Bahati Bukuku Aishiwa Nguvu
Kwa mujibu wa shuhuda wetu, Bahati alikumbwa na hali hiyo mara baada ya kuuaga mwili wa mama yake, tayari kwa safari ya kwenda kuupumzisha kwenye Makaburi ya Mlima James jijini humo.
…..Akiweka shada la maua.
“Jamani kifo cha mama kinauma sana! Bahati amejikuta akiishiwa nguvu
msibani. Nimemhurumia sana huyu dada, lakini naamini Mungu atamtia nguvu
maana yeye ndiye aliyetoa na ndiye aliyetwaa, jina lake libarikiwe,”
alisema shuhuda huyo.Akaendelea: “Lakini nimeona waimba Injili wenzake, nilimwona Bonny Mwaitege naye kutoka Dar amekuja kumzika mama wa mwimba Injili mwenzake. Bahati anahitaji uangalizi kwa siku mbili hizi, kwani muda mwingi namwona ana simanzi tu.”
“Asante. Tumeshamzika mama. Mimi naendelea vizuri, Mungu ni mwema. Jumatatu inayokuja nitarudi Dar,” alisema Bahati kwa majonzi.
Comments
Post a Comment