Posts

Kitwanga, JPM Wakutana Uso kwa Uso

Image
Rais John Magufuli jana alikutana ana kwa ana na rafiki yake, Charles Kitwanga ikiwa ni siku 80 baada ya kumvua cheo cha Waziri wa Mambo ya Ndani kwa kosa la kuingia bungeni kujibu maswali akiwa amelewa. Wawili hao walikutana kwenye Jimbo la Misungwi ambako Rais alisimama akitokea Wilaya ya Sengerema ambako alihutubia wananchi. Rais alitengua uteuzi wa Kitwanga Mei 20, wakati sakata la utekelezwaji mbovu wa mkataba wa Sh37 bilioni baina ya Jeshi la Polisi na kampuni ya Lugumi Enterprises likivuma kwenye Bunge la Jamhuri ya Muungano. Lakini jana, hali ilionekana ya kikazi zaidi wakati Rais alipofika kwenye jimbo hilo. Kitwanga, ambaye ni mbunge wa Misungwi mkoani Mwanza, alitumia nafasi hiyo kukutana na Rais kwa mara ya kwanza hadharani, kuwasilisha kero za wananchi wake, hasa ya maji. Katika tukio hilo lililovutia hisia za waliokuwepo, Rais aliuthibitishia umma kuwa yeye na Kitwanga ni marafiki wa muda mrefu, alipokuwa akijibu ombi la mbunge huyo la kutaka Ser

Njemba Avamia Makao Makuu ya Trump, Apanda Ghorofa 21 kwa Saa 3

Image
Polisi wakijitahidi kumtoa njemba huyo aliyepanda juu ya ghorofa. Njemba huyo katika haakati za kukwea jengo hilo la ghoofa 58. Akikazana kukwea. Hali ilivyokuwa Mashuhuda wakitahauki. Polisi wakijitahidi kumdhibiti Akitolewa na polisi NEW YORK: Njemba mmoja nchini Marekani aliyejiita kuwa ni mtafiti binafsi na shabiki wa Donald Trump, jana Agosti 10, 2016 alitumia masaa matatu kupanda jengo la mfanyabiashara huyo maaufu duniani ambaye pia ni mgombea urais wa nchi hiyo kwa tiketi ya Chama cha Republican lililopo jijini New York. Taarifa zimeeleza kuwa njemba huyo mwenye umri wa miaka 21 mkazi wa Virginia alitumia vifaa maalum kupanda ghorofa hilo lililojengwa kwa vioo ambalo pia ni Makao Makuu ya Kampeni za Bwana Trump na ndiyo Makao yake Makuu Kibiashaa kabla ya polisi kumtoa akiwa amefikia ghorofa ya 21 huku akiwa amechomwa vibaya na vioo vya jengo hilo. Trump anaishi kwenye ghorofa ya ya juu kabisa ya jengo hilo lakini kwa sasa an

RAIS DKT. MAGUFULI AANZA ZIARA YAKE MKOANI MWANZA.

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella mara baada ya kuwasili katika Wilaya ya Sengerema Mkoani Mwanza.    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia mamia ya wakazi wa Sengerema mkoani Mwanza mara baada ya kuwasili akitokea Chato mkoani Geita. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia wanakwaya wa UWT Kisima cha maji Chumvi mara baada ya kuhutubia wakazi wa Sengerema mkoani Mwanza.     Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mwalimu Mstaafu wa Shule ya Sekondari Sengerema Wilson Fumbuka Mbanga ambaye walifundisha naye shule hiyo tokea mwaka 1982-1985 mara baada ya kumaliza mkutano wa hadhara Sengerema Mkoani Mwanza.   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiaagana na wakazi wa Sengerema mkoani Mwanza mara baada ya kumaliza kuwa

WANACHAMA NA MASHABIKI WA YANGA WAMSHAMBULIA MKUU WA MKOA PAUL MAKONDA BAADA YA KUANDIKA MANENO HAYA MTANDAONI

Image
Kitendo cha wanachama wa klabu ya Young Africans kumruhusu mwenyekiti wao, Yusuph Manji kuikodi klabu hiyo kwa kipindi cha miaka 10 kinaendelea kuwagusa watu wengi na mmoja wapo ni mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ambaye amefikia hatua ya kuandika ujumbe katika mitandao ya kijamii. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Makonda ameandika “Unataka kujuwa kwa nini Tanzania ni masikini pamoja na UTAJIRI MKUBWA WA MALIASILI tulizonazo? Soma Mkataba wa Yanga wanaosaini LEO” Baada ya kuweka picha hiyo wadau mbalimbali wa soka nchini wamekua wakianzika maoni yao katika ujumbe wa Makonda, wengine wakimtaka asizungumze mambo ya Young Africans, na wengine wakimtaka afanye kazi za serikali na aache kujihusisha na soka na mashabiki wa klabu hiyo nguli hapa nchini. Awali Makonda aliweka picha ya Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Clement Sanga na kusema kuwa alikuwa na maswali 87 kwa kiongozi huyo wa Yanga lakini baada ya kutizama mahojiano aliyofanyiwa, aligundua kwamba kiongozi

Hukumu Kesi Ya Babu Tale Bofya Hapa!

Image
ILE kesi inayomkabili Meneja wa Staa wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, Babu Tale ya kusambaza na kuuza DVD za mawaidha ya Shehe Hamis Mbonde bila ridhaa yake imeahirishwa tena na Mahakama Kuu ya Kanda ya Dar es Salaam hadi Agosti 24, mwaka ambapo hukumu itatolewa. Akizungumza mbele ya mawakili na wahusika wa pande zote mbili leo asubuhi, Msajili wa Mahakama, Kayonza alianza kwa kutupilia mbali hoja ya mawakili wa upande wa Babu Tale, Robert Mkoba na Augustino Aluta iliyoomba kupewa muda zaidi kwa sababu ya mmoja kati ya mawakili wao (Paul Mgaya) ana udhuru na kwamba yupo jijini Arusha kwa semina. “Mawakili mnaosikiliza kesi hii kwa upande wa Tale mpo watano, siwezi kuruhusu tena kuahirishwa kwa kesi hii kisa mmoja hayupo. Agosti 24 itakuwa siku ya hukumu na kutekelezwa ambacho kipo na niwaombe wote muwepo,” alisema Kayonza. Awali kesi hiyo ilitakiwa itolewe hukumu Agosti 1 lakini kutokana na Mgaya kuumwa ilibidi kuahirishwa hadi leo (Agosti 10). Wakili wa

REAL MADRID NA SEVILLA WALIVYOTOANA JASHO KWENYE MCHEZO WA UEFA SUPER CUP USIKU WA KUAMKIA LEO

Image
Nahodha wa Real Madrid Sergio Ramos akishangilia huku akinyanyua kombe na wenzake baada ya kutwaa ubingwa wa Uefa Super Cup baada ya kushinda 3-2 dhidi ya Sevilla huko Norway  Beki wa Real Madrid Dani Carvajal akishangilia baada ya kuifungia timu yake bao la tatu na ushindi dhidi ya Sevilla kwenye mchezo wa Uefa Super Cup. Sergio Ramos akiifungia Real Madrid goli la kusawazisha kwa kichwa na kufanya matokeo kuwa 2-2 dhidi ya Sevilla kwenye mchezo wa Uefa Super Cup, kabla ya kuibuka na ushindi ndani ya dakika 120.  Konoplyanka, ambaye hakuwa kwenye kiwango bora kwenye Michuano ya Euro 2016 na Ukraine, akifunga mkwaju wa penati na kuipa Sevila uongozi wa mabao 2-1.

Mzungu Dar Afumwa Live Akilawitiwa na Vijana 3

Image
  Mzungu akilawitiwa, OFM wamfumania. MWANDISHI WETU, WIKIENDA DAR ES SALAAM: Ushoga? Mzungu mmoja ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja lakini akijitambulisha kuwa ni raia kutoka nchini Italia, hivi karibuni alinaswa akiwa katika harakati za kulawitiwa na vijana watatu, Wikienda limeinyaka. Tukio hilo lililotafsiriwa kuwa linakwenda kinyume na msimamo wa Serikali ya Tanzania kuhusu sheria za makosa ya kujamiina, lilijiri Agosti 4, mwaka huu, nyumbani kwa Mzungu huyo, Mikocheni jijini Dar es Salaam.   YALIANZA MALALAMIKO Awali, kijana mmoja alipiga simu kwenye ofisi za Global Publishers na kutaka msaada kutoka kwa kitengo maalum cha Oparesheni Fichua Maovu ‘OFM’ na kusema kuwa kuna Mzungu amekuwa akimtaka awapeleke vijana nyumbani kwake kwa ajili ya mambo yasiyopendwa na watu wengi na pia ni kinyume na msimamo wa serikali. Lakini atatoa mshiko wa nguvu.   Baada kudakwa na polisi, kupigwa pingu na kupelekwa kituoni. “Jamani kuna Mzu

Wanafunzi 80 Mkoani Kilimanjaro Wasimamishwa Masomo kwa Ujauzito.

Image
WANFUNZI 80 wa shule za msingi na sekondari mkoani Kilimanjaro wamesimamishwa masomo katika kipindi cha kuanzia mwezi January hadi Julai mwaka huu baada ya kubainika kuwa na ujauzito. Afisa elimu mkoa wa Kilimanjaro Bi Euprasia Buchuma amemweleza Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia kuwa tatizo la ujauzito kwa wanafunzi mkoani Kilimanjaro ni kubwa hali ambayo inasababisha kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi wa kike kushuka kila mwaka. Amesema tatizo hilo limeonekana kubwa baada ya agizo la Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro kutaka wanafunzi wakike wapime ujauzito wakati wanarudi mashuleni baada ya kumaliza likizo na kwamba muamko wa jamii kuwachukulia hatua wale wanaowabebesaha wanafunzi ujauzito ni mdogo. Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Bw.Saidi Meck Sadick amesema wilaya ya Rombo inaongoza kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi 22 wenye ujauzito ikifuatiwa na wilaya ya Siha wanafunzi 12,Hai 11 huku wilaya ya Same ikiwa haijabainika kuwa na mwanafunzi wa kike mwe

KUFURU YA WANAFUNZI BAADA YA KUMALIZA MITIHANI.

Image

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI TAREHE 7/8/2016.

Image