Povu la Ndikumana kwa Uwoya Lachafua Hali ya Hewa

Ndikumana na Uwoya.

Mwanasoka wa Kimataifa kutoka Rwanda, Hamad Ndikumana ambaye ni mume wa ndoa wa staa wa filamu za Bongo, Irene Uwoya, amekubali kumpa talaka Irene ili andelee na maisha yake baada ya kutengana muda mrefu huku akieleza kuchoshwa na skendo chafu za mke wake huyo.
Kwenye ukurasa wake wa Instagram, Ndikumana ameandika ujumbe akisema amekubali kumpa Irene talaka, hivyo asisubiri hadi afe ili aolewe, ili ampe uhuru anaouhitaji aweze kufanya mambo yake bila yeye kuhusishwa.
“Ulilia muda kwamba unataka talaka ili uolewe, sina kipingamizi tafuta kila utakacho ulete nitakusainia, usisubiri nife ili uolewe maana naweza kuishi zaidi ya unavyofikiria, Mungu akusimamie”, aliandika Ndikumana.
Wanandoa hao wakitambo wakiwa pamoja. (Picha na Maktaba)

Pia Ndikumana amesema kitendo cha Irene kumnyima kuzungumza na mwanae tangu watengane, ni kitendo kinachomuumiza sana, lakini yote anamuachia Mungu.
“Ungekuwa na roho ya kibinadamu ungekuwa unataka hata niwasiliane na mtoto, ila miaka miwili hujawahi chukua simu unipigie umpe mtoto niongee naye, hata picha tu hutaki nitumia ila naelewa kwa nini unafanya hivyo, na baada ya yote haya hutotaka nimuone tena, lakini ni sawa Mungu yupo na ipo siku”, aliendelea kuandika Ndikumana.
Irene na Ndikumana walifunga ndoa mwaka 2009 na kufanikiwa kupata mtoto mmoja wa kiume, lakini ndoa yao haikudumu muda mrefu na kutengana, hivyo sasa Ndikumana ameonyesha kuridhia kutoa talaka kwa msanii huyo wa bongo movie.
ALICHOKIANDIKA NDIKUMANA
 

Comments

Popular posts from this blog