BABY MADAHA AZIDI KUTAFUTA KIKI KUPITIA KWA DIAMOND

Baby Joseph Madaha akipozi na Nasibu Abdul ‘Diamond’. MWIGIZAJI na mwanamuziki Bongo, Baby Joseph Madaha amemchana Nasibu Abdul ‘Diamond’ kwa kumwambia awatishie watoto wa Tandale kwani hana ubavu wa kuchuana naye.

Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz'.
Akizungumza na paparazi wetu, Baby alifunguka kuwa anamshangaa Diamond kujibu kuhusu jinsi alivyomchana wiki kadhaa zilizopita gazetini na kusema yeye hamuwezi kwani alimtangulia kuchomoka kistaa.
“….akiwa bado ana-struggle kupata mkwanja awatishie watoto wenzake wa Tandale, mimi nishazindua brand yangu ya manukato na mikoba ya zawadi, bidhaa ambazo zinaingia sokoni rasmi Desemba 31, awatishe haohao watoto wenzake, mimi siyo saizi yake,” alisema Baby. 

Baby Joseph Madaha.
Diamond alipotafutwa, simu yake iliita bila kupokelewa.

Comments

Popular posts from this blog