Posts

Kama Unaumwa Tumbo Wakati Wa Hedhi soma hapa

Image
KARIBU sana katika makala yetu inayohusu afya. Kutokana na simu nyingi ninazozipata nikiulizwa maswali juu ya maumivu yanayowapata akina mama wengi wakati wa hedhi nimeona ni bora niandike makala hii ili iweze kuwasaidia na wengine kujua nini chanzo na mhusika afanye nini pale anapopatwa na tatizo hilo. Maumivu wakati wa hedhi (period pains) au kitaalamu dismenorrhea, ni maumivu yanayojitokeza sehemu ya chini ya tumbo au kiunoni wakati mwanamke anapoanza kupata siku zake au kabla ya hapo. Maumivu hayo huweza kuwa madogo au ya wastani huku baadhi ya wanawake wakipata maumivu makali sana. Maumivu hayo huanza pale yai linapotoka katika mrija (fallopian tube) na kuteremka chini ya mrija huo wakati wa Ovulation. AINA YA MAUMIVU Maumivu ya tumbo la hedhi yapo ya aina mbili.  Ya kwanza  ni maumivu yasiyokuwa na sababu zozote za kimsingi za kitiba. Katika aina hii maumivu ni ya kawaida na huhisiwa sehemu ya chini ya tumbo na kiunoni. Maumivu hayo huanza siku moja au mbi

Mali za Lugumi Mikononi mwa TRA

Image
Kampuni  ya udalali ya Yono, imefanikiwa kukamata mali za wafanyabiashara wanaodaiwa kodi ya serikali inayofikia zaidi ya Sh bilioni 68.1. Operesheni ya kukamata mali hizo kwenye maeneo mbalimbali ndani na nje ya Jiji la Dar es Salaam imefanywa ndani ya wiki moja. Katika operesheni hizo maofisa wa Yono wamekuwa wakishirikiana na maofisa wa Mamlaka ya Mapato(TRA), ambayo ndiyo imeipa kampuni hiyo kazi ya kukusanya kodi kwenye maeneo mbalimbali nchini. Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Yono, Scholastica Kevela, Yono imepewa kazi na TRA kukusanya madeni yake ya kodi kwenye mikoa ya Dar es Salaam, Pwani Njombe, Mbeya, Iringa na Zanzibar. Aliwataka watanzania kuunga mkono jitihada za Rais John Magufuli za kuleta maendeleo kwa kulipa kodi bila shuruti ili zipatikane fedha za kujenga miundombinu kama barabara, reli, shule, madaraja, hospitali na zahanati. Kuhusu taarifa zilizozagaa kwenye mitandao ya kijamii kwamba hata baadhi ya mali za Kampu

RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA DKT. JOHN POMBE MAGUFULI AONGOZA WANANCHI KATIKA SHEREHE ZA MIAKA 53 YA MUUNGANO WA TANGANIKA NA ZANZIBAR YENYE KAULI MBIU “MIAKA 53YA MUUNGANO; TUULINDE NA KUUIMARISHA,TUPIGE VITA DAWA ZA KULEVYA NA KUFANYA KAZI KWA BIDII” APRIL 26,2017

Image
 Amir jeshi mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono wananchi katika sherehe za miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar zilizofanyika kitaifa katika uwanja wa Jamhuri Mkoani Dodoma April 26,2017   Amiri jeshi mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati akipokea heshima na wimbo wa taifa ukipigwa  Amiri jeshi mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati akilekea kukagua gwaride liloandaliwa na vyombo vya ulizi na usalamaliloandaliwa na vyombo vya ulinzi na usalama kwa ajili ya kusherehekea miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar zilizofanyika kitaifa katika uwanja wa Jamhuri Mkoani Dodoma April 26,2017 Amiri jeshi mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikagua gwaride liloandaliwa na vyombo vya ulinzi na usalama kwa ajili ya kusherehekea miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar zilizofanyika k

Rais atoa msamaha kwa wafungwa katika kuadhimisha miaka 53 ya Muungano wa Tanzania

Image
Katika kuadhimisha Miaka 53 ya Muungano wa Tanzania tarehe 26 Aprili, 2017 Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutumia madaraka aliyopewa chini ya Ibara ya 45(1)(d) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ametoa msamaha kwa wafungwa wafuatao:- Wafungwa wote ambao baada ya punguzo la kawaida la moja ya tatu (1/3) linalotolewa chini ya Kifungu 49(1) cha Sheria ya Magereza Sura ya 58, wawe wametumikia nusu (½) ya vifungo vyao vilivyobaki, isipokuwa wafungwa walioorodheshwa katika Ibara ya 2(i – xxi). Wafungwa wagonjwa wenye magonjwa kama UKIMWI, Kifua kikuu (TB) na Saratani (Cancer) ambao wako kwenye “terminal stage”. Wafungwa hawa wathibitishwe na Jopo la Waganga chini ya Uenyekiti wa Mganga Mkuu wa Mkoa/Mganga Mkuu wa Wilaya. Wafungwa wazee wenye umri wa miaka sabini (70) au zaidi. Umri huo uthibitishwe na Jopo la Waganga chini ya Uenyekiti wa Mganga Mkuu wa Mkoa/Mganga Mkuu wa Wilaya. Wafungwa wa kike walioingia na mi

Warembo Washikiana Visu Kisa Penzi la Chuz

Image
WAREMBO wawili wanaofanya tamthiliya ya Closet Chapter, waliofahamika kwa majina moja moja ya Shugga na Kanjo, hivi karibuni walishikiana visu katika ugomvi unaotajwa kuwa ni wa kumgombea bosi wao, Jumanne Kihangala ‘Mr Chuz’. Kwa mujibu wa chanzo chetu kilicho karibu na wasanii hao, sekeseke hilo lilitokea mwishoni mwa wiki, baada ya Shugga ambaye ni mchumba wa Chuz kumuonya Kanjo apunguze mazoea na mpenzi wake huyo. “Ishu hiyo ilitokea wakati wapo kambini Lushoto wakiwa wanashuti, ndipo Shugga akampiga mkwara Kanjo aache kumshobokea, mwenzake naye akaja juu wakaanza kudundana hadi kushikiana visu, wakidai bora wauane wakose wote, ” kilisema chanzo. Baada ya kupata habari hizo, Za Motomoto News ilimtafuta Mr Chuz  mbaye alikiri kutokea kwa ishu hiyo na kusema kinachomponza mchumba wake ni wivu wa kupindukia alionao.

Shuhudia LIVE Makomando Wakionesha matukio ya ujasiri Kwenye Sherehe za Miaka 53 ya Muungano

Image
Sherehe za maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar zinafanyika leo April 26, 2017 mjini Dodoma ambapo mgeni rasmi ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli.Tanganyika na Zanzibar ziliungana April 26, 1964 chini ya hayati Baba wa Taifa, Mwalim Julius Nyerere na hayati Sheikh Abeid Karume. Kikosi cha makamandoo wakitoa saluti mbele ya Amri Jeshi mkuu katika sherehe za miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar zilizofanyika kitaifa katika uwanja wa Jamhuri Mkoani Dodoma April 26,2017 Kikosi cha makomandoo wakionyesha umahili wa mazoezi  mbele ya Amri Jeshi mkuu katika sherehe za miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar zilizofanyika kitaifa katika uwanja wa Jamhuri Mkoani Dodoma April 26,2017 Hapa ni kikundi cha Makomando wakionyesha uwezo, Bonyeza play hapa chini kutazama

Sakata la Bosi wa UN kufukuzwa latua bungeni

Image
Dodoma. Sakata la kufukuzwa nchini la bosi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Tanzania, Awa Dabo, limetua bungeni. Mbunge wa Mbozi, Pascal Haonga(Chadema) akizungumza bungeni leo,  aliitaka serikali kufafanua sababu za kumfukuza nchini Mkurugenzi Mkazi huyo wa UNDP Tanzania kwa kumpa saa 24. Hata hivyo, Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge aliliambia bunge kuwa serikali ina mamlaka yote katika masuala ya kidiplomasia na hivyo bunge haliwezi kuhoji  sababu za mkurugenzi huyo kufukuzwa.

MREMBO DAYNA NYANGE NA GONJWA LA KUWEWESEKA

Image
Staa wa Bongo Fleva, Mwanaisha Saidi ‘Dayna Nyange’. STAA wa Bongo Fleva, Mwanaisha Saidi ‘ Dayna Nyange ’ amefunguka kuwa siku za hivi karibuni amekumbwa na gonjwa la kuweweseka linalomkosesha raha. Akipiga stori na  Uwazi Showbiz , Dayna alieleza kuwa kuweweseka huko kunatokana na msongo wa mawazo alionao kwani anawaza kazi mpya atakayoitoa baada ya Wimbo wa Komelo kuendelea kufanya vizuri kwani muziki kwa sasa una ushindani mkubwa mno. “Kiukweli ninavyowaza kuhusu ujio mpya mpaka najikuta naweweseka usiku wakati nikiwa nimelala, nikishtuka natuliza mawazo na kujipa moyo kuwa Mungu atanisaidia nitaandaa kazi nzuri ambayo itafika mbali zaidi ya hii niliyotoa sasa,” alisema Dayna.

WABUNGE WA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WATINGA UBALOZI WA TANZANIA WASHINGTON, DC

Image
Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo siku ya Jumatatu April 24, 2017 wametembelea Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani na kukutana na Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Mhe. Wilson Masilingi. Katika picha toka kushoto ni Mkuu wa Utawala na Fedha Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani Bi. Swahiba Mdeme,Mwambata wa Jeshi Ubalozi wa Tanzania na Canada Col. Adolph Mutta, Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Bajeti Mhe. Hawa A. Ghasia, Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Mhe. Wilson Masilingi, Mbunge Mhe. Janeth Z. Mbene, Mhe. Josephat S. Kandege, Afisa wa Ubalozi Bwn. Dismas Assenga na Afisa wa Bunge Bwn. Godfrey Godwin. Wabunge hao wa Bunge la Jamhuri ya Muungano waTanzania walikuja Washington, DC kuhudhuria mikutano ya kipupwe ya Benki ya Dunia na IMF Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Mhe. Wilson Masilingi. Katika picha toka kushoto ni Afis

Nafasi za kazi leo tarehe 25

Image
Nafasi za kazi Leo Tanzania Nafasi za Kazi Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania Communications Officer Job at PATH, Dar es Salaam Programme Support Officer Job, Mwanza, Tanzania Consultant-Female Food Hero, Job at Oxfam, Tanzania Consultant- Baseline Survey Job at Oxfam, Tanzania Financial Management Experts Job, Arusha, Tanzania Consultant-Female Food Hero Five Years Evaluation, DSM Senior Monitoring & Evaluation Officer Job, Tanzania Program Assistant (Education) Job at UNICEF, Dar es Salaam Tembelea  STUFFZOOM  Kwa nafasi zaidi

ANGALIA PICHA PRINCE WILLIAM NA MKEWE KATE WALIVYOPAMBA MBIO ZA LONDON MARATHON

Image
Wikiendi hii yalifanyika mashindano ya riadha ya London Marathon, ambako Mtanzania Alphonce Simbu aliibuka mshindi wa tano. Prince William na mkewe Catherine Elizabeth (Kate) ni baadhi ya wageni waliohudhuria katika mashindano hayo. Katika mbio hizo Daniel Wanjiru kutoka Kenya aliibuka mshindi wa kwanza kwa upande wa wanaume baada ya kukimbia kwa muda wa masaa 2:05:48 na upande wa wanawake Mary Keitany naye kutoka Kenya alishinda baada ya kukimbia kwa muda wa masaa 2.17.01. Hizi ni baadhi ya picha za Prince William na mkewe Kate Middleton katika mashindano hayo.

Shehe Mkuu DSM Aibua Utata Freemason

Image
  Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhadi Musa Salumu mwishoni mwa wiki iliyopita alizua utata katika kona mbalimbali za kijamii kufuatia kufanya dua maalumu ya kumwombea aliyekuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Freemason Afrika Mashariki, marehemu Sir Jayantilal Keshavji ‘Andy Chande’ (pichani). Tukio hilo lilifanyika Aprili 21, mwaka huu katika Shule ya Sekondari ya Shabani Robert na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa nchi, akiwemo Rais Msaatafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin William Mkapa sanjari na wanafunzi wengine waliowahi kusoma katika shule hiyo. HABARI KAMILI Sir Andy Chande alifariki dunia, Aprili 7, mwaka huu nchini Kenya kwa maradhi ya presha na kuzikwa katika Makaburi ya Baniani, Makumbusho jijini hapa kwa kuchomwa moto. Katika enzi za uhai wake, Sir Andy Chande aliwahi kuweka wazi kuwa yeye ni mfuasi na kuhani mkuu wa Jumuiya ya Freemason, jumuiya ambayo inaaminika na baadhi ya watu kwamba iko kinyume na mafundisho ya dini za Kiislamu na

Aliyeua mwanawe kwa nyundo atakiwa kupimwa akili

Image
JAJI wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, Joaquine De-Mello ameamuru mtuhumiwa wa mauaji ya mwanawe kwa kutumia nyundo na ambaye ni mchinja nguruwe, Ezekiel Magige akapimwe akili Dodoma. Magige, ambaye ni mkazi wa mji mdogo wa Sirari alifikishwa mahakamani jana kwa tuhuma za kumuua mtoto wake kwa kumpiga kwa nyundo kichwani na ubongo kusambaa. Mahakama Kuu ipo katika vikao vyake vya kikanda Tarime kwa wiki mbili na Jaji De-Mello anasaidiwa na Jaji Rose Ebrahim. Kesi zaidi ya 40 ama zitatajwa au kusikilizwa, zikihusisha makosa ya mauaji, madawa ya kulevya na ujambazi wa kutumia silaha. Wakili wa Serikali, Harry Mbogoro alidai kuwa Desemba 28, 2014 na akiwa nyumbani kwake Sirari, mtuhumiwa Magige alimpiga kwa nyundo kichwani mwanawe Julias Michael na kusababisha kifo chake papo hapo. Jaji De-Mello alisema "ninaagiza mtuhumiwa huyu Ezekeil Magige apelekwe Isanga Dodoma kupimwa akili ka

FLORA MBASHA KUOLEWA NA KUZINDUA ALBAMU MPYA SIKU MOJA

Image
Aliyekuwa Mke wa Muimbaji wa Muziki wa Injili Emmanuel Mbasha, Flora Mbasha aka Madame Flora, anatarajia kufunga ndoa na mume wake mtarajiwa Daudi Kusekwa katika bustani za hoteli ya Rock Beach jijini Mwanza. Madame Flora alisema kuwa ndoa hiyo itaambatana na uzinduzi wa albamu yake mpya inayoitwa ‘Wakati Wake’ pamoja na kitabu alichokipachika jina la ‘Siri za Flora Mbasha.’“Ndoa itafungwa asubuhi na jioni kutakuwa na sherehe ya harusi, utambulisho wa albamu yangu mpya pamoja na kitabu kipya. Watu wote wanakaribishwa, ingawa kadi zimebaki chache tu kutokana na idadi ambayo imepangwa na kamati,” alisema Flora. Chanzo Mtanzania.

Steve Nyerere aporomosha jambo lingine leo

Image
Muigizaji na mchekeshaji maarufu nchini Steve  Nyerere amemuombea msamaha msanii wa muziki Nay wa Mitego kwa kuwaita wasanii wa filamu wote walioandamana kupinga uingizwaji wa filamu kutoka nje ya nchi kuwa ni 'Matahira' Akizungumza leo kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Steve Nyerere amesema kwamba yawezekana  Nay wa Mitego alikuwa na hasira hivyo akashindwa kutumia lugha sahihi ya kuwaelekeza wasanii wenzake walivyokuwa wanakosea ndio maana alitoa lugha yenye maneno makali ijapokuwa alikuwa sahihi kukosoa maandamano yale. "Kwanza naomba nimuombee msamaha ndugu yangu Nay wa Mitego, hakuwa na nia mbaya lakini hakutumia maadili kufikisha ujumbe wake, Unajua sisi watanzania hatupendi kuambiwa ukweli na hata tukisemana tuna lugha zetu laini za kusemeshana. Nay wa Mitego mpaka kutoa maneno makali vile ujue anaipenda tasnia yetu ya filamu alikuwa kaaumia, si unajua hata yeye alishawahi kuwa huku anatuonea huruma na anatupenda mimi niseme

Kambi ya Upinzani Walivyogoma Kusoma Hotuba Yao Bungeni

Image
Msemaji wa upinzani katika Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira na Muungano, Ally Salehe amesusa kusoma hotuba yake ya upinzani kuhusu wizara hiyo baada ya kuamriwa kuacha kusoma baadhi ya maneno yakiwamo yanayohusu Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar na mgogoro wa CUF. Hali  hiyo imetokea bungeni leo Jumatatu baada ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), George Masaju kusimama na kupinga baadhi ya maneneo aliyotumia kama  “Kila wizara imekiona cha moto, wamebanwa mpaka wamevunjwa mbavu” na kuwa Ofisi ya Makamu wa Rais imeathirika vibaya na kisu cha ngariba kwa kukata bajeti yake. Baada ya malumbano, Mwenyekiti wa Bunge, Musa Zungu alitoa uamuzi kuwa maneno yaliyoandikwa kuanzia ukurasa wa tatu hadi wa saba kwenye hotuba hiyo yasisomwe wala kurekodiwa kwenye kumbukumbu rasmi za Bunge. Baada ya uamuzi huo, Salehe alisema basi asingeendelea kuisoma hotuba yake na yaliyobaki anamwachia ‘ngariba’ afanye anavyotaka.

RAIS DKT. MAGUFULI AWASILI MKOANI DODOMA

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana mara baada ya kuwasili mkoani Dodoma. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana mara baada ya kuwasili mkoani Dodoma. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa mara baada ya kuwasili mkoani Dodoma. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai mara baada ya kuwasili mkoani Dodoma. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi Abdallah Bulembo mara baada ya kuwasili mkoani Dodoma. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisaini kitabu cha Wageni mara baada ya k