Posts

BREAKING NEWSS: BAADA YA JPM KUWA MWENYEKITI CCM,ZITTO ATOA UJUMBE HUU DHIDI YAKE

Image
KATIKA hali isiyo ya kawaida,Kiongozi wa chama cha ACT- Wazalendo leo hii muda mfui tu mara baada ya Rais Magufuli kutangazwa kuwa Mwenyekiti wa tano wa CCM,aliasambaza ujumbe mzito mitandaoni kuhusu hatua hiyo. Zitto ambaye mara kadhaa amekuwa akisikika kumtuhumu JPM kuwa ni Dikteta,aesambaza ujumbe huo wenye lengo la kumpongeza Dr JPM  na kuhaidi kuwa atampa ushirikiano ote unaohitajhika katika kuboresha siasa ya tanzania. Facebook Comments

Mlipuko Waua 80 Afghanistan

Image
Wizara ya afya  nchini Afghanistan imesema takribani watu 80 wameuawa na zaidi ya wengine 150 kujeruhiwa katika shambulio la kujitoa mhanga lililofanyika kwenye Mji Mkuu Kabul. Baadhi ya taarifa zinasema kulikuwa na milipuko miwili. Shambulio hilo linaonyesha kuwa lililenga maandamano ya maelfu ya watu kutoka jamii ndogo ya Hazara, ambao hujikuta wakidhalilishwa na kufanyiwa ukatili. Walikuwa wakiandamana kupinga mpango wa serikali wa kuhamisha umeme kutoka kwenye majimbo yao katikati ya nchi.

WOLPER AREJEA CCM

Image
Wolper akitangaza sababu za kurejea CCM. Wolper akiongea na Mwenyekiti Mstaafu Mhe. Jakaya Kikwete. Wolper akiongea wakati wa hafla ya wasanii ya kumuaga Mwenyekiti Mstaafu Mhe. Jakaya Kikwete. Na Leonard Msigwa/GPL MWANADADA gumzo kwenye tansia ya Bongo Movie nchini, Jacqueline Wolper hatimaye jana ametangaza rasmi kurejea Chama Cha Mapinduzi (CCM). Wolper ambaye alikuwa kada wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na mfuasi mkubwa wa aliyekuwa mgombea urais wa chama hicho na Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Ngoyai Lowassa alitangaza uamuzi huo wakati wa hafla ya wasanii ya kumuaga Mwenyekiti Mstaafu Mhe. Jakaya Kikwete mjini Dodoma. Baada ya kupewa nafasi kuongea, Wolper alikuwa na haya; “Nilipotea kwenda kule, nimeamua kurudi nyumbani” Ikumbukwe kwamba Wolper alikuwa mstari wa mbele miongoni mwa wasanii wa kike nchini kumpigia debe bila kificho Edward Lowassa wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka jana na alienda mbali zaidi kwa kumwita Edward Lowassa kam

Msindai arudi CCM

Image
Mgana Msindai (kulia) akiongea jambo. ALIYEKUWA Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida na baadaye kuhama chama na kujiunga na Chadema, Mgana Msindai amerudi CCM leo.  Mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman  Mbowe alipokuwa akimkabidhi kadi Mgana Msindai (katikati). Msindai alitangaza uamuzi huo leo mjini Dodoma baada ya kupewa nafasi na Mwenyekiti Mstaafu wa CCM, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete wakati anaendesha mkutano mkuu wa CCM uliomchagua Rais Dk John Magufuli kuongoza chama. Msindai alisema aliamua kurudi CCM baada ya kuona hakuna cha kupinga baada ya Rais Magufuli kuchaguliwa kuwa rais wa nchi. Msindai aliingia Chadema baada ya aliyekuwa mgombea wa Ukawa, Edward Lowassa kujiunga na Chadema mwaka jana wakati wa uchaguzi mkuu.

Rais Magufuli avunja rekodi ya Uchaguzi wa Mwenyekiti wa CCM Taifa

Image
Dodoma Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amevunja rekodi baada ya kutangazwa kuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa kwa kupata asilimia 100 ya kura zote zilizopigwa. Rekodi hiyo ya kupata asilimia 100  ya kura zote kwenye uchaguzi wa aina hiyo (Uenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Taifa) haijawahi kufikiwa na kiongozi yeyote ndani ya CCM tangu kuanzishwa kwa chama hico Februari 5, 1977 ambapo ni miaka 39 sasa. Wenyeviti wa CCM waliyopita ambao ni Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Ali Hassan Mwinyi, Benjamin William Mkapa wala Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete hawakuwahi kupata kura zote zilizopigwa kwenye uchaguzi wa ngazi hiyo. Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo uliyofanyika mjini Dodoma leo, Mwenyekiti wa CCM aliyemaliza muda wake, Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amesema matokeo kuwa; ifuatavyo Kura zilizopigwa zilikuwa ni 2398, kura halali ni 2398, kura zilizoharibika ni 0, kura za hapana ni 0 na kura za Ndiy

NITAHAKIKISHA SERIKALI INAHAMIA DODOMA :RAIS MAGUFULI

Image
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Rais Dk. Jakaya Kikwete akizungumza na wajumbe wa mkutano mkuu maalum wa CCM uliofanyika mjini Dodomabaada ya kuchaguliwa kwa kupigiwa kura za kishindo leo, kulia anayecheka ni Mwenyekiti mstaafu wa CCM Mzee Benjamin Williamo Mkapa.. Na. Immaculate Makilika- Dodoma Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  amesema katika kipindi cha uongozi wake atahakikisha Serikali inahamishia makazi yake mjini Dodoma. Amesema hayo leo, wakati alipokuwa  akihutibia wajumbe  wa Chama cha Mapinduzi(CCM) katika Mkutano Mkuu Maalumu  wa  Chama hicho uliofanyika  mjini Dodoma mara baada ya kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti. “Nitahakikisha katika awamu ya uongozi wangu, Serikali inahamia Dodoma, najua viongozi wengine wote nao watanifata, kwa kuwa sasa miundombinu ya Dodoma inaweza kukidhi mahitaji yote” alisema Rais Magufuli. Rais Magufuli aliendelea kusema kuwa katika kipindi cha miezi nane ya uongozi wake chini ya Serikali ya

JK AKABIDHI RASMI KIJITI CHA UENYEKITI KWA DKT JOHN POMBE MAGUFULI JIONI YA LEO MJINI DODOMA

Image
 Mwenyekiti aliyemaliza Muda wake Dkt Jakaya Kikwete pamoja na Mwenyekiti mpya wa chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt John Pombe Magufuli wakiwapungia mkono Wajumbe wa mkutano Mkuu Maalum mara baada ya matokeo kutangazwa rasmi na Dkt John Pombe Magufuli kuibuka kwa kura zote za ndio ziapatazo 2398 na hakuna kura zilizokuwa zimeharika. Mwenyekiti Mstaafu Dkt Jakaya Kikwete akimkumbatia Mwenyekiti Mpya,Rais Dkt John Pombe Magufuli mara baada ya kutangazwa rasmi kuwa Mwenyekiti wa chama hicho kwa miaka kumi.   Mwenyekiti aliyemaliza muda wake leo,Rais wa awamu ya nne Dkt Jakaya Kikwete akimkabidhi vitendea kazi mbalimbali vya chama cha Mapinduzi (CCM),Mwenyekiti Mpya,Rais Dkt John Pombe Magufuli aliyepigiwa kura na Wajumbe wa Mkutano Mkuu maalum na kuibuka na kura zote za ndio kutoka kwa Wajumbe 2398 na hakuna kura zilizokuwa zimeharika  Makamu Mwenyekiti-Zanzibar Dkt Shein akimpongeza Mwenyekiti Mpya,Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa kuteuliwa kuw

Lowassa na Sumaye Wapewa MAKAVU Ndani ya Mkutano wa CCM .........Mpendazoe Ahamia CCM, Mrema Alalama Kuitwa CCM B

Image
VIGOGO mashuhuri wa Chadema waliowahi kuwa mawaziri wakuu; Edward Lowassa na Frederick Sumaye, jana waligeuka gumzo ndani ya Mkutano Mkuu Maalumu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa kumchagua Rais John Magufuli, kuwa Mwenyekiti wa tano wa chama hicho. Gumzo hilo, lilianzishwa na Katibu Mkuu wa zamani wa CCM, Yusuf Makamba, alimpomtaka Askofu wa Kanisa la Ufufuko na Uzima, Josephat Gwajima, asimpotoshe Magufuli ili yasije yakampata ya Sumaye, ambaye sasa anachezea mchangani Kibaha. Sumaye mchangani “Hata akina Sumaye hawakuunda vyama vyao. Bado wanahangaika; na sasa Sumaye anacheza mchangani Kibaha,”  alisema Makamba. Sumaye ambaye aliwahi kuwa mjumbe wa Kamati Kuu na NEC ya CCM, kwa sasa anawania uongozi wa Kanda ya Pwani katika Chadema. Kabla ya kusema kuwa Sumaye anahangaika na siasa za mchangani, Makamba alimtaka Gwajima kuacha uongo na kusingizia viongozi wa CCM. Makamba aliyepewa nafasi ya kumuombea kura Rais John Magufuli kwa wajumbe wa Mkut

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AZUNGUMZA NA WAJUMBE WANAWAKE WA MKUTANO MKUU WA CCM MJINI DODOMA

Image
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wajumbe Wanawake wa Mkutano Mkuu wa CCM mjini Dodoma ambapo aliwasihi kuendelea kudumisha umoja na mshikamano pamoja na kujishughulisha na shughuli mbali mbali za kiuchumi na kujiunga na Mabaraza mbali mbali ya kuwezesha wanawake.  Baadhi ya Wajumbe walishindwa kujizuia na kuamka kwa shangwe na vifijo.  Mke wa Mwenyekiti wa CCM na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo pia ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM ,wilaya ya Lindi Mama Salma Kikwete akizungumza na Wajumbe Wanawake wa Mkutano Mkuu wa CCM mjini Dodoma .  Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Dk. Tulia Ackson akungumza kwenye mkutano uliowakutanisha Wajumbe Wanawake wa Mkutano Mkuu wa CCM pamoja na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan mjini Dodoma. Sehemu ya Wajumbe waliohudhuria. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tan

Matukio Yanayoendelea Mkutano Mkuu wa CCM, Dodoma

Image
Sehemu ya Meza kuu kama ionekanavyo pichani tayari wamekwisha ingia ndani ya ukumbi wa Dodoma Convetion Center (DCC) kukamilisha mchakato wao wa kumchagua Mwenyekiti mpya wa chama hicho cha CCM.Pichani kulia ni Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana,Mwenyekiti wa CCM ambaye leo anatarajiwa kukabidhi kijiti kwa Mwenyekiti Mpya,Rais wa awamu ya nne Dkt Jakaya Kikwete,Makamu Mwenyekiti Zanzibar Rais Dkt Shein pamoja na Mwenyekiiti mtarajiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli. Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitoa ratiba na miongozo mbalimbali kwa Wajumbe wapatao zaidi ya 2000 wa mkutano Mkuu Maalum wa CCM ambao tayari wako ndani ya ukumbi wa Dodoma Convetion Center (DCC) kukamilisha mchakato wao wa kumchagua Mwenyekiti mpya wa chama hicho cha CCM. Mwanana mahiri wa nyimbo za Taarab kutoka kundi la Tot Plus Khadija Kopa akiimba mbele ya Wajumbe wapatao zaidi ya 2000 wa mkutano Mkuu Maalum wa CCM ambao tayari w

Taarifa Kuhusu Kufunguliwa kwa Mfumo wa Udahili wa Pamoja NACTE

Image
  Baraza linapenda kutoa taarifa kuwa Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) umefunguliwa tena kuanzia tarehe 22 Julai 2016 ili kujaza nafasi za udahili zilizo wazi baada ya Baraza kuchagua waombaji udahili waliowasilisha maombi yao kuanzia tarehe 4 Machi 2016 hadi tarehe 3 Juni 2016. Mwisho wa kuwasilisha maombi ni  tarehe 5 Agosti 2016 saa sita usiku. Waombaji wapya na baadhi ya waombaji walioshindwa kukamilisha maombi yao kupitia mtandao ilipofika tarehe 3 Juni 2016, wanaarifiwa kuanza kuwasilisha maombi ya udahili kupitia Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) ili kujaza nafasi zilizo wazi. Waombaji wanahimizwa kutumia muda huu wa nyongeza ili kuwasilisha maombi. Baraza linapenda pia kuwaarifu waombaji udahili na umma kwa ujumla kuwa vikao vya Kamati za kuidhinisha majina ya waombaji udahili kupitia Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) vilipitisha orodha ya majina  ya wenye sifa za udahili kulingana na nafasi za udahili kwa kila kozi zitolewazo na vyuo husika kat

Vigogo wote Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) Watumbuliwa MAJIPU

Image
SERIKALI imemuondoa katika nafasi yake Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Misitu Tanzania (TFS), Gerald Kamwenda na wakurugenzi wenzake, katika jitihada za kufumua na kusuka upya shirika hilo. Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe, ametangaza hatua hiyo ya serikali jana alipokutana na vyombo vya habari na kuongeza kuwa, watumishi wengine 41 wamehamishwa vituo vya kazi. Alifafanua kuwa hatua hizo ni sehemu ya utekelezaji wa agizo la Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, lililotaka kufumuliwa na kusukwa upya kwa TFS ili kuongeza ufanisi. Kutokana na hatua hiyo, Waziri Maghembe alisema Profesa Dos Santos Silayo ameteuliwa kuwa Kaimu Mtendaji Mkuu wa TFS, wakati Kamwenda anahamishiwa Chuo cha Viwanda vya Misitu kilichopo Moshi. Aidha, Mwanaidi Kijazi aliyekuwa Mkurugenzi wa Usimamizi wa Raslimali za Misitu na Nyuki, yeye amekwenda kuwa Mhifadhi Mkuu Amani Nature Reserve na nafasi yake inachukuliwa na Zawadi Mbwambo. Waziri Maghembe alisema