazeti hili, Esma alisema Wema ametoka naye mbali kiasi kwamba leo hii hawezi kumuweka pembeni na kujiweka zaidi kwa wifi wake wa sasa,  Zarina Hassan ‘Zari’. “Jamani Wema hata kidogo siwezi kumuweka pembeni, hata kama aliachana na kaka yangu lakini kwangu bado ana umuhimu. Kama kila anayeachana na kaka basi niwe naye mbali, nikifa inabidi nikazikwe Uganda au Sauzi maana Bongo sitakuwa na rafiki,” alisema Esma

JOKATE: 2018 NI NDOA NA FAMILIA PIA

Image
Jokate Mwegelo MWANAMITINDO ambaye ni kada wa CCM, Jokate Mwegelo baada ya kuanika kuwa mwaka huu ni sahihi kuingia kwenye maisha ya ndoa, ameibuka tena na kuanika kuwa 2018 ni mwaka wa kuwa na familia pia. Akiongea na Risasi Jumamosi Jokate alisisitiza kuwa mwaka huu ni wa neema kwake na kufafanua kuwa ana mpango wa kuanzisha familia yake. “Watu wajue tu kuwa mwaka huu nitaanzisha familia, sio kama ninawafumba lakini kwa uwezo wake Mungu wataona tu, wakae wakisubiri kwani lisemwalo lipo kama halipo linakuja,” alisema Jokate ambaye hakuweka wazi mwanaume atakayemuoa na kuanzisha naye familia

KISA BONGO FLEVA…AGNESS WA PICHA ZA UTUPU ASHAMBULIWA

Image
       Agness Mmasi MUUZA  nyago aliyejipatia umaarufu kwa kutupia picha za utupu mtandaoni, Agness Mmasi ameshambuliwa na mashabiki baada ya kujikita rasmi kwenye Muziki wa Bongo Fleva na kuachia Wimbo wa Danga unaoonekana  kukosa maadili. Akipiga stori na Mikito Nusu Nusu mara baada ya kuachia ngoma hiyo ambayo imejadiliwa sana kwa sababu ya maneno makali yaliyomo kwenye mashairi yake alisema, ngoma hiyo ameiimba kwa kuanika ukweli wa kile kinachoendelea kwenye jamii. “Nashangaa wanaonishambulia lakini ninachojua watu wengi   walikuwa hawaelewi nafanya kazi gani ya kunipa umaarufu, nikaona isiwe tabu bora nitimize ndoto yangu ya kuwa msanii wa muziki, sioni kama nimeimba maneno yasiyo na maadili ni vitu ambavyo vipo kwenye jamii, “alisema.

Figa Ya Sasha Yazua Utata

Image
Sasha Kassim. KALIO la muuza nyago wa video mbalimbali za wanamuziki Bongo, Sasha Kassim limezua utata kwa kudaiwa kuwa si halisi. Chanzo kimepenyeza ubuyu kuwa, Sasha amekuwa ‘akijiedit’ kupitia simu yake hivyo watu kumuona ana kalio kubwa tofauti na uhalisia. Sasha akionyesha figa yake bomba. “Wewe kutana naye hivi laivu halafu utaniambia,” alisema mtoa ubuyu. Alipoulizwa Sasha kuhusiana na hilo alisema; “Siwezi kuwazuia watu kuongea sifoji kitu mimi, siri kubwa ya shepu yangu ni mapozi kwenye picha na aina ya mavazi ninayovaa.”

RAIS DKT MAGUFULI MGENI RASMI KATIKA MAADHIMISHO YA MWAKA MPYA WA MAHAKAMA

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wakati wa maadhimisho ya mwaka mpya wa mahakama ama Siku uya Sheria kwenye uwanja wa Mahakama kuu Ocean Road jijini Dar es salaam leo. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea jambo na Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Juma baada ya kuhutubia katika maadhimisho ya mwaka mpya wa mahakama ama Siku uya Sheria kwenye uwanja wa Mahakama kuu Ocean Road jijini Dar es salaam leo. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma na Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe. Othman Omar Makungu, , Naibu spika Dkt. Tulia Ackson, Waziri wa Sheria na Katiba Profesa Palamagamba Kabudi na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora – Mhe George Mkuchika katika picha ya pamoja na viongozi wa dini na Wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama baada ya kuhutubia wakati wa maadhimisho ya mwaka mpya w

Msigwa afunguka haya Bungeni

Image
Kamatakamata ya viongozi wa vyama vya siasa, wakiwemo wabunge leo Februari1, 2018 imemuibua bungeni Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa kusema vitendo hivyo ni ukiukwaji wa haki za binadamu. Msigwa ameibua hoja hiyo katika kipindi cha maswali na majibu, baada ya kuulizwa swali la nyongeza akihoji sababu za wanaokamatwa kushikiliwa kwa muda mrefu katika vituo vya polisi. “Mimi ni mhanga wa jambo hili napenda kujua msingi wake ni nini, lini mambo haya yatakoma,” amesema. Mbunge huyo amehoji lini taarifa ya Tume ya Haki za Binadamu ambayo ilieleza kuhusu kamatakamata itawasilishwa bungeni kwa ajili ya kujadiliwa. Akijibu suala hilo, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu Anthony Mavunde amesema “..,  naomba wananchi wawe watulivu na kujiepusha kufanya mambo yasiyofaa.” Amesema kwa mujibu wa Katiba, tume hiyo inapaswa kuwasilisha taarifa zake kwa Waziri mwenye dhamana ya masuala ya haki za binadamu.

Ridhiwani atoa agizo afisa mtendaji kuondolewa mara moja

Image
Chalinze.  Mbunge wa Chalinze (CCM), Ridhiwani Kikwete ametaka kuondolewa mara moja kwa ofisa mtendaji wa kata ya Vigwaza, Elizabeth Msenga kwa maelezo kuwa ameshindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo. Ridhiwani ametoa kauli hiyo leo Februari1, 2018 katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini humo, kutaka mtendaji huyo kupangiwa eneo jingine la kazi. Amesema haiwezekani wananchi wanapata matatizo na kukosa mtu wa kuwasikiliza na kuwasilisha kero zao sehemu husika. “Yaani akija mbunge ndio wananchi wanalalamika jukwaani. Uzembe huu unasababisha wananchi kuwa na hasira na kukichukia CCM wakidhani hakiwasilizi na hakiwajali kumbe ni uzembe wa mtu mmoja tu,” amesema na kuongeza, "Nimezunguka vijiji zaidi ya vinne kero zinazopewa ni nyingi lakini utatuzi wake upo chini ya Serikali ya kata. Nashangaa hata ofisa mtendaji hayupo katika ziara na si mara ya kwanza, hakuna taarifa ya Serikali iliyoandaliwa.” Wakati ombi lake la kutaka ofisa huyo kuondolewa l

TLS wammwagia sifa Rais Magufuli

Image
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS), Godwin Ngwilimi amepongeza Rais  John Magufuli kwa kutekeleza matarajio ya watanzania.  Ngwilimi ametoa kauli hiyo leo Februari mosi jijini Dar es Salaam wakati wa kilele cha Maadhimisho ya 22 ya siku ya Sheria na uzinduzi wa mwaka mpya wa kimahakama. Pia, ameomba uwezeshaji wa rasilimali fedha katika muhimili wa mahakama ili kushughulikia changamoto zinazoikabili. "Kama chama cha mawakili, tunakuunga mkono na tunaahidi kutoa ushirikiano kwa mahakama pale inapostahili." Ametoa wito akisema, watumishi wa mahakama, majaji, wasajili, watendaji , makarani  na watumishi wengine, mawakili, wanasheria popote walipo wanatakiwa  kutambua mwelekeo wa nchi unabadilika kwa kasi, matarajio ya wananchi , kuondokana na utamaduni wa kuendelea kufanya kazi kimazoea, kutumia fursa zilizopo ikiwamo Tehama ili kuboresha huduma kwa wananchi. Pia  kuendelea kusimamia maadili ya kitaaluma na uadilifu , hata Mungu anape

Lulu Diva arudisha mahari

Image
MWANAMUZIKI wa kike anayekuja kwa kasi Bongo, Lulu Abbas ‘Lulu Diva’ amerejesha kwa mikono yake mwenyewe mahari aliyokuwa ametolewa na mchumba wake aliyedumu naye kwa takriban miaka mitatu. Chanzo chetu makini kilisema kuwa, mwanamuziki huyo alikuwa afunge ndoa mwishoni mwa mwaka jana lakini kutokana na kuvuja kwa habari kuwa anatoka na mwanamuziki mwenziye wa Bongo Fleva, mwanaume huyo akadai mahari yake. “Kama kuolewa basi Lulu angeolewa mwaka jana mwishoni lakini mchumba huyo alibaini anatoka kimapenzi na mwanamuziki mwenzake akaomba mahari yake irudishwe,” kilisema chanzo. Gazeti hili lilipompigia simu Lulu na kumuuliza madai hayo alisema, ni kweli alirudisha mahari lakini si kwamba mwanaume huyo alijua anatoka na mwanaume mwingine bali alipata shinikizo kutoka kwa ndugu zake. “Aliposhinikizwa sana nikaona isiwe tabu nikamrudishia mahari yake kwa maana alikuwa akiwasikiliza sana ndugu zake ambao walikuwa hawataki anioe,” alisema Lulu. Na Imelda Mtema

BREAKING NEWS: KAMPUNI YA TTCL “YAFUTWA”

Image
Kampuni ya Mawasiliano Tanzania ya (TTCL), sasa haipo tena, imebadilishwa na kuwa Shirika la (TTCL Corporation). Akizungumza na waandishi wa habari, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Makame Mbarawa, amesema kuwa anamshukuru sana Rais Magufuli kwa kuona umuhimu wa kuona wa kuwa na shirika la mawasiliano madhubuti kwa ajili ya kuleta maslahi mapana ya nchi, huku akitoa shukrani pia kwa Wabunge wote kwa kukubali kupitisha muswada huo. Aidha Prof Mbarawa, amesema uwepo wa sheria ya shirika la mawasiliano unatoa fursa ya kuboresha sekta kwa kuweka mazingira mazuri ya usimamizi wa miundombinu ya mikakati chini ya shirika hilo. Profesa Mbarawa pia amewajulisha Watanzania wote kuwa mabadiliko ya kuhama kutoka kampuni kuwa shirika la mawasiliano hayatawaathiri kwa namna ya utoaji wa huduma mbalimbali ambazo zilikuwa zinatolewa na kampuni ya simu ya (TTCL) huku akielezwa kuwa wanaodaiwa na iliyokuwa kampuni hiyo watatakiwa kulia madeni yao kama mikataba yao ina

RAIS WA UGANDA AGUSWA NA KIFO CHA MSANII RADIO

Image
Kufuatia kifo cha msanii wa muziki Radio aliyefariki alfajiri ya leo nchini humo, Rais wa Uganda Yoweri Museven ameonyesha hisia zake kwa kuguswa na kifo cha msanii huyo. Kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter, Rais Museven ameandika “Have been told about the untimely death of musician Moses Ssekibogo aka Mowzey Radio. I had only recently made a financial contribution towards his treatment and hoped he would get better. He was a talented young person with a great future ahead of him. May he rest in peace.” Taarifa za kifo cha msanii huyo zinakuja baada ya siku chache zilizopita Rais Museven kutoa kiasi cha Milioni 30 kwa ajili ya matibabu ya msanii huyo. Vile vile wasanii mbalimbali kama Navio, Diamond, Eddy Kenzo, Professa Jay na wengineo wametumia kurasa zao za mitandao yao ya kijamii kama Instagram na Twitter kutoa pole kwa familia yake. Baada ya kutangazwa taarifa za kifo mashabiki wa msanii huyo na wa Goodkife walifika hospitali hapo kushuhudia kinachoendele

TAMISEMI Yaagiza Shule Ichunguzwe Baada ya Wanafunzi Wote Kupata 0

Image
WIZARA ya Ofisi ya Rais –Tamisemi kupitia kwa Naibu Wairi wake, Joseph Kakunda imemuagiza mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Njombe kuchunguza matokeo mabaya ya mtihani wa kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Viziwi Njombe. Akiji alipojibu swali la mbunge wa Buyungu (Chadema), Samson Bilago, bungeni leo Jumatano Januari 31,2018, Kakunda  amesema katika matokeo yaliyotangazwa jana na Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta), shule hiyo katika matokeo ya mtihani uliofanyika Oktoba na Novemba mwaka jana watahiniwa wote 21 wamepata daraja sifuri (0) yaani wamefeli. Bilago alitaka kujua ni kwa nini shule za wanafunzi wenye mahitaji maalumu zinafanya vibaya kwenye mitihani, ambapo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika amesema walimu waliosoma elimu maalumu watapata ajira bila kikwazo cha kusubiri huku akieleza kuwa anasubiri kupelekewa orodha ya walimu hao.

AIBU YA MWAKA..! WANASWA LIVE WAKIFANYA UFUSKA KAZINI!

Image
Baada ya kunaswa. NI aibu kubwa! Tangu kuanza kwa mwaka 2018, yapo yaliyotokea na kusisimua, lakini hili la mrembo kunaswa na mwanaume wakifanya ufuska kwenye eneo la kazi, limeibua hisia za aina yake kuwa huenda maisha hayaendi, Ijumaa Wikienda linaifumua. Habari kamili, tukio hilo lilijiri kwenye eneo la kazi la mrembo huyo ambalo ni saluni inayojihusisha na vitendo vya ’masaji’ lakini yeye akadaiwa kucheza mchezo wake wa ngono. Saluni hiyo ipo maeneo ya Sinza-Kwaremy jijini Dar ambapo kwa muda mrefu sasa imekuwa ikidaiwa kujihusisha na uchafu huo na kusababisha kero kwa wananchi wenye maadili yao. …Akiwa uchi baada ya kunaswa. OFM KAZINI Kikosi kazi cha Oparesheni Fichua Maovu (OFM) chini ya Global Publishers, kikiwa kimetulia ndani ya mjengo wa makao yake makuu, Sinza-Mori jijini Dar, kilipokea simu kutoka kwa mmoja wa wafanyakazi  wa saluni hiyo akimshitakia mwenzake kuwa amekuwa akijihusisha na ufuska na wanaume mbalimbali wakiwemo waume za

JPM Amjulia Hali Mzee Majuto Hospitalini, Afunguka Alivyomtabiria Makubwa

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amemtembelea muigizaji mkongwe, Mzee Majuto katika hospitali ya Tumaini jijini Dar es salaam ambako amelazwa akitibiwa. Akizungumza mara baada ya kutembelewa na Rais, Mzee Majuto amefunguka na kudai yeye ndio mtu wa kwanza kutabiri ujio wa Rais Magufuli katika kuongoza nchi ya Tanzania huku akisisitiza kwamba anajisikia faraja kuona ana misimamo iliyokuwa imara. “Mimi ndiyo mtu wa kwanza kumtabiri kwamba akiwa Rais itakuwa shughuli. Nilishukuru sana kuchaguliwa huyu bwana, tumepata Rais sio masihara watu wote sasa hivi wana adabu zao wanajua nini maana ya kazi”, alisema Majuto. Pamoja na hayo, Mzee Majuto aliendelea kwa kusema “sisi wazee tunafarijika sasa hivi, viwanda kila kona vimetapakaa na leo amekuja kutembea hospitalini hapa sijui kama wengine hawajikojolea huko kwa uoga maana hataki masihara. Hii ndio raha ya kupata viongozi wenye msimamo”. Kwa upande mwin

Mbunge na Mwanasheria Aliyemwapisha Odinga Atiwa Mbaroni

Image
Mwanasheria TJ Kajwang’ (kushoto) na Mbunge Miguna Miguna wakati wa kumuapisha Odinda. JESHI la Polisi nchini Kenya, leo Januari 31, 2018 mchana limemtia mbaroni mbunge wa Jimbo la Ruaraka, Tom J Kajwang’, ambaye alisimamia “kuapishwa” kwa kiongozi wa muungano wa Nasa Raila Odinga kwenye viwanja vya Uhuru Park jana Jumanne. Kajwang amekamatwa na maofisa hao waliokuwa wamevalia kiraia nje ya Mahakama ya Milimani jijini Nairobi muda mfupi baada ya kuhudhuria katika Mahakama Kuu mbele ya Jaji George Odunga kusikiliza uamuzi wa kesi aliyowawakilisha wabunge wanaopinga kukatwa mishahara yao na posho nchini humo. Kajwang’ na mwanasheria mwingine Miguna Miguna, ndiyo walisimamia matukio yote ya “kuapishwa” Odinga kama ‘rais wa watu’ katika viwanja vya Uhuru Park. Imeelezwa kuwa, Kajwang’ alikuwa amevaa vazi na wigi ambapo alishangiliwa sana na wafuasi wa Nasa wakati Odinga akila “kiapo”.

WEMA SEPETU TENA,CHUCHU AELEZA KUHUSU WEMA KUPATA MTOTO HUKU KUKIWA NA TETESI NA KUWA NA MIMBA

Image
Baada ya baadhi ya mashabiki kumtolea maneno yasiyofaa Wema Sepetu pindi alipoweka picha ya mtoto na Chuchu Hansy katika mtandao wa Instagram, muigizaji huyo amesema Wema hapaswi kuumizwa na hilo kwani utafika wakati wake atapata mtoto. Chuchu Hans ameiambia E-Newz ya EATV kuwa Wema ni rafiki yake na mara kadhaa wao kama wanawake wamekuwa wakiongea na kumshauri na kumtia Moyo. “Nilishamuambia wewe (Wema) utakuja kupata mtoto il sio pale unapohitaji wewe, ni pale ambapo Mungu amekuandikia muda wako ukifika, kwa hiyo hayo maneno wala asimuumie ni changamoto na kutokana na ustaa alionao,” amesema. Mtoto wa Chuchu Hansi anaitwa ambaye amezaa na muigizaji mwenzake, Ray Kigosi.

ANGALIA MPELELEZI ALIYEPOTEZA MIKONO, MIGUU NA UTUMBO,SASA KULIPWA BIL 245

Image
OFISA wa ujasusi (shushushu) katika jeshi la Marekani, Lisa Maria Carter, wa Florida, Marekani, anajitayarisha kulipwa Sh. bilioni 245 (Dola milioni 109 za Marekani) kutokana na kufanyiwa vibaya oparesheni ya kutibu uvimbe uliokuwa umejitokeza katika sehemu ya uzazi mwaka 2010. Lisa Maria Carter alivyo sasa. Hivi sasa, Carter anabidi ahudumiwe kila kitu kutokana na athari aliyopata kutokana na oparesheni hiyo. Mwaka huo, mwanamke huyo akiwa na umri wa miaka 45, alikuwa aondoke kwa ndege kwenda Iraq kukusanya habari za ujasusi ambapo aliambiwa alikuwa na uvimbe kwenye sehemu ya uzazi (ovarian cyst). …Anavyotembea kwa kutumia nyenzo maalum Katika oparesheni iliyofuata ya kumtibu, ambayo ilifanyika vibaya, ilisababisha apoteze mikono yake yote, miguu, utumbo na misuli ya tumbo. Hii ilitokana na kumsababishia kukumbwa na bacteria zilizoula mwili wake na kuharibu sehemu mbalimbali. …Akiwa na mtaalam wa tiba Katika upasuaji huo, shinikizo lake la damu lilishuka s