Posts

Mume amfunga mkewe mtini kisa kutopata mimba

Image
Jeni Marwa akiwa amefungwa kamba mtini na mumewe. Stori: Gregory Nyankaira, UWAZI MARA: Nyango Hakimu mwenye umri wa miaka 37, anatafutwa na polisi akidaiwa kumfunga mkewe Jeni Marwa (23) kwenye mti na kumpa kichapo kilichomsababishia majeraha kwa madai ya kutoshika ujauzito kwenye ndoa yao. Tukio hilo lilitokea jioni ya Februari 6, mwaka huu katika Kijiji cha Singu, kilichopo Kata ya Kukirango wilayani Butiama mkoani Mara, ambako mwanamke huyo alipigwa kwa fimbo sehemu mbalimbali za mwili wake, akidaiwa kutokuwa na faida nyumbani hapo. Mashuhuda wa tukio hilo wamesema, baada ya mumewe kumfunga mkewe kamba mikononi na miguuni kabla ya kumfunga kwenye mti na kuanza kumchapa, mwanamke huyo alipiga mayowe ya kuomba msaada ndipo watu walifika na kumkuta akitokwa damu nyingi baada ya kukatwa na kisu mguuni. Huku mumewe akiwa amekimbilia kusikojulikana, wasamaria wema walimchukua na kumpeleka Kituo cha Polisi cha Kiabakari ambako alipewa fomu ya matibabu (PF3) kabla ya

BREAKING NEWS:Waziri wa elimu amfuta kazi Mkurugenzi wa Bodi ya Mikopo

Image
Waziri wa Elimu Sayansi, Teknolojia na ufundi, Prof Joyce Ndalichako. Waziri wa Elimu Sayansi, Teknolojia na ufundi, Prof Joyce Ndalichako amesitisha mkataba wa kazi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo  George Nyatenga.    Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo  George Nyatenga. Pia amewasimamisha kazi wakurugezi watatu wa Bodi hiyo ambao ni Mkurugenzi wa Fedha na Utawala Yusufu Kisare, Mkurugenzi wa Urejeshaji Mikopo Juma Chagonja na Mkurugenzi wa Upangaji na Utoaji Mikopo. Prof Ndalichako  amemwagiza Mkaguzi wa ndani Mkuu wa Serikali ahakiki maelezo na Nyaraka zilizowasiliwa na Bodi ya Mikopo pamoja na kufanya ukaguzi maalum kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2013 hadi sasa. Mesothelioma Survival Rates About 40 percent of patients with mesothelioma survive the first year after diagnosis. That survival rate depends on many factors, including age, cancer stage,

MSANII WA BONGOFLEVA JONI WOKA AFARIKI DUNIA

Image
Maregehemu Michael Denis a.k.a Joni Woka enzi za uhai wake Akiongea kwa simu kaka wa marehemu Omari Milay, amesema walipigiwa simu alfajiri ya leo na kujulishwa kuwa Michael Denis  aliyejizolea umaarufu mkubwa kwa jina la Joni Woka amefariki katika hospitali ya Muhimbili, alipokuwa akipata matibabu ya ajali aliyopata siku ya jana. Michael Denis a.k.a Joni Woka alipata ajali ya kugongwa na kitu kizito kwenye paji la uso, alipokuwa garage maeneo ya Sinza akitengeneza gari yake, kwa bahati mbaya mtungi wa gesi ukalipuka na moja ya vipande vya chuma chenye ncha kali kikamchoma kichwani, Tarifa za awali za madaktari zilisema wanahofia kipande hiko kimefika mbali kiasi kwamba damu inamwagikia kwenye ubongo. Mipango ya mazishi familia imesema inakutana kujadili na mara itakapokamilika watajulisha watu nini kinaendelea. Msanii John Woka ambaye alikuwa kwenye kundi la Watukutu Family, alijipatia umaarufu kwa nyimbo zake za Sophia, baby gal na nyinginezo, ambazo aliziimba k

Aliyejipachika cheo cha usalama wa taifa akiona!

Image
Wakimfunga kamba. S tori: Makongoro Oging’ na Issa Mnally, UWAZI DAR ES SALAAM: Ujanja wa mjini! Jamaa aliyejipachika cheo kuwa yeye ni Afisa Usalama wa Taifa, Ofisi ya Waziri Mkuu akijitambulisha kwa jina moja la Manase amekiona cha moto baada ya kunaswa na kufungwa kamba mwilini na mtu aliyesema ni daktari wa Kliniki ya Head 2 ya jijini Dar, Fortdas Fidell. Tukio hilo la aina yake lilitokea Jumatano ya Februari 10, mwaka huu katika kliniki hiyo inayojishughulisha na tiba ya mifupa na mazoezi iliyopo Mtaa wa Ununio, Kata ya Kunduchi wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam ambapo risasi sita zilipigwa hewani na mtu aitwaye Mashaka Ndonde ili kumdhibiti mtuhumiwa huyo. UWAZI LAFIKA ENEO LA TUKIO Baada ya kusikika kwa milio ya risasi, baadhi ya watu walilipigia simu Uwazi na kuhabarisha tukio hilo ambapo waandishi wetu walifika mara moja eneo hilo na kuweza kukutana na Dk. Fidell ambaye alisimulia kisa cha kufyatuliwa kwa risasi na kushikiliwa kwa ‘afisa usalama’ huyo

MAJALIWA AKABIDHIWA NAKALA YAKE YA FOMU YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Image
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea nakala yake ya  fomu ya ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma kutoka kwa Kamishina wa Maadili, Jaji Mstaafu Salome  Kaganda ambayo aliitia saini na kuipeleka kwenye Secretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ambako ilitiwa saini na kamishina huyo. Makabidhiano hayo yalifanyika Ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam Februari 15, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Secretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ambao walikwenda ofisini kwake jijini Dar es salaam Februari 15, 2016 kumpatia nakala yake  ya fomu ya ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma  ambayo aliitia saini  na kuipeleka kwenye Secretarieti  hiyo ambako ilitiwa saini na Kamishina wa Maadili, Jaji Mstaafu Salome Kaganda (wapili kulia).Kushoto ni Katibu wa Idara ya Viongozi Watumishi wa Umma, Secretarieti ya Maadili , John Kaole na kulia ni Katibu wa Idara ya Viongozi wa Siasa, Secret

WATUHUMIWA WALIOKUTUNGUA HELKOPTA SERENGETI WATIWA MBARONI.

Image
Njile Gonga (28) Huyu ndiye Jangili anadaiwa kutungua helkopta katika pori la Akiba la Maswa lililopo katika Wilaya ya Meatu Mkoani, ambapo katika tukio hilo rubani wa helkopta hiyo Rodgers Gower (37) raia wa uingereza huku Mwenzake Nicholas Beste (43) raia wa Afrika Kusini akinususrika kifo.   Iddy Mashaka (49) ambaye ndiye alikuwa Mkuu wa kitengo cha Interejensia katika hifadhi ya taifa Ngorongoro, ambaye anadaiwa kuwa kiunganishi Mkuu wa kutekeleza tukio la kutunguliwa kwa helkpta hiyo.  Hali ya ulinzi na usalama ilivyokuwa imehimarsihwa mahakamani pamoja na kituo cha polisi Bariadi leo hii.  Watuhumiwa wakiwa ndani ya gari la polisi, baada ya kufikishwa kituo cha polisi Bariadi wakitokea wilayani Meatu kwa ajili ya kufikishwa mahakamani.

IMPORTANT OF HAVING SEX

1 . Having sex relieves headaches. Every time you make love , it releases the tension in the veins of the brain. 2 . A lot of sex can clear the stuffy nose. Sex is a natural antihistamine . It helps to fight against asthma and spring allergies . 3 . Making love is a spectacular beauty treatment. Scientists have discovered that when a woman has sex , it produces a large amount of estrogen that gives shine and softness to hair. 4 . Sex is one of the safest sports. Make love often strengthens the muscles of male and female body. It's more enjoyable than swimming 20 laps in the pool and there is not need special shoes! 5 . Make love slowly , smoothly and in a relaxed way reduces the chances of suffering dermatitis, skin rashes and acne . The sweat produced cleanses the pores and makes your skin glow . 6 . Lovemaking can burn all the calories you have accumulated during the romantic dinner before bedtime. 7 . Sex is a divine remedy for depression. It releases endorphins in

Bifu Za Mastaa Bongo… Zilizoacha Historia

Image
Makala: Chande Abdallah Ukiacha bifu nzito zilizotikisa dunia mpaka kusababisha vifo vya mastaa wakubwa kama Notorious BIG na Tupac, zifuatazo ni orodha ya bifu zilizotikisa kwenye tasnia ya muziki Kibongobongo na kuacha historia kubwa kiasi kwamba hata mastaa hao walivyopatana mashabiki wao walibaki vinywa wazi kwa kutoamini kilichotokea. Ali ChockVs Asha Baraka Ali Chock Asha Baraka Bifu lao lilianza baada ya kuhitilafiana kwenye uhamisho wa mpiga gitaa wa Twanga Pepeta, Shakashia ambapo Asha Baraka akaanza kudai gari alilomnunulia Chocky na kufikishana mahakamani ambapo bifu lao likazidi kushika kasi kiasi cha kuapiana kutozikana. Hata hivyo, wawili hawa walimaliza bifu lao na kukumbatiana ndani ya Studio za Global TV Online zilizopo Bamaga-Mwenge. Dudu Baya Vs Mr Nice Dudu Baya Mr Nice Wawili hawa walionesha kuwa na bifu zito baada ya Dudu Baya kumtwanga makonde Mr Nice mbele ya mashabiki wake na kufikishana mahakamani ambapo Dudu baya aliswekwa rumande. H

BREAKING NEWZ:HIVI NDIVYO WATU WALIVYO NUSURIKA NA KIVUKO CHA MV MAGOGONI

Image
Kigambon majanga  abiria imebidi wajitose baharini kuokoa maisha yao baada ya kivuko kupoteza muelekeo asubuhi hii baada ya kuzidiwa na idadi kubwa ya mizigo na abiria

BREAKING NEWZ:Ajali ya basi la Simba na lori yaua Tanga

Image
WATU kadhaa wanahofiwa kufariki dunia wakiwemo madereva wawili baada ya basi la abiria la Simba Mtoto lililokuwa linakuja jijini Dar es Salaam kupata ajali kwa kugongana na lori uso kwa uso katika kijiji cha Pangamlima mkanyageni, Barabara ya Tanga-Segera mkoani Tanga leo asubuhi na inasaidikiwa watu kadhaa wamefariki. Tovuti hii imeongea na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga ambaye amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kueleza kuwa zoezi la uokoaji bado linaendelea hivyo likimamilika atatoa taarifa rasmi kuhusu ajali hiyo. Taarifa zaidi zitawajia hivi punde

RAIS DKT. MAGUFULI AMJULIA HALI SHEIKH MKUU WA TANZANIA PAMOJA NA KUFANYA UKAGUZI WA KUSHTUKIZA KATIKA WODI YA WAZAZI YA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimjulia hali Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakary Zubeir ambaye amelazwa kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya matibabu. Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakary Zubeir akimuombea Dua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya Rais Dkt. Magufuli kumjulia hali Hospitalini hapo.  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiombewa Dua na ndugu na jamaa mbalimbali ambao walifika Muhimbili kuwaona wagonjwa wao. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akielekea katika Wodi ya Wazazi kufanya ukaguzi wa ghafla mara baada ya kuwasili akitokea Dodoma. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wagonjwa waliolazwa katika Wodi ya Wazazi na amewahidi kutatua kero zao ndani ya muda mfupi ujao.PICHA NA IKULU

BREAKING NEWZZ.....Mkuu wa majeshi wa Korea ya Kaskazini amenyongwa kwa tuhuma za ufisadi

Image
​ Mkuu wa majeshi ya Korea Kaskazini kanyongwa kwa tuhuma uhujumu/ufisadi kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Korea ya kusini. Mkuu huyo wa jeshi la Korea Kaskazini hajatajwa kwenye vyombo vya habari vya Korea tangu katikati mwa Januari. Generali Ri Yong-gil inaripotiwa alinyongwa wiki iliyopita na tukio hilo linatokea wakati dunia ikiinyooshea kidole Korea ya Kaskazini juu ya urushwaji roketi ya masafa marefu Jumapili iliyopita.  North Korea has executed its army chief of staff, Ri Yong Gil, South Korea's Yonhap news agency reported on Wednesday, which, if true, would be the latest in a series of executions, purges and disappearances under its young leader. The news comes amid heightened tension surrounding isolated North Korea after its Sunday launch of a long-range rocket, which came about a month after it drew international condemnation for conducting its fourth nuclear test. A source familiar with North Korean affairs also told Reuters that Ri had

Mrembo Adaiwa Kutelekeza Mwanaye Kisa Mlemavu

Image
  Mtoto Ilham Mohamed A RUSHA: Hujafa  hujaumbika! Mtoto Ilham Mohamed  19, (pichani) mkazi wa Ngarenaro jijini hapa amezaliwa akiwa na ulemavu wa viungo kiasi cha kumfanya aonekane mtoto mdogo, lakini bibi wa mtoto huyo, Zuleha Ismail anacholalamikia ni kitendo cha mama Ilham, Sapna Parakash kumtelekeza mwanaye. Mtoto huyo akiwa na bibi yake, Zuleha Ismail BIBI WA MTOTO NDIYE MWENYE KISA Akizungumza kwa masikitiko na gazeti hili mwanzoni mwa wiki hii nyumbani kwake, Ngarenaro, bibi Ilham alisema alitelekezewa mtoto huyo mwaka 1997 na mama yake kwenda kuishi na mwanaume mwingine baada ya kuachana na mtoto wake aliyemtaja kwa jina la Mohammed Ismail. Mama Ilham, Sapna Parakash MSIKIE MWENYEWE “Mama wa mtoto huyu amenitelekezea hapa. Aliwahi kuja mara moja lakini hakutaka kumshika wala kumbeba. Alimwambia ambariki ili apate mdogo wake kwani licha ya kutafuta tiba na mwanaume aliyenaye lakini ameshindwa kupata ujauzito.”  AELEZEA NDOA YA SAPNA NA MWAN

Kwani ni lazima uolewe???

Image
HAKIKA sifa na utukufu zimuendee yeye Jalali ambaye ametupa nafasi ya kuweza kukutana tena siku ya leo hii.Moja ya kitu kinachonishangaza kwa wanawake wengi ni kuwa na ndoto zaidi ya kuolewa kuliko kufikia ndoto zao halisi kwa maana ya maono ambayo wamekuwa wakiyawaza kwa muda mrefu. Tabia hii ya wanawake wengi ya kutaka au kukimbilia kuolewa si jambo baya, kama ikitokea ukapata bahati hiyo ya kuolewa lakini kama haitatokea sio ishu sana bali kumbuka kuwa kuna maisha nje ya kuolewa nayo si mengine ni maisha ya kufikia ndoto zako. Kama haujaolewa Ni kweli Mungu alituumba na kutuweka duniani ili tuujaze ulimwengu lakini hata hilo la upande wa pili nalo ni la kushukuru pindi linapokukuta, linauma ila kupunguza maumivu yake ni kulikuba li na kujifunza vitu vingine vingi ili uweze kuendelea na maisha mengine. Hulka ya wanawake kuolewa imekuwa ni sehemu ya wengi wao, utamsikia binti wa miaka 16 amemaliza darasa la saba anataka kuolewa eti kisa amefeli mtihani wa mwisho,

Mafuta ya Wizi ya Diesel Yakamatwa Bandari ya Dar

Image
Jeshi la Polisi kitengo cha majini limekamata tani zipatazo 20 za mafuta ya dizeli yaliyokuwa katika Jahazi lililokuwa kando ya bandari ya Dar es Salaam likijiandaa kwa safari ya kwenda Zanzibar. Mkuu wa Kitengo hicho cha Polisi cha Wanamaji, Bw. Mboje John Kanga amesema watu watano wanashikiliwa kuhusiana na tukio hilo na uchunguzi zaidi unaendelea.

ALIKIBA NA WILDAID WATOA WIMBO KUPINGA UJANGILI WA TEMBO.

Image
 Video ya wimbo huo imerekodiwa jijini Los Angeles Marekani ambapo Alikiba alikuwa mgeni rasmi kweye hafla maalum iliyoandaliwa na shirika la uhifadhi wanyamapori la kimataifa la WildAid. Chini ya kauli mbiu “Ujangili Unatuumiza Sote”, Alikiba amefanya kazi na WildAid kuongeza uelewa wa Watanzania kuhusu tatizo la ujangili wa tembo ambao wamechinjwa kwa maelfu miaka ya hivi karibuni kwa ajili ya meno yao. Hatimaye Alikiba ametoa wimbo wake “Lupela” uliokuwa ukisubiriwa na mashabiki wake Afrika Mashariki kwa wiki kadhaa sasa. Wimbo huo ni sehemu ya kampeni ya “Ujangili Unatuumiza Sote” iliyozinduliwa mwaka jana na WildAid na African Wildlife Foundation mashirikia yanayofanya kazi pamoja barani Afrika na Asia kupunguza mahitaji ya bidhaa zitokanazo na wanyamapori na kuongeza uelewa wa janga la ujangili linaloikabili Afrika. Katika uzinduzi uliofanyika mwishoni mwa wiki kwenye hoteli ya Slipway jijini Dar es salaam, wageni mbalimbali na waandishi wa habari walipata