Posts

MIMBA YA JOKATE KIDOTI YAZUA BALAA,MAZITO YAFICHUKAKUHUSU KIBA

Image
Jokate na mpenzi wake, Alikiba Saleh Na Waandishi wetu Kizaazaa! Kufuatia mwanamitindo nyota Bongo na Miss Tanzania Namba 2, 2006, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ kudaiwa kuwa na ujauzito wa Mbongo Fleva, Alikiba Saleh, mazito yameibuka kwa mademu waliowahi kusemekana ni ‘zilipendwa’ wa msanii huyo kusemwa kwamba, hawakuwa na uwezo wa kumzalia, Risasi Mchanganyiko linakuwa la kwanza kukudondoshea.   Chanzo makini kililiambia Risasi Mchanganyiko kuwa, warembo wanaodaiwa kuwa ni wapenzi wa zamani wa Kiba ni Gift Stanford ‘Gigy Money’, Lulu Euggen ‘Amber Lulu’ na Sabrina Omar ‘Sabby Angel’ kwamba hawakuwa na uwezo wa kuzaa, ndiyo maana hawakuweza kushika ujauzito wa staa huyo na kuishia kuachika tu. MSIKIE HUYU HAPA “Wapenzi wa zamani kina Gigy Money, Sabby Angel na Amber Lulu hawakuwa na uwezo wa kuzaa ndiyo maana hawakuwahi kuonekana wakiwa na ujauzito au kusikika kwamba walikuwa na mimba ikaharibika na sasa hivi hawataki hata kusikia habari za ujauzito wa Jokate hivyo tunams

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI TAREHE 21.07.2016

Image

MAGAZETI YA MICHEZO NA BURUDANI

Image
 

KATIBU MKUU WA CCM KINANA AKAGUA UKUMBI WA MKUTANO MKUU DODOMA LEO

Image
Katibu wa NEC, Itukadi na Uenezi, Nape Nnauye na Msemaji Mkuu wa CC, Christopher Ole Sendeka wakimkaribisha Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alipowasili kukagua ukumbi wa mikutano wa CCM, Dodoma Conversion Center nje kidogo ya mji wa Dodoma, leo Julai 20, 2016, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCM utakaofanyika Julai 23, 2016. Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akimpa maelezo Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alipokagua ukumbi wa mikutano wa CCM, Dodoma Conversion Center nje kidogo ya mji wa Dodoma, leo Julai 20, 2016, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCM utakaofanyika Julai 23, 2016. Kulia ni Msemaji Mkuu wa CCM, Christopher Ole Sendeka. Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akimpa maelezo Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alipokagua ukumbi wa mikutano wa CCM, Dodoma Conversion Center nje kidogo ya mji wa Dodoma, leo Julai 20, 2016, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum w

SIRI NZITO YAFICHUKA MTANZANIA ALIYEWEKWA REHANI PAKISTAN,MKE AHAMISHWA NA JUMA,APANGIWA NYUMBA

Image
NI mateso. Ndivyo unavyoweza kusema, hasa baada ya kundi la maharamia linalojishughulisha na bishara ya ‘unga’ nchini Pakistan kuelezwa kumtesa kijana Mtanzania, Adamu Akida. Kutokana na hali hiyo, timu ya MTANZANIA ilipiga kambi jana katika eneo la Magomeni, Mtaa wa Idrissa, ambako pamoja na mambo mengine, ilifanikiwa kuzungumza na kaka wa Adamu aliyejitambulisha kwa jina la Hemed Abdallah (si jina lake halisi). Akisimulia mkasa huo, alisema miezi minane iliyopita, Adamu alikwenda kwa kaka yake ambaye ni mtoto wa mama yake mdogo aliyetambulika kwa jina la Juma, na kuomba msaada wa mtaji kwani kazi yake ya kinyozi haikuwa ikilipa na hali ya maisha ilikuwa ngumu. Baada ya kueleza shida yake hiyo, kaka yake huyo (Juma) alimuhoji kama yupo tayari kwa ajili ya kutafuta maisha nje ya nchi, na Adamu alikubali kufanya kazi ya aina yoyote ili mradi aweze kupata pesa. “Adamu kwa sasa ameshikiliwa kwa muda wa miezi minane, hatujui kama alikuwa ameingia katika janga hili ha

Binti miaka 8 afanyiwa ukatili wa kutisha!

Image
Mtoto Mariam aliyezibwa uso. Na Issa Mnally, UWAZI DAR ES SALAAM: Mtoto aliyejulikana kwa jina moja la Mariam (10), mkazi wa Mavurunza ‘A’ Kimara King’ong’o, Dar yupo katika mateso makubwa kufuatia vitendo vya ukatili na unyanyasaji anavyofanyiwa na mwanamke anayedaiwa kuwa ni mama yake mzazi aitwaye Aisha.   Akionesha sehemu ya shingo alivyokwaruzwa kwa kucha. Kwa mujibu wa majirani, mtoto huyo ambaye hata mahudhurio yake shuleni si mazuri, amekuwa katika mateso hayo ya kupigwa mpaka kujeruhiwa kwa muda mrefu lakini majirani walikuwa wakishindwa jinsi ya kumnasua kuzingatia kuwa, anayedaiwa kufanya vitendo hivyo ni mama yake. Hivi karibuni, majirani wa eneo hilo wakishirikiana na Mjumbe wa Shina Namba 063, Mavurunza ‘A’ Kwa Kichwa, Janet Moshi waliamua kumwokoa mtoto huyo baada ya kufukuzwa nyumbani na mama yake huyo majira ya saa 4:30 usiku bila kuwa na sehemu ya kwenda. “Ilikuwa saa nne na nusu usiku, sisi tulikuwa tumekaa kule mbele tukipata moj

Wanafunzi 7,800 waliofukuzwa UDOM ni 382 tu wenye sifa – Prof. Ndalichako

Image
Serikali imetangaza orodha ya wanafunzi ambao watarejea kuendelea na masomo katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) baada ya uchambuzi kumalizika na kupatikana idadi ya wanafunzi ambao wana sifa za kuendelea na masomo. Akizungumza na waandishi wa habari, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako alisema kuwa kwa kipindi chote walikuwa wakifanya uchambuzi ili kuona ni wanafunzi gani walikuwa na sifa za kusoma kozi hiyo maalum ambayo ilianzishwa kutokana na tatizo la walimu wa Sayansi. Alisema kuwa programu hiyo ilikuwa inahitaji walimu ambao watakwenda kufundisha shule za sekondari lakini kulikuwa na wanafunzi 1,210 ambao walikuwa wanachukua stashahada ya ualimu wa shule za msingi ambao ni kinyume na malengo na 6,595 wakichukua stashahada ya kufundisha shule za sekondari. “Baada ya hatua ya kuwaondoa wanafunzi chuoni kuchukuliwa, serikali ilifanya uchambuzi wa wanafunzi hao kwa lengo la kujiridhisha na sifa zao. Sifa zilizotakiwa ni ufaulu wa daraja

RAIS DKT. MAGUFULI AZUNGUMZA NA MAAFISA WA JESHI LA POLISI WALIOPANDISHWA VYEO IKULU JIJINI DAR ES SALAAM,AWATAKA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA WANAOLETA MATATIZO

Image
Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Ahmada Abdalla Khamis akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya kula kiapo cha ahadi ya uadilifu Ikulu jijini Dar es Salaam. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa wa Jeshi la Polisi waliopandishwa vyeo vya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) na Naibu Kamishna wa Polisi DCP mara baada ya kula kiapo cha ahadi ya uadilifu Ikulu jijini Dar es Salaam. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa wa Jeshi la Polisi waliopandishwa cheo cha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) mara baada ya kula kiapo cha Maadili ya Watumishi wa umma Ikulu jijini Dar es Salaam Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwagaia vitafunwa wageni mbalimbali waliofika Ikulu kwa ajili ya kushuhudia Maafisa wa Polisi walipondishwa vyeo wakati wakil