Posts

BREAKING NYUZZZZZ...WAFANYAKAZI HEWA WAMPONZA MKUU WA MKOA WA SHINYANGA,MAMA ANNA KILANGO, RAIS DKT. MAGUFULI ATENGUA UTEUZI WAKE

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, mchana huu ametengua uteuzi wa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mama Anna Kilango Malecella, kwa kubaini kuwa alimwambia uwongo kuwa Mkoa wake hauna wafanyakazi hewa wakati kumbe wapo wengi tu. Rais Magufuli amesema kwamba hakuamini kwamba kuna mkoa ambao hauna wafanyakazi hewa, hivyo akatuma kikosi kazi ambacho hadi usiku wa kuamkia leo kimebaini kuwepo na wafanyakazi hewa 45 mkoani Shinyanya. Rais Magufuli, ambaye alikuwa anaongea baada ya kupokea Ripoti ya TAKUKURU  toka kwa Mkurugenzi wake Mkuu  Valentino Mlowola,  amesema kasikitishwa sana na kauli ya Mama Malecela ambaye bila shaka alikuwa amepata ushauri mbaya toka kwa watendaji wake.  Amesema idadi hiyo ya wafanyakazi hewa mkoani Shinyanga huenda ikaongezeka zaidi kwani wilaya mbili zilikuwa bado zinaendela kuhakikiwa. Rais Magufuli amesema pia kwamba hadi jana jumla ya wafanyakazi hewa zaidi ya 5, 507 wamebainika nchi nzima, wengi wao w

Msanii Mwigine wa Bongo Anayeteketea Kwa Madawa ya Kulevya Huyu Hapa....

Image
Wauza unga kuweni na huruma kwa watanzania wenzetu,yule Dogo Mfaume wa enzi zile za "kazi yangu ya dukani" ndo basi tena sasa hivi kashakua teja....daah vipaji vya ukweli vinazidi kupotea kwa ngada. Mlaaniwe wote mnaouza unga kuanzia nyie wenyewe na vizazi vyenu vyote. ..."kazi yangu ya dukanii aaahahh yaniweka matataniii wanao nirudisha nyuma wengi wao majiraniii"

Msafara wa Rais Magufuli Kutozidi watu 10.....Balozi Mahega Asema Anategemea Kwenga Ng'ambo hivi Karibuni

Image
Rais John Magufuli anataraji kusafiri tena kwenda nje ya nchi hivi karibuni akiwa na msafara ambao unawezekana usizidi jumla ya watu 10. Ilimchukua Rais Magufuli siku 153 tangu kuapishwa kwake kufanya ziara ya kwanza ya nje ya nchi baada ya kwenda Rwanda kwa mwaliko wa Rais Paul Kagame Jumanne iliyopita. Rais alikwenda Rwanda kwa ajili ya kufungua daraja la kimataifa la Rusumo na kituo cha biashara chenye huduma za pamoja, ambacho ni kiunganishi muhimu kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Katika safari hiyo, katika kile kinachoonekana kuwa ni muendelezo wa hatua yake ya kubana matumizi ya serikali kadri iwezekanavyo, Rais Magufuli alikuwa na msafara usiozidi watu 10. Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ushirikiano wa Kikanda na Kimataifa, Balozi Augustino Mahiga, alisema jana kuwa Rais Magufuli anatarajia kusaifiri tena kwenda nje ya nchi hivi karibuni. Balozi Mahiga alisema katika safari hiyo, msafara wake utaendelea kuhusisha watu wachache w

Mrema wa TLP Amuomba Rais Magufuli Atimize Ahadi yake ya Kumpa KAZI Kama Alivyokuwa Amemwahidi Wakati wa Kampeni

Image
Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour (TLP) taifa, Augustine Mrema amemuunga mkono Rais John Mgufuli kwa kasi yake ya kupambana na ufisadi na kumuomba ampe kazi ili amsaidie kutekeleza jukumu hilo. Mrema alimuomba Rais Magufuli atambue uzoefu wake kwa kukumbuka jinsi alivyopambana na mafisadi wakati akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani na Naibu Waziri Mkuu. Huku akieleza CV yake hiyo, Mrema alimkumbusha Rais kuhusu ahadi aliyompa wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka jana, ya kumpa kazi katika Serikali ya Awamu ya Tano ikiwa atashinda na kuwa Rais. Akizungumza na waandishi wa habari kijijini kwake Kiraracha mkoani Kilimanjaro, Mrema alisema kuwa anasikitishwa na ukimya wa Rais Magufuli kwa sababu aliamini kuwa angetekeleza ahadi hiyo ya kumpa kazi muda mfupi baada ya kutangaza Baraza la Mawaziri, jambo ambalo hadi sasa hajalifanya. Alisema, alikutana na Rais Magufuli mwaka jana katika kampeni jimboni Vunjo kwenye eneo la Njia Panda l

Huyu Ndiye Rubani wa Kwanza Mwanamke Tanzania Kurusha Boeing Airbus

Image
KATI ya wanawake wa Kitanzania waliopeperusha bendera yetu vizuri nje ya nchi kielimu ni Kapteni Hilda Wendy Ringo ambaye sasa ni rubani. Elimu yake ya sekondari aliipata katika Shule ya Tambaza jijini Dar es Salaam na baadaye Chuo Cha Urubani cha Progress Flight Academy cha jijini Pretoria, Afrika Kusini. Ni mwanamke wa kujivunia katika nchi yetu kwa sababu amekuwa akirusha ndege yaani rubani. Amewahi kuhojiwa na vyombo mbalimbali vya habari nchini na kuhusu kazi yake hiyo anasema: “Kurusha ndege ni jambo zuri linalofurahisha.” Rubani Hilda ni mama mwenye umri wa miaka 33, anasema alianza kurusha ndege akiwa na umri wa miaka 22 lakini sasa anarusha ndege hapahapa nchini katika Kampuni ya Precision Air. Ana uzoefu mkubwa na kazi hiyo ya urubani kwa sababu ameifanya kwa zaidi ya miaka 10 sasa na ni mwanamke wa kwanza Mtanzania kurusha ndege aina ya Boeing Airbus. Anasema wazo la kuwa rubani lilimuingia katika akili yake akiwa bado mdogo baada ya kujiuliza m

Waziri Mkuu Majaliwa ashiriki mazishi ya kaka yake

Image
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiweka udongo kwenye kaburi la kaka  yake, Selemani Selemani katika mazishi yaliyofanyika kwenye kijiji cha  Narung’ombe wilayani Ruangwa Aprili 9, 2016.

WAZIRI MKUU MAJALIWA ATEMBLEA HOSPITALI YA BENJAMINI MKAPA

Image
Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akikagua mashine ya MRI katika hospitali ya Benjamin Mkapa kwenye Chuo Kikuu cha Dodoma wakati alipoitembela Aprili 9, 2016. Wapili kushoto ni Naibu Waziri wa Afya, , Dkt. Hamis Kigwangala. Waziri Mkuu, Kassim Majliwa na Naibu Waziri wa Afya Dkt. Khamis Kigwangala wakikagua mashine ya Mobile Digital xray wakati walipotembelea hospitali ya Benjamin Mkapa kwenye Chuo Kikuu cha Dodoma Aprili 9, 2016.Kulia ni Kaimu Mkuu wa Hospitali hiyo ProfesaGesai. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 

Mambo 8 Muhimu Kuhusu Huduma Mpya ya WhatsApp

Image
KUTOKANA na tatizo la kuingiliwa kwa mawasiliano ya watumiaji wa WhatsApp, hivi karibuni kampuni hiyo ilianzisha huduma ya  end-to-end encryption ili kuboresha huduma zao za mawasiliano hasa katika nyanja ya kuimarisha ulinzi wa mawasiliano ya wateja wao. 1. End-to-end encryption ni nini? Hii ni huduma mpya ya WhatsApp inayotumiwa kwa ajili ya kulinda mawasiliano baina ya mtumaji na mpokeaji kwenye mtandao huo bila mtu wa kati kuingilia mawasiliano hayo. huduma hii pia inapatikana iwapo mtumianji wa ataingiza toleo jipya la WhatsApp. Inatumika kwenye simu zote za iOS na Android. 2. Unawezaje kuwezesha (activate ) huduma hii? Haya yote yanafanyika kwa mfumo kujiendesha wenyewe (automatically), hauhitaji kufanya mpangilio (setting) ili kuwezesha usiri wa mawasiliano yako. 3. Je, huduma hii pia inahusisha upigaji simu wa kwenye WhatsApp call? Ndiyo, kama meseji zako zinalindwa hata WhatsApp calls pia zinalindwa kwa mfumo wa end-to-end encryption ambapo m

SPIKA JOB NDUGAI AKUTANA NA WATAFITI TOKA WASHINGTON DC-MAREKANI.

Image
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Job Ndugai (kulia) akizungumza na Bwana Tye Ferrell kutoka Shirika la Utafiti la Tetra Technology lililopo nchini Washington DC Marekani, pamoja na Makamu Mkuu wa Chuo cha Dar es Salaam, Profesa Rwekaza Mkandala (katikati) wakati walipomtembelea ofisini kwake Jijini Dar es Salaam 08 Aprili, 2016. Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Job Ndugai (kulia) akimweleza jambo Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Rwekaza Mkandala (katikati) wakati wa mazungumzo katika ofisi ya Mhe. Spika jijini Dar es Salaam leo 08 Aprili, 2016. Mtafiti toka Shirika la Utafiti la Tetra Technology lililopo nchini Washington DC Marekani Bwana Tye Ferrell akimweleza jambo Mhe. Spika Job Ndugai (hayupo pichani) wakati wa mazungumzo katika ofisi ya Mhe. Spika jijini Dar es Salaam leo 08 Aprili, 2016. Watafiti kutoka Shirika la Utafiti lililopo Washington DC-Marekani Bwana Patrick McGoven (kushoto

Dkt. Shein Atangaza Baraza Lake la Mawaziri

Image
Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dkt. Ali Mohamed Shein RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dkt. Ali Mohamed Shein leo Jumamosi, April 9, 2016 ametangaza Baraza la Mawaziri litakalosimamia kazi za serikali kwa kipindi cha uongozi wake wake kwa mujibu wa sheria. Dkt. Shein amesema amepunguza ukubwa wa baraza hilo kutoka wizara 16 hadi kuwa wizara 13 zenye Mawaziri ni 13 na Manaibu waziri 7, ambapo wizara tatu amezivunja na kuzigawa ndani ya hizo wizara 13 za sasa. Ameongeza kuwa, mawaziri aliowatangaza leo atawaapisha kesho Jumapili asubuhi katika Viwanja vya Ikulu visiwani Zanzibar. Baraza la Mawaziri Zanzibar hao ni; 1). Ofisi ya Rais na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi – Issa Haji Ussi Gavu. 2). Katiba na Sheria Utumishi wa Umma – Haroun Ali Sleiman. 3). Tawala za Mikoa na Idara maalum – Haji Omari Kheir. 4). Makamo wa 2 wa Rais – Mohd Aboud. 5). Waziri wa Fedha na Mipango – Dk. Khalid Salum Mohd. 6). Afya – Mahmoud Thabit Kombo. 7)

SHAMSA FORD AMSEKWA RUMANDE MZAZI MWENZIE,MAZITO YAFICHUKA

Image
Staa wa filamu Bongo, Shamsa Ford. NA IMELDA MTEMA, Risasi Jumamosi STAA wa filamu Bongo, Shamsa Ford juzikati amemsweka lupango mzazi mwenziye Dick Matoke, katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay kwa kile kinachodaiwa kuwa mzazi mwenzake huyo kuwa na tabia ya kumtukana mara kwa mara akishirikiana na mpenzi wake wa sasa ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja. Kwa mujibu wa chanzo makini, Dick na mwanamke wake wa sasa wamekuwa wakimtumia meseji za matusi Shamsa kitendo ambacho mwigizaji huyo alikuwa akikivumilia lakini katikati ya wiki hii, uvumilivu ukamshinda, akaamua kwenda kumshtaki. “Yaani hakuna kitu ambacho Shamsa alikuwa hakipendi kama kutumiwa meseji na mzazi mwenzake huyo na mwanamke wake zikimtusi kwa maana alivumilia mpaka akachoka, akaona bora aende polisi kumshtaki,” kilisema chanzo.   Shamsa Ford enzi akiwa na mzazi mwenziye Dick Matoke.   Chanzo hicho kilizidi kueleza kuwa, baada ya kwenda polisi na kufungua mashtaka yaliyosomeka; OB/RB/6522/2

SABABU ZA RAIS MAGUFULI Kwanini Hapendi Sana Kusafiri Nje ya Nchi

Image
Tunajua Rais Magufuli amekuwepo nchini Rwanda kwa ziara ya siku mbili kuanzia April 6 2016 mpaka April 7 jioni aliporudi Tanzania, kwenye moja ya maongezi yake mbele ya Wananchi wa Rwanda ameongea pia kuhusu kwanini hapendi kusafiri nje ya nchi na toka achaguliwe October 2015, amesafiri nje ya nchi kwa mara ya kwanza April 2016. ‘Nataka niwaeleze ndugu zangu, mimi sipendi sana kusafiri kwasababu ninapenda kubana matumizi… nimealikwa sehemu nyingi nimealikwa Ulaya lakini na sehemu nyingine bado sijaenda, nilipoalikwa na Muheshimiwa Kagame nimekuja na ninataka niwaeleze ndugu zangu wa Rwanda hii ndio safari yangu ya kwanza kutoka nje ya Tanzania‘ – Rais Magufuli" .

DIAMOND PLATINUMS YAMKUTA MAZITO,MASHEHE WAMJIA JUU,GUMZO KILA KONA

Image
  NA mwandishi wetu, Risasi Jumamosi Dar es Salaam: Kitendo cha kuposti picha inayomuonesha akiwa ametoboa pua na kuvaa kipini kilichofanywa na staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kimemfanya yamkute mazito kufuatia mashehe kumjia juu na kuwa gumzo. Gumzo lilianza juzikati baada ya Diamond kutupia picha kwenye akaunti yake ya Instagram, ikimuonesha akiwa amevaa kipini, kama wafanyavyo wanawake, kitendo kilichoamsha mjadala mkubwa kwa mashabiki na wadau mbalimbali wa muziki wake. Wapo waliomuunga mkono kwa maelezo kwamba hakuna mtu anayepaswa kumuingilia kwa sababu hayo ni maisha yake binafsi, huku wengine wakienda mbele kwa kuwatolea mfano mastaa wengine wakubwa duniani kama Chris Brown, Wiz Khalifa, marehemu 2Pac na wengineo kwamba nao waliwahi au wametoboa pua. Hata hivyo, kundi jingine kubwa, lilimjia juu msanii huyo na kumtaka kuacha kuiga mambo yanayofanywa na wasanii wa Ulaya na Marekani na badala yake, awe kioo cha jamii kwa kuenzi na kudumisha

KUHUSU SAKATA LA WALIMU KUANZA KUVAA SARE,WIZARA YA ELIMU YATOA UFAFANUZI HUU..!!

Image
WIZARA ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi imekanusha taarifa inayosambazwa katika mitandao ya kijamii kuwa Waziri wake Profesa Joyce Ndalichako ametaka walimu kuandaliwa sare. Taarifa iliyotolewa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini inasema kuwa taarifa hizo si za kweli na kuwaonya watu wanaotoa taarifa za uzushi kuacha mara moja. Imesema imejipanga kuhakikisha inachukua hatua za kisheria kwa watakaobainika kuanzisha na kueneza uzushi huu. “Tunapenda kuufahamisha umma kuwa taarifa hizi si za kweli. Watu wanaoeneza taarifa za kizushi za aina hii waache kufanya hivyo ili kuepusha usumbufu unaojitokeza,” ilisema taarifa hiyo. Taarifa zilizokuwa zimeenea kwenye mitandao zinasema kuwa Profesa Ndalichako amesema nguo kwa ajili ya walimu zinaandaliwa ambazo zitakuwa aina tatu. Sare hizo zitakuwa ni mashati matatu meupe yenye nembo ya taifa, suruali na sketi zitakuwa za rangi ya bluu, kijani na kaki na kofia yenye nembo ya taifa. Ilidai mwongoz

KIGOGO WA WEMA SEPETU NA KAJALA ,CK ANASWA LIVE AKICHOMA NA KUUZA MISHIKAKI

Image
Dar es Salaam: Upepo umebadilika! Aliyekuwa kigogo serikalini katika idara nyeti kabla ya ‘kutumbuliwa’ na kufikishwa  Mahakama ya Kisutu jijini Dar kwa tuhuma za kughushi hundi na kujichotea fedha kwenye Ofisi ya Waziri Mkuu ambaye aliwahi kudaiwa kuwa mwandani wa staa wa Bongo, Wema Isaac Sepetu, Clement Kiondo ‘CK’ au Kigogo wa Wema amenaswa laivu akichoma na kuuza mishikaki. RISASI JUMAMOSI LAPEWA ‘UBUYU’ Hivi karibuni, Gazeti la Risasi Jumamosi lilipokea simu kutoka kwa chanzo chake kikisema CK ziku hizi anauza mishikaki. Mazungumzo yalikuwa hivi… Chanzo: “Haloo…naongea na Risasi Jumamosi hapo?” Risasi Jumamosi: “Ndiyo…karibu, tukusaidie nini?” Chanzo: “Hivi mna habari kuwa yule Kigogo wa Wema. Mnamuita CK, siku hizi anatuhudumia mishikaki baa?” Risasi Jumamosi: “Lakini sisi hatuoni tatizo. Kwani ni yake au anamsaidia mtu? Na ni sehemu gani?” Chanzo: “Hakuna tatizo lakini sasa amekuwa gumzo. Hebu fikirieni alivyokuwa na Wema na Kajala (Masanja) alikuwa a

BOSI WA ZAMANI WA TRA HARRY KITILLYA, SHOSE SINARE NA SIOI SOLOMONI WANYIMWA DHAMANA

Image
Kamishna wa zamani wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitilya, akipunga mkono kwa baadhi ya wanahabari waliokuwepo kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es salaam leo. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam imepuuza ombi la dhamana ya kesi inayowakabili Harry Kitillya, Shose Sinare na Sioi Solomoni ambapo wamerejeshwa rumande. Kitillya, alikuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA); Sinare, Mkuu wa Idara ya Ushirikiano na Uwekezaji katika Benki ya Stanbic na Sioi Solomoni, Mwanasheria wa Benki ya Stanbic. Dhamana yao imesikilizwa mbele ya Amilis Mchaura, Hakimu Mkazi Kisutu ambapo mawakili wa pande zote mbili waliwasilisha hoja zao. Dk. Lingo Tenga ndiye aliyeongoza jopo la mawakili upande wa watetezi ambapo upande wa serikali umesimamiwa na Oswadi Tibabyekonya, Wakili Mkuu wa Serikali Mahakama ya Kisutu. Upande wa utetezi uliomba mahakama kubatilisha mashitaka ya utakatishaji pesa haramu uliosa

Ujumbe mzito wakutwa kaburini kwa Kanumba!

Image
Ujumbe uliokutwa kaburini kwa Kanumba. Stori:  Mayasa Mariwata na Gladness mallya, Ijumaa Wakati mama yake, Flora Mtegoa (pichani), baadhi ya wasanii na mashabiki wake wakikumbuka miaka minne ya kifo cha aliyekuwa staa mkubwa wa filamu za Kibongo, Steven Charles Kanumba ‘The Great’, kumezuka sintofahamu ya kukutwa ujumbe mzito wa kimapenzi kaburini kwa msanii huyo ambao unadaiwa kuwekwa na mrembo aliyefika mahali hapo mapema wiki hii. TUJIUNGE MAKABURI YA KINONDONI Kwa mujibu wa mtu aliyedai ni mmoja wa walinzi wa Makaburi ya Kinondoni, Dar, alikolazwa Kanumba kwenye nyumba yake ya milele, ishu hiyo ilijiri Jumanne wiki hii, majira ya jioni ambapo mwanadada huyo alionekana akishuka kwenye gari (halikutajwa ni aina gani) na kuelekea kaburini hapo. Mrembo aliyekutwa kaburini. Alisema kuwa, huku akiwa amejitanda mtandio na maua mkononi, baada ya kufika kaburini hapo alionekana akiangua kilio na kuangusha maombi mazito kabla ya kuacha ujumbe na kuondoka zake.

HATIMAYE CCM WAMJIBU LOWASA BAADA YA KUMPONDA RAIS MAGUFULI KWA UTENDAJI WAKE

Image
Aliyekuwa mgombea Urais wa UKAWA kupitia CHADEMA, Ndugu Edward Lowassa, Aprili 7, 2016 alifanya mazungumzo na Wanazuoni kutoka katika vyuo vikuu vya ndani na nje ya nchi. Katika mazungumzo hayo, Ndugu Lowasa aligusia masuala mbalimbali ya Kitaifa yakiwemo hali ya siasa nchini, kuachisha kazi watumishi wenye tuhuma mbalimbali, na kile alichokiita tatizo la mfumo nchini. Alichokifanya Ndugu Lowassa ni kutaka kuwaaminisha Watanzania masuala yasiyo sahihi kwa maslahi ya kisiasa, kwani ukweli ni kwamba; Mosi, Rais John Pombe Magufuli hatafuti umaarufu, badala yake yeye na Serikali yake wanachapa kazi ili kuwaletea maendeleo Watanzania kwa ujumla. Pili, kuhusu suala la mfumo, Tanzania haina tatizo la kimfumo, kwani iliyopo, iliyowekwa tangu awali na waasisi wa Taifa letu, Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Hayati Abeid Aman Karume ni imara na imekuwa ikiboreshwa kulingana na mahitaji. Ifahamike hakuna mahali popote duniani ambako mfumo wa nchi unaji

BREAKING NEWZZZ.....HATIMAYE EDWARD LOWASSA AANDIKA MANENO HAYA USIKU HUU KUHUSU UTAWALA WA RAIS MAGUFULI

Image
  Hali ya siasa nchini ni ya hamasa, lakini isiyokuwa na misingi endelevu. Kwakuwa Rais amekuwa akigawa fedha wakati chombo cha kufanya hivyo kipo ambacho ni bunge. Pia nasononeshwa ninapoona watu wanaachishwa kazi na mashirika mbalimbali kwasababu ya hali ngumu ya uendeshaji wa mashirika hayo. Bandari sasa hivi nasikia uingizaji mizigo umeshuka kwa asilimia 50, kampuni nyingi za mizigo zimefunga s hughuli zake na pale palikua na vijana wetu wengi wameajiriwa,sasa hivi wako mtaani hakuna mbadala wa ajira, hii inasababisha hali ya maisha ya wananchi yanakua magumu. Kuhusu swala la MCC ni pigo kwa mustakabali wa uchumi, kutaka nchi ya viwanda kunahitaji uwekezaji mkubwa,katika hili fedha tutatoa wapi kama sio wafadhili wa ndani na nje kufanikisha? Hawa wafadhili sio watu wa kuwabeza kwakuwa tunafanya nao miradi mingi ya kimaendeleo na wanavyotoka hivi itaturudisha nyuma, Tunahitaji kujitegemea, ndiyo, ila kwa mipango huku tunatafuta mbadala wa kila msaada. Hapa kinacho

PROFESA MUHONGO ASISITIZA MAPINDUZI YA KIUCHUMI KATIKA SEKTA YA NISHATI NA MADINI.

Image
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Mhungo akizungumza na wafanyakazi wa wizara ya nishati na madini na kufungua baraza la wafanyakazi wa wizara yake katika  ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam leo. Mwenyekiti wa Baraza la wafanyazaki wa wizara ya Nishati na Madini, Selina Msumbushi akizungumza na wafanyakazi wa wizara ya nishati na madini na kusoma mapendekezo ya wafanyakazi hao leo katika mkutano wa kufungua baraza la wafanyakazi uliofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam leo. Baadhi ya wafanyakazi wa wizara ya Nishati na Madini wakiimba wimbo wa Solidarity leo katika ufunguzi wa Baraza la wafanyakazi katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam. Wafanyakazi wa wizara ya Nishati na Madini wakimsikiliza Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Mhongo wakati wa ufungunzi wa Baraza la wafanyakazi jijini Dar es Salaam leo. Picha na Avila Kakingo, Globu ya Jamii. WAZIRI wa Nishati