Posts

DEREVA TEKSI AFUMANIWA, AUAWA KWA KUCHOMWA KISU KIFUANI

Image
DEREVA teksi Hamis Seleman (18), mkazi wa Vingunguti jijini Dar es Salaam, amekufa baada ya kuchomwa kisu kifuani na Ali Kimodo, aliyemfumania akiwa na mpenzi wake. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Mary Nzuki alisema tukio hilo lilitokea usiku wa saa 9:00 wa kuamkia mwaka mpya, katika eneo la Vingunguti mtaa wa Magenge, ambapo Seleman alifumaniwa na msichana mmoja (jina tunalihifadhi), mwenye umri wa miaka 15, mkazi wa Tabata. Nzuki alisema kuwa baada ya tukio hilo kutokea, Kimodo pamoja na binti huyo walitoroka, hivyo polisi inaendelea na upelelezi kwa ajili ya kuwapata watu hao. Aliongeza kuwa katika maeneo mengine ya mkoa huo, hali ilikuwa shwari katika sherehe hizo za sikukuu ya Mwaka Mpya. Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Kihenya Kihenya alisema hali ilikuwa shwari katika eneo lake, kuanzia Krismasi na Mwaka Mpya. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillus Wambura alisema katika eneo lake, pia hakukuwa na tukio lolote kubwa la u

PICHA ZA BAADHI YA WAKE WA MFALME MSWATI>>EBWANA JAMAA ANAJUA KUCHAGUA

Image
Meet some of KING MSWATI's wives, Very Hot, the Guy must be lucky

KUNDI LA PANYA ROAD LATIKISA DAR JANA

Image
KIKUNDI kinachodaiwa kuwa Panya Road kimetikisa maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam kwa kupora mali, kujeruhi watu na kuzua sintofahamu katika maeneo ya jiji hilo wakiwa na mapanga mikononi. Maeneo yaliyokumbwa na dhooruba hiyo ni pamoja na Sinza, Tandale, Mwananyamala na maeneo mengineyo usiku huu. Maduka na baa zimefungwa na kupelekea polisi kupiga risasi hewani kuwatawanya watu waliokuwa wamekaa kimakundimakundi. Imeelezwa kuwa fujo zilianzia mchana leo baada ya kiongozi wa Panya Road aitwaye Diamond kuuawa maeneo ya mpakani mwa Tandale na Mwananyamala darajani usiku wa kuamkia mwaka mpya  kwa kukatwakatwa na mapanga . Baada ya kumzika mwenzao leo, vijana hao wakajipanga kwa ajili ya kufanya fujo. Usiku ulipoingia wakaanza kazi na kusababisha taharuki kwa wakazi wa Jiji la Dar. Baadhi ya mashuhuda walioshuhudia matukio hayo wanadai vijana hao walikuwa na silaha mbalimbali yakiwemo mapanga na walivamia maeneo kadhaa zikiwemo baa. Wateja waliokuwa

JOKATE KIDOTI AFUNGUKA KUHUSU SIRI ZA KUTOMASWA KIMAPENZI!

Image
Mwanamitindo ambaye pia ni msanii wa filamu Bongo, Jokate Mwegelo. MWANAMITINDO ambaye pia ni msanii wa filamu Bongo, Jokate Mwegelo amesema kuwa hapendi kuigiza sini za mapenzi hasa zile anazotakiwa kushikwashikwa na mwanaume hasa asiyemjua.Jokate alifunguka hayo wakati paparazi wetu alipotaka kujua namna ambavyo wazazi na mpenzi wake wanavyolipokea suala la yeye kuigiza sini za kushikwashikwa na wanaume tofauti katika filamu ndipo alipofunguka kuwa suala hilo limekuwa likipigwa vita na wazazi wake lakini analazimika kufanya kwa sababu ndiyo kazi aliyoichagua. Jokate Mwegelo akipozi. “Wazazi wangu wanachukia sana jambo hili na huwa wanasema bora niache filamu, hata mimi mwenyewe huwa sipendi ila huwa navumilia kwa kuwa ni kazi, sina jinsi,” alisema Jokate.

RAIS AMTEUA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI MPYA

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Bwana George Mcheche Masaju kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Uteuzi wa Bwana Masaju ulianza jana, Ijumaa, Januari 2, 2015 na ataapishwa keshokutwa, Jumatatu, Januari 5, 2015, Ikulu, Dar Es Salaam.Kabla ya uteuzi wake, Bwana Masaju alikuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Bwana Masaju pia amepata kuwa Mshauri wa Sheria wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Imetolewa na: Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, DAR ES SALAAM. 3 Januari, 2015 

MUME AMLIPUA KWA PETROL MKE WAKE BAADA YA KUKATAA KUPASHA MOTO CHAKULA

Image
Matuko ya kupiga na kunyanyaswa wanawake bado yameendelea kuchukua nafasi katika nchi malimbali za Afrika. Tumekuwa tukiona ripoti mbalimbali za matukio mabaya ya unyanyasaji, kutoka Kenya mwanaume mmoja amefunguliwa mashtaka baada ya jaribio la kutaka kumuua mke wake kwa madai alishindwa kumpatia chakula cha moto. Mwanaume huyo Peter Muthii alimmwagia mkewe petrol akiwa amelala, akawasha moto na kumfungia ndani ambapo muda mfupi baadaye majirani walikuja kumwokoa na kumkimbiza hospitali. Kisa cha tukio hilo kimetajwa kuwa ni baada ya mwanaume huyo kurudi nyumbani usiku na kumtaka mkewe kumpashia chakula lakini mkewe alimwambia apashe mwenyewe kitendo kilichomkwaza, akaamua kumlipua kwa kutumia petrol iliyokua chini ya kitanda chao.

JE! WAJUA KUWA WEWE UNAWEZA KUWA MCHAWI WA MAHUSIANO/MAPENZI YAKO?

Image
WATU wanaamini mno katika uchawi. Wanamaliza fedha kwa waganga wa kienyeji wakiamini kwamba wamerogwa, hivyo wanatafuta ufumbuzi kutoka kwa wataalamu wa mambo ya asili. Wapo wanaoita mambo ya Kiswahili. Kwangu napinga kuita hivyo kwa sababu nami ni Mswahili na kwa uzoefu wangu, sisi Waswahili hatuna utamaduni wa kutegemea mitishamba kuamua hatma za uhusiano wetu wa kimapenzi.  Ila baadhi wapo, tena wengi haswaaa! Shika hili kwamba wewe mwenyewe pengine ndiye mchawi wa mapenzi yako. Hujiulizi kwa nini wengine wanadumu? Ni vipi wenzi wengine wanaheshimiana? Inakuaje kwako imekuwa kinyume? Siyo suala la upepo, wakati mwingine ni kujitakia. Kivipi mwenzi wako hakuheshimu? Ni makosa gani ambayo wewe umefanya? Ukishapata majibu ya maswali hayo, utaweza kujua faida za wewe kujitambua. Nakuasa ushike moja kuu kwamba mapenzi ni nidhamu. Yapo kama kioo, ukiyaheshimu nayo yatakuheshimu na utayaona murua. Endapo utayachukulia kwa mzaha, n

WATU WANNE WANASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KWA KUTOROKA NA ALBINO MKOANI MWANZA

Image
  Jeshi la Polisi mkoani Mwanza linawashikilia watu wanne akiwemo baba mzazi wa mtoto mwenye ulemavu wa ngozi Albinism aliyetekwa nyara na watu wasiojulikana usiku wakiwa wamelala na kuondoka naye kusikojulikana hali iliyozua hofu kubwa kwa jamii. Amebainisha hayo kamishina msaidizi mwandamizi ambaye ni kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Bw.Valentino Mulowola wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake amemtaja mtoto wa kike aliyetekwa nyara mwenye umri wa miaka minne Pendo Emmanuel mkazi wa kijiji cha Ndambi kata ya fukalo tarafa ya mwamashimba wilayani kwimba ambaye ni mlemavu wa ngozi amesema kuwa tarehe 27 Desemba mwaka huu majira ya saa nne na dakika 30 za usiku watu wasiojulikana walivamia nyumba ya Bw.Emmanuel Shilinde kwa kupiga jiwe mlango na kuvamia kisha wakamchukua mtoto mmoja kati ya watoto watatu waliokuwemo ndani ya nyumba hiyo kisha wakatoweka naye kusiko julikana. Kufuatia hali hiyo makao makuu ya jeshi la polisi Tanzania im

HAPPYNESS MAGESE AMSAPRAIZ JOKATE KIDOTI!

Image
Mwanamitindo maarufu Bongo, ambaye anafanya kazi zake nje ya nchi Happyness Magesse ‘Millen’.Mwanamitindo maarufu Bongo, ambaye anafanya kazi zake nje ya nchi Happyness Magesse ‘Millen’ ambaye pia alishawahi kunyakua taji la Miss Tanzania 2001, ‘amemsapraiz’ mwanamitindo na mbunifu Jokate Mwegelo, kwa kumpatia keki yenye sura ya mdomo wake.Awali, kulikuwa na kikao cha kawaida cha kujadili mambo mbalimbali ya kikazi baina yao kilichofanyika ndani ya hoteli ya Hyatt Kempisky, iliyopo Posta Jijini Dar, lakini kumbe Millen alikuwa ameandaa keki. Mwanamitindo na mbunifu Jokate Mwegelo. “Yaani mimi nilijua tunakutana kama tulivyopanga, lakini cha kushangaza nikakuta watu wakiongozwa na dada yangu Millen wameniandalia keki mbalimbali ikiwemo moja kama mdomo wangu kabisa na kidoti juu, kwa kweli nilifurahi sana siwezi kuelezea,” alisema Jokate

Zari The Bosslady na Diamond Platnumz ni KIMYE wa Afrika!

Image
Kabla ya kukutana na Diamond Platnumz, Zari the Bosslady alikuwa tayari ni mwanamke maarufu nchini Uganda.  Utajiri na urembo wake ulimfanya aitwe Kim Kardashian wa Uganda. Zari anamiliki msululu wa magari ya kifahari yakiwemo Range Rovers, Bentley, Limousine, Mercedes Benz, Chrysler na mengine ambapo mengi kati yake yana plate number za jina lake. Anamiliki mijengo kibao pamoja na biashara mbalimbali kikiwemo chuo kikubwa kilichopo nchini Afrika Kusini. Kukutana na Diamond Platnumz ambaye ukubwa wake tunaufahamu, umemfanya msichana huyo mwenye watoto watatu kuwa na nguvu zaidi na ndio maana couple yao inaweza kufananishwa na ya Kanye West na Kim Kardashian. Kama ilivyo kwa Kimye, Zari na Diamond wana sumaku ya skendo. Ni hivi juzi tu mkanda wa ngono wa Zari ulisambaa mtandaoni ambao uliisha kulikuza tu jina na umaarufu wake. Kwa sasa wawili hao wameanza kuongozana kama kumbikumbi. Baada ya kumsindikiza Diamond kwenye tuzo za Channel O kish

MACHOZI YAWATOKA DIAMOND NA ZARI BAADA YA KUONA MABAKI YA MIILI KATIKA VITA YA KIMBALI NCHINI RWANDA

Image

KUNDI LA ISIS LAWACHINJA WAPIGANAJI WAKE ZAIDI YA 120 KWA KUJARIBU KUTOROKA

Image
Wapiganaji wa ISIS wakiua kundi la watu kwa risasi©RT Kundi hatari linalodai kutetea na kufuata haki za dini ya kiislamu linalopigana nchini Iraq na Syria la Islamic State limewanyonga wapiganaji wake wa kigeni zaidi ya120 kufuatia wapiganaji hao kutaka kuondoka na kurudi makwao na kuachana na kundi hilo. Wapiganaji waliouwawa ni waliokuwa wakitumikia kundi hilo katika mji wa Raqqa nchini Syria walikamatwa wakijaribu kutoroka kurudi makwao kama chanzo cha taarifa hii kilipozungumza na mwandishi wa  The Financial Times  ambaye amedai watu wanaopinga vitendo vya ISIS na utawala wa Rais Bashar al-Assad amesema watu waliouwawa walikuwa wakijaribu kutoroka baada ya ISIS kutoa mwongozo mpya wa wapiganaji wake katika kuwazuia kukimbia. Ingawa kuna wapiganaji wengi kutoka sehemu mbalimbali duniani wanaojiunga na kundi hilo kwakuhadaiwa kwamba ISIS itawasaidia kuielewa vyema dini ya kiislamu na mara baada ya kujiunga wanajikuta walidanganywa na matokeo yake wanajiing

JB WA BONGO MUVI AAMUA KUJIPOTEZA!

Image
Muigizaji mkongwe kwenye filamu nchini, Jacob Steven ‘JB’. MUIGIZAJI mkongwe kwenye filamu nchini, Jacob Steven ‘JB’ ameamua kujipoteza kwa makusudi katika uigizaji akiwa na lengo la kuweka mbele kazi zinazofanywa na kampuni yake ya uzalishaji sinema ya Jerusalemu.Akipiga stori na gazeti hili, JB alisema mwaka 2014 filamu zake tatu za Bado Natafuta, Wageni Wangu na Chausiku zilifanya vizuri sokoni.  “Kwa asilimia 80 mwaka huu kwangu umekuwa mzuri kikazi, nimefanya kazi nzuri bila mimi kuonekana kwa sababu nataka Jerusalemu ianze halafu mimi baadaye ndiyo sababu kubwa iliyofanikisha muvi zangu zote kufanya vizuri, sitaki kuwa naonekana mara kwa mara kwenye filamu,” alisema.

TAZAMA WANAUME WAOANA MBELE YA MAELFU YA WATU KATIKA KANISA LA ...MBELE YA PADRI MARKOS THONG

Image
"Dunia hii itafanywa tupu kabisa, na kuharibiwa kabisa; maana BWANA amenena neno hilo. Dunia inaomboleza inazimia; ulimwengu unadhohofika unazimia; watu wakuu wa dunia wanadhoofika. Tena dunia imetiwa unajisi kwa watu wanaoikaa, kwa maana wameziasi sheria, wameibadili amri, wamelivunja agano la milele". ISAYA 24:3-5. Mambo 3 yamezungumziwa ktk msitari wa 5 ambayo ndiyo sababu ya dunia hii kuwa ktk hali hii mbaya: 1. KUZIASI SHERIA - Hii inamaanisha ni kutenda kinyume na sheria za Mungu zinavyosema 'KUTOKA 20:3-17. 2. KUIBADILI AMRI - Hii inamaanisha kuna amri moja iliyobadilishwa maana inazungumzia uchache. Na ukiangalia leo amri ya 4 ndiyo iliyobadilishwa 'KUTOKA 20:8-11, hata Daniel naye alitabiri kuhusiana na jambo hili "DANIEL 7:25". 3. KUVUNJA AGANO LA MILELE - Agano hili la milele lilivunjwa ni Sabato ya Bwana 'KUTOKA 31:16 "Dunia hii itafanywa tupu kabisa, na kuharibiwa kabisa; maana BWANA amenena neno hilo. Duni

DIVA MWENYE SHEPU YA HATARI BONGO MUVI, MATILDA APIGWA MIMBA TENA FASTA FASTA!

Image
Msanii wa filamu Bongo mwenye shepu ya hatari sana, Wellu Sengo, ‘Matilda’. IMEVUJA! Msanii wa filamu Bongo, Wellu Sengo, ‘Matilda’, licha ya kuwa na mtoto mdogo ambaye hajafikisha hata mwaka, inadaiwa tayari amenasa ujauzito mwingine.Chanzo makini kinaeleza kuwa ujauzito huo ni wa mmoja wa wasanii wenye majina maarufu hapa nchini, ambao wamekuwa katika uhusiano kwa muda mrefu sasa.Katika mawasiliano kwa njia ya simu, Wellu baada ya kubabaika, alikiri kuwa na ujauzito na kumtaja msanii huyo kama ndiye mwenye mzigo, lakini jina lake linahifadhiwa kwa sasa kwa vile mwenyewe hakupatikana ili kuzungumzia madai hayo.  “Haa, wewe nani kakuambia habari hizi, lakini aah, ni kweli bwana nina ujauzito na mwenyewe ni (anamtaja jina). Si unajua tena mambo ya kawaida haya,” alisema muigizaji huyo.  Msanii huyo anayetajwa kuhusika na jambo hilo, ambaye hata hivyo ni mume wa mtu, amekuwa akionekana kuwa Wellu karibu katika maeneo mengi ya starehe na kijamii akiwa. Baadhi ya w

BREAKING NEWS : MTUHUMIWA WA MADAWA YA KULEVYA APIGWA RISASI KATIKA HARAKATI ZA KUTAKA KUTOROKA MAHAKAMANI

Image
Mtuhumiwa wa madawa ya kulevya raia wa Sierra Leone akiwa amepigwa risasi baada ya kutaka kuwatoroka askari magereza katika Mahakama ya Kisutu jijini Dar es Salaam.

LICHA YA KUSHUTUMIWA KATIKA SAKATA LA ESCROW MUHONGO AKEMEA RUSHWA TANESCO

Image
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) akizungumza na wananchi wa kijiji cha Surubu, Kata ya Komaswa wakati wa ziara yake wilayani Tarime Mkoa wa Mara. Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amewataka wananchi wa vijiji vya wilayani hapa kutoa taarifa za mianya ya rushwa wakati wanapoomba kuunganishiwa umeme majumbani. Muhongo alisema hayo juzi alipokuwa akikagua awamu ya pili ya Mradi wa Umeme Vijijini unaoendelea kwa nchi nzima na ambao mkoani Mara unatekelezwa katika vijiji 197. Alisema katika mradi huo, Serikali haitamwonea huruma mfanyakazi yeyote wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) atakayebainika kuomba rushwa ili atoe huduma. “Msitoe hongo,” alisema Profesa Muhongo. “Kati ya vitu ambavyo Serikali haitaki kuvisikia ni rushwa. Msidanganywe kuwa mkitoa rushwa ndiyo mtarahisishiwa kupata umeme kwa haraka.” Alisema gharama zote za kuunganishiwa umeme kwa mwanakijiji zinalipwa na Serikali na kiasi cha Sh2

JESHI LA POLISI LIMELAZIMIKA KUVUNJA CHUMBA KUTOA MWILI WA MTU ALIYEKUFA SIKU NNE ZILIZOPITA.

Image
Mtu mmoja Timotheo kweka (30) mkazi wa kiwanja cha ndege manispaa ya Morogoro amekutwa chumbani kwake amefariki dunia siku nne ziizopita na jeshi la polisi limelazimika kuvunja mlango na kutoa mwili huo . Akizungumza na ITV mmiliki wa nyumba alikokuwa amepanga Leonard Benedicti amesema kwa mara ya mwisho marehemu alionekana nje siku ya jumamosi hadi leo walipohisi harufu nzito chumbani kwake ndipo walitoa tarifa kwa jeshi la polisi na kumkuta ndani amefariki na kichwa kikiwa kimebanwa kwenye stuli. Wakizungumzia tukio hilo ndugu wa marehemu wamesema hawanawasiwasi na kifo cha ndugu yao kwani alikuwa mlevi wa pombe kwa muda mrefu ambapo wamesema siku ya jumamosi walikuwa na sherehe ya ukoo lakini marehemu hakuweza kufika ingawa hawakujua kama amefariki. Jeshi la polisi mkoa wa Morogoro limedhibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo mwili wa marehemu umehifadhiwa kwenye chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya mkoa wa morogoro.

MVUA KUBWA ILIYONYESHA LEO MAENEO KADHAA YA JIJI LA DAR ES SALAAM IMESABABISHA USUMBUFU KWA WAKAZI WA JIJI LA DAR9

Image
MVUA INAYONYESHA LEO JIJINI DAR ES SALAAM IMEZUA BALAA CHENI ZINAONDOKA NA MAJI