Posts

MBUNGE Godbless Lema ALETA HALI TETE BUNGENI…Adai Waziri Alimshauri Wafanye Fujo Arusha ili Aingilie

Image
GODBLESS Lema, Mbunge wa Arusha Mjini amesema kwamba, alishauriwa na George Simbachawene, Waziri wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kuwa, amfungie ofisini Athumani Kihamia, Mkurugenzi wa Jiji la Arusha ili kuibua vurugu na kisha (Simbachawene) aingilie, anaandika Charles William.Akizungumza bungeni leo asubuhi, Lema amesema Simbachawene alimtaka yeye na viongozi wengine wa Chadema wamfanyie vurugu mkurugenzi huyo kisha tukio hilo lioneshwe katika Runinga ili waziri aingilie kati mgogoro huo kwa madai, utakuwa umedhihirika. “Nilimwambia Waziri Simbachawene kuwa Arusha tuna tatizo kwenye halmashauri tunaomba msaada, akanishauri tukafanye fujo ili aone kwenye vyombo vya habari na apate nafasi ya kuingilia mgogoro huo kwasababu rais amewapa nguvu wakuu wa mikoa. “Akaniambia siwezi kuja kichwa kichwa nenda kafanye fujo, mfungieni mkurugenzi nje halafu mimi nione kwenye TV ili niingilie mgogoro huo. Yaani waziri anaogopa kuingilia migogoro

HIVI NDIVYO MAMBO YALIVYOKUWA KATIKA TUKIO LA MOTO, BANDARINI JIJINI DAR LEO

Image
Moto ukiendelea kuwaka katika Makontena yaliandaliwa na kujazwa matairi kwa lengo la kufanya mazoezi, ingawa mitaani tayari zilikwisha enea habari kuwa moto mkuwa umeteketeza makontena, Bandarini jijini Dar es salaam leo. Afisa mawasiliano mkuu wa Bandari, Peter Milanzi, akizungumza na waandishi wa habari waliofika katika eneo hilo ulipotokea moto ambapo alisema kuwa moto huo, ni sehemu ya mazoezi ya wafanyakazi wa Bandari ili kupima uwezo wa wafanyakazi wa Jeshi la kuzima moto na vifaa wanavyotumia wakati wa ajali za moto.  Aidha Peter, aliwaondoa hofu wananchi kwa kusema kuwa Makontena hayo yaliandaliwa na kujazwa matairi na kuyachomwa moto kwa lengo la kufanya mazoezi, ingawa mitaani tayari zilikwisha enea habari kuwa moto mkuwa umeteketeza makontena.  Baadhi ya majeruhi 

Miss Kinondoni Atwaa Taji la Miss Tanzania 2016

Image
  Diana Edward Lukumai akiwapungia mkono mashabiki mara baada ya kuvikwa taji la Miss Tanzania 2016 usiku wa kuamkia leo jijini Mwanza. Miss Tanzania 2016, Diana Edward (katikati) akiwa na mshindi wa pili, Grace Malikita na wa tatu,  Maria Peter. Warembo walioingia Top 5. Miss Kinondoni 2016, Diana Edward Lukumai aimeibuka kidedea kwa kutwaa taji la Miss Tanzania 2016. Shindano hilo kwa mara ya kwanza limefanyika jijini Mwanza katika ukumbi wa Rock City Mall. Diana ameibuka kidedea na kuwabwaga wenzake 30. Miss Tanzania 2016, Diana Edward Lukumai katika pozi tofauti.

RAIS DKT MAGUFULI AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII NA KUSHUHUDIA PEMBE ZA NDOVU 50 ZILIZOKAMATWA

Image
  Rais Dkt John Pombe Magufuli akimpongeza kwa kazi nzuri Katibu Mkuu wa  Wizara ya Maliasili na Utalii Meja Jenerali Gaudence Milanzi baada ya kukagua akikagua pembe za ndovu 50 zilizokamatwa katika operesheni maalum ya  ya kusaka majangili alipofanya ziara ya kushtukiza makao makuu ya Wizara ya Maliasili na Utalii (MPINGO HOUSE) jijini Dar es salaam leo Oktoba 29, 2016. a

DC Hapi Atembelea Wajasiriamali Wa Airtel Fursa

Image
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi akikagua bidhaa za wajasiriamali wadogo waliowezeshwa kupitia mpango wake wa Airtel Fursa. Kulia aliyeambatana naye ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel, Beatrice Singano. …Hapi akipata maelekezo ya changamoto mbalimbali zinazowakabili kutoka kwa mjasiriamali aliyewezeshwa na Airtel Fursa (aliyeko kulia). …Hapi akiendelea kukagua nembo za TBS na Bar Code katika bidhaa za wajasiriamali hao waliowezeshwa na mpango mkakati wa Airtel Fursa. …Hapi akikabidhiwa keki na Diana Moshi aliyokuwa ameiandaa (kushoto) ambaye ni mjasiriamali anayemiliki kampuni yake iitwaye Diana’s Oven aliyowezeshwa na Airtel Fursa. Mjasiriamali wa kuchora aitwaye, Theresia Deus (kushoto) akimuonyesha bidhaa zake mkuu huyo baada ya kuwezeshwa Laptop kwa ajili ya kuchorea na Airtel Fursa miezi mitano ilyopita sasa. Hapi na RPC wa Kinondoni Suzan Kaganda wakiangalia mayai ya kienyeji kutoka kwa mjasiriamali wa kufuga kuku wa Wilaya ya

Wahukumiwa Kifo kwa Kumuua Albino Bukoba

Image
Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba leo imewahukumu kunyongwa hadi kufa watuhumiwa waili Lameck Bazil na Pankras Minago kwa kumuua albino Magdalena Andrea. Hukumu hiyo imetolewa na Jaji Firmin Matogolo baada ya kuridhika na ushahidi kuwa watu hao ndiyo waliomuua mlemavu huyo ambaye ni mkazi wa Wilaya ya Biharamulo mwaka 2008. Credit: Fahari News

Hizi Ndizo Shule Zilizofanya Udanganyifu Kwenye Mtihani wa Darasa la 7

Image
Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), Dk. Charles Msonde akitangaza matokeo ya Kumaliza Elimu ya Msingi 2016, mapema leo. … Msonde akionyesha baadhi ya nguo za wanafunzi zilizokamatwa katika kipindi cha mitihani zikiwa zimeandikwa majibu ya mitihani hiyo. …Akionyesha kaptula ya mmoja wa wanafunzi wa Shule ya Msingi Tumaini iliyopo Wilaya ya Sengerema yenye majibu ya maswali ya mtihani wa Darasa la Saba iliyokamatwa. … Akionyesha karatasi ya mfano wa majibu inayoonyesha baadhi  ya wanafunzi yenye ufanano wa aina moja katika shule. Mkutano na wanahabari ukiendelea.

BREAKING NEWSS:HAYA NDIO MATOKEO YA DARASA LA SABA

Image
Kuyatazama matokeo ya darasa la saba mwaka 2016; Bofya Hapa  au Bofya Hapa

MANCHESTER UNITED WAITANDIKA MAN CITY NA KUTINGA ROBO FAINALI

Image
      Kikosi cha Manchester United kinachoongozwa na Jose Mourinho usiku huu kimeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Manchester City. Mchezo huo wa Kombe la EFL uliopigwa kwenye Uwanja wa Manchester United, Old Trafford ulimalizika kwa bao pekee lililofungwa na Juan Mata dakika ya 54. VIKOSI MANCHESTER UNITED: De Gea, Valencia, Rojo, Blind, Shaw, Carrick, Herrera, Mata (Schneiderlin 73), Pogba, Rashford (Lingard 82), Ibrahimovic Benchi: Romero, Depay, Young, Fellaini, Darmian MANCHESTER CITY: Caballero, Maffeo, Otamendi, Kompany (Kolarov 46), Clichy, Garcia Serrano, Fernando, Sane (Sterling 63), Jesus Navas, Iheanacho, Nolito (Aguero 71) Benchi: Gunn, Gundogan, Fernandinho, Adarabioyo