Wazee wa Baraza: Lulu Alimuua Kanumba Bila Kukusudia
Lulu mwenye (kilemba chekundu) akiwa amejiinamia, kulia ni mama yake na kushoto baba yake wakisubiri kesi kuanza. Mama Lulu (kulia) akisubiri kwa umakini kesi ianze. Ndugu wa Kanumba ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja akiwa mahakamani hapo. Lulu akiondoka mahakamani huku amejifunika kanga baada ya kesi yake kuahirishwa. …Akitolewa nje. Mama Lulu akiingia kwenye gari ili kuondoka. Mzee Michael Kimemeta akijiandaa kuingia kwenye gari. IKIWA ni wiki moja sasa tangu Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam ianze kusikiliza mfululizo kesi inayomkabili muigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’ , wazee wa Baraza la mahakama hiyo leo Oktoba 26, 2017 wametoa maoni yake kuwa Lulu alimuua Kanumba bila kukusudia. Katika maoni hayo yaliyotolewa na Jopo la Wazee watatu wa mahakama kwa nyakati fofauti, wote wamesema Lulu alimuua msanii mwenzake huyo bila kukusudia. Awali k abla ya kutoa maoni yao, Jaji anayesikiliza kesi hiyo, Sam Rum