Posts

Rais Kagame Amjibu Rais Magufuli Twitter

Image
Rais wa Rwanda amejibu tweet ya dr John Pombe Magufuli , aliyomwandikia kwa ajili ya kumpongeza kwa kuchaguliwa tena kwa awamu nyingine kuwa rais wa Rwanda. ANGALIZO; Inaonekana hawa viongozi wawili wametokea sana kuelewana mpaka kufikia hatua Paul Kagame kumwita rais Magufuli ndugu yangu, hongera sana Rwanda na Tanzania kwa mshikamano huu. Replying to @MagufuliJP Nakuahidi kuuendeleza Undugu na ushirikiano wetu katika nyanja zote kwa ajili ya maendeleo ya nchi zetu. Replying to @MagufuliJP Kwa niaba ya Wananchi wa Rwanda na kwa niaba yangu binafsi, nakushukuru sana Ndugu yangu Mheshimiwa Rais

RAIS DKT. MAGUFULI AREJEA JIJINI DAR ES SALAAM NA KUHUTUBIA WANANCHI WA BUNJU B

Image
   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Bunju wakati akirejea jioni ya leo jijini Dar es Salaam mara baada ya kumaliza ziara yake ya siku tano katika mkoa wa  Tanga.   Baadhi ya wananchi wa eneo la Bunju wakimsikiliza  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza aliposimama eneo hilo kwa ajili ya kuwasalimia  wakati akirejea jijini Dar es Salaam mara baada ya kumaliza ziara yake ya siku tano katika mkoani    Tanga. PICHA NA IKULU

Rais Magufuli Agoma Kukaa Madarakani Miaka 20

Image
Rais John Magufuli akiwahutubia  wananchi. amesema hawezi kukaa madarakani kwa miaka 20 kwa kuwa anaheshimu Katiba na kwamba kazi ya urais ni ngumu. Magufuli amesema hayo leo Jumatatu, Agosti 7 katika Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga alipozungumza na wananchi na kuzindua stendi ya kisasa ikiwa ni mwendelezo wa ziara ya siku tano mkoani humo. Kauli hiyo ya Rais imekuja baada ya Mbunge wa Korogwe Vijijini, Steven Ngonyani ‘Prof. Maji Marefu’ (CCM) kusema kwa kuwa Magufuli anafanya kazi nzuri na ingekuwa vizuri akiongezewa hata miaka 20. “Nadhani Profesa Maji Marefu unataka niishi miaka 20 zaidi na siyo kuwa rais kwa miaka 20, sitafanya hivyo kwa kuwa naheshimu Katiba,” alisema Magufuli.

Aveva, Kaburu hali tete

Image
Kesi inayowakabili Rais wa Simba Evans Aveva na Makamu wake Geofrey Nyange 'Kaburu' imehairishwa hadi Agosti 16 mwaka huu kutokana na kuwa upelelezi hujakamilika dhidi yao. Uamuzi huo umetolewa na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu Jijini Dar es Salaam, Victoria Nongwa ambapo washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka matano ambayo mawili kati ya hayo ni ya utakatishaji fedha. Viongozi hao walikamatwa na TAKUKURU miezi miwili iliyopita kutoka sasa wakikabiliwa na mashitaka ya kutakatisha fedha mpaka kupelekea kunyimwa dhamana.

Waziri Mwijage Afunguka Baada JPM Kutoridhishwa na Utendaji Wake

Image
Waziri Mwijage (kulia) akiwa kwenye kipindi cha Clouds 360 kufafanua yaliyosemwa na rais Magufuli jana. Jana (August 6, 2017) Rais Magufuli  alitoa kauli ya kutoridhishwa na hatua zinazochukuliwa na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji dhidi ya watu waliouziwa viwanda na kuvitelekeza ambapo alimtaka Waziri Mwijage kuwanyang’anya na kuwapatia wawekezaji watao viendeleza. Leo August 7, 2017 Waziri wa Viwanda Charles Mwijage amehojiwa kwenye Clouds 360 Clouds TV na kuelezea kuhusu hiyo kauli ya rais na kutoa hizi kauli. ”Kujenga viwanda sio mchezo, yapo maelekezo ya Rais viwanda vilivyo binafsishwa na havitumiki virudishwe, Rais alichokitegemea kwangu sio kile anachokiona sababu viwanda haviendi kwa kasi anayoiona na hii kuna sababu kadhaa.   “Hii sekta ya viwanda ni multi-sector maana kuna viwanda vipo chini ya Wizara ya Mifugo, vingine maliasili…. kuna viwanda vimechukuliwa lakini havipo kwenye orodha ya viwanda vilivyobinafsishwa, nahitaji Wakuu wa mik

RAIS DKT. MAGUFILI AZINDUA STENDI MPYA NA YA KISASA YA MABASI MJINI KOROGWE LEO

Image
 Taswira za Stendi mpya na ya kisasa ya mabasi mjini Korogowe mkoani Tanga ambayo imezinduliwa asubuhi hii na Rais Dkt. John Pombe Magufuli

PENZI LA GWAJIMA, FLORA JIPU PWAA!

Image
Askofu Gwajima. TAKRIBAN miaka miwili iliyopita kuliibuka sarakasi ya aina yake  katika ndoa ya waimba Injili wawili Bongo, Emmanuel Mbasha na Flora Mbasha ambazo zilisababisha mastaa hao kutalikiana mahakamani. Katika sakata hilo, Mbasha alishusha tuhuma nzito zisizobebeka kwamba Flora alikuwa na uhusiano wa kimapenzi (penzi la Gwajima Flora) na baba mchungaji wao ambaye ni Askofu wa Kanisa la Glory of Christ Tanzania Church almaarufu Ufufuo na Uzima, Dk Josephat Gwajima. KIMYA KIREFU Baada ya tuhuma hizo palipita kimya kirefu bila ufafanuzi toshelezi wa skendo hiyo ‘hevi’ lakini kwa mara ya kwanza, Flora amepasua jipu pwaa juu ya ni nini kilichotokea. Kupitia kitabu chake ambacho Ijumaa Wikienda lina nakala yake kilichoingia sokoni wiki iliyopita, pamoja na mambo mengine yasiyoandikika gazetini, Flora alimtuhumu Mbasha kwa mambo mazito ikiwemo hilo la kumpa penzi Askofu Gwajima. TUJIUNGE NA FLORA “Wakati tatizo lile linatokea tulikuwa tunasali kwa As

Mzee wa Upako kumbadili dini Q-Chief?

Image
Msanii wa muziki wa bongo fleva Q Chief ambaye hivi karibuni ameachia ngoma yake mpya ya 'Naogopa', amezungumzia suala la kubadili dini na kuingia kwenye dini nyingine, baada ya kuwa karibu na mchungaji Anthony Lusekelo. Akizungumza na mwandishi wa East Africa Television, Q Chief amezungumzia suala hilo na kusema huwa familia yake upande wa mama ni Wakristo na ana amini katika Mungu, lakini sio rahisi kwake kubadilisha imani yake. "Familia yangu upande wa mama wengi ni wakristo, lakini wamegawanyika kutoka kwenye uislam kwenda ukristo, baba yangu ni muislam, babu yangu ana msikiti kwa hiyo sio jambo jepesi kutoka kwenye dini yangu imani yangu kwenda kwenye imani nyingine, naamini Mungu ndiye jibu sahihi, lakini huwa nachukua ushauri wa viongozi wa dini tofauti tofauti", alisema Q Chief Q Chief aliendelea kwa kuzungumzia kitendo chake cha kuwa karibu na Mchungaji Anthony Lusekelo 'Mzee wa Upako', na kusema Mchungaji huyo ni sawa na ka

Rais Magufuli Amaliza Bifu la Makonda na Ruge Jukwaani

Image
Paul Makonda akishikana mkono na Ruge Mutahaba. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli , amemaliza bifu kubwa lililokuwepo kati ya Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media, Ruge Mutahaba na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kwa kuwakutanisha wawili hao jukwaani na kuwataka washikane mikono. Tukio hilo la aina yake, limetokea kwenye Kijiji cha Chongoleani, Tanga ambapo kulikuwa na tukio kubwa la uwekaji wa jiwe la msingi kwenye mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Hoima, Uganda mpaka kwenye Bandari ya Tanga.

SOL CAMPBELL WA ARSENAL ANATUA DAR LEO

Image
Beki wa zamani wa Arsenal, Sol Campbell. BEKI wa zamani wa Arsenal, Sol Campbell anatarajiwa kutua nchini leo Jumamosi mchana kwa mwaliko wa Kampuni ya Michezo ya Kubahatisha ya SportPesa.Campbell ambaye pia amewahi kuichezea Tottenham Hotspur ya England, akiwa nchini kesho atajumuika na baadhi ya wadau wa soka kutazama mechi ya Ngao ya Jamii kati ya Arsenal na Chelsea.Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Utawala na Utekelezaji wa SportPesa, Abbas Tarimba, akiwa nchini Campbellpia atafanya mafunzo kwa timu ya Magnet kwenye Uwanja wa Gymkhana na kutembelea timu ya Muungano. “Huyu ni nyota wa pili wa zamani wa soka baada ya Leon Osman wa Everton, tunajua bado watu wanakumbuka ujio wa Everton huu ni muendelezo wa kampuni yetu kuleta hamasa ya soka nchini,” alisema Tarimba.Tarimba alisema SportPesa inaendelea kuwapa hamasa ya soka Watanzania kwa ujio wa nyota huyo ukiachana na udhamini iliyoutoa kwa Simba, Yanga na Singida United.

Povu la Ndikumana kwa Uwoya Lachafua Hali ya Hewa

Image
Ndikumana na Uwoya. Mwanasoka wa Kimataifa kutoka Rwanda, Hamad Ndikumana ambaye ni mume wa ndoa wa staa wa filamu za Bongo, Irene Uwoya , amekubali kumpa talaka Irene ili andelee na maisha yake baada ya kutengana muda mrefu huku akieleza kuchoshwa na skendo chafu za mke wake huyo. Kwenye ukurasa wake wa Instagram, Ndikumana ameandika ujumbe akisema amekubali kumpa Irene talaka, hivyo asisubiri hadi afe ili aolewe, ili ampe uhuru anaouhitaji aweze kufanya mambo yake bila yeye kuhusishwa. “Ulilia muda kwamba unataka talaka ili uolewe, sina kipingamizi tafuta kila utakacho ulete nitakusainia, usisubiri nife ili uolewe maana naweza kuishi zaidi ya unavyofikiria, Mungu akusimamie”, aliandika Ndikumana. Wanandoa hao wakitambo wakiwa pamoja. (Picha na Maktaba) Pia Ndikumana amesema kitendo cha Irene kumnyima kuzungumza na mwanae tangu watengane, ni kitendo kinachomuumiza sana, lakini yote anamuachia Mungu. “Ungekuwa na roho ya kibinadamu u

Gwajima Anunua Ndege aina ya JET, Pia kuleta Umeme megawati 250

Image
Baaada ya kimya cha muda mrefu Askofu Mkuu wa kanisa la ufufuo na uzima, Mchungaji Josephat Gwajima ameibuka na kutangaza kuleta ndege aina ya 'Jet' Tanzania kwa ajili ya kutoa huduma kwa watumishi wake. Mchungaji Gwajima ambaye hivi sasa yupo mjini Birmingham, Alabama nchini Marekani kwa shughuli zake za injili na mikutano mbalimbali ameahidi ataleta ndege aina ya 'Jet' "Muda si mrefu nitaleta Tanzania ndege hii 'Jet' kwa lengo la kukuza falme ya Mungu" alisema Gwajima Mbali na hilo Mchungaji Gwajima akiwa katika ziara zake hizo za kiroho alidai kuwa amepata umeme megawati 250 kutoka nchini Ujerumani ambazo anaamini zitasaidia taifa letu la Tanzania katika kukuza sekta ya viwanda. "Nimepata Umeme Megawati 250 kutoka Ujerumani kwa ajili ya Taifa letu katika juhudi za kuunga mkono Tanzania ya Viwanda. Nilimtuma Engineer Mkuu wa Ufufuo na Uzima Duniani Eng.Yeconia Bihagaze huko Ujerumani kufanya ufuatiliaji, Umeme huu ni k

Hii Ndiyo Sababu ya Lowassa Kumpigia Debe Kenyatta

Image
Rais Kenyatta na Edward Lowassa. Zikiwa zimebaki siku mbili nchi ya Kenya kufanya Uchaguzi Mkuu, Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Edward Lowassa amefunguka sababu kuu zinazofanya amtetee na kumnadi mgombea Urais kupitia chama cha Jubilee Uhuru Kenyatta kuwa ni kiongozi shupavu. Lowassa ambaye jana alishiriki katika mkutano wa chama cha Jubilee alisema kuwa kuna watu wanauliza kwanini yeye pamoja na CHADEMA wanamnadi kwa kuwa kiongozi huyo ni shupavu na mpenda watu. “Kuna watu wananiuliza kwanini mnamnadi Uhuru Kenyatta, nasema tena hadharani bila aibu yoyote huyu ni kiongozi shupavu anayependa watu, anaweza kuongoza watu wetu, lakini cha pili Uhuru Kenyatta anapenda Afrika Mashariki akiingia madarakani ataturuhusu tuendelee kuzunguka zunguka kwenye mipaka hii kama Namanga pale bila hata shida, la tatu ni kwamba aliingia madarakani nchi ikiwa kwenye vita lakini amewapa suluhu ameingoza nchi imekwenda taratibu na akafanikiwa” alisema Lowassa. Kenyatta akisim

RWANDA: Rais Paul Aweka Historia Ushindi Urais

Image
Rais Paul Kagame akishangilia ushindi. Tume ya Uchaguzi nchini Rwanda imemtangaza Paul Kagame kuwa mshindi wa urais wa nchi hiyo katika uchaguzi uliyofanyika jana Ijumaa, Agosti 4. Tume hiyo imesema matokeo ya awali yameonyesha kuwa Rais huyo ambaye amekuwa madarakani kwa miaka 17 sasa, atahudumu muhula wa tatu wa miaka saba baada ya kushinda kwa asilimia 98 ya kura zilizohesabiwa. Wafuasi wake wanamsifu Kagame kwa kuonyesha utulivu na maendeleo ya kiuchumi nchini humo baada ya mauaji ya Kimbari ya mwaka 1994 ambapo maelfu ya watu waliuaawa. Kutoka kushoto Paul Kagame, Frank Habineza na Philippe Mpayimana. Wapinzani wa Kagame walikuwa ni Frank Habineza na Philippe Mpayimana ambao amewaburuza vibaya kwenye matokeo hayo ambapo wapinzani hao wamelalamika kuwa wafuasi wao wamepigwa zengwe ndiyo maana imesababisha kuwepo watu wachache katika mikutano yao ya kabla ya kura. Hata hivyo chama tawala kimekana madai hayo. Rais Kagame aliingia madarakani mwa

RAIS DKT MAGUFULI AMWANDALIA RAIS MUSEVENI WA UGANDA DHIFA YA KITAIFA JIJINI TANGA

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Rais Yoweri Kaguta Museveni wakati wa dhifa ya kitaifa aliyomwandalia Ikulu ndogo jijini Tanga. Pamoja nao meza kuu ni Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa na Mama Janeth Magufuli. Hii ikiwa ni bado masaa machache kabla ya uwekaji wa jiwe la Msingi la ujenzi wa mradi mkubwa wa usafirishaji wa Mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda mpaka katika bandari ya Tanga. Sehemu ya mawaziri na manaibu waziri wa Tanzania na Uganda wakiwa wamesimama wakati wa nyimbo za Taifa za nchi hizo mbili na wa Afrika Mashariki kwenye dhifa ya Taifa aliyoandaa Rais Dkt. Magufuli kwa heshima ya mgeni wake Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda Ikulu ndogo jijini Tanga Ijumaa usiku Sehemu ya viongozi mbalimbali wakiwa wamesimama wakati wa nyimbo za Taifa za nchi hizo mbili na wa Afrika Mashariki kwenye dhifa ya Taifa aliyoandaa Rais Dkt. Magufuli kwa heshima ya

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA

Image
Utengenezaji wa sabuni hii una njia nyingi Hatua  ya kwanza Chemsha vipimo 7 vya mafuta ya mawese au mafuta ya shea hadi ifikie hatua ya kimiminika chuja na yaweke kwenye chungu cha mfinyanzi au chombo cha plastiki. Hatua ya pili Pima vipimo 5 vya maji baridi kwenye chombo cha plastiki ongeza kipimo 1cha sodium hydroxide kwa uangalifu mkubwa kwenye maji acha hadi mchanganyiko huo uyeyuke. Subiri mchanganyiko wa sodium hydroxide na mafuta ukaribie kupoa. Hatua ya tatu Taratibu ongeza mchanganyiko wa sodium hydroxide kwenye mawese,huku ukikoroga haraka haraka bila kusitisha ukitumia ubao .hii ni njia nzuri zaidi. Njia ya pili Chemsha mafuta kwenye joto la kadiri ya 55C Changanya maji na sodium hydroxide na uache mchanganyiko huu upoe hadi kufikia joto hilohilo. Baada ya kuandaa mchanyiko wako changanya vimiminika hivyo viwili huku ukikoroga kwanguvu sana kadiri uwezavyo, taratibu sabuni itageuka kuwa laini. Kabla sabuni haijawa ngumu mwaga sabuni ndani ya

NIMEKUWEKEA VICHEKESHO NILIVYOVISIKIA MTAANI: VUNJA MBAVU!

Image
MWALIMU : Alex, simba akianza kukufukuza utafanya nini? Alex: Nitapanda juu ya mti. Mwalimu: Je, na simba naye akipanda juu ya mti? Alex: Nitakimbilia mtoni niogelee. Mwalimu: Je simba naye akikufuata mtoni? Alex: Mwalimu uko upande wangu au wa simba? Maana sikuelewi kabisa, kila ninavyojaribu kumkwepa simba we unamwelekeza niliko, kama hunipendi sema tu. Kama hukuwahi kupata mia darasani usijali, utapata ukiwa unachaji simu. Ukimpa ‘demu’ hela mzazi wake hata hamuulizi, mpe mimba uone, utatafutwa hadi ‘Google’. Kumbe bangi haina madhara… nimetoka kuvuta pafu moja nipo fresh kabisa bila tatizo..saivi nimekaa juu ya tv naangalia makochi. Dua zenu jamani nipo ugenini nimefumwa naongeza maji ya ugali nijitetee vipi? Nimepika ugali ya watu wawili nikakula ya mtu mmoja nikashiba alafu nikatoka nje nikabisha mlango kama mgeni, nikaingia na nikakula iyo ingine! Mwili haijengwi na mbao. Mnamkumbuka yule Subira aliyekuwa anavuta her

WAZIRI MWAKYEMBE AWAPA ‘DAWA’ WASANII BONGO

Image
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe akizungumza na wasanii. Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe  amewataka  Wasanii wa Muziki wa Kizazi   kipya  nchini kuanzisha mfuko wa wasanii kwa lengo la kutatua changamoto ya udhamini inayowakabili. Ameyasema hayo  Jijini Dar es Salaam  katika kikao kazi na Wasanii hao ambacho kilijadili changamoto mbalimbali zinazowakabili na namna ya kukabiliana nazo hivyo kuwataka kutokata tamaa Amesema kuwa kutokana na malalamiko na changamoto mbalimbali zinazowakabili Wasanii, ambazo nyingi zinasababishwa na mikataba inayowanyonya Wasanii katika kazi zao, ni vema sasa Wasanii hao kupitia Chama chao cha Tanzania Urban Music Association (TUMA) kuanzisha mfuko ambao utakua unatoa mikopo kwa Wasanii ili kuwezesha utendaji wa kazi zao pasipo kutegemea wadhamini. Dkt. Mwakyembe akisalimiana na wasanii. “Ninafikiri dawa tunayohitaji ni kuanzishe mfuko wa Wa

Ofisa wa tume ya uchaguzi ya Kenya aliteswa na kunyongwa

Image
Uchunguzi uliofanywa kwenye mwili wa aliyekuwa mkuu wa idara ya Tehama ya tume ya uchaguzi ya Kenya Bw Chris Msando, umeonyesha kuwa aliteswa na kuuawa. Kwa mujibu wa mwanapatholojia mkuu wa serikali Dk Johansen Oduor na daktari wa familia Dk Bessie Byakika, mwili wa Bw Msando umeonesha kuwa wauaji walitumia mikono kumnyonga na pia walimpiga na kitu chenye ncha kali na kumsababishia jeraha. Matokeo ya uchunguzi wa kipatholojia umekuwa ni msingi wa uchunguzi kufuatia kifo chake, na tayari watu watatu wametiwa mbaroni kuhusiana na kifo cha Bw Msando, lakini bado haijulikani walihusika vipi na kifo chake. Mwili wa Bw Msando pamoja na wa msichana mwanafunzi mwenye umri wa miaka 21 uliokotwa jumamosi kwenye msitu wa viunga vya Nairobi.

Sakata la Acacia, Bangi Vyawaweka Matatani Wabunge Wawili wa Mara

Image
John Heche. Mbunge wa Tarime Vijijini John Heche anashikiliwa na Jeshi la Polisi Tarime, huku Mbunge wa Tarime Mjini Esther Matiko naye akisakwa. John Heche amekamatwa na kushikiliwa na Jeshi hilo kwa madai alizungumza bungeni kuhamasisha wananchi kuzuia shughuli za kampuni ya ACACIA huko Nyamongo, North Mara.   Esther Matiko. Jeshi hilo pia linadai Heche kupitia mkutano wa hadhara alisema atapeleka hoja bungeni ili bangi ihalalishwe kuuzwa nje ya nchi, Polisi wanasema kauli hiyo inachochea ulimaji bangi. Halikadhalika linamsaka Esther Matiko ili kumuunganisha katika madai hayo kuwa alizungumza katika mkutano huo kauli zinazochochea kilimo cha bangi. Polisi wamechukua simu za alizokuwa nazo, pia wameagiza simu nyingine iliyopo Dar es salaam kwenye matengenezo pia ipelekwe Tarime. -Makene