Posts

Bahati Bukuku Aishiwa Nguvu

Image
Mwimba Injili mahiri Bongo, Bahati Bukuku akiwa na huzuni baada ya kufiwa na mama yake. DAR ES SALAAM: Pole! Mwimba Injili mahiri Bongo, Bahati Bukuku hivi karibuni aliishiwa nguvu wakati akimzika mama yake mzazi, Enea Bukuku aliyefariki dunia Januari 12, mwaka huu jijini Mbeya kwa ugonjwa wa shinikizo la damu (presha). Kwa mujibu wa shuhuda wetu, Bahati alikumbwa na hali hiyo mara baada ya kuuaga mwili wa mama yake, tayari kwa safari ya kwenda kuupumzisha kwenye Makaburi ya Mlima James jijini humo. …..Akiweka shada la maua. “Jamani kifo cha mama kinauma sana! Bahati amejikuta akiishiwa nguvu msibani. Nimemhurumia sana huyu dada, lakini naamini Mungu atamtia nguvu maana yeye ndiye aliyetoa na ndiye aliyetwaa, jina lake libarikiwe,” alisema shuhuda huyo. Akaendelea: “Lakini nimeona waimba Injili wenzake, nilimwona Bonny Mwaitege naye kutoka Dar amekuja kumzika mama wa mwimba Injili mwenzake. Bahati anahitaji uangalizi kwa siku mbili hizi, kwani muda mwingi namwona an

RAIS DKT. JOHN POMBE MAGUFULI AKIONESHA UMAHIRI KATIKA USHONAJI.

Image
 Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akionesha umahiri wake wa kutumia Cherahani na kushona nguo za wafanyakazi wakati alipofanya ziara ya kutembelea na kuvifahamu vitengo mbalimbali vya Ikulu jijini Dar es salaam Januari 20, 2016   Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kushona kwa ustadi wa hali ya juu Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akimalizia moja ya nguo za wafanyakazi wa Ikulu.

BREAKING NEWZZZ.....ZITTO KABWE AANDIKA UJUMBE MZITO KUHUSU KUIBIWA KWA KOMPUTA YA KAMISHNA WA TRA.

Image
 

RAIS DKT JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI AONGOZA WAOMBOLEZAJI KUAGA MWILI WA MAREHEMU LETICIA NYERERE

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Rais mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho  Kikwete nyumbani kwa Baba wa Taifa  Msasani Dar es salaam wakati wa kuaga mwili wa aliyekua Mbunge wa Viti Maalum (Chadema) Marehemu Leticia Nyerere aliyefariki mwishoni mwa wiki Nchini Marekani alikokuwa akitibiwa leo Januari 20, 2016.   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na waombolezaji wakati wa kuaga mwili wa aliyekua Mbunge wa Viti Maalum (Chadema) Marehemu Leticia Nyerere aliyefariki mwishoni mwa wiki Nchini Marekani alikokuwa akitibiwa leo Januari 20, 2016.   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiweka saini katika kitabu cha maombolezo wakati wa kuaga mwili wa aliyekua Mbunge wa Viti Maalum (Chadema) Marehemu Leticia Nyerere aliyefariki mwishoni mwa wiki Nchini Marekani alikokuwa akitibiwa leo Januari 20, 2016.   Rais wa Jamhuri ya Mu

RUVU YAKUBALI KICHAPO CHA MABAO 2 -0 KUTOKA KWA SIMBA

Image
Mshambuliaji wa Simba, Daniel Lyanga akielekea kuifungia timu yake bao la pili dhidi ya JKT Ruvu baada ya kumtoka golikipa wa JKT Ruvu, Hamis Seif katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo. Simba ilishinda 2-0. (Picha na Francis Dande)  Patashka. Raha ya ushindi. Kutoka kushoto, Amis Kiiza, Daniel Lyanga na Kihongera Raphael wakishangilia bao la pili la timu ya Simba lililofungwa na Lyanga.

DK. JOHN POMBE MAGUFULI AMRUDISHA MANYARA MASWI BAADA YA KUMALIZA KAZI MAALUM TRA

Image

A - Z YA TIMBWILI LA SHILOLE KIUNO NA NUH MZIWANDA STUDIO

Image
Kimenuka mbaya! Gumzo kubwa mjini ni timbwili ‘hevi’ aliloliangusha Mbongo-Fleva wa kike, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ au Shishi’ ndani ya Studio za Clouds TV mara tu baada ya kumuona aliyekuwa mwandani wake, Naftal Mlawa ‘Nuh Mziwanda’ katika zoezi la kutaka kuwapatanisha baada ya kutemana hivi karibuni hivyo mahojiano yakavurugika na kwamba upatanisho haukufanikiwa. Mara tu baada ya kuchomoka kwenye ‘intavyu’ hiyo, Shilole alitimkia nchini Afrika Kusini (Sauz) lakini alipata nafasi ya kuzungumza na gazeti hili kuelezea kile kilichotokea. Shilole alisema, hakuna siku amewahi kufikia wakati mgumu kama siku hiyo ambapo aliitwa na mmoja wa watangazaji wa Clouds TV, akimuomba wafanye mahojiano na akakubali akijua yatakuwa ni mahojiano ya kawaida yahusuyo muziki na shughuli zake zingine kama msanii wa kawaida. Alisema kuwa kwa upande wake intavyu hiyo ilikuwa ngumu mno kwani hakutarajia na maswali yaliyomhusu Nuh Mziwanda ndiyo maana yakatokea yaliyotokea. “Ile ku

SERIKALI YAKANUSHA UZUSHI UNAOENEZWA KATIKA MITANDAO YA KIJAMII KUMHUSU RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Image
Kaimu Mkurugenzi wa idara ya Habari MAELEZO Bi Zamaradi Kawawa akitoa ufafanuzi juu ya taarifa za uzushi unaosambazwa katika mitandao ya Kijamii ya ndani na nje ya nchi kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimwa Dkt. John Pombe Magufuli amefukuza wageni kutoka nje waliokuwa wanafanya biashara hapa nchini kwa kuwa Serikali yake haitataki wageni wafanye bishara zao nchini ambapo ukweli ni kwamba Serikali haijafukuza wageni wanaofanya biashara zao nchini na haina mpango wa kufanya hivyo kwa wageni wanaoishi nchini kwa vibali vilivyotolewa kisheria na Serikali.kushoto ni Naibu Kamishna na Msemaji wa Idara ya Uhamiaji Bw. Abbas Irovya na mwisho kushoto ni Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani Isaac Nantanga,Kulia ni Naibu Kamishna wa Idara hiyo Bw.Wilson Bambaganya. Naibu Kamishna na Msemaji wa Idara ya Uhamiaji Bw. Abbas Irovya akitoa wito kwa Watanzania kuwafichua wale wote wanaoingia na kuishi nchini kinyume cha sheria ili hatua stahiki ziweze kuch

JAJI LUBUVA AFUNGUA MKUTANO WA BARAZA LA WAFANYAKAZI WA NEC

Image
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Mstaafu Damian Lubuva (kulia) akiongea na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa NEC (hawapo pichani) leo 20 Januari, 2016  katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere uliopo Jijini Dar es Salaam  wakati alipofungua Mkutano wa Wajumbe wa Baraza hilo uliojadili mambo mengi yakiwemo Afya, rushwa ufanisi kazini na Utawala bora. Kushoto ni Mkurugenzi wa Uchaguzi Bwana. Ramadhani Kailima. Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Mstaafu Damian Lubuva (kushoto) akiongea na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa NEC (hawapo pichani) leo 20 Januari, 2016 katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere uliopo Jijini Dar es Salaam wakati alipofungua Mkutano wa Wajumbe wa Baraza hilo uliojadili mambo mengi yakiwemo Afya, rushwa ufanisi kazini na Utawala bora. Kulia ni Katibu wa Mkoa TUGHE Bwana Gaudensi Kadyango na katikati ni Katibu wa Baraza hilo Bi. Rose Malo. Mkurugenzi wa Uchaguzi Bwana. Ramadhani Kailima akiongea  na Wajumbe wa Baraz