Ujenzi wa kituo cha Afya Dongobesh awamu ya pili waendelea kutekelezwa kwa zaidi ya aslimia 80- Mbulu



muonekano wa jengo la wodi ya mama na mtoto kituo cha Afya Dongobesh likiwa katika hatua ya ukamilishaji

Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu inategemea kukamilisha ujenzi wa majengo matano ya kituo cha Afya Dongobesh ifikapo Juni 30 2018, hatua hii imefikiwa ikiwa ni utekelezaji wa  kiwango cha aslimia 80 kilichobainishwa baada ya kufanyika ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa kituo cha Afya Dongobesh,tathimini hiyo ilitolewa na  timu ya Wataalam toka Tamisemi, wakilishirikiana na wataalam toka  Mkoa wa Manyara.
 
Timu ya wataalam wakiwa katika moja ya majengo mapya ya kituo cha afya wakiendelea na ukaguzi.
Timu hizo ziliweza kufanya ukuaguzi wa majengo hayo mapya yanayoendelea kukamilishwa kabla ya Mwezi Juni kukamilika ili kubaini kama  kiasi cha fedha Tsh.  Milioni 400  zilizotolewa  na Serikali ya awamu ya tano kwa ajili ya ujenzi wa majengo hayo unakamilika kwa wakati. Mgawao huo wa fedha uliotolewa ikiwa na mgawao awamu ya pili baada ya maeneo mbalimbali nchini kupokea mgawo wa awali. 

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Mbulu akiteta jambo na wataalam waliofika kituoni hapo kwa ajili ya ukaguzi.
 
Sambamba na ukaguzi huo timu hiyo haikusista kutoa pongezi kwa  uongozi wa Halmashauri ya  Wilaya nchini ya Mkurugenzi wake ndugu Hudson Kamoga kwa kusimamia ipasavyo fedha zinazotolewa na Serikali na kuwataka kuhakikisha wanakamilisha kwa wakati  licha ya kuchelewa kuanza ujenzi kutokana na kuchelewa kupata mgawao wa fedha.

Kazi ya ukaguzi jengo la mtumishi ikiwa imekamilika kwa wataalam mbalimbali toka Tamisemi, Mkoani, Wilayani na Wajumbe kushiriki kwa pamoja.
Kituo cha Dongobesh kilipokea kiasi hicho cha fedha ili kujenga majengo matano ambayo ni Jengo la Upasuaji, Jengo la Maabara, Jengo la Mama na Mtoto, Jengo la Kuhifadhi Maiti na Jengo la Mtumishi, Ujezi huo unafanyika kwa  kutumia nguvu ya wananchi (force Account) ambayo hutoa fursa kwa jamii husika kufaidika na kazi kwa malipo yaliyotolewa.

 muonekano wa jengo la upasuaji kama jinsi linavyoonekana katika hatua mbalimbali za ujenzi.
Aidha wajumbe wa kamati inayosimamia ujenzi huo wameishukuru Serikali ya awamu ya tano kwa kutoa fedha hizo ambazo zimeweza kuleta mabadiliko makubwa katika kituo hicho  kwani wananchi wa kata nzima wanategemea kituo hicho kwa ajili ya kupata matibabu kituoni hapo  na hivyo wameimbo Serikali kuendela kutoa msaada mbalimbali ya fedha na Vifaa tiba ili kuboresha kituo na kutoa tiba iliyo bora zaidi kuepusha vifo visivyo na lazima.
 
wajumbe wakiwa katika moja ya majengo yanayoendelea kujengwa ili kuona ujenzi umefikia kiwango gani.

Comments

Popular posts from this blog