Je,wajua Rais Kim alisafiri na choo chake mpaka Singapore?



Imebainika kuwa Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un alisafiri na choo chake maalumu wakati wa mkutano wake na Rais Trump nchini Singapore.
Sababu ya Kiongozi huyo kusafiri na choo chake imetajwa kuwa ni kuzuia kinyesi cha Kiongozi huyo kufanyiwa upembuzi na watu wa usalama wa mataifa mengine.
Aidha imeelezwa kuwa Kiongozi huyo amekuwa na tabia ya kutembea na choo chake kila mahala anapokwenda kwani huwa hapendi kutumia vyoo vya umma.
Kwa upande mwingine Kiongozi huyo alibeba gari lake aina ya Limousine ambalo halipitishi risasi pamoja na chakula chake mpaka nchini Singapore.

Comments

Popular posts from this blog