Kocha wa timu ya taifa ya Ubelgiji asema Samatta anauwezo wa kucheza ligi kuu Uingereza
Kocha wa timu ya taifa ya Ubelgiji Roberto Martinez amekiri kuwa, mshambuliaji na nahodha wa Taifa Stars Mbwana Samatta ana-ubora wa kucheza ligi kuu ya England maarufu kama EPL. Shaffihdauda ilifanya juhudi za kumtafuta kocha huyo ambaye amewahi kufundisha soka England katika vilabu vya Wigan kabla haijashuka daraja pamoja na Everton kabla ya kupewa majukumu ya kuifundisha timu ya taifa ya Ubelgiji. Juhudi zilifanywa na Mbwana Samatta kuiunganisha shaffihdauda.co.tz na Martinez, hatimaye kocha huyo akatoa ushirikiano. Martinez amesema, Samatta ni mshambuliaji mwenye kiwango kikubwa na uwezo wa kucheza soka kwenye ligi yoyote ikiwemo EPL, pia amesema ameongea na kushauriana vitu vingi na Samagoal. Shaffihdauda.co.tz: Umeshawahi kumshuhudia Samatta akiwa uwanjani akiitumikia klabu yake ya Genk? Martinez: Mimi ni kocha wa timu ya taifa ya Ubelgiji kwa hiyo nafatilia kwa karibu sana ligi za hapa kwa hiyo nimeshamuona mara kadhaa akiwa uwanjani.