Posts

DIAMOND PLATINUMZ ANA MTOTO MWINGINE MWANZA ....AELEZA STORY NZIMA SOMA HAPA

Image
Tiffah Dangote ana ndugu yake, aliyezaliwa na msichana aliyekutana kimapenzi na baba yake (one night stand), Diamond Platnumz enzi anaanza kuupata ustaa. Taarifa hizo zilitolewa hivi karibuni na Diamond mwenyewe wakati akihojiwa kwenye kipindi cha Papaso cha TBC FM. Anasema tukio hilo lilitokea mwaka 2010, Mwanza alikoenda kufanya show. “Huyo mwanamke story ilivyokuwa alikuwa ametoka kwenye chumba cha brother Dully akaja kwangu mimi nikafanya yangu, mimi nikarudi huku mtoto akawa ananimbia ‘ebwana mimi nina mimba,” alisimulia Diamond. “Basi ilivyokuwa mtoto ‘bana eeh mimi nina mimba’ na mimi nikawa nachezesha nini nikawa namhudumia, huku na huku bahati mbaya nikaanza na demu fulani hivi kwahiyo demu mwenyewe akanimind, nikawa nampigia simu hapokei nikaenda Mwanza kumsakanya huku na huhu nasikia kwao wakanimind nikaonekana kama mimi nazingua,”alisema. “Siku moja nikaenda nikambanabana ‘nikamwambia wewe una mtoto’ akanikatalia kwasababu aliniambia ile mimba n

Mkurugenzi Mamlaka ya Viwanja vya Ndege afariki dunia

Image
  Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Mhandisi Suleiman Said enzi za uhai wake. Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Mhandisi Suleiman Said amefariki dunia mapema leo asubuhi akiwa katika mazoezi ya kuogelea,taarifa zinaeleza kuwa baada ya tukio hilo Bwa.Suleiman alikimbizwa hospitali ya Agakhan kwa matibabu, na baadae ikaelezwa kuwa amekwisha fariki na kuwa mazishi yanatarajiwa kufanyika leo.

Waziri Mkuu amwakilisha Rais Magufuli mkutano wa SADC Gaborone

Image
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi wa Botswana, Bw. Tshenolo Mabeo baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Sir Seretse Khama uliopo Gaborone Januari 17, 2016. Majaliwa amemwakilisha Rais John Magufuli katika Mkutano wa SADC. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Katibu Mtendaji wa SADC,Dkt, Srergomena Tax mjini Gaborone ambako Mheshimiwa Majaliwa anamwakilisha Rais John Magufuli kwenye mkutano wa SADC Januari 17, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

BREAKING NEWS : WANANCHI WA BONDE LA MKWAJUNI WAFUNGA BARABARA NA KUFANYA FUJO

Image
Hali si shwari hivi sasa katika eneo la Bonde la Mkwajuni Kinondoni jijini Dar es salaam, na inaelezwa kuwa baadhi ya Wananchi wamechoma mataili pande zote za barabara na hakuna gari kupita. Jeshi la Polisi lipo eneo la tukio hivi sasa kukabiliana na tukio hilo ambalo chanzo chake unadaiwa ni baadhi ya vijana wanaodaiwa kuwa walikuwa wakazi wa eneo lililobomolewa ambao wameingia barabarani na kufanya fujo. Pia gari la zimamoto limefika eneo la tukio ili kuzima moto huo. (Picha zote na Henry Mdimu) Endelea kutufuatilia kwa habari zaidi.  

Wakurugenzi watendaji Manispaa za Kigoma, Mpanda wasimamishwa

Image
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mhe. George B. Simbachawene. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mhe. George B. Simbachawene amewasimamisha kazi wakurugenzi watendaji wa manispaa za Kigoma, mkoa wa Kigoma na manispaa ya Mpanda, mkoa wa Katavi kwa tuhuma za kuridhia na kutekeleza maamuzi ambayo yamesababishia serikali hasara na upotevu wa fedha. Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma, Mhandisi Boniface Nyambele anakabiliwa na tuhuma ya uuzaji wa nyumba za halmashauri bila kufuata sheria, kanuni na taratibu zilizopo na bila kibali cha waziri mwenye dhamana kama sheria inavyoelekeza. Mkurugenzi wa Manispaa ya Mpanda, Ndugu Suleiman Lukanga anakabiliwa na tuhuma za ununuzi hewa wa gari la kusomba taka kwa kiasi cha shilingi milioni tisini na mbili, laki saba na elfu hamsini (92,750,000/=) na ubadhirifu wa fedha za ujenzi wa skimu ya umwagiliaji ya Kakese kiasi cha shilingi milioni mia m

UKAWA WASHINDA KITI CHA UMEYA MANISPAA YA ILALA.

Image
Meya wa Manispaa ya Ilala, Charles Kwiyeko akizungumza na madiwa wa Manispaa ya Ilala leo mara bada ya kushinda  kwa Kura 31 katika uchaguzi wa meya wa manispaa hiyo katika ukumbi wa Karimjee leo jijini Dar es Salaam. Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala Omary Salum Kumbilamoto  akiwashukuru madiwani waliompigia kura leo mara ya kuibuka kidedea katika uchaguzi uliofanyika katika ukumbi wa Karimjee leo jijini Dar es Salaam. Baadhi ya  wapiga kura wakipiga kura za Meya na Naibu leo katika uchaguzi  wa kuwapata viongozi hao wa Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam. Matokeo ya Meya na Naibu Meya yakujumlishwa na baadhi ya wajumbe wa Meya,naibu Maya  wakiwa na Mwanasheria wao leo mara baada ya kumaliza kugika kura katika uchaguzi uliofanyika katika ukumbi wa Karimjee leo jijini Dar es Salaam.  Baadhi ya viongozi wakiwa kwenye ukumbi wa Karimjee leo jijini Dar es Salaam.  Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala, Isaya Mgurumi akitangaza matokeo ya Ume

HATUA AMBAZO ZIMECHUKULIWA DHIDI YA STANBIC BANK TANZANIA LIMITED KUHUSU USHIRIKI WAKE KUWEZESHA MKOPO WA SERIKALI WA DOLA ZA KIMAREKANI MILIONI 600

Image
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt Philip Mpango (kushoto) akiongea na waandishi wa habari (hawamo pichani)jijini Dar es Salaam, kuhusu hatua zilizochukuliwa na Serikali dhidi ya Benki ya Stanbic Tanzania kutokana na ushiriki wake katika kuwezesha mkopo wa Serikali wa Dola za Kimarekani Milioni 600 na Kulia kwake ni Naibu Gavana  wa Benki Kuu ya Tanzania(BOT) Bw. Lila Mkila. Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt Philip Mpango (katikati)  akitoa tamko kwa waandishi wa habari (hawamo pichani) jijini Dar es Salaam, kuhusiana na kusudio la kuitoza Benki ya Stanbic faini ya shilingi bilioni 3.  Kulia kwake ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dkt. Servicius Likwelile na Kushoto kwake ni Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Bw. Lila Mkila. ……………………………………………………………………………………… Utangulizi Mwezi Julai 2013, Benki Kuu ya Tanzania kupitia ufuatiliaji wa kawaida wa shughuli za mabenki iligundua matatizo yaliyohusiana na hasara i

Vidokezo · Tanzania

Vidokezo · Tanzania

AUNT EZEKEL MKE WA IYOBO WAPATANA

Image
 Mwigizaji Aunt Ezekiel akiwa na mke wa Iyobo. DAR ES SALAAM: Yamekwisha! Baada ya kudumu ndani ya bifu kwa muda mrefu huku wakituhumiana uchawi, hatimaye mwigizaji Aunt Ezekiel na mzazi mwenzie na Moses Iyobo, Mwengi Ally wamekutana na kumaliza tofauti zao. Mapema mwaka jana, wawili hao waligombana kufuatia Iyobo ambaye ni dansa wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kummwaga Mwengi kisha kuanzisha uhusiano na Aunt ambapo uhusiano huo ulijibu na wakafanikiwa kupata mtoto. Aunt ndiye aliyeamua kufuta ‘kinyongo chao’ ambapo alisema hakuona sababu ya wao kuendeleza bifu lisilokuwa na msingi wowote na kuwa wao ni wazazi na watoto wao ni ndugu wa damu moja, alimshauri Iyobo awakutanishe, wamalize tofauti zao.   Baada ya kukubaliana, Aunt na Mwengi walikutana katika Hoteli ya Girrafe iliyopo Mbezi Beach, jijini Dar wakiwa na Iyobo ambaye alisimamia zoezi zima la mapatano kwa wawili hao kuzungumza, wakaelewana, ‘wakazika’ tofauti zao n

RAIS MAGUFULI AENDELEA KUTUMBUA MAJIPU,KIGOGO MWINGINE ATUNBULIWA JIJINI MWANZA

Image

KESI YA KUPINGA MATOKEO INAYOMKABILI MBUNGE WA JIMBO LA BUNDA MJINI MKOANI MARA YAAHIRISHWA

Image
Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza leo imeanza kusikiliza Kesi ya Kupinga Matokeo ya uchaguzi Mkuu uliofanyika Novemba 25 mwaka jana katika Jimbo la Bunda Mjini, Mkoani Mara ambapo Mgombea kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Esther Bulaya aliibuka mshindi. Na:George Binagi-GB Pazzo Jaji wa Mahakama hiyo Mhe.Mohamed Gwae ameahirisha kesi hiyo hadi jumatatu ijayo ya Januari 25 mwaka huu baada ya mawakili wa pande zote mbili kuchuana vikali kwa muda mrefu.  Waleta maombi (Mlalamikaji) katika kesi hiyo wametajwa kuwa ni wapiga kura wa jimbo hilo la Bunda Mjini ambao walikuwa wakiiomba Mahakama kutengua matokeo ya uchaguzi huo katika jimbo hilo kutokana na uchaguzi huo kukumbwa na kasoro mbalimbali ikiwemo uchaguzi kutokuwa huru pamoja na idadi ya wapiga kura kutofautiana na idadi ya waliojiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura. Madai hayo yamepingwa na upande wa Mjibu Maombi (Walalamikiwa ambao ni Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI TAREHE 16.01.2016

Image
  MAGAZETI YA UDAKU LEO   MAGAZETI YA MICHEZO NA BURUDANI v

KAJALA ADAIWA KUNASA UJAUZITO WA KIGOGO MKUBWA,MENGI YAFICHUKA

Image
Mwigizaji Kajala Masanja ‘Kay’. Mwandishi Wetu, Huenda mambo yanaweza yakawa yamejipa kwa mwigizaji Kajala Masanja ‘Kay’ kwani kuna taarifa zinadai kuwa mwigizaji huyo amenasa mimba ya kigogo serikalini. Chanzo makini kilicho karibu na staa huyo ambaye ana mtoto mmoja aliyezaa na prodyuza mkongwe Bongo, Paul Matthysse ‘P Funk’ (Paula), kimepenyeza ubuyu huo kuwa Kajala ana mimba ya zaidi ya miezi mitano na amegusiwa kuwa ni ya kigogo serikalini ambaye hataki kumtaja jina. “Hivi hamna habari? Kajala mbona mjamzito. Tena yeye alianza kunasa kabla hata ya Wema, nashangaa mnakomalia kuripoti mimba ya Wema tu, Kay mmemuacha na kigogo wake,” kilimwaga ubuyu chanzo hicho. Baada ya kupewa ubuyu huo, juzi Alhamisi, mwanahabari wetu wakati anaanza kuichimba habari hiyo, alitembelea kwenye ukurasa wa Instangram wa Kajala na kukutana na ujumbe ulionesha dhahiri kuwa mwigizaji huyo anajiandaa kuitwa mama kwa mara nyingine. “Hey IG...do me a favor...help me to choose

MILIPUKO YA MABOMU YAUWA WATU ZAIDI YA 7A INDONESIA

Image
Jengo la mgahawa wa Starbucks Coffee lililopo Mji Mkuu wa Indonesia, Jakarta ambapo mabomu hayo yamelipuliwa mapema leo. Milipuko ya mabomu takribani sita imetokea katika Mji Mkuu wa Indonesia, Jakarta na baadaye ufyatulianaji mkali wa risasi na watu zaidi ya saba wameripotiwa kuuawa japo polisi wanasema huenda kuna idadi kubwa zaidi ya waliouawa. Kati ya hao waliouawa ni maofisa watatu wa polisi, raia wawili akiwemo Mreno mmoja pamoja na washambuliaji watano. Polisi wa Indonesia wakijihami Milipuko imetokea maeneo kadha, ikiwa ni pamoja na mgahawani katika duka la kibiashara lililoko karibu na Ikulu ya rais wa nchio hiyo na ofisi za Umoja wa Mataifa (UN). Kuna ripoti za maafisa wa polisi kuonekana kwenye majengo na barabara za mji huo karibu na kituo hicho cha kibiashara. Eneo hilo limezingirwa na maafisa wa usalama. Rais Joko Widodo amehimiza raia wawe na utulivu na kushutumu “kitendo hicho cha ugaidi”. “Tunaomboleza watu waliofariki kwa sababu ya kisa hiki,