TONTO DIKEH AOLEWA, ABADILI JINA INSTAGRAM

Muigizaji kiwango kutoka Nigeria, Tonto Dikeh.
Lagos ,NIgeria
MUIGIZAJI kiwango kutoka Nigeria, Tonto Dikeh ameolewa rasmi na aliyekuwa mpenzi wake, Churchill Olakunle Oladunni wiki iliyopita.Tarifa za kuolewa zilianza kuzagaa mapema wiki iliyopita baada ya staa huyo kubadili jina lake kwenye Mtandao wa Kijamii wa Instagram na kujiita, Mrs Tonto Wigo Dikeh-Churchill.
Lakini wikiendi iliyopita zilizagaa picha mitandaoni zikimuonyesha staa huyo akiwa na mumewe huyo mpya lakini kubwa zaidi ni ile ambayo amepiga na bibi yake wakiwa wanapongezwa kwenye sherehe hiyo.
Tayari inadaiwa kuwa Tonto ni mjamzito na bibi yake huyo ameonekana kuumia zaidi baada ya kudai kuwa anamuacha peke yake kwani alizoea kuishi naye lakini amemtakia maisha mema na mumewe huyo.

Comments

Popular posts from this blog