Posts

RC MAKONDA ATAJA LISTI NYINGINE YA MAJINA 65 YA WANAOHUSIKA NA DAWA ZA KULEVYA

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ametaja majina ya watuhumiwa wengine 65 wa madawa ya kulevya, wakiwemo Mwenyekiti wa Chadema na Mbunge wa Jimbo la Hai, Freeman Elikael Mbowe, Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji, Askofu Josephat Gwajima na Mbunge Mstaafu wa Kinondoni, Idd Azzan. Makonda amesema hii ni awamu ya pili ya oparesheni ya kusaka watuhumiwa wa mtandao wa biashara haramu ya madawa ya kulevya, ambapo amesema awamu hii itakuwa ngumu ikilinganishwa na ile ya kwanza iliyohusisha polisi na wasanii kukamatwa. Makonda amewataka watu wote 65 waliotajwa, kuhakikisha wanaripoti kwenye Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam (Sentro) siku ya Ijumaa saa 5 asubuhi kwa mahojiano zaidi. Akizungumza na wanahabari ofisini kwake, Makonda amesema kuwa, waliokamatwa awali ndiyo waliofanikisha kupatikana kwa orodha hiyo mpya.

WIZARA YA HABARI YAZINDUA PROGRAMU YA WADAU TUZUNGUMZE

Image
Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akizungumza na waandishi wa habari (hawapo Pichani) leo Februari 07, 2017 Jijini Dar es Salaam kuhusu mkakati wa Wizara kuanza kuzungumza na wadau katika sekta zinazosimamiwa na Wizara yake. Waandishi wa Habari wakifuatilia mkutano wa Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (hayupo pichani) akizungumza leo Februari 07,2017 Jijini Dar es Salaa kuhusu mkakati wa Wizara kuanza kuzungumza na wadau wa sekta zinazosimamiwa na Wizara yake. Picha na Raymond Mushumbusi Na: Genofeva Matemu  Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imebuni na kutanganza Programu ya kushirikisha wadau inayoitwa wadau tuzungumze itakayosaidia wizara kupata vionjo, maoni, mawazo na fikra za wadau katika kuhakikisha kwamba Wizara inafanya kama wadau wake wanavyotegemea. Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof.

MTOTO WA DARASA LA NNE AFANYIWA UKATILI KWA KUCHOMWA MOTO MIKONO JIJINI DAR ES SALAAM

Image
Bi.Tatu Rashid mkazi wa Kivule jijini Dar es Salaam amemfanyia ukatili mtoto wake wa kumzaa kwa kumfunga mikono yake miwili,kisha kumuwekea mifuko ya plastiki na kumchoma moto baada ya mtoto huyo kudaiwa kuchukua shilingi 1000. Tukio hilo la kikatili alilofanyiwa mwanafunzi wa darasa la nne jina linahifadhiwa, limetokea jana eneo la Kivule jijini Dar es Salaam,ambapo ITV baada ya kubaini ukatili huo ilifuatilia sakata hilo na kukuta suala hilo likiwa limefikishwa katika ofisi ya serikali ya mtaa wa huo, ambapo mtoto huyo ambaye jina lake limehifadhiwa ambaye ni mwanafunzi wa darasa la nne ameeleza kwamba licha ya licha kumuomba msamaha mama yake mzazi kwa kuchukua shilingi 600 bila kumuomba lakini mama yake hakumuhurumia na badala yake alilazimisha kuwa kachukua shilingi 1000 jambo ambalo limemuhuzunisha baba mzazi wa mtoto ambaye hakuwepo nyumbani wakati wa tukio. Majirani wa familia hiyo wamesema mama huyo baada ya kuona mtoto wake atagundulika kach

MAJALIWA AMTEMBELEA MALECELA DODOMA

Image
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu, John Malecela wakati alipomtembelea nyumbani kwake, Kilimani mjini Dodoma Februari 1, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waziri Mkuu Mstaafu, John Malecela wakati alipomtembelea nyumbani kwake, Kilimani mjini Dodoma Februari 1, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiagana na Waziri Mkuu Mstaafu, John Malecela wakati alipomtembelea nyumbani kwake, Kilimani mjini Dodoma Februari 1, 2017. baada ya kuzungumza naye (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

RAIS DKT MAGUFULI AZINDUA MWAKA MPYA WA KIMAHAKAMA JIJINI DAR ES SALAAM LEO

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akihutubia wakati wa uzinduzi wa Mwaka Mpya wa Kimahakama katika viwanja vya Mahakama vya Mtaaa wa Chimala Ocean Road jijini Dar es salaam leo February 2, 2017. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiongea na Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Hamisi Juma wakati wa uzinduzi wa Mwaka Mpya wa Kimahakama katika viwanja vya Mahakama vya Mtaaa wa Chimala Ocean Road jijini Dar es salaam leo February 2, 2017. Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Hamisi Juma akihutubia wakati wa uzinduzi wa Mwaka Mpya wa Kimahakama katika viwanja vya Mahakama vya Mtaaa wa Chimala Ocean Road jijini Dar es salaam leo February 2, 2017 wakati wa uzinduzi wa Mwaka Mpya wa Kimahakama katika viwanja vya Mahakama vya Mtaaa wa Chimala Ocean Road jijini Dar es salaam leo February 2, 2017. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph M

STAA WEMA SEPETU ATAJWA KWENYE LIST YA MADAWA YA KULEVYA

Image
Msanii wa filamu nchini Wema Sepetu ametajwa kuwa ni kati ya wasanii ambao wanatumia dawa za kulevya hivyo anapaswa kesho kukutana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda katika kituo cha polisi. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaama amewataja wasanii wengine akiwepo TID, Chid Benz, pamoja na Recho na kusema anahitaji kesho wafike makao makuu ya kituo cha polisi. "Naomba tukutane kesho pale polisi Central akiwepo TID, akiwemo Wema Sepetu, wakiwepo wakina Junior Sniper, wakina Ditto, Titoo, kuna Ally Denya, kuna wakina Chacha, kuna kina Mecky wengine hawa wakina Petit Man tayari nishawatia mikononi mwa sheria, kuna watu kama kina Recho, Chid Benz wote hawa nawahitaji ni vijana wenzangu nafikiri tutaelewana vizuri" alisema Paul Makonda

MATUKIO MBALIMBALI KUHUSU WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO BUNGENI MJINI DODOMA

Image
    Waziri wa Fedha na Mipango, mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), akifafanua baadhi ya vipengele vya Muswada wa marekebisho ya Sheria mbalimbali Namba 4 ya Mwaka 2016, kuhusu marekebisho ya Sheria ya Mikopo, Misaada na Dhamana. Muswada huo ulipitishwa kuwa Sheria na Bunge Februari Mosi, 2017.   Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Bw. George Masaju, akihitimisha mjadala wa Muswada wa Marekebisho ya Sheria mbalimbali Namba 4 ya Mwaka 2016, uliopitishwa na wabunge kuwa Sheria Februari Mosi, 2017, Mjini Dodoma   Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) na Naibu Waziri wake, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), wakipitia nyaraka za Muswada wa Marekebisho ya Sheria mbalimbali Namba 4 ya Mwaka 2016, Bungeni Mjini Dodoma, Muswada ambao tayari Bunge limeupitisha kwa kishindo kuwa Sheria Februari Mosi, Mjini Dodoma.   Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), akitoka nje ya ukumbi wa Bunge Mjini Dodoma baada ya kutetea na kufafa

UFAULU WA KIDATO CHA NNE MWAKA 2016 WAPAA

Image
  Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) limetangaza matokeo ya kidato cha nne mwaka 2016 ambapo umefaulu wa jumla umeongezeka kwa 2.56% kutoka 67.53% mwaka 2015 hadi 70.09% mwaka 2016. Katibu Mtendaji wa barza hilo, Dkt Charles Msonde amesema kati ya wanafunzi 408,372 waliofanya mtihani, jumla ya wanafunzi 277,283 wamefaulu, wakiwemo wasichana 135,859 sawa na asilimia 67.06 na wavulana 141,424 sawa na asilimia 73.26. Kwa upande wa watahiniwa wa shule, Dkt Msonde amesema kuwa 244,762 sawa na asilimia 70.35 ya waliofanya matihani wamefaulu ikilinganishwa na wanafunzi 240,996 sawa na asilimia 67.91 waliofaulu mwaka 2015. Kwa upande wa ubora wa ufaulu, amesema watahiniwa wa shule wenye ufaulu mzuri wa Daraja la kwanza hadi la tatu ni 96,018 sawa na asilimia 27.60

RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA KATIBU MKUU UMOJA WA MATAIFA (UN) PIA AHUDHURIA MKUTANO WA AU MJINI ADDIS ABABA ETHIOPIA

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa(UN) Antonio Manuel Olveira Guterres kabla ya kuanza mazungumzo yao katika Ofisi za Makao Makuu ya Umoja wa Umoja wa Afrika (AU), Addis Ababa nchini Ethiopia. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Manuel Olveira Guterres akimkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kabla ya kuanza mazungumzo yao katika Ofisi za Makao Makuu ya Umoja wa Umoja wa Afrika (AU), Addis Ababa nchini Ethiopia. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa(UN) Antonio Manuel Olveira Guterres katika Ofisi za Makao Makuu ya Umoja wa Umoja wa Afrika (AU), Addis Ababa nchini Ethiopia. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa(UN) Antonio Manuel Olveira Guterres mara baada ya mazungumzo yao.