Rais Kikwete Alipowasili Viwanja vya Bunge Dodoma na kukagua Bwaride Maalum.
Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Mh. Samuel John Sita akibadilishana mawazo na Makamu Mwenyekiti wake nje wa Ukumbi wa Bunge Mjini Dodoma kabla ya Kuanza kwa uzinduzi wa Bunge Maalum uliofanywa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete.kushoto Katibu wacBunge Maalum Yahya Hamad Khamis. Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete akiingia ndani ya Viwanja vya Bunge kulihutubia Bunge Maalum la Katiba Mjini Dodoma leo. Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Tanzania Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride rasmi lililotayarishwa na Jeshi la Polisi kabla ya kuzindua Bunge Maalum la Katiba Mjini Dodoma.( Picha na Hassan Issa wa – OMPR ) Othman Khamis Ame Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibnar Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete amesema Umma wa Watanzania utajaa matumaini endapo jukumu walilopewa wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba watalizingatia