Posts

NAIBU WAZIRI MASAUNI, KAMISHNA JENERALI WAKAGUA MPAKA WA TANZANIA KENYA ULIOPO WILAYANI TARIME

Image
Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dk, Anna Makakala, Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima (katikati) wakiangalia jiwe la mpaka unaotenganisha nchi ya Tanzania na Kenya uliopo katika kijiji cha Nyamhunda, wilayani Tarime ambapo upande wa pili ni Kaunti ya Migori nchini Kenya. Naibu Waziri yupo katika ziara ya kikazi ikiwa na lengo la kukagua mipaka na kudhibiti uingiaji wa wahamiaji haramu kupitia vipenyo katika mipaka hiyo.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza wakati wa ziara ya kutembelea alama ya Mpaka unaotenganisha nchi za Tanzania na Kenya uliopo katika kijiji cha Nyamhunda wilayani Tarime.Wengine ni Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dk, Anna Makakala, Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima (katikati) na Mkuu wa Wilaya ya Tarime Glorius Luoga. Naibu Waziri yupo katika ziara ya kikazi ikiwa na lengo la kukagua m

NANDY ATOA YA MOYONI,AFUNGUKA TENA KUHUSU KUPENDA

Image
MWANA-DADA anayefanya vizuri katika Bongo Fleva Faustina Charles ‘Nandy’ ameeleza kuwa hampendi mwanaume kwa sababu ya mkwanja isipokuwa anataka mapenzi ya kweli. Akipiga stori na Risasi Vibes, Nandy ambaye anatamba na ngoma ya Kivuruge alisema anachopenda yeye ni mwanaume mcha Mungu na mchapakazi, haijalishi kama hiyo kazi inamuingizia kipato kikubwa au la. “Fedha siyo kigezo cha mwanaume kuwa na mimi, muhimu mtu awe na hofu ya Mungu, asiwe mtu wa kujibweteka awe anajish-ughulisha kwa kazi yoyote ile, tutapambana wote kutafuta maisha hadi mambo yatakapokuwa vizuri na kujivunia kwa pamoja,”alisema. STORI: MAYASA MARIWATA | GLOBAL PUBLISHERS

Jide, FA Wanaurudisha Muziki wa Bongo Juu

Image
Judith Mbibo Wambura. KAMA ilivyokuwa wakati walipotibuana, kwamba watu wachache walio karibu yao ndiyo waliojua chanzo, ndivyo inavyotokea tena sasa hivi inapofahamika kuwa bifu baina yao limeisha. Nawazungumzia ma-legend wawili katika Bongo Fleva, Judith Mbibo Wambura ambaye wengi tunamfahamu kama Lady Jaydee na Hamis Mwinjuma, hapa akifahamika zaidi kama Mwana FA. Na watu wasingejua kirahisi kama wawili hawa wako kwenye ugomvi kama siyo wote wawili kutangaza kufanya shoo kwa siku moja. Jide alikuwa na onyesho lake la kutimiza miaka 13 katika Bongo Fleva ambayo ilipangwa kufanyika pale Nyumbani Lounge huku Mwana FA, akiitangaza siku hiyo kuwa na onyesho alilolipa jina la The Finest, ambalo lilipangwa kupigwa katika viwanja vya Makumbusho, kule Posta, jijini Dar. Hiyo ilikuwa ni Mei 2013. Mwana FA. Shoo zao hizo zilikuwa zipigwe Mei 31, 2013 lakini ghafla likaibuka tukio kubwa Bongo Fleva, baada ya taarifa kuwa rapa mkali, bingwa wa freestyle Bongo,

RC Makonda Atembelea Ofisi za Clouds Media Group Kutoa Pole

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam,  Paul Makonda (wa pili kulia),  akinena jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group, Joseph Kusaga (kushoto). MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam,  Paul Makonda ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Dar es Salaam mapema leo ametembelea Ofisi za Clouds Media Group kutoa pole ikiwa ni siku moja baada ya ofisi hizo kukumbwa na janga la moto uliotokea hapo jana majira ya saa nne asubuhi. Makonda akiongea na maofisa wa vikosi vya usalama. Viongozi wengine wa serikali waliofika ofisini hapo ni Mkuu wa Wilaya wa Kinondoni, Ally Hapi na Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Benjamin Sitta. Hata hivyo, tayari matangazo ya vituo vya Clouds FM na Clouds TV yamerejea hewani baada ya kupotea siku nzima  jana kutokana na hitilafu ya iliyosababishwa na moto huo ambao chanzo chake hadi sasa hakijajulikana.

MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU AMJULIA HALI MZEE ABDULRAZACK MUSSA SIMAI ‘KWACHA’ ALIYELAZWA MOI

Image
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan leo alimtembelea na kumjulia hali Mzee Abdulrazack Mussa Simai ‘Kwacha’ ambaye amelazwa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Upasuaji wa Ubongo, Mgongo na Mishipa ya Fahamu (MOI).Mzee Abdulrazack Mussa Simai ‘Kwacha’ ni Mzee wa Chama Cha Mapinduzi lakini pia alishawahi shika nafasi mbali mbali za Uongozi katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Post Views: 50

ENGO LA CLOUDS MEDIA GROUP LAUNGUA MOTO

Image
Mafundi umeme na Zimamoto wakiingia kupitia dirishani katika jengo la Clouds Media Group kuzima moto uliounguza baadhi ya ofisi leo jijini Dar es Salaam. …Juhudi za kuingia ndani zikiendelea. Mkurugenzi wa Vipindi wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba (wa pili kulia, T-shirt ya bluu) akiwa na askari, wakiangalia juhudi za kuuzima moto uliotokea. …Akiongea na polisi. Wafanyakazi wa Clouds na wananchi wakiwa nje ya jengo lililoshika moto. Muonekano wa Jengo la Clouds Media Group.   Magari ya Zimamoto yaliyofika kupambana na moto huo. SEHEMU  ya jengo la kituo cha Clouds Media Group lililoko Mikocheni jijini Dar es Salaam limeungua moto leo ambapo Mkurugenzi wa Vipindi wa kituo hicho, Ruge Mutahaba, amesema moto huo ulitokea bila ya mtu yeyote kuwa na taarifa nao ambapo ulianzia katika studio ndogo ya kurekodia. Aliongeza kwamba kituo hicho si mara ya kwanza kupatwa majanga ya moto ambapo mara ya kwanza walipokuwa katika jengo la Kitegauchumi eneo la

Rais Magufuli awaonya Masha na Msando

Image
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Rais John Pombe Magufuli amewaonya wanachama wapya ambao wamehamia ndani ya chama hicho leo kwenye mkutano mkuu wa NEC unaoendelea Ikulu jijini Dar es salaam. Wanachama hao ambao wamehamia na kutangazwa leo ni Mwanasheria Alberto Msando aliyekuwa mwanachama wa ACT-Wazalendo, Mbunge wa zamani wa Nyamagana Laurent Masha aliyekuwa mwanachama wa Chadema pamoja na Mwenyekiti wa Baraza la vijana Chadema taifa Patrobas Katambi. Wengine ni Profesa Kitila Mkumbo ambaye naye alikuwa mwanachama wa ACT-Wazalendo pamoja na Sophia Simba ambaye ameomba kurejeshewa uanachama baada ya kufukuzwa kwa muda Akiongea baada ya kuwapokea wanachama hao Rais Magufuli amesema, “Nawaomba msije mkabadilika tena, mmekuja huku na wanachama wamewakubali msirudi tena kule, hiki ni chama cha wote hata watoto watazaliwa watakikuta na watajiunga kwasababu kina misingi imara, kwahiyo msije huku kujaribu”. Rais Magufuli amemaliza kwa kuwapa ruhusa ya kugo

Profesa Kitila, Katambi, Msando waingia CCM

Image
Dar es salaam. Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Profesa Kitila Mkumbo ametangazwa rasmi leo Jumanne mbele ya mkutano wa NEC, CCM unaoendelea Ikulu jijini Dar es salaam. Mbali na Profesa Kitila ambaye alikuwa kada wa ACT, pia kuna Mwenyekiti wa Bavicha, Patrobas Kitambi ambaye ni Mwenyekiti wa Bavicha, Lawrence Masha, Samson Mwigamba na Albert Msando. Akizungumza mbele ya mkutano huo, Profesa Kitila amesema: "Nguvu ya CCM zipo tano, moja ni kwamba ni chama cha watu, ni chama pekee chenye nguvu siyo chama kuogopa watu, tulijaribu huko tulipokuwa lakini yalishindwa." Kwa upande wake, Masha amesema alipoamua kuondoka, baba yake alisikitishwa na uamuzi huo lakini baada ya kutafakari ameamua kurejea nyumbani. Amesema yeye ni mwanaCCM na kijana alilelewa ndani ya chama hicho. "Mwenyekiti wewe ni mfugaji, ng'ombe akiingia zizini amekatwa mkia unamwangalia mara mbili mbili, mimi sijakatwa mkia ni mwaminifu, ukinihitaji nitumie, kudumu Chama cha Mapind

Sophia Simba arudi CCM

Image
Dar es Salaam. Aliyekuwa Mwenyekiti wa Wanawake CCM (UWT), Sophia Simba aomba radhi na kuomba kurejea CCM baada ya kufukuzwa uanachama. Mwenyekiti wa CCM Rais John Magufuli amesoma barua ya Sophia kuomba radhi mbele ya Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) na kuwahoji wajumbe kama wanakubali kumsamehe jambo lililokubaliwa. "MwanaCCM aliyefukuzwa uanachama amekuwa akiandika barua nyingi za kuomba radhi lakini tumekuwa tukinyamaza,  kikao hiki ndiyo kilimfukuza," amesema Rais Magufuli katika kikao hicho kinachofanyika leo Jumanne. Baada ya kuwahoji wajumbe na kukubaliwa Rais Magufuli aliandika kwenye barua hiyo kuwa amekubaliwa kurudi CCM.

BREAKING : MWANAMKE AFANYIWA UKATILI NA MUMEWE WA KUTISHA KISA KUPATA KAZI,AMWAGIWA TINDIKALI

Image
Mwanamke mmoja kutoka katika wilaya ya Malwani, Mumbai nchini India amejikuta akipata kilema cha kudumu baada ya kumwagiwa tindikali usoni na mumewe siku mbili baada ya kupata ajira serikalini.Zakira Ali SheikhMwanamke huyo aliyetambulika kwa jina la Zakira Ali Sheikh (26) amesema alikatazwa na mumewe ‘Roobab Ali Sheikh’ kutafuta kazi yoyote ya kuajiriwa na kuambiwa kuwa abaki tu nyumbani kwa ajili ya kulea familia na kazi ndogo ndogo. Mwanamke huyo wakati anasimulia kisa hicho kwenye mahojiano yake na gazeti la Hindu Times la nchini India amesema mumewe alikuwa ni fundi magari na alikuwa haachi pesa ya matumizi nyumbani kitu ambacho kilikuwa kinamuumiza kichwa jinsi ya kuendesha familia yao yenye watoto wawili.Bi. Zakira ambaye tayari jicho lake moja limeshapata upofu amesema alishindwa kuvumilia hali hiyo ndipo alipoamua kupeleka maombi ya kazi kwenye kiwanda cha Serikali cha Sabuni baada ya kuona matangazo ya kazi. Anasema baada ya siku mbili aliona jina lak

ANGALIA PICHA YA KWANZA IRENE UWOYA NA NDUGU ZAKE WALIVYO TEMBELEA KABURI LA MUME WAKE

Image
Familia ya @ireneuwoya8 yafanikiwa kuzulu (kutembelea) kaburi la marehemu NDIKUMANA… mama mdogo na mama uwoya washindwa kujizuia… Wamwaga machozi na kugala Gala juu ya kaburi huku wakihuzunika kupita kiasi… Taarifa zilizo tufikia ni kwamba walinusurika kuzimia kutokana na Pressure iliyosababishwa na kulia sana Post Views: 532

Rais Magufuli Aongoza Kikao Cha Kamati Kuu Ya Ccm Jijini Dar Leo

Image
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt John Pombe Magufuli akiwa kaongozana na Katibu Mkuu wake Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasili kuongoza kikao cha Kamati Kuu ya CCM jijini Dar es salaam leo Jumatatu Novemba 20, 2017 Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein akiwa kaongozana na Katibu Mkuu wa chama hicho Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasili katika kikao cha Kamati Kuu ya CCM jijini Dar es salaam leo Jumatatu Novemba 20, 2017 Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt John Pombe Magufuli akiweka sawa makabrasha kabla ya kuanza kwa kikao cha Kamati Kuu ya CCM jijini Dar es salaam leo Jumatatu Novemba 20, 2017 Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt John Pombe Magufuli akiweka sawa makabrasha kabla ya kuanza kwa kikao cha Kamati Kuu ya CCM jijini Dar es salaam leo Jumatatu Novemba 20, 2017 Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Ndug

BREAKING NEWS: MAHAKAMA KENYA YAIDHINISHWA USHINDI WA KENYATTA

Image
Tumefurahishwa na uamuzi wa MahakamMmoja wa waliogombea urais nchini Kenya, Ekuru Aukot, amesema amefurahishwa na uamuzi wa mahakama ambayo alisema imedhihirisha uhuru wake na kujitolea kwake kudumisha sheriaAmesema: “Wanasiasa hawawezi kuwa majaji na mahakimu.” (Majaji wa Mahakama ya Juu) Walifanya hivyo 1 Septemba walipofuta ushindi wa Kenyatta, na wamerudia tena leo,” amesema. Tunatumai kwamba sasa Kenya inaweza kusonga mbele, na wanaochochea ghasia kutokana na mzozo wa uchaguzi sasa hakuna mzozo tena baada ya uamuzi wa mahakama. Tunaweza sasa kuangazia mambo ya uzito zaidi. Chama chetu (Thirdway Alliance) sasa kutaangazia kuhakikisha Serikali inafanya kazi ipasavyo.” Kenyan President Uhuru Kenyatta addresses a news conference at the State House in Nairobi December 2, 2014. Kenyatta said on Tuesday he had nominated a new interior minister and accepted the resignation of the head of the police, both of whom have been criticised for failing to stop a spate of a

FAMILIA YA NDIKUMANA YAZUIA IRENE UWOYA ASIPIGWE RWANDA

Image
FAMILIA ya aliyekuwa Kocha Msaidizi wa Timu ya Rayon Sports ya Rwanda, Hamad Ndikumana ‘Katauti’ (39), imezuia staa wa filamu Bongo, Irene Uwoya ambaye alikuwa mke wa jamaa huyo asifanyiwe fujo baada ya kutinga nchini Rwanda jioni ya Ijumaa iliyopita. Hatua hiyo ilikuja baada ya Ndikumana kupoteza maisha huku Uwoya akishushiwa tuhuma za hapa na pale na kwamba huenda alichangia kifo hicho. Hamad Ndikumana ‘Katauti’ (39) enzi za uhai wake akiwa na staa wa filamu Bongo, Irene Uwoya. Kwa mujibu wa chanzo chetu kilichoambatana na Uwoya, familia ya Ndikumana ilichukua uamuzi huo baada ya watu mbalimbali nchini humo kuwa na hasira na Uwoya.          Kutokana na kifo cha Ndikumana, Uwoya alilazimika kwenda Rwanda kuhani msiba akiwa na mwanaye aliyezaa na jamaa huyo, Krish, mama na baba yake na mabaunsa wa kumpa ulinzi. Chanzo hicho kilieleza kwamba, watu mbalimbali nchini humo walikuwa na hasira juu ya Uwoya kwamba ndiye aliyesababisha kifo cha Ndikumana kwani alikuwa na m

MAGAZETI YA LEO JUMATATU TAREHE 20.11.2017

Image