WATU WANNE WANASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KWA KUTOROKA NA ALBINO MKOANI MWANZA

 

Jeshi la Polisi mkoani Mwanza linawashikilia watu wanne akiwemo baba mzazi wa mtoto mwenye ulemavu wa ngozi Albinism aliyetekwa nyara na watu wasiojulikana usiku wakiwa wamelala na kuondoka naye kusikojulikana hali iliyozua hofu kubwa kwa jamii.
Amebainisha hayo kamishina msaidizi mwandamizi ambaye ni kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Bw.Valentino Mulowola wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake amemtaja mtoto wa kike aliyetekwa nyara mwenye umri wa miaka minne Pendo Emmanuel mkazi wa kijiji cha Ndambi kata ya fukalo tarafa ya mwamashimba wilayani kwimba ambaye ni mlemavu wa ngozi amesema kuwa tarehe 27 Desemba mwaka huu majira ya saa nne na dakika 30 za usiku watu wasiojulikana walivamia nyumba ya Bw.Emmanuel Shilinde kwa kupiga jiwe mlango na kuvamia kisha wakamchukua mtoto mmoja kati ya watoto watatu waliokuwemo ndani ya nyumba hiyo kisha wakatoweka naye kusiko julikana.
Kufuatia hali hiyo makao makuu ya jeshi la polisi Tanzania imetuma timu ya askali upelelezi watakao shirikiana na askari polisi mkoa wa Mwanza kuwasaka wahalifu walio husika kumteka nyara mtoto na kutoweka naye pasipojulikana pamoja na kutoa ahadi ya zawadi ya fedha kiasi cha shilingi milioni tatu kwa yeyote atakaye fanikisha kukamatwa kwa wahalifu hao ambapo kikosi hicho kwa pamoja kimewatia mbaloni wahamiaji haramu saba raia wa Ethiopia na watanzania wawili wanashikiliwa kwa tuhuma za kusaidia wahamiaji haramu hao kuingia nchini kinyume cha sheria za nchi. 

Comments

Popular posts from this blog