RAIS KIKWETE AZIONYA NCHI CHOKOZI DHIDI YA ARDHI YA TANZANIA
RAIS Jakaya Kikwete amesema Serikali ya Tanzania iko tayari kukabiliana na mtu yeyote atakayejaribu kuichezea au kuichokoza kwa namna yoyote ile, ikiwamo kumega ardhi yake, itamfundisha kama ilivyomfundisha aliyekuwa Rais wa Uganda, Idd Amin Dada, katika Vita ya Kagera. Kikwete alisema serikali ilimshikisha adabu Amin alipojaribu kumega sehemu ya ardhi ya Tanzania, hivyo haitosita kufanya hivyo tena kwa asiye na nia njema na Tanzania. Kiongozi huyo mkuu wa nchi alitoa onyo hilo jana wakati akizungumza na wananchi katika maadhimisho ya Siku ya Mashujaa yaliyofanyika kitaifa katika makaburi yaliyopo Kambi ya Kaboya, wilayani Muleba, mkoani Kagera. Rais Kikwete alisema serikali iko tayari kukabiliana na kupambana kwa nguvu yoyote ile bila kuogopa mtu anayejaribu kuichezea nchi ya Tanzania kwa lengo la kukwaza amani na utulivu uliopo hivi sasa. “Laleni usingizi salama. Msisikilize maneno ya mitaani, kwa sababu jeshi letu liko