Rais Kikwete Alipowasili Viwanja vya Bunge Dodoma na kukagua Bwaride Maalum.

Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Mh. Samuel John Sita akibadilishana mawazo  na Makamu Mwenyekiti wake nje wa Ukumbi wa Bunge Mjini Dodoma kabla ya Kuanza kwa uzinduzi wa Bunge Maalum uliofanywa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete.kushoto Katibu wacBunge Maalum Yahya Hamad Khamis.
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete akiingia ndani ya Viwanja vya Bunge kulihutubia Bunge Maalum la Katiba Mjini Dodoma leo.
Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Tanzania Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride rasmi lililotayarishwa na Jeshi la Polisi kabla ya kuzindua Bunge Maalum la Katiba Mjini Dodoma.(Picha na Hassan Issa wa – OMPR )
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibnar

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete amesema  Umma wa Watanzania utajaa matumaini endapo jukumu walilopewa wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba watalizingatia vizuri na kulithamini ipasavyo.
Alisema jukumu hilo litaweza kufanikiwa vyema kama wajumbe hao watazingatia ipasavyo misingi ya utulivu, hekima, na busara wakati wa kujadili rasimu ya Katiba ya pili iliyopo mikononi mwao hivi sasa.

Dr. Kikwete alisema hayo wakati akizungumza na Wabunge wa Bunge Maalum kwenye uzinduzi rasmi wa Bunge hilo Maalum la Katiba linaloendelea Mjini Dodoma lilijumuisha Wawakilishi zaidi ya Mia 620 kutoka vyama vya siasa,Taasisi na Jumuiya tofauti za Kijamii.

Alifahamisha kwamba kazi ya wajumbe hao wa Bunge Maalum la Katiba ni kujadili, kuamua na hatimae kutunga katiba Mpya inayosubiriwa na Wananachi kwa ajili ya kuitolea maamuzi.

“ Fursa ya Utungaji wa Katiba mliyoipata Mkiipatia Tanzania Katiba Mpya bila shaka Historia itawaandika kwa wino wa dhahabu hasa mkitunga Katiba itakayotekelezeka na kuondoa changa moto zilizopo kwa pande zote mbili za Muungano “. Alisisitiza Rais Kikwete.

“ Hamna budi kujidhirisha juu ya vifungu kwa vifungu vya rasimu, neno kwa neno, Sentensi jkwa sentensi ili mfikie pahali kwa kujidhihirisha. Tunachotaka Watanzania kupata Katiba iliyo bora, Vyenginevyo tutakua na katiba itakayokujahitaji kutengenezwa tena haliambayo si rahisi “. Aliendelea kufafanua Dr. Kikwete.

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania alieleza kwamba Demokrasia ndani ya Tanzania imestawi na kujenga mizizi kwa vile wananachi walio wengi wako wazi kutoa maoni na mawazo yao kwa uhuru mpana zaidi.

Alifahamisha kuwa madai ya Tanzania kuwa na Katiba Mpya yalianza kuibuka ndani ya mfumo wa vyama vingi vya siasa hapa nchini na kupelekea kufikia hatua ya kuanzishwa kwa mchakato wa kutunga katiba mpya alioamua kuutangaza rasmi  Tarehe 31 Disemba mwaka 2010.

Amewataka wajumbe hao kuwa makini katika kuyapitia kwa kina mapendekezo ya yaliyomo ndani ya rasimu hiyo kwa vile mengi yamekuwa katika utaratibu mpya ili kuepuka kabisa mwanzo wa Katiba hiyo kushindwa kurekelezeka.

Dr. Jakaya Mrisho Kikwete alifafanua kwamba mfumo wa Serikali mbili ulipo hivi sasa hauna mashaka katika kutekelezeaka lakini kazi ya Wajumbe hao wa Bunge Maalum la Katiba ndio itakayosubiriwa na Wananachi katika kutoa Maamuzi.

Alisema kitakachohitajika kwa wakati ujao na kwa Viongozi hao kujenga hoja na ushawishi utakayowaridhisha wananchi kukubali mfumo wa Katiba watakayopendekeza.

Akizungumzia suala la muundo wa Serikali ya Muungano Mh. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete aliwatahadharisha wajumbe hao wa Bunge Maalum la Katiba kuwa makini katika maamuzi ya mfumo utakaowaletea tija Wananchi wa pande zote Mbili.

Dr. Kikwete aliwaasa kwamba maamuzi yasio sahihi katika mfumo wa muundo huo ama kuwa wa Serikali Mbili au Tatu  unaweza ukaitia hasara kubwa nay a muda mrefu Nchi.

Uzinduzi huo wa Bunge Maalum la Katiba la Muungano umeshuhudiwa pia na Viongozi Mashuhuri wa Kitaifa, Wawakilishi wa Taasisi na Mashirika ya Kimataifa wapatao 52 , Viongozi wasataafu wa Serikali zote mbili za SMT na SMZ pamoja na Wakuu wa Vikosi vya ulinzi na Usalama Muungano na Vile vya SMZ.

Mapema Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania  Dr. Jakaya Mrisho Kikwete alipokea saluti iliyoandaliwa rasmi Kabla ya uzinduzi wa Bunge hilo kutoka kwa Jeshi la Polisi  pamoja na kuimbwa wimbo wa Taifa wa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.        

Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba tayari wameshatunga Kanuni za Bunge Maalum za Mwaka 2014 chini ya Kifungu cha 26 {1} cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83.

Comments

Popular posts from this blog